Habari zenu Tanesco,ivi ajira zenu hua mnazitoaga wapi kwani sijawahi ona nafasi zenu mkitangaza?
 
Mita ikishafungea eneo moja haihamishiki kwenda eneo lingine.unachoweza kufanya ni kufunga kifaa cha kusoma matumizi yako vinapatikana maduka ya vifaa vya umeme

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanesco tangazeni mgawo wa umeme tujue rasmi na kututesa na majoto huku jua kali sana!
Kila siku lazima mkate umeme kwanini?
Mnatukwaza sana aisee!
Hata hapa nandika ujumbe hakuna umeme!
Inabidi tumwambie Rais kuwa tanensco mnatukwaza kwa kushindwa kutupatia umeme wa uhakika muda wote !


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu mnatudisha maendeleo nyumba, shughuli nyingi za uzalishaji zinakwama shauri ya ukosefu wa nishati ya umeme!
Yani inabidi mjitafakali na kubadilika la sivyo


Sent using Jamii Forums mobile app
 
jamani Tanesco na mtupe update kila zinapotokeaga nafasi za kazi
 
Nimelipa gharama zote za kuunganishiwa umeme toka October mpka sasa nazungushwa tuu.. basi nirudishieni pesa yangu hamtaki!!

Sio Siri mnatufelisha Sana wakazi wa chanika tutumiayo Tanesco Kisarawe..

Wafanyakazi wana majibu ya kero mpka basi...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekusudia kukarabati nyumba yangu, mafundi wamenishauri kuwa ili kazi Yao iende vizuri ni vyema aitwe fundi wa umeme kwa ajili ya kuisogeza MITA YA LUKU, upana wa mita mbili tu kutoka mahali ilipo sasa katika ukuta huohuo.

Fundi alipofika akaniambia kuwa kwa kawaida natakiwa kuwajulisha TANESCO na gharama za kuhamisha MITA YA LUKU kihalali eti ni shilingi laki mbili (200,000) isipokuwa kama nataka nimuachie yeye aihamishe hiyo mita mwenyewe kwa malipo ya shilingi laki moja tu. Nimemwambia nitamjibu kesho!

Kwa hiyo naomba wajuzi mnijuze kama ni kweli gharama ya kusogeza mita ya LUKU ni shs 200,000?? Maana mimi nilidhani ni bure isipokuwa nilipe gharama ya ufundi tu.

Au nimpe hiyo laki moja ili kukwepa mlolongo wa kwenda TANESCO kama anavyodai, na kazi hiyo aifanye mwenyewe?

Naomba mnijuze ili niendelee na zoezi au la
 
Tunachokusihi mpwendwa mteja wetu pamoja na wateja wengine ni kupenda kupokea taarifa na kutoa taarifa sehemu husika.njoo ofisini utajaza fomu wataalamu wetu watafika kwako na kufanya savey kisha tutakupatia gharama halisi kumbuka kuhamisha mita kinyemela ni kosa kwa mujibu wa sheria

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunachokusihi mpwendwa mteja wetu pamoja na wateja wengine ni kupenda kupokea taarifa na kutoa taarifa sehemu husika.njoo ofisini utajaza fomu wataalamu wetu watafika kwako na kufanya savey kisha tutakupatia gharama halisi kumbuka kuhamisha mita kinyemela ni kosa kwa mujibu wa sheria

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…