Tunaposema ndani ya siku kadhaa haina maana mpaka zifike hii ni kuruhusu waliolipa mbele yako kupatiwa huduma ndio tukufikie wewe
Mbona mimi nimejaza form toka tar 5 September mpaka leo hata control namba sijapata kwa ajili ya kulipia na nipo ya mita 30. Kuna nini hapa
 
TANESCO mtaa wa Tabata mwananchi karibia na white house hakuna umeme baadhi ya nyumba leo siku ya pili mnapigiwa simu hamjali wala kushtuka.
Tatizo la hii line ni la muda mrefu lakni mmegoma kutoa ufumbuzi.

Mnataka wananchi wafanye Nini ninyi mjali jukumu lenu?

TANESCO
TANESCO
 
Tanesco mafundi wenu wametubadilishia mita isee hii iliyowekwa inakunywa UNIT mno matumizi yetu hayajabadilika toka mita ya kwanza iliyobadilishwa hii mpya umeme wa 40000 ndani ya wiki mbili umeisha
 
Hatimaye jana limetoa mlipuko na tumelala kiza hadi leo muda huu hamna umeme.ukipiga simu wanasena tunalifanyia kazi kama watu wa substation wameshindwa mseme basi mnatuzingua hamna msaada wowote
 
Tannesco Msaada wenu huku kisesa iseni Bondeni watu wanaunganishiwa umeme kwa rushwa tumejitaidi kulipia siku 30 za kazi zimeisha bila umeme
 
Ahsante kwa taarifa tumepokea kwa hatua zaidi
 
Tannesco Msaada wenu huku kisesa iseni Bondeni watu wanaunganishiwa umeme kwa rushwa tumejitaidi kulipia siku 30 za kazi zimeisha bila umeme
Je umelipia lini? Jina, wilaya namba ta simu tafadhali.je nani anachukua rushwa?
 
Jina Henry Juma lusoba

Eneo Tegeta Boko Chasimba

Wilaya Kinondoni

Namba ya simu
0687 482196
Tatizo ni kutokufungiwa umeme kwa muda tumekamilisha malipo toka Julai 02 lakini mpaka leo bado hatujafungiwa umeme kila mara tunaambiwa wiki hii haishi,naomba msaada tafadhali tumechoka maanà ni miezi mitatu sasa inaenda kukamilika toka tumelipia.
 
Ahsante kwa taarifa tumepokea kwa hatua zaidi
 
Ahsante kwa taarifa tumepokea kwa hatua zaidi
Kwanini mnapokea tu lakini hamtupi mrejesho? Maana hapa majibu kama haya yanatolewa lakini tatizo lako huambiwi limefikia wapi na linatarajiwa kufanyiwa kazi lini.
 
Kwanini mnapokea tu lakini hamtupi mrejesho? Maana hapa majibu kama haya yanatolewa lakini tatizo lako huambiwi limefikia wapi na linatarajiwa kufanyiwa kazi lini.
Utaupata usiwe na shaka ndio kwanza tumepokea lazima tutakupigia simu na kufanyia kazi taarifa zako
 
Jaribu kuzima Fridge siku moja uone kama ndio inashida. Angalia pia vifaa kama pasi, mara nyingine husahaulika kuzimwa
 
Habari ndugu Admin naomba kujuzwa gharama zaku ongeza meter ya luku katika nyumba ambayo tayari ina meter, Nipo Ilala bungoni vilevile naomba kujuzwa taratibu gani ni fwate na kipi na kipi kina hitajika ili kukamilisha mchako na itachukua siku ngapi mpaka kua tayari?

Sent from my SM-G9550 using JamiiForums mobile app
 
Mimi kwangu surveyor alikuja toka 28/04/2021 nipo ndani ya mita 45 panahitaji nguzo moja ila mpaka leo TANESCO hawataki kunipa control number, sasa sijui hizo siku 60 zinaanza kuhesabiwa kuanzia kwa surveyor au kuanzia siku uliyopewa control number.

TANESCO naombeni majibu
 
TANESCO MPYA IMEZALIWA LEO, TUNATAKA IENDESHWE KIBIASHARA- Waziri Makamba

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba amesema ni wakati sasa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO kuanza kujiendesha kibiashara, kwa ufanisi ili kuchangia uchumi wa Taifa.

Mhe. Makamba amesema hayo leo Septemba 26, 2021 wakati akizungumza na Mameneja wa TANESCO wa ngazi ya Kanda, Mikoa, Wilaya na Makao Makuu.

Aidha Mhe. Makamba amewatambulisha Wajumbe wa Bodi ya TANESCO wakiogozwa na Mwenyeki, Bw. Omari Issa, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji, Bw. Maharage Chande, walioteuliwa Septemba 25, 2021 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Wajumbe wa Bodi ya TANESCO waliotambulishwa ni pamoja na Bw. Nehemia Mchechu, Bi. Zawadia Nanyaro, Bw. Lawrence Mafuru, Mhandisi Cosmas Masawe, Balozi Mwanaidi Maajar, Mhandisi Abdallah Hashim, Bw. Abubakar Bakhresa na Bw. Christopher Gachuma.

Mhe. Makamba amesema Bodi iliyochaguliwa ina wajumbe kutoka nyanja mbalimbali na watasaidia Shirika kufikia malengo.

"Tunataka baada ya miaka mitatu Shirika liingie katika orodha ya mashirika bora, yenye thamani na yanayoheshimika Afrika" alisema Mhe. January Makamba

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO, Bw. Omari Issa, amesema atahakikisha Bodi inafanya kazi na kutimiza malengo yake kwa kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa malengo na uwajibikaji.

Mkurugenzi Mtendaji, Bw. Maharage Chande, ameeleza vipaumbele ambavyo ni masilahi ya rasilimaliwatu, Wateja wa Shirika na utekelezaji wa mipango, hivyo ameomba ushirikiano kutoka kwa wafanyakazi wa TANESCO.

"Nimhakikishie Mhe. Waziri tutahakikisha tunarudisha heshima ya Shirika na ufanisi kupitia ushirikiano wenu, hakuna Shirika lolote linalotoa huduma ya umeme zaidi yetu sisi, yamkini tuwape wateja wetu huduma wanayostahili", " alisema Bw. Maharage Chande

Meneja Mwandamizi Rasilimaliwatu, Bw. Francis Sangunaa, aliwahakikishia viongozi ushirikiano kwa niaba ya wafanyakazi wa TANESCO.
 
Kazi iendelee
 
Ndugu mteja,
Gharama ni shilingi 27,000 hivyo tunakushauri ufike ofisi ya TANESCO iliopo karibu na wewe na utapewa maelekezo zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…