TANESCO watoa ufafanuzi kuhusu Bwawa la kufua umeme la Mwl. Nyerere kuwa na nyufa

TANESCO watoa ufafanuzi kuhusu Bwawa la kufua umeme la Mwl. Nyerere kuwa na nyufa

aliyeandika hii taarifa ni kiazi, na kama md wa tanesco naye kaipitia kabla haijatolewa, md naye ni kiazi++
 
View attachment 2752996

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

HALI YA UBORA WA MRADI WA JNHPP NA UHIFADHI WA WANYAMA PORI

Jumapili, 10 Septemba 2023.
Kuna taarifa zinasambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mradi wetu wa Bwawa la Kufua Umeme la Mwalimu Nyerere (JNHPP). Taarifa hizo zinaelezea na kuleta hofu kuhusu Ubora wa Mradi, pamoja na Uhifadhi wa wanyama pori.

Taarifa sahihi kuhusu mradi wetu ni kwamba, mradi huu umesanifiwa kwa kuzingatia ubora wa hali ya juu na ujenzi wake unasimamiwa na wataalam walio bobea kwenye fani ya ujenzi(Civil Engineering) na Usimikaji Mitambo(Electromechanical Engineering) kutoka ndani na nje ya nchi ili kuhakikisha tunapata mradi ulio bora.

Kila hatua ya mradi hukaguliwa na kuhakikiwa kabla ya kwenda kwenye hatua nyingine, na pale ambapo hatua iliyotekelezwa inashindwa kufuzu ukaguzi na uhakiki basi marekebisho hufanyika kabla ya kuendelea hatua inayo fuata.

Bwawa letu ndani ya kuta zake limesimikwa vifaa vinavyo pima uimara kadri maji yanavyoingia kwenye bwawa, vifaa hivyo vina pima kama kuna hitilafu zozote zitakazo hatarisha ubora wa bwawa. Mpaka mwisho wa mwezi Agosti bwawa letu lina ujazo wa maji yalioingia wa mita za ujazo zaidi ya bilioni 14, na uzito wa maji unahimiliwa vizuri na bwawa letu kwani hakuna tatizo lolote la ubora au uimara linaloonekana kupitia vifaa vilivyosimikwa kwenye bwawa hilo.

Vilevile, uhifadhi wa wanyama pori na utunzaji wa mazingira unazingatiwa kama vile ilivyoainishwa katika mpango uliopitishwa wakati mradi huu unaanza kutekelezwa.

Mpaka mwezi Agosti 2023, Mradi mzima wa ujenzi umefikia asilimia 91.72%, na ni matarajio yetu mitambo yote itakuwa imefika nchini kabla ya mwisho wa mwezi Disemba 2023, na tutaanza kujaribu kupitisha maji kwenye mitambo mitatu ya kwanza mwezi Februari na tunategemea kupata Umeme wa kwanza mwezi Juni 2024 kama tulivyo ahidi.

Tunashukuru wananchi kwa kushirikiana nasi katika safari hii ya kujenga taifa letu, na hususan ufuatiliaji wa maendeleo ya mradi wetu huu mkubwa wenye manufaa makubwa kwa Taifa letu.

Imetolewa Na;
KURUGENZI YA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMMA TANESCO- MAKAO MAKUU.
DODOMA

Pia soma: Bwala la kufua umeme la Mwl. Nyerere, limeanza kutoa nyufa
Taarifa haijitoshelezi...wamejibu kisiasa
 
JF 'mtaua watu kwa pressure''. Jumapili wamekaa kikao wakiwa wamechanganyikiwa
Hawajakanusha kuhusu nyufa, wanatueleza kuhusu watalaam. Kwani nani alisema watalaam ni 'mama ntilie''

JokaKuu
 
Mbona hawajakanusha sasa kuhusu uwepo wa nyufa? Porojo tu.....
 
Tanesco wanasema kuna watalaam kutoka ndani na nje ya nchi waliobobea! Hili linatusaidiaje kujibu swali.
Mradi umefikia 92 %, hivi hizi si namba tu mtu anaweza kusema, je zinaeleza ubora wa kazi

Ukisoma barua nzima, kwanza imeandika katika ubora hafifu sana

Maudhui ya barua anaonyesha kuna kitu kinafichwa! na swali linabaki pale pale, je kuna nyufa?

Ili kufanya damage control iliyotokana na barua , mkurugenzi akiwa na contractor na consultant wafanye press conference. Kuna tatizo ima la nyufa aua mawasiliano lakini kuna tatizo linafichwa.

Kuna tatizo linafichwa

Pascal Mayalla JokaKuu
 
Huu ufa ni mkubwa sana.. watoe maelezo vizuri..
5BC00105-F4D7-4DC0-A1BE-BD78F089D992.jpeg
 
Tanesco wanasema kuna watalaam kutoka ndani na nje ya nchi waliobobea! Hili linatusaidiaje kujibu swali.
Mradi umefikia 92 %, hivi hizi si namba tu mtu anaweza kusema, je zinaeleza ubora wa kazi

Ukisoma barua nzima, kwanza imeandika katika ubora hafifu sana

Maudhui ya barua anaonyesha kuna kitu kinafichwa! na swali linabaki pale pale, je kuna nyufa?

Ili kufanya damage control iliyotokana na barua , mkurugenzi akiwa na contractor na consultant wafanye press conference. Kuna tatizo ima la nyufa aua mawasiliano lakini kuna tatizo linafichwa.

Kuna tatizo linafichwa

Pascal Mayalla JokaKuu

..Na mradi ukifika 92% maana yake kazi zote kubwa zimeshafanyika, kilichobaki ni marekebisho ya hapa na pale.
 
..Na mradi ukifika 92% maana yake kazi zote kubwa zimeshafanyika, kilichobaki ni marekebisho ya hapa na pale.
Kwa maana kilichobaki ni kuangalia mifumo kama ya maji taka, maji safi, umeme, barabara za kuzunguka mradi n.k.

Kazi kubwa ya tuta, bwawa na mitambo imekamilaika. Hizi nyufa zipo? Mbona Tanesco wanatoa hadithi badala ya habari? Kuna kitu kinafichwa lakini ni suala la muda tu.

Tanesco wakumbuke mkataba wa Bandari ulikuwa katika makaratasi seuse nyufa kama zipo
 
Kwa hiyo hizo nyufa zinazosemwa zipo au hazipo maana taarifa haijazigusia hizo na ndiyo concern ya watu
Yaani kuwe na nyufa na lita bilioni 14 nyufa zihimili??? huo ni uzito mkubwa sana kama nyufa zingekuwepo ni dhahiri lingepasuka....
 
Dalili za mvua ni mawingu.. Hao wanaoitwa watalam nawafahamu vilivyo
Labda uniambie kama hizo nyufa zipo kama sehemu ya ujenzi ama kuna tatizo mahali?
Kumbuka kabla ya kujazwa maji hakukuwa na ufa wowote.. Hizi nyufa zilizoanza kuonekana je zitaishia hapo? Na zikiendelea je? Unayajua madhara yake!?
Daily tuna watu wako site na wanatueleza yanayoendelea huko! Hivi hujiulizi ni nani kavujisha hili la nyufa? Unadhani ni mtu wa kutoka nje?
Na je unajua kuna nyufa za aina ngapi? Mradi haujaanza tayari kuna tatizo limeonekana na bado baadhi yenu mnashupaza shingo kulitetea.. [emoji848][emoji2827]

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu achana na hao matade wameshavimbiwa na asali ndio sababu wanaropoka ovyo
 
Doto awe mkali na hawa jamaa vinginevyo watamchezea sana..

Tunashukuru ile kauli yake "watanzania wanataka umeme"..tangu aseme hayo maneno huku tuliko sisi umeme tangu walivorudisha jumamosi usiku hawajakata tena hadi sasa..
 
Back
Top Bottom