Tanga: Afisa Upelelezi ashikiliwa na Polisi kwa kudaiwa kuwaachia huru Watuhumiwa wa uhujumu uchumi

Tanga: Afisa Upelelezi ashikiliwa na Polisi kwa kudaiwa kuwaachia huru Watuhumiwa wa uhujumu uchumi

Ni huko Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga.

Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Mkinga amewatorosha watuhumiwa wa uhujumi uchumi na hawajulikani walipo.

Kwa mjibu wa mkuu wa Mkoa wa Tanga Afisa huyo wa Polisi alidai alipewa maelekezo ya kuwaachia huru watuhumiwa wale na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Tanga.

Afisa huyo amewekwa mahabusu kwa hatua zaidi.

View attachment 2361782
Daaah
Mungu anatupigania, wasiofaa wanaanza kujitokeza kabla hata hakujakucha
 
Ni huko Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga.

Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Mkinga amewatorosha watuhumiwa wa uhujumi uchumi na hawajulikani walipo.

Kwa mjibu wa mkuu wa Mkoa wa Tanga Afisa huyo wa Polisi alidai alipewa maelekezo ya kuwaachia huru watuhumiwa wale na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Tanga.

Afisa huyo amewekwa mahabusu kwa hatua zaidi.

View attachment 2361782

Huyu jamaa mvi zake zimeenda wapi?


 
Uhujumu uchumi ndio nini? Nyie walipisheni kodi waachieni na mizigo yao wakauze maisha yaendelee,
Mkitaifisha hiyo mali mnaenda kuuwa na kulostisha watu wengi sana,
Matokeo yake ni panya kuzaliana
Mambo mengine ni hekima inahitajika tu
 
Ni upigaji tu...
👇
=====

Mkinga. Ofisa upelelezi wa Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, anashikiliwa na Polisi kwa madai ya kuwaachia huru watuhumiwa wa uhujumu uchumi.

Watuhumiwa hao wanadaiwa kukamatwa na mali za magendo zenye thamani ya zaidi ya Sh1.2 bilioni.

Hayo yalisemwa juzi na Mkuu wa Mkoa Tanga, Omary Mgumba alipokuwa akitoa taarifa ya ziara yake ya kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Serikali na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa kuhusu hatua zilizochukuliwa kwa watuhumiwa 24 waliokamatwa na magendo ya vitenge.

Mgumba alisema alishangazwa na hatua hiyo na alipofanya kikao na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, ndipo alibaini aliyewaachia huru watuhumiwa ni ofisa upelelezi wa Wilaya Mkinga aliyedai kupokea maelekezo kutoka kwa ofisa upelelezi wa mkoa (bila kutaja majina).

Alisema tayari ofisa huyo amekamatwa na yuko mahabusu uchunguzi unaendelea na ukikamilika hatua nyingine za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

“Nimshukuru Kamanda wa Polisi Mkoa Tanga, baada ya kuona yametokea makosa haraka alichukua hatua ya kumuweka ndani na hatua nyingine zitafuata,” alisema Mgumba.

Akizungumzia hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa Tanga, Sophia Jongo alisema amepokea maagizo kutoka kwa mkuu huyo wa mkoa na anaendelea kuyafanyia kazi.

Chanzo: Mwananchi
 
Sasa kosa lake ni lipi hapo? Si kila mtu anapokea maagizo kutoka Kwa wa juu yake?

Hebu tulete katiba mpya tuweke mifumo mipya ya taasisi zote kuondoa huu upumbavu wa maagizo, kila kitu kifuate sheria na katiba tu na siyo utashi wa mtu.

Kwahiyo Sasa mnaowalaumu Polisi ndio mjifunze hapa wao huwa wanapewa maagizo tu.
 
Sasa kosa lake ni lipi hapo? Si kila mtu anapokea maagizo kutoka Kwa wa juu yake?

Hebu tulete katiba mpya tuweke mifumo mipya ya taasisi zote kuondoa huu upumbavu wa maagizo, kila kitu kifuate sheria na katiba tu na siyo utashi wa mtu.

Kwahiyo Sasa mnaowalaumu Polisi ndio mjifunze hapa wao huwa wanapewa maagizo tu.
Ulimaliza la saba ?
 
Alipokea maagizo toka juu,kwa namna nyingine,alitakiwa kutekeleza, asingetekeleza, ina maana angekua termed as MUASI. Muhimu asije kufa katika hali ya kutatanisha, ikasemwa amejipiga risasi au kajinyonga, halafu wapewe kazi ya kufanya uchunguzi HAOHAO.
 
ukimsikiliza mh DC ni kama analalamika kapigwa mgao[emoji23][emoji23][emoji23]

hii ni kwa waliohitimu cuba tu.eti hii case mh anaijua yaani anajaribu kishtaki.
Ni RC huyo unayesema analalamikia mgao..... Hahahaha.
 
Sasa kosa lake ni lipi hapo? Si kila mtu anapokea maagizo kutoka Kwa wa juu yake?

Hebu tulete katiba mpya tuweke mifumo mipya ya taasisi zote kuondoa huu upumbavu wa maagizo, kila kitu kifuate sheria na katiba tu na siyo utashi wa mtu.

Kwahiyo Sasa mnaowalaumu Polisi ndio mjifunze hapa wao huwa wanapewa maagizo tu.
kuweka mambo sawa na huyo aliyetoa maagizo akamatwe na kuwekwa ndani asionewe mmoja tu hapana.kwa kweli katiba ni muhimu ku leverage mambo haya.
 
Ni upigaji tu...
👇
=====

Mkinga. Ofisa upelelezi wa Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, anashikiliwa na Polisi kwa madai ya kuwaachia huru watuhumiwa wa uhujumu uchumi.

Watuhumiwa hao wanadaiwa kukamatwa na mali za magendo zenye thamani ya zaidi ya Sh1.2 bilioni.

Hayo yalisemwa juzi na Mkuu wa Mkoa Tanga, Omary Mgumba alipokuwa akitoa taarifa ya ziara yake ya kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Serikali na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa kuhusu hatua zilizochukuliwa kwa watuhumiwa 24 waliokamatwa na magendo ya vitenge.

Mgumba alisema alishangazwa na hatua hiyo na alipofanya kikao na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, ndipo alibaini aliyewaachia huru watuhumiwa ni ofisa upelelezi wa Wilaya Mkinga aliyedai kupokea maelekezo kutoka kwa ofisa upelelezi wa mkoa (bila kutaja majina).

Alisema tayari ofisa huyo amekamatwa na yuko mahabusu uchunguzi unaendelea na ukikamilika hatua nyingine za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

“Nimshukuru Kamanda wa Polisi Mkoa Tanga, baada ya kuona yametokea makosa haraka alichukua hatua ya kumuweka ndani na hatua nyingine zitafuata,” alisema Mgumba.

Akizungumzia hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa Tanga, Sophia Jongo alisema amepokea maagizo kutoka kwa mkuu huyo wa mkoa na anaendelea kuyafanyia kazi.

Chanzo: Mwananchi
Tukisema samia anafungua nchi kwa fisadi kuna hawatuelewi. Hebu niulize swali. Afisa upelelezi wa wilaya anatoa wapi ujasiri wa kuwaachia wafanya magendo wakubwa wengi hivyo kwa pamoja? Ingekua ni enzi ile ya jpm usingeweza ona au kusikia kitu kama hicho.
Tatizo mama kajibainisha kama mtu wa ufisadi pale aipoanza kumpiga vijembe jpm na kisha kuwaambia vigogo kila mmoja ale kwa urefu wa kamba yake.
Hima hima wandugu 2025 tusake magufuli mpya.
 
Tukisema samia anafungua nchi kwa fisadi kuna hawatuelewi. Hebu niulize swali. Afisa upelelezi wa wilaya anatoa wapi ujasiri wa kuwaachia wafanya magendo wakubwa wengi hivyo kwa pamoja? Ingekua ni enzi ile ya jpm usingeweza ona au kusikia kitu kama hicho.
Tatizo mama kajibainisha kama mtu wa ufisadi pale aipoanza kumpiga vijembe jpm na kisha kuwaambia vigogo kila mmoja ale kwa urefu wa kamba yake.
Hima hima wandugu 2025 tusake magufuli mpya.
Siyo kwamba enzi za Magufuli kulikuwa hakuna uovu bali uovu mkubwa ulikuwa unafanywa na yeye mwenyewe na watu wake.

Mfano alipoingia Gereza la Butimba Mwanza na kuamuru wale walioshikwa na dhahabu waachiliwe.

Tumia akili unapoandika, Wacha kumuabudu Mwendazake
 
Tukisema samia anafungua nchi kwa fisadi kuna hawatuelewi. Hebu niulize swali. Afisa upelelezi wa wilaya anatoa wapi ujasiri wa kuwaachia wafanya magendo wakubwa wengi hivyo kwa pamoja? Ingekua ni enzi ile ya jpm usingeweza ona au kusikia kitu kama hicho.
Tatizo mama kajibainisha kama mtu wa ufisadi pale aipoanza kumpiga vijembe jpm na kisha kuwaambia vigogo kila mmoja ale kwa urefu wa kamba yake.
Hima hima wandugu 2025 tusake magufuli mpya.
Kwani unafikiri wakati wa jpm watu walikuwa hawapitishi magendo kwa njia za pwani
Watu walikuwa wanakamatwa na wanamalizana na polisi

Ova
 
Back
Top Bottom