Tanga ilitakiwa uwe mkoa wa pili kwa uchumi baada ya Dar Es Salaam

Tanga ilitakiwa uwe mkoa wa pili kwa uchumi baada ya Dar Es Salaam

Correction.

Ulitakiwa kuwa hata wa Kwanza kiuchumi.

Ukifuatilia Dar ni port city tu kama mombasa. Ila haina natural advantage yoyote nyingine, si rasilimali wala hali ya hewa iliyoifanya kuwa kubwa zaidi ya serikali kuirundikia vitu vyote haswa kiutawala.

Tanga ilikuwa na reli, viwanda, mkonge, mpaka na kenya na pia ipo karibu zaidi na Uganda kuliko dar..

Ina ardhi nzuri ya kilimo, bandari na vivutio vya utalii kama ambani, saadani etc

Kiufupi Dar ni mji uliotengenezwa na Serikali. Nimeshukuru kuona Dodoma imechukuliwa serious, japo ni pakame lakini pataleta decentralization
Ukiwa vizuri kiuchumi Tanga ni mahali pazuri Sana Kwa kuishi.
 
Correction.

Ulitakiwa kuwa hata wa Kwanza kiuchumi.

Ukifuatilia Dar ni port city tu kama mombasa. Ila haina natural advantage yoyote nyingine, si rasilimali wala hali ya hewa iliyoifanya kuwa kubwa zaidi ya serikali kuirundikia vitu vyote haswa kiutawala.

Tanga ilikuwa na reli, viwanda, mkonge, mpaka na kenya na pia ipo karibu zaidi na Uganda kuliko dar..

Ina ardhi nzuri ya kilimo, bandari na vivutio vya utalii kama amboni, saadani etc

Kiufupi Dar ni mji uliotengenezwa na Serikali. Nimeshukuru kuona Dodoma imechukuliwa serious, japo ni pakame lakini pataleta decentralization
Uko sahihi kabisa mku
 
Tanga ni mkoa wa 5 kwa uchumi na uchumi wake hauja tofauti ana sana na mkoa wa 4 kiuchumi (Arusha), imepitwa na Dar, Mwanza na Mbeya.

Mikoa iliyoipita Tanga Mbeya na Mwanza ni mikoa ambayo kwenye kanda zake inategemewa, Mwanza inabeba Uchumi wote Wa lake zote, na Mbeya Uchumi wa Kusini.

Kwa situation ya sasa ni fair, kwa hio position ya Tanga, ila ni kweli inaweza fanya vizuri zaidi, tatizo kubwa ni serikali kutopeleka Bajeti ya kutosha, Ukiangalia Bajeti ya jiji la Tanga na kiasi inachoingiza kwenye pato la Taifa ni mbingu na Ardhi, hio barabara tu ya Tanga - Dar kila siku tunapewa promise haijengwi.
Tanga inanyonywa na Dar pamoja na Arusha ,bandari inapigwa chini kwa vile ya Dar iko promoted sana kama ingekuwa serikali ina maono mapana basi ingekuwa inapambana na ya Mombasa...Katika shughuli za kiserkali imepokwa na Arusha kwa sababu Arusha ndio makao makuu ya kaskazini so zile regional offices kubwa za taasisi zote ziko Arusha hata kama bandari ingekuwa inahamishwa wangepeleka Arusha ...Kiufupi hakuna hata ofisi kubwa moja zote ziko Arusha.

Better Tanga ijitoe ukanda wa kaskazini ili iwe huru.
 
Tanga inanyonywa na Dar pamoja na Arusha ,bandari inapigwa chini kwa vile ya Dar iko promoted sana kama ingekuwa serikali ina maono mapana basi ingekuwa inapambana na ya Mombasa...Katika shughuli za kiserkali imepokwa na Arusha kwa sababu Arusha ndio makao makuu ya kaskazini so zile regional offices kubwa za taasisi zote ziko Arusha hata kama bandari ingekuwa inahamishwa wangepeleka Arusha ...Kiufupi hakuna hata ofisi kubwa moja zote ziko Arusha.

Better Tanga ijitoe ukanda wa kaskazini ili iwe huru.
Uko sahihi ila tanga nusu ipo kaskazini,Lushoto,korogwe,kilindi, nusu ipo pwani,tanga muheza,oangani,handeni,shida iko hapo,makai makuu yamkoa yangekuwa lushoto mkoa ungekuwa mbali,hata kitabia watu walushoto ni wapambanaji kuliko tanga mjini
 
Ukiangalia Bajeti ya jiji la Tanga na kiasi inachoingiza kwenye pato la Taifa ni mbingu na Ardhi, hio barabara tu ya Tanga - Dar kila siku tunapewa promise haijengwi.
Wadaini wabunge wenu...
 
Sijui ndugu mwandishi unaongelea Tanga as mkoa au Tanga as mji, kwa Tanga as mji ni mji ulianza tangu mwaka 1890 wajerumani walipo ingia, Mji wa tanga ulipata hadhi ya kuwa manispaa tangu 1930, tokea hapo tanga ulikuwa mji kimbilio na namba moja kwa uchumi tanganyika mpka tunapata uhuru, mji wa tanga uliumbwa kwa mfumo wa capitalistic town, yaan walikuwepo watu na kampuni nyingi zenye nguvu ambazo ziliubeba uchumi, nani haikumbuki amboni na product zao kama ndoo za amboni na ndala za umoja? Uchumi wa kikapitalisti ulileta watu wengi tanga ili kufanya kazi, mji ulikuwa na mkoa ulikua miaka ya 70 mpka 80 sera za mwalimu nyerere ndio ziliua mji wa tanga na uchumi wake, azimio la arusha ndio lilimaliza kabisa uchumi wa pale, isingekuwa rahisi mji wenye uchumi wa mtu mmoja na makampuni ghafla ubadili upeo uwe mji wa kijamaa, walowezi wote waliikimbia tanga kwenda kenya, uingeleza na marekani, tanga kwa sasa uwekezaji una rudi taratibu, uchumi wa pale utakua, saivi wageni ni wengi, wenyeji siku zote huchelewa kujua kukimbizana na uchumi, ila soon uchumi wa kikapitalisti uta take over, sasa hivi wafanya biashara wenye asili ya ki asia wameanza jenga majengo marefu mjini, nina jamaa angu eng. Kwa mara ya kwanza ana tenda tanga ya kujenga jengo la orofa 10 pale mjini, jengo la wahindi, wale jamaa walinyang'anywa majengo yao yote mijini na sera ya kutaifisha, sekta ya ujenzi nayo huchangia uchumi
 
Mkoa umebarikiwa kila kitu
Sijui wagosi wanafeli wapi
Yaani Hako kabandari ndio Kila kitu?

Tanga inatakiwa kuwazidi kina Arusha na Mikoa dhaifu mingine kama Singida.

Ila Tanga haiwezi na haitakuja kupita Mwanza,Mbeya au Morogoro
 
Back
Top Bottom