Tanga: Milioni 21 waliyoiomba Wazee kwa ajili ya Tambiko yakwamisha Ujenzi wa Barabara

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Hii ndio Taarifa mpya kutoka Kijiji cha Kwa Msisi Mkoani Tanga ambapo imeombwa kwanza hela ya Tambiko mil 21 ili ujenzi wa barabara unaohusisha ukataji wa miti uendelee.

Tambiko la pili litafanyika baada ya barabara hiyo kukamilika ambapo wazee watafanya dua maalum. Juhudi za Mkuu wa Wilaya kuomba punguzo zinaendelea.

Habari kamili hii hapa

Your browser is not able to display this video.
 
Hii nchi tunaelekea pabaya sana aisee.

Tunafikia hatua ya kuamini mambo ya kishirikina hadi kutumia mamilioni ya wananchi kuyapeleka milima korelo?
 
sasa hawa wazee si wafanye tambiko barabara ipite juu ya miti yenyewe, wafanye tena tambiko lingine kijiji chao kiwe kama malaga spain vile..
[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Yaani watu wanacheleweshewa maendeleo eti kisa tambiko....sasa hayo matambiko yao yangekuwa na maana sitayari wangukuwa na barabara zao wenyewe tangu zama za kale...hayo matambiko na mizimu ingekuwa na msaada wote hao wazee wasingekuwa wamechoka hivyo na kuvaa manguo yamechanika.....DC acha story na hao watu peleka watu waanze kazi tena ikiwezekana peleka JWTZ kabisa hapo wajenge hiyo barabara... kila tukikwama tembezeni kipigo..
 
Ndio maana kuna wakati tunasema hakuna demokrasia kwa mpumbavu, ona sasa watu wanakosa barabara eti kisa tambiko na mizimu..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…