Tanga: Mjamzito adaiwa kufa baada ya kuwekewa damu kimakosa, Watano wasimamishwa kupisha uchunguzi

Tanga: Mjamzito adaiwa kufa baada ya kuwekewa damu kimakosa, Watano wasimamishwa kupisha uchunguzi

Kuna muda unampeleka mgonjwa wako hospital ila ukifika ule wakati daktari anakwambia hebu tupishe tumfanyie vipimo mgojwa unatamani umkatalie ubaki ukitazama ili ukiona walakini umuulize maswali ya msingi kwamba nini kinaendelea hapo, kwann unampa hiyo dawa, kwann unafanya hicho?

Maana madaktari na wauguzi wa sasa wamekuwa kama fundi shabani ukimuachia gari yako inakuwa ndio mwanzo wa magonjwa yasiyokuwa na mwisho.
 
M

Mkuu hata kama Una HIV huwezi kuwekewa damu ya mtu mwenye HIV
Zamani walikuwa wanaleta huo upuuzi ila siku hizi sababu umakini wa vipimo hizo kesi zimepungua. Ila hayakosekani majitu mazembe ambayo yanafanya kazi utadhani yalilazimishwa, anaweza pima damu juu juu au akachanganya vitendea kazi akakuchoma vyenye contamination ya virus.
 
Watumishi watano wa Kituo cha Afya cha Mikanjuni kilichopo Jijini Tanga wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi baada ya kufanya uzembe uliosababisha kifo cha Mama mjamzito Fatuma Mussa Suleiman (36) Mkazi wa Magaoni, aliyefariki baada ya kuwekewa damu ambayo hakustahili kupewa na hakuwa na uhitaji nayo kwa wakati huo.

Mkuu wa Wilaya ya Tanga, James Kaji amesema kuwa Mama huyo alilazwa katika Kituo cha Afya Mikanjuni March 27, 2204 saa kumi alfajiri kwa tatizo la uchungu ambapo damu aliyowekewa Marehemu ilikuwa ni ya Mgonjwa mwingine ambaye alikuwa amelazwa kwenye kituo hicho akipatiwa matibatu ambapo baada ya kupatiwa damu hiyo Fatuma alianza kuonesha dalili za Mtu mwenye mzio mkali (Allergic reaction) kisha akafariki.

Watumishi hao waliosimamishwa kazi kupisha uchunguzi ni pamoja na Wauguzi watatu Fadhila Ally Hozza aliyekuwa zamu ya mchana, Restitua Kasendo Deusdedit na Muya Ally Mohamed walioingia zamu ya usiku na pia Madaktari waliomfanyia upasuaji Andrew Eliasikia Kidee na Hamis Mohamed Msami.

“Mgonjwa alifanyiwa upasuaji ambapo alifanikiwa kupata Mtoto wa kike wa kilo 3.4 na hakuwa na changamoto yeyote na baada ya upasuaji na aliendelea kupatiwa matibabu chini ya uangalizi wa Wauguzi na Madaktari wa zamu, katika wodi aliyokuwa amelazwa marehemu kulikuwa na mgonjwa ambaye alikuwa anahitaji kuwekewa damu na damu yake ilikuwa tayari imeandaliwa, Muuguzii aliyekuwa zamu alimuwekea Marehemu damu ambayo hakustahili kupewa na hakuwa na uhitaji huo, baada ya kuwekewa damu marehemu alipatwa na mzio mkali (Allergic reaction) iliyopelekea kifo chake”
Umakini mdogo sana, unachezaje na afya ya mtu aisee?
 
Selian ni hospitali nzuri na pia na shauri wkwa tanga ni ile ya mkoa wa jitahidi sana kuwa wasafi na ninzuri
 
Kuna madokta hawapo makini katika kazi zao, especially mikoani
I think Kosa sio La daktari Kosa ni umakini wa Manesi na kuchanganya Mafailu ya Wagonjwa..
Daktari anaandika but anayemuhudumia mgonjwa ni mwingine..

But hakukuwa na Njia yoyote ya kumsaidia hata kama wangetaka Reaction ikishaanza imeanza and hence Death
 
Duh nimeumia sana,Roho isiyo hatia imedhurumiwa,hawa matabibu wetu wanashida kubwa sana,unakuta anahudumia mgogwa utadhani wana ugomvi,hata askari magereza hawezi kuwa katili hivyo kwa mfungwa,sasa vipi hawa tabibu wetu?

Yaani hawako communicative kabisa,kumsaili mgonjwa,kumuuliza unasumbuliwa na nini ,vipi hali yako,hawawezi ,unafika ku kutundika drip ya damu bila usaili kwa mgonjwa wakati mgonjwa yuko katika hali nzuri ya kuzungumza.

Walaniwe wote waliohusika na uhuni huu.
 
Back
Top Bottom