Tanganyika iiombe radhi Zanzibar?

Tanganyika iiombe radhi Zanzibar?

Tanganyika hatuna la kupoteza muungano ukivunjika ila Zanzibar watapoteza bajeti, nafasi tele za uteuzi, biashara, ajira nyingi, na mali nyingi ikiwemo ardhi wanazomiliki huku bara.
Wazanzibar washalalmika sana kuwa Watanganyika wanawazibia vingi!

1. Nafasi za ubalozi

2. Uhuru wa kukopa

3. Haki ya kujiunga katika taasisi na jumuia za kimataifa kama OIC

Kwa kiasi kikubwa, Zanzibar inaiona Tanganyika kama kikwazo kikubwa sana kwa ustawi wake.
 
Wazanzibar washalalmika sana kuwa Watanganyika wanawazibia vingi!

1. Nafasi za ubalozi

2. Uhuru wa kukopa

3. Haki ya kujiunga katika taasisi na jumuia za kimataifa kama OIC

Kwa kiasi kikubwa, Zanzibar inaiona Tanganyika kama kikwazo kikubwa sana kwa ustawi wake.
Ni kinyume na hayo. Zanzibar wamekuwa kupe mkubwa kwenye mgongo wa Tanganyika. Mwisho wa ukupe huo ufike sasa.
 
Ni kinyume na hayo. Zanzibar wamekuwa kupe mkubwa kwenye mgongo wa Tanganyika. Mwisho wa ukupe huo ufike sasa.
Lakini ujue wanaoulinda Muungano kwa nguvu ni Watanganyika walio kwenye nafasi za uongozi.
 
Yawezekana hata hapo ulipo upo bara muungano ndio dili kubwa kwa wanzanzibari chungeni usivunjike.
Mimi sipo "bara", nipo Tanganyika.

Mimi ni Mtanganyika Halisi. Hata Zanzibar kwenyewe nilishaenda mara Moja tu.

Mimi ni Mtanganyika ninayeidai Tanganyika yangu.

Nawapenda Wazanzibar kwa sababu ni ndugu zetu, lakini turudishiwe Tanganyika yetu!
 
Tanganyika hatuna la kupoteza muungano ukivunjika ila Zanzibar watapoteza bajeti, nafasi tele za uteuzi, biashara, ajira nyingi, na mali nyingi ikiwemo ardhi wanazomiliki huku bara.
Lakini pamoja na yote hayo, hawatuthamini kabisa. Wanatuona mabwege mtozeni tu. Hawataki kabisa nasaba na sisi. Angalau kwa maswahiba wao wa pwani.

Hivyo inayumkinika kabisa kwamba Tanganyika ndiyo inayolazimisha muungano huu. Nyerere was shortsighted on this strategic blunder. Sijui lengo lake lilikuwa nini hasa kulazimisha muungano wa aina hii - lopsided (muungano wa serikali mbili?)
 
Kwahiyo waingereza waliogopa kupigwa na Nyerere wakageuza meli?

Vyovyote ilivyo, suala la kuongelea kuvunja muungano si busara especially baada ya miaka 60 toka tuungane. Busara ni kujadili kero zilizopo kwa haki na kuzitatua kwa haki kila upande ukawa umeridhika.

Wenye akili ndogo tu ndo watang'ang'ania kuvunja muungano kwa hapa tulipofika.
Honestly speaking, tuache unafiki na ubabaifu. Huo muungano hauna kero yoyote; bali ni MBOVU, period. Zaidi ya kujadiliana (to negotiate) kuwa na serikali moja tu, mengine yote ni UBATILI mtupu.

Aidha, muungano lazima uwe na lengo la kimkakati. Miaka yote 60 lengo la muungano huu “halijadiliki”; ni “siri”; ni “nyeti”; limefunikwa na kivuli cha kutisha na kufisha cha Mwalimu JKN kinacholindwa na wakuu wa CCM wasio na maadili. Ukweli ni kuwa maradhi hayafichiki milele. Tusubiri kilio tu. Na bado.
 
Sii kweli!, baada ya yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Manowari za Uingereza zilitia nanga Mombasa tayari kuivamia Zanzibar, kuikomboa. Karume akaja kwa Nyerere kuomba ulinzi, ndipo, Nyerere akamshauri Karume tuungane kuwa nchi moja, Karume akajibu hata leo, wewe Rais mimi Makamo.

Sii kweli, huo ni uongo wa wapinga Mapinduzi Matukufu, ukweli ni huu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar: Kumbe Waarabu Hawakufukuzwa! Walikimbia Wenyewe - Mzee Sukari

Sii kweli

Sii kweli

Sii kweli, Zanzibar ilikuwa sehemu ya Tanganyika kabla haijamegeka!. Hivyo ni sehemu yetu kihalali kabisa!.

Sii kweli

ni kweli ila mengine ni ya kweli, mengine ni ya uongo!

Si kweli

Na kama ni uongo?.

Uungwana ni vitendo ni kweli kuna ndivyo sivyo

Naunga mkono hoja na hata mimi hili nilishauri Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja

Hapa tuko pamoja.
P
Kwamba kuunganisha nchi na nyerere kubakia kuwa Rais ndo kulizui manowari za uingereza kuivamia Zanzibar?
 
Kuwapa uhuru wao!?? Ambaye hana uhuru si huwa anaudai au kuupigania? Waliwahi kuudai?

Zanzibar wakiambiwa wajitegemee, hata mwaka hauiishi, wataanza kutaka mwungano uvunjike. Lakini kwa sasa, wakati huu wanaoutunzwa na bara, hawawezi kuthubutu kutaka mwungano uvunjike.
Wakianza kuudai bara wanaenda kuwakamata wahusika
Umesahau masheikh wa uamsho?
Si bara iliwafunga kisa kudai Zanzibar huru?
 
Hahahahajaj inashangaza kweli, hawasemi ila ukweli ni kwamba mwingereza alikua stand by kusaidia iwapo zanzibar wangekataa au marafiki wangesaidia kukataa muungano
Zanzibar ilikuwa Hadi na Sarafu yake
Leo hi iko wapi?
Aah au Basi mengine ni machungu hata kuyasema .
 
Tulichofundishwa shuleni kuhusu Muungano, ni tofauti na ninayoyasikia Sasa!

Inasemekana, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar haikuwa takwa la wananchi, bali la Karume na Nyerere, lakini zaidi, Nyerere.

Inasemekana, hata yale yanayoitwa Mapinduzi Tukufu ya Zanzibar, yalikuwa ni mauaji katili, na yaliratibiwa na kusaidiwa, kwa sehemu kubwa, na Tanganyika. Hata silaha zilizotumika kwenye mapinduzi zilitoka Tanganyika.

Inasemekana, mapinduzi hayakulenga kumwondoa Mwarabu, bali Serikali halali kwa lengo la kukiweka madarakani Chama kilichokuwa kikiungwa mkono na Tanganyika.

Inasemekana, tokea mfumo wa Vyama vingi uanze, chama kinachoungwa mkono na Tanganyika kimekuwa kikishinda uchaguzi bila ridhaa ya wapiga kura. Kwamba kishinde kisishinde, lazima kiingie madarakani, maadam tu kinaungwa mkono na Tanganyika.

Inasemekana, hata huu Muungano uliopo kwa sasa si Muungano bali ni Ukoloni. Kwamba Tanganyika inaitawala nchi nyingine kimabavu.

Inawezekana, kama Zanzibar ingekuwa na uwezo, ingeshajitoa kwenye Muungano. Kuenedelea kwake kuwepo kwenye Muungano ni kwa sababu tu inalazimishwa na Tanganyika.

Yameshasemwa mengi na kuandikwa mengi.

Uungwana ni vitendo. Ikiwa hayo yote yanayosemwa ni kweli, basi Zanzibar wana haki ya kuulakamikia Muungano.

Kama ni kweli, nini kifanyike?

Mosi, Tanganyika iiombe radhi Zanzibar kwa yote inayoamini imeitendea Zanzibar ndivyo isivyo, na kwa yale ambayo Zanzibar inailalamikia.

Pili, kura ya maoni iitishwe kwa wananchi wa nchi ya Tanganyika na Zanzibar kuamua juu ya mustakabali wa Muungano.

Tatu, maamuzi ya wananchi yaheshimiwe.
Hivi ni ajali raia wa nchi jirani kuongoza nchi ya Tanganyika badala ya kubaki kiti cha umakamu madhali znz wana serikali kamili isiohusu nchi ya Tanganyika?
 
Back
Top Bottom