Tangazo la Haki Elimu linadhalilisha kada ya Ualimu

Hiyo leonel messi uko nchini kwake wanakitumia kingereza kama lugha rasmi?
si mnasema ni international language, sasa mtu anazaliwa usukumani, utotoni lugha anayoijua ni kisukuma tuu, akianza shule ya msingi ndio anajifunza kiswahili, baadae ndio aje kwenye kingereza


Tatizo wa bongo mnataka mtu aongee kingereza kama waingereza wakati siyo lugha mama yake, mmeshasikia kingereza cha wahindi? au mzungu akiongea kiswahili anaongea kama mtu wa pwani?
 
1. Which country has the most teachers in the world?
Vs
2. Which country has most of the teachers in the world?

Which sentence? Or which of those sentences is correct?
Hizi sentensi zote zinaweza kuwa sahihi kama grammar ndio mada iliyopo mezani japo kwa sentensi ya pili bado na mashaka nayo

Nasema hivyo kwa sababu katika sheria za matumizi ya articles, nadhani katika most of the teachers,article 'the' siyo lazima kuwepo.Hapa tunaongelea walimu kwa ujumla.Kwahiyo kama ni hivyo, rule ya article 'the' inazuia matumizi yake kwa count na non count nouns linapokuja jambo la ujumla

Again,sentensi zote zinaweza kuwa na changamoto kama semantics ndio kigezo kitatumika.
 
Hii kada wanaidharau sana mbona uo mzaa hawaufanyi katika kada zingine
 
Wako sahihi, Kuna mwalimu mwenzangu hapa nafundisha naye, kasoma kiswahili na kingereza, ukimuuliza anakwambia yeye hawezi kufundisha kiswahili, anapenda kufundisha kingereza

Njoo kwenye kingereza chenyewe Sasa, unaweza mtandika Kofi, siku moja alikuwa zamu, akawa anajaza daftari la zamu, Sasa nikawa nalipitia maana zamu yake na yangu zinafuatana, na daftari hujazwa kwa kingereza, unaweza tamani dunia ishuke, kwenye TEACHER'S REMARKS: yeye kaandika " the day it did well" sasa hiki ni kitu gani

Haki elimu wako sahihi.
 
Mi headmaster wangu advance amewahi kusema " your parents gives you money and you give to sister sisters and buying pleasures metals you don't pay school fees"

Akimanisha wazazi wanatupa ada badala tulipe ada tunahonga wasichana na kununua viito vya thamani
 
Wewe unataka kukuza mada tu, kuna watu na digrii 3 wameshindwa na wakatetewa kwamba kiingereza siyo muhimu, halafu wewe unaongelea walimu?
Mfano mwingine kingereza sio kipimo cha kuwa na akili angalia wachina hawajui kingereza na hawana mpango wa kukikuza lakini angalia maendeleo Yao.

Halafu ukisema wanaoenda ualimu ni wenye daraja 3 na 4,hio ilikuwa zamani,mfano Mimi ni mwalimu mwaka wa 10 sasa,kidato cha sita nilipata division one, PCB.nafundisha SAYANSI A,LEVEL
kwa kingereza na kiswahili na watoto wanafaulu Sana.

Akili ya mtu haipimwi kwa kigezo cha kufahamu lugha peke yake.learn about principle of multiple intelligence
 
Okay homeboy thanks [emoji108]
 
Haki Elimi wako vizur sana, matangazo yao huwa hayachoshi Bila shaka ujumbe umefika vizur, haiwezkani ufundishwe lugja na asiyeijua vizur lugha yenyewe, nakumbuka Enzi za Kikwete washawahi pigwa ban eti wanaidhalilisha serikali
Hawa ban zilikuwa nje njee
Tatizo wanaikaba serekali kooni kwa mambo ambaya mamlaka inashindwa kuwekeza kikamilifu
 
Ukweriii ndio nini janja?
 
Na wale ni walimu kabisa wenye PhD wakiwakilisha walimu wote wenye bachelor degrees, diploma, na certificates!
Bongo raha sana kizungu ni janga la kitaifa ukimsikiliza tu Profesa Dr Ndalichako na Dr ******** na wengi wengi
 
Duh! Sasa mnamruhusu vipi afundishe .. maana watoto wanachukua toka kwake .!!!

Aisee..ndo baadae tunaongea "fent fod''
 
Tulishazungumza sana hapa! Kimalkia ni kigumu sana kwa mtoto wa Baba Jesika. Waalimu wengi, wanatoka shule zisizo na kipaumbele cha serekali.
 
"But bikoz of form one I going to use kiswahili"
 
Hivi yule ticha wa kwenye tangazo la haki elimu hazeeki tu? Jamaa nimeanza kumuona kitambo nikiwa mtoto wa miaka Kama 7-13 lakin yuko vilevile
 
Duh! Sasa mnamruhusu vipi afundishe .. maana watoto wanachukua toka kwake .!!!

Aisee..ndo baadae tunaongea "fent fod''
Sasa utakataa vipi wakati wote ni walimu, na aliyemthibitisha kuwa ni mwalimu ni serikali kwahiyo sisi hatuna mamlaka ya kum- disqualify, kidato Cha nne matokeo two ya mtihani wa taifa kulikuwa na A 0,B 0,C 3, D 12 na F 67
 
Kiongozi, hiyo ndio hali halisi ya elimu yetu, hali ni mbaya na ndipo elimu yetu imefikia hapo. Haki Elimu hawakurupuki, wanafanya utafiti na ku-dramatize matokeo ya tafiti zao.

Binafsi nimefanya utafiti kuhusu sababu za watoto wa sekondari, nimekutana na walioacha shule kwa sababu hawaelewi kitu darasani kwa kuwa hawaelewi lugha ya Kiingereza ambayo ndio lugha ya kufundishia.

Vv
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…