Tanzania imetimiza hatua zote 4 kuwa nchi ya kidikteta

Tanzania imetimiza hatua zote 4 kuwa nchi ya kidikteta

Udikteta ni relative.

Kuna wengine wanaweza kusema hata wewe ni dikteta ndani ya ACT-Wazalendo kwa sababu cheo chako hakina tofauti na Supreme Leader of Iran. Sayyid Ali Hosseini Khamenei

Acheni kulisha wananchi matango ya kisiasa.

Udikteta upi unaosema katika mazingira ya kuweza kusema serikali ya sasa inaongozwa na dikteta!

Udikteta siyo relative term. Hii revisionism yenu ya Chuo Kikuu cha Mlimani na maprofesa wake inawadanganya. Kisheria na Kisiasa Udikteta ni utawala wa kiimla katika ngazi ya kitaifa tu (No exceptions). Kwenye ngazi ya kichama huwaga hakuna udikteta...

Kumlinganisha Khomeni mwenye dola na Zitto ambaye hana dola ni ujuha wa hali ya juu sana. Chama ni chombo ambacho mtu anaweza kuamua kuwepo au kutokuwepo hivyo hakuwezi kuwa na udikteta kama mtu anaamua mwenyewe kuwepo, kama hukubaliani na chama unaruhusiwa kutoka. Taifa ni tofauti kabisa, hata usipokubaliana na watawala utakuwepo tu maana huna jinsi.Ndiyo maana tunasema udikteta ni hatari sana kwa taifa.....

Hili ni la mwaka wa kwanza Chuo Kikuu kwenye aina ya mifumo ya Utawala duniani. Waalimu wenu hawakuwambia kwamba Udikteta ni nadharia inayotumika kwenye ngazi ya kitaifa tu ???
 
Hilo baadhi yetu tumeshawaambia sana lakini wapi! Watu wenyewe hawajielewi.

Baadhi yetu hatuna shida na kuongozwa na ccm. Miaka hii yote tumeongozwa na ccm na hata kuichagua. Wametuongoza kwa kiwango cha kuridhisha. Ndiyo maana demokrasia iliendelea kushamiri nchini. Wala hatutamani sana siku moja ccm ishindwe; tunachotamani ni ushindani utakaopelekea wenye madaraka kujiheshimu na kuwaheshimu wapigakura. Wazee wa ccm tuko nao huku mtaani nao wanajuta. Wengi wao wanasubiri tu muda upite. Ila baadhi yenu mngependa sana uovu wote unaolalamikiwa uelekezwe ccm badala ya rais. No way. Kinachosababisha kelele hizi ni sera za ccm kutelekezwa na katiba ya nchi kusiginwa. Na aliyefanya haya yote ni mtu aliyepewa mamlaka za kifalme na katiba yetu tukidhani atatumia kwa manufaa yetu sote na mengine kajiongezea mwenyewe kinyemela kwa maslahi yake binafsi. Ndipo Mzee mmoja wa ccm akamtaka aache kujitukuza yeye mwenyewe na badala yake apeleke sifa na utukufu ccm! Je, amefanya hivyo? Sasa ccm inatoka wapi hapa? Pambaneni wenyewe; ccm msiingizi kwenye vita vyenu vya utukufu binafsi!
 
Dikteta huchukua hatua kadhaa kupandikiza utawala wa Imla - Zitto Kabwe

( Andiko la July, 2016 na uhariri kidogo 2018. Uhariri tena mdogo Jan, 2019 )

  1. Hupambana na Wafanyabiashara wakubwa ' matajiri ' ili kuweka matajiri wake wapya watakaokuwa msaada kwake. Rais Putin wa Russia alifanya hili vizuri sana alipochukua madaraka. Adolf Hitler yeye aliamua kuwaua wayahudi ( Jews ) kwani wakati huo Jews ndio walikuwa wanashikilia uchumi wa Ujerumani. Hapa kwetu Tanzania kwa miaka mitatu tumeshuhudia Wafanyabiashara wanakipata cha mtema kuni. Wafanyabiashara wakubwa na wadogo wanabambikiziwa Kodi na wakibisha wanapewa kesi zisizo na dhamana, wanatupwa jela, wananyanganywa Mali zao na wengine kufilisiwa.
  2. Huteua Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambao ni Watu wake wa Karibu. Rais Vladimir Putin yeye alifuta kabisa chaguzi za Magavana na akateua majenerali wa jeshi na watu wa KGB badala yake. Hapa Tanzania tumeshuhudia Wakuu wa Mikoa miungu Watu wenye kufanya lolote bila kuhojiwa na yeyote. Tumeshuhudia Wakuu wa Wilaya wakifunga watu bila kufuata sheria, wakinyanganya watu mali zao na kila aina ya vituko bila kuchukuliwa hatua.
  3. Hudhibiti vyombo vya habari. Rais Vladimir Putin alihakikisha TV zote zinakuwa za Serikali kwa kutaifisha TV binafsi na ilikuwa marufuku DUMA ( Bunge la Urusi) kuonyeshwa na ni yeye tu ndiye mwanasiasa aliyepaswa kuonekana kwenye TV. Hapa Tanzania Bunge limezuiwa kuonyeshwa moja kwa moja Lakini shughuli zote za Rais Magufuli zinaonyeshwa hata kwa masuala yasiyopaswa kuonyeshwa kama vile kusaini mikataba au mashauriano na Viongozi wa dini. Sheria ya Huduma za Habari nchini imeviweka vyombo vya Habari hatarini Katika kuchapisha au kutangaza Habari zao. Serikali imeweka kanuni za leseni ili kudhibiti kuwepo na kufanya kwao shughuli zao. Waandishi wanatekwa na kupotezwa kwa Mfano Azory Gwanda wa Gazeti la Mwananchi.
  4. Hudhibiti Vyama vya Siasa. Adolf Hitler wa alifuta vyama vyote Ujerumani. Vladimir Putin alizuia mikutano ya kisiasa na kuanzisha vyama vibaraka. Hapa Tanzania, kama tulivyotabiri katika makala Hii Mwaka 2016, “ Ndio mpango utakaofanywa Tanzania kwa kuanza na kuzuia mikutano ya vyama vya siasa. Sheria pia itabadilishwa na kuifanya nchi ya Chama kimoja pekee, CCM”. Hili limetokea kwa tarehe 29/1/2019 Bunge kutunga sheria ya mabadiliko ya sheria ya vyama vya Siasa na kumfanya Msajili wa Vyama kuwa Mdhibiti wa Vyama vya Siasa. Utekelezaji wa sheria mpya ya vyama vya siasa utapelekea ama vyama kutii maelekezo ya Serikali au kufutwa na hivyo CCM kuhodhi siasa za nchi.

Mtu yeyote mwenye akili timamu na mwenye kupata japo muda kidogo wa kujisomea anajua nini kinaendelea. Watu wasioona ama wana maslahi au uwezo wao wa kuona ni mdogo sana. Wengine wameamua tu kuvaa miwani za mbao. Wahanga wa Demokrasia wanajua maana ya haya tunayosema. Tanzania sasa imefunga duara ( Full Circle ) kwenye hatua Muhimu za nchi kuwa ya kidikteta.

Ni dhahiri kuwa Dunia ina madikteta wengi waliowahi kuwaletea wananchi wao maendeleo. Ethiopia. Malaysia. Singapore. Hata Rwanda. Tofauti yao na Sisi ni kwamba Madikteta wao ni wanazuoni wenye uwezo wa kutumia akili na utulivu kufanya maamuzi. Madikteta wao wanasoma vitabu na majarida ya uchambuzi wa sera. Rais Paul Kagame wa Rwanda hakosi Harvard Business Review. Meles alikuwa na akili Kama mchwa mpaka wazungu walikuwa wanamwogopa na kitu cha kwanza alichoomba kupewa Kama msaada ni ' vitabu vya uchumi'. Hata hivyo tunashuhudia Ethiopia ikifuta sheria kandamizi na kuelekea kwenye barabara ya Demokrasia baada ya kuona uimla haulipi.Lee Kuan Yew wa Singapore na Mahathir Mohammed wa Malaysia ni waandishi wazuri wa vitabu. Hawa sio too technical...... Ni Intellectuals.

Pamoja na kuwa hao niliowataja wanasoma na wenye MAARIFA Mengi, Bado udikteta haukuwasaidia sana na wengi wamebadilika na kuwa wana Demokrasia.

( last edit 30/1/2019 )
Pamoja na Demokrasia ya Ethiopia Mheshimiwa unajua kwasasa kwa jina la demokrasia kuna mauuaji makubwa ya raia yanaendelea Ethiopia.

'Thousands flee' Ethiopia ethnic conflict

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dikteta huchukua hatua kadhaa kupandikiza utawala wa Imla - Zitto Kabwe

( Andiko la July, 2016 na uhariri kidogo 2018. Uhariri tena mdogo Jan, 2019 )

  1. Hupambana na Wafanyabiashara wakubwa ' matajiri ' ili kuweka matajiri wake wapya watakaokuwa msaada kwake. Rais Putin wa Russia alifanya hili vizuri sana alipochukua madaraka. Adolf Hitler yeye aliamua kuwaua wayahudi ( Jews ) kwani wakati huo Jews ndio walikuwa wanashikilia uchumi wa Ujerumani. Hapa kwetu Tanzania kwa miaka mitatu tumeshuhudia Wafanyabiashara wanakipata cha mtema kuni. Wafanyabiashara wakubwa na wadogo wanabambikiziwa Kodi na wakibisha wanapewa kesi zisizo na dhamana, wanatupwa jela, wananyanganywa Mali zao na wengine kufilisiwa.
  2. Huteua Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambao ni Watu wake wa Karibu. Rais Vladimir Putin yeye alifuta kabisa chaguzi za Magavana na akateua majenerali wa jeshi na watu wa KGB badala yake. Hapa Tanzania tumeshuhudia Wakuu wa Mikoa miungu Watu wenye kufanya lolote bila kuhojiwa na yeyote. Tumeshuhudia Wakuu wa Wilaya wakifunga watu bila kufuata sheria, wakinyanganya watu mali zao na kila aina ya vituko bila kuchukuliwa hatua.
  3. Hudhibiti vyombo vya habari. Rais Vladimir Putin alihakikisha TV zote zinakuwa za Serikali kwa kutaifisha TV binafsi na ilikuwa marufuku DUMA ( Bunge la Urusi) kuonyeshwa na ni yeye tu ndiye mwanasiasa aliyepaswa kuonekana kwenye TV. Hapa Tanzania Bunge limezuiwa kuonyeshwa moja kwa moja Lakini shughuli zote za Rais Magufuli zinaonyeshwa hata kwa masuala yasiyopaswa kuonyeshwa kama vile kusaini mikataba au mashauriano na Viongozi wa dini. Sheria ya Huduma za Habari nchini imeviweka vyombo vya Habari hatarini Katika kuchapisha au kutangaza Habari zao. Serikali imeweka kanuni za leseni ili kudhibiti kuwepo na kufanya kwao shughuli zao. Waandishi wanatekwa na kupotezwa kwa Mfano Azory Gwanda wa Gazeti la Mwananchi.
  4. Hudhibiti Vyama vya Siasa. Adolf Hitler wa alifuta vyama vyote Ujerumani. Vladimir Putin alizuia mikutano ya kisiasa na kuanzisha vyama vibaraka. Hapa Tanzania, kama tulivyotabiri katika makala Hii Mwaka 2016, “ Ndio mpango utakaofanywa Tanzania kwa kuanza na kuzuia mikutano ya vyama vya siasa. Sheria pia itabadilishwa na kuifanya nchi ya Chama kimoja pekee, CCM”. Hili limetokea kwa tarehe 29/1/2019 Bunge kutunga sheria ya mabadiliko ya sheria ya vyama vya Siasa na kumfanya Msajili wa Vyama kuwa Mdhibiti wa Vyama vya Siasa. Utekelezaji wa sheria mpya ya vyama vya siasa utapelekea ama vyama kutii maelekezo ya Serikali au kufutwa na hivyo CCM kuhodhi siasa za nchi.

Mtu yeyote mwenye akili timamu na mwenye kupata japo muda kidogo wa kujisomea anajua nini kinaendelea. Watu wasioona ama wana maslahi au uwezo wao wa kuona ni mdogo sana. Wengine wameamua tu kuvaa miwani za mbao. Wahanga wa Demokrasia wanajua maana ya haya tunayosema. Tanzania sasa imefunga duara ( Full Circle ) kwenye hatua Muhimu za nchi kuwa ya kidikteta.

Ni dhahiri kuwa Dunia ina madikteta wengi waliowahi kuwaletea wananchi wao maendeleo. Ethiopia. Malaysia. Singapore. Hata Rwanda. Tofauti yao na Sisi ni kwamba Madikteta wao ni wanazuoni wenye uwezo wa kutumia akili na utulivu kufanya maamuzi. Madikteta wao wanasoma vitabu na majarida ya uchambuzi wa sera. Rais Paul Kagame wa Rwanda hakosi Harvard Business Review. Meles alikuwa na akili Kama mchwa mpaka wazungu walikuwa wanamwogopa na kitu cha kwanza alichoomba kupewa Kama msaada ni ' vitabu vya uchumi'. Hata hivyo tunashuhudia Ethiopia ikifuta sheria kandamizi na kuelekea kwenye barabara ya Demokrasia baada ya kuona uimla haulipi.Lee Kuan Yew wa Singapore na Mahathir Mohammed wa Malaysia ni waandishi wazuri wa vitabu. Hawa sio too technical...... Ni Intellectuals.

Pamoja na kuwa hao niliowataja wanasoma na wenye MAARIFA Mengi, Bado udikteta haukuwasaidia sana na wengi wamebadilika na kuwa wana Demokrasia.

( last edit 30/1/2019 )
Rais Magufuli alikuwa na haki ya kutumia mkono wa chuma kurejesha nchi hii kwenye maadili aliyotuacha nayo baba wa taifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii nchi ni kichekesho cha kipekee, unaanzisha uzi kuhusu udikteta na unasomwa na watu!.

Nchi za kidikteta unaweza hata kuanzisha uzi na ukapata mrejesho wa jamii?.

Unashangaa nini, kwani hujawahi kuona ?
Unachochanganya wewe ni Freedom of Speech and Freedom after Speech. Kwenye nchi za kidikteta watu huwa wanaongea sana, lakini wanakipata cha mtema kuni baada ya kufanya hivyo.

Ndiyo maana leo nchi kama Korea Kaskazini ina maelfu ya wafungwa wa kisiasa. Uturuki ndiyo imeipiku hadi Uchina kwa kufungia waandishi wa habari.

Udikteta huwa hauzuii watu kuongea, watu kusema watasema tu. Bali udikteta ni kuwashughulikia watu baada ya kuongea sasa......
 
Hoja za Zitto kwa kifupi ni......

1. Vita dhidi Wafanyabiashara Wakubwa
2. Nepotism - Undugunazation katika teuzi
3. Kudhibiti vyombo vya habari
4. Kudhibiti vyama vya siasa.

Hayo ni maoni yake na mtazamo wake. Zitto anatakiwa kusema jitihada zake binafsi za siri alizofanya kujipendekeza kwa JPM baada tu ya uchaguzi Mkuu hadi Mwaka 2016 lakini aliposhindwa ushawishi wake ndio aliapa atampinga mwanzo mwisho.
Hizi ndo Siasa purely za Kinafiki.
 
Unafahamu kwamba A. Hitler alishinda Uchaguzi Ujerumani? Unafahamu kwamba the rise of A.Hitler kulisaidiwa na USA akiwemo baba yake HW Bush aliyeitwa Prescot Bush? Unafahamu Ulaya yote pamoja na English monarchy walisapoti nazism?

Unafahamu apartheid AK ni ideology ya nazism na ilisapotiwa na Muzungu wote USA na Ulaya? Unafahamu Mandela alikuwa kwenye orodha ya terrorist USA?
Unafikiri ni kwa nini Mandela alitambulika kama terrorist na USA?
Acha wongo, Hitler hakushinda dhidi ya Raisi Hindenburg mara zote mbili. Adolf Hitler alitokea bungeni baada ya chama chake kuwa kikubwa na chenye nguvu na kumfanya Herman Gōring kuwa kama spika: Wakaunganisha nguvu na vyama vingine kuwapinga wakomunisti.

Hitler aliteuliwa kuwa Chancellor "Waziri Mkuu" hakushinda uchaguzi wowote ule nchini Ujerumani.....

Wewe ni mwongo sana......
 
Unashangaa nini, kwani hujawahi kuona ?
Unachochanganya wewe ni Freedom of Speech and Freedom after Speech. Kwenye nchi za kidikteta watu huwa wanaongea sana, lakini wanakipata cha mtema kuni baada ya kufanya hivyo.

Ndiyo maana leo nchi kama Korea Kaskazini ina maelfu ya wafungwa wa kisiasa. Uturuki ndiyo imeipiku hadi Uchina kwa kufungia waandishi wa habari.

Udikteta huwa hauzuii watu kuongea, watu kusema watasema tu. Bali udikteta ni kuwashughulikia watu baada ya kuongea sasa......
Huwezi kuwa unatukana viongozi wakubwa wa nchi halafu uachwe eti kwa kigezo cha uhuru wa kujieleza. Toa maoni ya kiungwana, hakuna atakayekugusa.
 
Naona wewe ni wale wale, ungekuwa una muda kidogo wa kusoma madikteta wa Duniani usingeandika Hata.

Baath Party ya Iraqi uliifahami, je chama cha Hitrer unakijua kilianzaje? Je wanachama kama wewe washanhiliaji waliendelea kushangilia?

Mmezidiwa akili na mtu mmoja ambaye nahisi alitakiwa asiwazidi, sidhani kama ana IQ kubwa kuzidi wengiwenu, msichotaka kukiri ni kuwa kama tinavyo shughulikiwa sisi wapimzani nyie mmejazwa hofu, mkija kustuka ntakuwa mmechelewa hamtaweza kufanya chochote

Sidhani kama hapa ni suala la IQ. Hapa ni maslahi tu. Siku hizi nadhani hata njia ya ya kulipia hayo maslahi imebadilika kutoka "in kind" kwa njia ya uteuzi kwenda "in cash". Ndiyo maana hata jambo liwe la hovyo kiasi gani watetezi watakuwepo tu alimradi haliwaathiri wao moja kwa moja. Kikokotoo tu ndiyo iliyokosa watetezi kwani kila mmoja aliguswa!
 
Duh, wewe sasa unataka kuleta Ligi, Dunia nzima inajua Chama cha nazi kilishinda Uchaguzi Ujerumani unataka kulibishia hilo? Kuwa Kansela ni jambo lingine kwa mfumo wao ni lazima Raisi/ Mfalme akubali kama mtu ambaye Chama kilichoshinda anafaa kuongoza Serikali na ndiyo Hindenburg alichofanya, lkn nazi party kilichoongozwa na A.Hitler kilishinda Uchaguzi Ujerumani, hilo halina ubishi.

Ni kama Uingereza tu, ni lazima Ufalme ukubali kama Kiongozi aliyrchaguliwa na chama chake anafaa kuwa mkuu wa Serikali!
Hiyo dunia nzima ni yako wewe na ukoo wako ??? Hitler hakushinda uchaguzi wa Uraisi dhidi ya Hindenburg mara zote mbili. Wala chama chake hakikushinda. Wanazi walifanikiwa kupata siti nyingi bungeni tu.
Paul Hindenburg alikuwa na kura milioni 19 sawa na asilimia 50%, huku Adolf Hitler akiwa na kura milioni 13 sawa na asilimia 36.8% na Thälmann alikuwa na kura milioni 3 sawa na asilimia 10%. Sasa wewe hili la Chama cha wanazi kushinda uchaguzi umelitoa wapi ??

Chama cha wanazi kwenye uchaguzi wa mwaka 1932 kilishinda viti 196 sawa na asilimia 33.09% wakifuatiwa na Social Democrats walioshinda viti 121 sawa na asilimia 20.43% na mwisho kabisa Communist Party wakishinda viti 100 sawa na asilimia 16.86%. Wanazi walipata siti nyingi bungeni hadi wakaweka spika, lakini hawakushinda uchaguzi.....

Wongo wako peleka kwenu.....
 
Athene ya Ugiriki iliendelea kwasababu ya Demokrasia, hadi kufikia hatua ya kutishia nchi za kidikteta zenye nguvu kubwa za kijeshi kama Sparta: Wasparta hawakupenda Demokrasia na mifumo ya Athene na wakaamua kuivamia kwenye vita ya Peloponnesian ya Mwaka 431 BC. Unachokisahau ni kwamba waathene walienda mbali na kutengeneza mfumo wa Demokrasia wa moja kwa moja (Direct Democracy)

Roma ya kale lilikuwa ni dola la kifalme lakini kimsingi ndiyo dola ambalo tunaiga mifumo yake ya kidemokrasia katika dunia yetu ya leo. Kaisari na nguvu zake zote zile ilikuwa ni lazima atii matakwa ya Seneti ya Roma na aliposhindwa kufanya hivyo alishughulikiwa. Kaisari Julius alipigwa visu baada ya kutaka kushindana na Seneti ya Roma. Ile nchi ilikuwa inaheshimu sana utawala wa sheria.

Wanafalsafa wakubwa wengi ambao tunawasoma ni aidha walitoka kwenye nchi ya Ugiriki au Roma, ambazo zilikuwa ni za kidemokrasia na zilitawala dunia kwa muda mrefu. Roma ilitawala dunia kwa miaka zaidi ya elfu moja kwasababu ya mfumo wake wa kidemokrasia.

Pengine hujasoma vizuri, Ufalme wa Uingereza ilipata mafanikio makubwa sana baada ya kutengeneza kuruhusu mifumo ya kidemokrasia. Walipitisha The Magna Carta mwaka 1215 iliyotoa mashauri makubwa ya haki za raia wa Uingereza. Wakatengeneza The Common Law ambao ni mfumo wa kisheria unaoruhusu Demokrasia. Wakaja wanafalsafa kama wakina A.V Dicey wakazungumzia The Rule of Law na mengineyo.

Huu mfumo wa kidemokrasia ndiyo uliyoifanya Uingereza kuwa taifa la kwanza duniani kuleta mapinduzi ya viwanda mwaka 1776. Akawa na nguvu sana na ndiyo ukawa mwanzo wa PAX BRITANNICA na Uingereza likawa taifa lenye nguvu duniani lililomiliki makoloni barani Marekani, Asia na Afrika.

Uchina yenyewe ya leo imebadilika sana. Baada ya kuona Mao Zedong kafariki wakaamua kuachana na falsafa za kidikteta zisizokuwa na kichwa wala miguu. Deng Xiaoping aliruhusu uhuru wa kiuchumi na mfumo wa masoko. Ambao mpaka leo hii Maraisi Jiang Zemin, Hu Juntao na Xi Jinping wanauheshimu.

Hoja ya mkuu Zitto iko katika nyanja kuu mbili. Mosi, Uhuru wa kisiasa ambao kwa lugha ya kiingereza ni Civili and Political Rights. Pili, Uhuru wa Kiuchumi ambao kwa lugha ya kiingereza ni Economic, Social and Cultural Rights. Unaweza kubana uhuru wa kisiasa lakini ukaachia uhuru wa kiuchumi. Ametoa na mfano hai kabisa wa Meles Zenawi, Vladmir Putin na Paul Kagame: Wanabana siasa lakini Uchumi uko wazi, kwasababu Uchumi ni masoko na namba.

Raisi wetu ametuvuruga kote, kwenye Siasa na kwenye Uchumi. Huyu ni mtu wa aina gani aisee ??? Uchumi ni namba mzee: Hauna morality, hela hata itoke kwa shetani kama tu inaongeza mzunguko then its all good for the economy. Sema cha muhimu tu ni kusimamia mgawanyo wa keki ya taifa pamoja na ushindani.

Sisi tumebugi kote na hatujui hata tunakoenda. Hivi mkuu chige wewe unaelewa sisi tunaenda wapi ?? Hebu mje na mkuu JokaKuu mtusaidie hapa.
Umenichanganya mkuu! Unazitaja Greek na Roman empire kama mifano ya demokrasia na kuiweka pia uchina. Je, kwa vigezo vya leo unaweza ukasema China ina demokrasia? Ni yale yale ya akina Zitto wanayokataa kwamba TZ hakuna Demokrasia. Demokrasia ya Greek na roman haikumaanisha vyama vingi. Hii ya akina Zitto inamaanisha vyama vingi, na kama hakuna basi demokrasia hakuna. Wakigomewa mambo yao huo ni udikteta.

Back to democracy, je, unafahamu kuanguka kwa Greek na Roman empire haikutokana na u-dikteta? Ilitokana na ustaraabu (Wa wakati huo). The recent long Ottoman empire nayo hivyo hivyo. UHuru wa kiuchumi wa China siyo ingredient ya demokrasia.
btw. Ulimuelewaje Zitto bungeni kuamini kwamba umaskini TZ ulipungua wakati wa utawala wa kikwete? Indicator yake ni idadi ya watu walioingia ktk kipato kikubwa, lakini hataji walioingia ktk umaskini. He is just another stupid pretender.
 
Siasa zinachukua mda wa maendeleo tunakaa tunalumbana badala ya kufanya kazi.CCM kupitia Rais Magufuri waliomba kura kupitia Irani yao hili wachaguliwe wakafanikiwa waachwe wafanye kazi..Uhuru wakujieleza ni mkubwa sana Tatizo letu badala ya kuelezo changamoto zinatukabili katika maeneo yetu tunaanza kutukana na kashifa juu.Toka Mkuu ameingia madarakani
amefanya kazi kubwa sana Kuanzia
huduma za afya miundombinu kununua
ndege na kununua meli ziwa Victoria
japo aijafika. Kasimamia maadili kwa
viongozi wa umma na serikali ukienda
kwenye madini kaboresha mikataba ya
ovyo kaongeza uwazi hayo anayosemwa
kwa mabaya ni propaganda.Mungu
azidi kumsimamia hii kazi sio ndogo..
 
Huwezi kuwa unatukana viongozi wakubwa wa nchi halafu uachwe eti kwa kigezo cha uhuru wa kujieleza. Toa maoni ya kiungwana, hakuna atakayekugusa.
Unachanganya mambo tena: Kuna wafungwa wa makosa ya jinai na wafungwa wa makosa ya jinai yatokanayo na shughuli za kisiasa. Huwezi kumdhuru mtu kwa kusema kwamba ununuzi wa ndege siyo kipaumbele, au kusema kupeleka SGR Rwanda ni kukosa mkakati wa kibiashara. Huyu Mzee hataki aambiwe ukweli, yeye amekuwa nani ?
 
Maana/Dhana ya DEMOKRASIA hasa ni ipi mkuu!
Demokrasia ni pana sana, lakini hasa iko katika nyanja kuu mbili. Mosi, nyanja ya kinadharia au kitunu. Pili, nyanja ya kimfumo.

Kwenye nadharia tunasema Democracy is a highest morality of aspiration which nations strives to reach, this value entails greater freedom, adherence to the rule of law and protection of human rights and civil liberties which enables the development of human faculties.

Kwenye mfumo wa kiutawala tunasema Democracy is a state that is governed/ruled by following democratic principles and values: And such system can be manifested through the Supremacy of the Constitution, Separation of Powers, Independence of the Judiciary and Parliamentary Sovereignty. Mfano Uingereza na Marekani.

Hivyo basi hata Ukomunisti unaweza kuwa ni nadharia na mfumo wa kiutawala pia.
 
Dikteta huchukua hatua kadhaa kupandikiza utawala wa Imla - Zitto Kabwe

( Andiko la July, 2016 na uhariri kidogo 2018. Uhariri tena mdogo Jan, 2019 )

  1. Hupambana na Wafanyabiashara wakubwa ' matajiri ' ili kuweka matajiri wake wapya watakaokuwa msaada kwake. Rais Putin wa Russia alifanya hili vizuri sana alipochukua madaraka. Adolf Hitler yeye aliamua kuwaua wayahudi ( Jews ) kwani wakati huo Jews ndio walikuwa wanashikilia uchumi wa Ujerumani. Hapa kwetu Tanzania kwa miaka mitatu tumeshuhudia Wafanyabiashara wanakipata cha mtema kuni. Wafanyabiashara wakubwa na wadogo wanabambikiziwa Kodi na wakibisha wanapewa kesi zisizo na dhamana, wanatupwa jela, wananyanganywa Mali zao na wengine kufilisiwa.
  2. Huteua Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambao ni Watu wake wa Karibu. Rais Vladimir Putin yeye alifuta kabisa chaguzi za Magavana na akateua majenerali wa jeshi na watu wa KGB badala yake. Hapa Tanzania tumeshuhudia Wakuu wa Mikoa miungu Watu wenye kufanya lolote bila kuhojiwa na yeyote. Tumeshuhudia Wakuu wa Wilaya wakifunga watu bila kufuata sheria, wakinyanganya watu mali zao na kila aina ya vituko bila kuchukuliwa hatua.
  3. Hudhibiti vyombo vya habari. Rais Vladimir Putin alihakikisha TV zote zinakuwa za Serikali kwa kutaifisha TV binafsi na ilikuwa marufuku DUMA ( Bunge la Urusi) kuonyeshwa na ni yeye tu ndiye mwanasiasa aliyepaswa kuonekana kwenye TV. Hapa Tanzania Bunge limezuiwa kuonyeshwa moja kwa moja Lakini shughuli zote za Rais Magufuli zinaonyeshwa hata kwa masuala yasiyopaswa kuonyeshwa kama vile kusaini mikataba au mashauriano na Viongozi wa dini. Sheria ya Huduma za Habari nchini imeviweka vyombo vya Habari hatarini Katika kuchapisha au kutangaza Habari zao. Serikali imeweka kanuni za leseni ili kudhibiti kuwepo na kufanya kwao shughuli zao. Waandishi wanatekwa na kupotezwa kwa Mfano Azory Gwanda wa Gazeti la Mwananchi.
  4. Hudhibiti Vyama vya Siasa. Adolf Hitler wa alifuta vyama vyote Ujerumani. Vladimir Putin alizuia mikutano ya kisiasa na kuanzisha vyama vibaraka. Hapa Tanzania, kama tulivyotabiri katika makala Hii Mwaka 2016, “ Ndio mpango utakaofanywa Tanzania kwa kuanza na kuzuia mikutano ya vyama vya siasa. Sheria pia itabadilishwa na kuifanya nchi ya Chama kimoja pekee, CCM”. Hili limetokea kwa tarehe 29/1/2019 Bunge kutunga sheria ya mabadiliko ya sheria ya vyama vya Siasa na kumfanya Msajili wa Vyama kuwa Mdhibiti wa Vyama vya Siasa. Utekelezaji wa sheria mpya ya vyama vya siasa utapelekea ama vyama kutii maelekezo ya Serikali au kufutwa na hivyo CCM kuhodhi siasa za nchi.

Mtu yeyote mwenye akili timamu na mwenye kupata japo muda kidogo wa kujisomea anajua nini kinaendelea. Watu wasioona ama wana maslahi au uwezo wao wa kuona ni mdogo sana. Wengine wameamua tu kuvaa miwani za mbao. Wahanga wa Demokrasia wanajua maana ya haya tunayosema. Tanzania sasa imefunga duara ( Full Circle ) kwenye hatua Muhimu za nchi kuwa ya kidikteta.

Ni dhahiri kuwa Dunia ina madikteta wengi waliowahi kuwaletea wananchi wao maendeleo. Ethiopia. Malaysia. Singapore. Hata Rwanda. Tofauti yao na Sisi ni kwamba Madikteta wao ni wanazuoni wenye uwezo wa kutumia akili na utulivu kufanya maamuzi. Madikteta wao wanasoma vitabu na majarida ya uchambuzi wa sera. Rais Paul Kagame wa Rwanda hakosi Harvard Business Review. Meles alikuwa na akili Kama mchwa mpaka wazungu walikuwa wanamwogopa na kitu cha kwanza alichoomba kupewa Kama msaada ni ' vitabu vya uchumi'. Hata hivyo tunashuhudia Ethiopia ikifuta sheria kandamizi na kuelekea kwenye barabara ya Demokrasia baada ya kuona uimla haulipi.Lee Kuan Yew wa Singapore na Mahathir Mohammed wa Malaysia ni waandishi wazuri wa vitabu. Hawa sio too technical...... Ni Intellectuals.

Pamoja na kuwa hao niliowataja wanasoma na wenye MAARIFA Mengi, Bado udikteta haukuwasaidia sana na wengi wamebadilika na kuwa wana Demokrasia.

( last edit 30/1/2019 )

Hivi Zitto, kati yako na Magufuli nani diktekta? Ndani ya chama cha ACT hakuna wa kukohoa mbele yako, mwenyewe unajiita 'kiongozi mkuu' , kila kitu wewe.
 
Kosa kubwa mnalofanya Upinzani ni kumtenganisha Magufuli na CCM, wengine hata mnaifanyia CCM promo kwa kumsifia Kikwete kwamba alifanya mazuri TZ mnachoshindwa kuelewa ni kwamba 2020/25 Kikwete ataikampenia CCM Magufuli ataenda atakuja mwingine lkn bado atakuwa ni CCM hivyo mtarudi tena hapa kuanza moja na kumchukia pia mwishowe hakuna mahali mnaenda.

Tuliona mlimchukia Mwinyi, Mkapa, hata Kikwete na sasa Magufuli.

Hivyo mkitaka mfanikiwe ni lazima mumjue adui yenu, na Adui yenu siyo Magufuli kwani huo Mswada ungepita hata kama Raisi asingekuwa Magufuli.
Emenena vizuri sana,
ILA NCHI HII ITABAKI KAMA ILIVYO MPAKA ITAKAPOPATA RAIS MZALENDO WA KWELI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
wamebadilika na kuwa wana Demokrasia.
Nini maana ya Demokrasia ...maana kukosoa mnakosoa tena muda mwingine mnatoa kashfa na kukashifu ..na mnaishi vizuri tu ,labda milango ya madili ndio imefungwa
 
Ndugu, nazi party kilikuwa na majority kwenye German Reichtag (Bunge) kwanza unaelewa Uchaguzi wa Ujerumanina Kansela anavyopatikana, tuanzie hapo isije kuwa tunabishana wakati mambo ya msingi hayako sawa!
Wewe mimi siyo ndugu yako: Halafu aliyemchagua Hitler kuwa Chancellor ni Raisi Paul Von Hindenburg, January 1933. Cheo hiki siyo cha kuchaguliwa bali kuteuliwa ambapo chama chenye viti vingi ndiyo hupata nafasi.

Baada ya Raisi Hindenburg kufariki Hitler ndiyo akawa dikteta kamili, Mkuu wa Serikali na Mkuu wa nchi.

Hizi nyingine ni blah blah zake zisizo na maana yoyote ile.
 
Back
Top Bottom