Tanzania inawezekana? Ruto asitisha ununuzi wa Magari ya Serikali kwa mwaka mzima, Mashirika ya umma 47 yafutwa hayana tija

Tanzania inawezekana? Ruto asitisha ununuzi wa Magari ya Serikali kwa mwaka mzima, Mashirika ya umma 47 yafutwa hayana tija

View attachment 3034199




Leo mchana Ruto anajindaa kwa kile kinacho aminika ni hotuba ya kupunguza baadhi ya mawaziri wake na kuunganisha baadhi ya wizara ili kubana matumizi ya pesa za walipa Kodi wa nchi ya kenya ambao ndio wanao umia na mzigo mkubwa wa kuendesha Serikali.

Kwa Tanzania hali ni tofauti, huku tunahimiza kulioa kodi ambayo sana inatumika kuendesha Serikali hasa hasa kununua Magari ya anasa.

Tuna hadi Naibu waziri mkuu cheo cha mchongo ambacho hakipo kikatba ila kimewekwa kwa sababu za siasa na mzigo tunabeba sisi.

Ukiachana na hayo bado tuna Baraza la Mawaziri kubwa sana na sana limekaa kimchongo sana.

Tanzania tuna Baraza kubwa sana la Mawaziri nazani kiliko hata Kenya ilivyo, na baadhi ya wizara zimekaa kimchongo hazina maana yoyote ile zaidi ya kuongeza mzigo kwa wananchi.

Huku tunahimizwa sana hata na mwigulu tulipe Kodi, Ila tusicho kijua hio kodi inatumika kugharamikia anasa za Watawala wa hili Taifa, huku wananchi wakiendelea kuwa masikini.

Na Watawala hawako tayari kupunguza Mzigo wa Baraza la mawaziri kwa sababu limekaa kisiasa hasa kulipana fadhila.
Ni baada ya GNz kumnyoosha...
 
Haya mambo yanayo fanyika Kenya huku yanawezekana? Tuzungumzie tu hata Mashitika ya Umma yanayo jiendesha kwa hasara na still yanakumbatiwa na kupewa pesa za walipa kodi.

View attachment 3034252

Bajati ya mwaka huu ya kununua magaru ya Kifahari ya Serikali ni kubw akulilo bajeti ya wizara kama 3 hivi.
View attachment 3034248

Ni lazima tukate huu uhuni.
Kumbe nguvu ya umma huleta mabadiliko chanya
 
Inawezekana ikiwa wananchi watakomaa na kuwa ngangari, mkiwa mlenda urojo urojo lazima mburuzwe tu.
 
Machawa wa CCM wanawaita Wakenya wajinga kuandamana kudai uadilifu serikalini.
  • Wizi ruhsa,
  • rushwa ruhsa,
  • uongo ruhsa na...
Masikini Watanganyika...utajiri wa asili unatapanywa ohvyo huku wakishuhudia
 
Na baada ya hili linalo fuata Kenya ni kupunguza idadi ya Wabunge huenda uchaguzi ujoa Kenya ikawa na udadi ndogo sana ya Wabunge, make Raia walisha ona mzigo mkubwa uko kwenye kuendesha Serikali.

Huku tunawaza kugawa majimbo, ili kuendelea kuwapa watu ulaji.
Wananchi wa Tanganyika ni mateka wa watawala. Pia wananchi wa Tanganyika hawajitambui hawana uwezo wa kujua ukweli ni upi, kila jambo linatazanwa kishabiki na kinazi ( subjectively) badala ya kuangaliwa objectively.

Back to topic, ili serikali iwepo gharama lazima ziwepo na hazikwepeki kuna gharama zingine zinapaswa kufutwa na zingine ni ukosefu wa uelewa kwa wanaozipinga, mfano waziri, RC, DC kuwa na gari la serikali sio kosa na anapaswa awe nalo kwa ajili ya kazi zake lakini kuna watu kwa kukosa uekewa wanaona hawastahili kuwa na magari etti magari ya kifahari! Sijui wanataka Kiongozi atumie pikipiki au baiskeli! Aina ya gari la kiongozi linatdegemea vitu vingi mazingira ya barabara anazotumia , usalama nk. Pia gari likinunuliwa keo huyo kiongozi hatanunuliwa tena gari hadi baada ya miaka kadhaa..

Gharama zinaxitakiwa kuindolewa hapa Tanganyika ni zifuatazo:
1. Uundaji wa majmbo ya uchaguzi ambayo huundwa kukidhi matakwa ya kisiasa uachwe. Majimbo ya sasa yanapaswa kupunguzwa na uwakilishi wa ubunge ufuate wilaya tu yaani kila wilaya ndio iwe na mbunge.
2. Viti naalum vufutiliwe mbali visiwepo.
Wabunge wa Zanzibar wahudhurie vikao vya mambo ya muungano tu.
3. Wizara zisizidi ishirini na zisipungue kumi na nane.
4. Wabunge na mawaziri wasilipwe posho mbili mbili. Waziri anapoenda bungeni asichukue posho wizarani kwake akalipwe huko bungeni tu. Pia wabunge wakitembelea kukagua wizara/ taasisi wasilipwe posho wala kununuliwa chakula na wizara/ taasisi wanazotembelea.
5. Sitting allowances zote zifutwe kuanzia bungeni hadi katika wizara na taasisi zisiwepo kabisa..
6. Vyama vya siasa visipewe ruzuku na serikali gharama za uendeshaji vyama iwe mzigo wa wanachama wao tu na sio wananchi .
7. Siku za vikao vya bunge la bajeti zipunguzwe kwa nusu

Kwa kuanzia haya yakifanyika gharana za uendeshaji zitapungua kwa kiasi kikubwa.
 
Wananchi wa Tanganyika ni mateka wa watawala. Pia wananchi wa Tanganyika hawajitambui hawana uwezo wa kujua ukweli ni upi, kila jambo linatazanwa kishabiki na kinazi ( subjectively) badala ya kuangaliwa objectively.

Back to topic, ili serikali iwepo gharama lazima ziwepo na hazikwepeki kuna gharama zingine zinapaswa kufutwa na zingine ni ukosefu wa uelewa kwa wanaozipinga, mfano waziri, RC, DC kuwa na gari la serikali sio kosa na anapaswa awe nalo kwa ajili ya kazi zake lakini kuna watu kwa kukosa uekewa wanaona hawastahili kuwa na magari etti magari ya kifahari! Sijui wanataka Kiongozi atumie pikipiki au baiskeli! Aina ya gari la kiongozi linatdegemea vitu vingi mazingira ya barabara anazotumia , usalama nk. Pia gari likinunuliwa keo huyo kiongozi hatanunuliwa tena gari hadi baada ya miaka kadhaa..

Gharama zinaxitakiwa kuindolewa hapa Tanganyika ni zifuatazo:
1. Uundaji wa majmbo ya uchaguzi ambayo huundwa kukidhi matakwa ya kisiasa uachwe. Majimbo ya sasa yanapaswa kupunguzwa na uwakilishi wa ubunge ufuate wilaya tu yaani kila wilaya ndio iwe na mbunge.
2. Viti naalum vufutiliwe mbali visiwepo.
Wabunge wa Zanzibar wahudhurie vikao vya mambo ya muungano tu.
3. Wizara zisizidi ishirini na zisipungue kumi na nane.
4. Wabunge na mawaziri wasilipwe posho mbili mbili. Waziri anapoenda bungeni asichukue posho wizarani kwake akalipwe huko bungeni tu. Pia wabunge wakitembelea kukagua wizara/ taasisi wasilipwe posho wala kununuliwa chakula na wizara/ taasisi wanazotembelea.
5. Sitting allowances zote zifutwe kuanzia bungeni hadi katika wizara na taasisi zisiwepo kabisa..
6. Vyama vya siasa visipewe ruzuku na serikali gharama za uendeshaji vyama iwe mzigo wa wanachama wao tu na sio wananchi .
7. Siku za vikao vya bunge la bajeti zipunguzwe kwa nusu

Kwa kuanzia haya yakifanyika gharana za uendeshaji zitapungua kwa kiasi kikubwa.
Kongole
 
Back
Top Bottom