Tanzania kuna familia ambazo zinaishi kifalme bila Watanzania kuzifahamu au wamepiga kimya tu

But in all honesty mwisho wa siku wao ni watu kama mimi na wewe na wana hobbies zao ambazo zinakuwa rahisi kuzifanya kutokana na status na depth ya mfuko wao.

Haimaanishi just because wapo privileged wasiwe na miradi yao, dreams zao nk. Kisichotakiqa ni kudhulumu ama kunyanyasa wenzao ili wao wapate unafuu katika haya maisha.
 
Shida ni sehemu mbili kuna baadhi ya watoto wa viongozi wachache wanaodhani kuongoza nchi ni haki yao, na baadhi ya wastaafu au wenzawao (sio watoto zao) wasiotosheka mtu kama Salma Kikwete unashida gani ya ubunge si uwaachie na wengine wale.
Umeshaandika kila mtu ana haki ya kufuata ndoto zake.....

Hata huyu uliyemtaja muache afate ndoto zake...hayo ya kutosheka ni maamuzi yake binafsi kama akitaka.
 
Umeshaandika kila mtu ana haki ya kufuata ndoto zake.....

Hata huyu uliyemtaja muache afate ndoto zake...hayo ya kutosheka ni maamuzi yake binafsi kama akitaka.
Upo sahihi kimanti ya haki zake bali kuna mapungufu ya morality. Walau basi angekuwa ameonyesha awali kuwa na political interest ajawahi kuwa ata mlezi ndani ya UWT au kuwa mwanaharakati wa cause yoyote ata kupambania maslahi ya walimu wenzake toka mumewe awe waziri mpaka anamaliza uraisi zaidi ya miaka 30 ya siasa.

Hilary Clinton ukimpekua alikuwa anafanya harakati za siasa tangia yupo chuo; lakini wewe huna historia ya siasa utumie mgongo wa mwenzawako kufuata fursa tu for the sake of it (wakati tajiri tayari) hiyo sasa ni tamaa ajifunze kusaza na kuwaachia wengine nafasi.
 
Katiba ya sasa haijakataza Mlalahoi kugombea nafasi yoyote na katiba mpya haitazuia Mtoto au Mke wa kiongozi kugombea nafasi yoyote ile

Una umri gani duniani mkuu?

Kwani wewe hujui:

1. Katiba ya sasa inaruhusu wizi na ujambazi wa kura kama ule wa 2019/20?

2. Katiba iliyopo haitoi fursa sawa kwa wote?

3. Mtake au mstike rais ajaye 2025 ni mwanamke kutoka Zanzibar?

4. Mtake au mstike rais ajaye 2030 naye ni mzanzibari?

5. Rais ndiye mgawa hizi fursa kama njugu?

Kwani kina Nape, January na kina Riz moko wao ni dhambi kujiajiri kunako hubiriwa siku zote majukwaani?

Au ni kujitoa ufahamu tu mjomba?
 
baba jambazi ,mama kahaba,mtoto ni tapeli,mjomba ni mpiga rarmi chonganisha,bamdogo mfanyakazi wa mwochari.
 
Mkuu hapo unamaama kwamba wanaofaidi kodi zetu kwa kiasi kikubwa hapa nchini ni hizo familia tatu tu.

Familia ya Jakaya Kikwete.

Familia ya Alhassan Mwinyi

Na Ya Rais Samia Suluhu.

Hapo upo sawa kabisa.

 
Katiba ya sasa haijakataza Mlalahoi kugombea nafasi yoyote na katiba mpya haitazuia Mtoto au Mke wa kiongozi kugombea nafasi yoyote ile
Tatizo mizania haiwezi ruhusu huyo mlalahoi kupenya.

Mfano ukaingia kwenye mchuano na mtoto wa mstaafu hata ukiwa na vipaji gani mfumo utamruhusu tu mtoto wa mstaafu hawatakuchukua wewe.
 
hiyo ndio CCM
Kunahitajika jitihadi za haraka kufanyika Ili Kekin ya taifa wafaidike watanzania wote,

Kinachoendelea sasa kuna siku utasikia Mtoto wa fulani anamiliki bandari ya Bagamoyo, Ngorongoro na uwanja wa ndege wa Julius Nyerere.
 
Tatizo mizania haiwezi ruhusu huyo mlalahoi kupenya.

Mfano ukaingia kwenye mchuano na mtoto wa mstaafu hata ukiwa na vipaji gani mfumo utamruhusu tu mtoto wa mstaafu hawatakuchukua wewe.
Watoto wa Sumaye nao wapo humo humo kwenye huu mtandao?
 
Huku kwetu baba ni mkata mkaa...

Mama ni mama wa nyumban!!!

Na watoto hawataki shule...wanavuta bange tuu..

Kweli tupo dunia tofaut,

Huku kwetu Baba mshona viatu
Mama mchoma vitumbua
Mimi muendesha boda boda
Sister Fundi chereani
Brother Balozi wa nyumba 10
Watoto wote shule vidumu ufagio hakuna aliyekatiza form 4.

Kuna siku hii familia yetu itatoa Mkuu wa Wilaya au Katibu Kata !.
 
Watoto wa Sumaye nao wapo humo humo kwenye huu mtandao?
Usipowaona kwenye siasa basi utawakuta wamejichimbia kwenye taasisi nyeti na mashirika ya umma.
Huko ndiko walipo wote.

Yaani wanahakikisha ile kitu inaitwa national cake yote wanaikomba.
 
Wewe unachuki tu aongoze nani asie na ndugu?

Au upinzani gani ulio sawa
 
Na wewe pambana familia yako iishi kifalme.
Soma sana,
Fanya kazi kwa juhudi sana.
Tafuta konekeksheni sana,
Jipendekeze sana sehemu sahihi kwa wakat sahihi
AU
Pigani katiba mpya itakoyotoa fursa kwa yoyote mwenye talents na jitihada
Unafikiri hao wasemwao wamesoma sana basi! Hamna lolote. Kuna misomi kibao hadi uprofesor inataabika huku. Hukumbuki prof mmoja anamshukuru rais kumtoa jararani? Siasa TZ zinaendeshwa na wajanja wajanja na hawataki katiba mpya
 
Hawana mshipa wa aibu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…