We Pelle mza usinichekeshe kuhusu sound zilivyokuwa zikiimbwa wkt ule mipango na mbinu zilizokuwa zimepangwa namna ya kuyabeba masalia ya yule mjusi mkuubwa aliyechimbwa mikoa ya kusini,na kwamba mahali pa kuja kumhifadhi pamekwisha andaliwa,so wale watalii waliokuwa wakitoka pande mbalimbali za dunia waliokuwa wanakwenda Ujerumani watakuja kwetu na kuongeza pato la Taifa,ngonjera hiyo iliisha kimya kimya kama mshumaa,najiuliza sisi Watanzania aliyeturoga ni nani,maana kila kitu tumejaaliwa kuwa nacho,malia asili,mito,madini ya kila aina,maji yapo ya kutosha lkn ukame mikoa iliyoko kando kando ya maziwa,achilia mbali maji safi na salama ya kutumia,migodi tumewapa wageni wanachimba lkn kila siku wanasema wanapata hasara,vijiji vilivyoko pembezoni mwa migodi mikubwa hakuna maji,barabara,zahanati,shule zenye vifaa vya kufundishia,ndani ya mgodi ni kuzuri huwezi kuamini kama ni Tanzania hii hii,watumishi wa serikali waliowekwa humo kuona kinachozalishwa ili kuhakikisha maslahi ya nchi yanalindwa,nao wanakula njama na wageni kutoa Taarifa za uongo,ndege zinatua ndani ya mgodi na kubeba madini huku zikisindikizwa na walinzi wa kampuni binafsi,polisi kazi yao ni kulinda uwanja tu tena nje.Mbuga ya Serengeti kwa sehemu kubwa iko Tanzania ila Kenya wanaitumia ipasavyo kuingiza watalii huku wakiitangaza nje kuwa iko kwao kama ilivyokuwa Mlima Kilimanjaro,tunashindwa nini kujenga uwanja mkubwa wa Kimataifa Musoma,hoteli zenye hadhi Kando Kando ya ziwa na makampuni ya Tours ili wageni waje moja kwa moja kwetu,tukawachukua kwa magari wakaingia Mwitongo nyumbani kwa Baba wa Taifa kisha mbugani tukapata fedha nyingi za kutosha kusukuma maendeleo ya nchi yetu?