Tanzania kupokea mkopo wa dollar million 150

Wapi iliposemwa Mkopo utafanya hayo uliyoeleza wewe?
 
Nchi haina mikakati hata kidogo, Una Chuma Liganga na mchuchuma ukashindwa kuwekeza na kutafuta muwekezaji aje awekeze ndio utengeze reli matokeo yako ndio haya,Chuma biadhaa namba 2 kuwa inaingizwa kutoka nje.

Mafuta ya kula,Sio swala la kufikirika kabisa tunashindwa kuzalisha mafuta ya kukidhi nchi hii,Wale vijana wa BBT waliweza kuzalisha Alizeti na soko lipo matokeo wamepelekwa kwenye zone za ajabu ajabu.

Gesi,Matumizi ya gesi kwenye Magari CNG.Mpaka leo vituo havizidi 10 vya kujaza gesi na hh ni kwa Dar tu why usitandaze vituo T1 yote mpaka Tunduma,mafuta yangepungua uhitaji hata wageni wangekuja kuweka gesi nchini.

Bado tunawabania wakenye kuwauzia gesi wakati wao biadhaa zao ni kama takakataka humu nchini,sarafu yako itabaki salama? Unaagiza sabuni nje? Sabuni ya kufulia kabisa bila aibu,piga ban kuingiza sabuni au toza kodi juu zaidi,Mbina simple.

Leo bodi ya wa kamdarasi wa ndani wana vikao kila siku sababu wanafanya kazi hawalipwi,daraja anapewa mgeni na analipwa in USD simple kabisa.

Akipewa mzawa ni mkopo atazunguka Mpaka afilisike kudai serlikari,

Tunaua wazawa, na kubeba wageni.

Madarasa ya shule za msingi,haya ya sasa hivi sijui kama yatafikisha miaka 100 ni ubovu kabisaa wa nchi katika usimamizi wa pesa za uma.

Wizi kila sehem ,ukionyeshwa jengo la milioni 50 utakimbia ni aibu.
 
Je,baada ya kulijua hilo,,ameleta sera gani mpya ya kuinua uchumi...
 
Sasa wewe unaona ni sawa kukopa kuongeza thamani ya shillingi?

Unafikiri kuna mtu atakwambia tunakopa kwenda kununua V8VXR au kulipa wabunge posho? au kuongeza safari za nje Kwa viongozi wa umma? JIONGEZE NDUGU.
Nioneshe waliposema wanakopa kuongeza thamani ya Shilingi.

Pili unajua logic yake kwenye hicho unachoongea Kwanza?
 
Nioneshe waliposema wanakopa kuongeza thamani ya Shilingi.

Pili unajua logic yake kwenye hicho unachoongea Kwanza?
Soma hiyo habari ya mleta Uzi na hiyo attachment ya Gazeti.

Hakuna cha logic, ni uleule ujinga wetu.
Ingekuwa tuna Logic basi Shillingi ingekuwa stable na dollar zingeonekana mitaani.
 
Hivi zile VX mpya za Wakuu wa Wilaya,nazo alinunua Magu ama...?
Kwanza kwani Kuna shida gani kununua hizo VX?

Pili Aliyesema Mkurugenzi wa Kahama na Geita waachwe wanunue ma VX eti wamekusanya pesa nyingi ni nani?
 
Mama yule ni mkopaji na sijajua nani atakuja kulipa hizo fedha😳
 
Kama kawaida 50/50 zenji/Tanganyika

Alafu Tanganyika ndo analipa deni
Mtajua hamjui kwa muungano huu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…