Tanzania Labour Law (Sheria ya Kazi Tanzania)

Tanzania Labour Law (Sheria ya Kazi Tanzania)

Naomba nitoe kauzoefu kangu kadogo kuhusu hii sekta binafsi.
1. Nadeclare interest kwanza kwamba mimi nimewahi kufanya kazi katika makampuni ya simu chini ya hawa wanaojiita recruitment agency. Yaan huko ni full unyonyaji
2. Sekta nyingi binafsi hasa za mawasiliano zina tabia ya kukwepa kutimiza mahitaji ya msingi kwa mujibu wa sheria na kuwakandamiza wafanyakazi wake mfano mikataba huwa hawatoi na ukianza kudai basi ujue siku zako kazin zinahesabiwa.
3. Nimeshuhudia wafanyakazi wenzangu kibao wakifukuzwa kwa hila na mambo ya hovyo kabisa,kwa hiyo kwa mwenzangu huyo aliyekutana na hicho kisanga si ajabu kuna kitu alifanya kizuri au alitoa maoni yake akaonekana mbaya mwisho wa siku anapigwa chini bila sababu za msingi.
4. Sekta binafsi hasa kwa upande wa sekta ya mawasiliano ni jipu kubwa sana kwa sababu serikali bado haijafanyia kazi kikamilifu pamoja na kwamba kila wakati wanapelekewa taarifa na waziri mwenye dhamana anajua lakin ndio hivyo wameamua kupuuza.
5. Ushauri wangu ni kwamba hizi kazi tunazofanya tuzitumie kama daraja la akuanzisha vyanzo vingine vya mapato maana siku hizi redundancy zipo nje nje sasa ukibweteka kutegemea kazi hata kama upo serikalini umeisha rafiki yangu,hali ni mbaya sana msione watu wanapita na magari yenye brands za majina makubwa ya kampuni kumbe ni tabu tupu aisee.
Unachokisema ni kweli. Bila kusahau na sekta ya utalii. Yaan wanagandamiza wafanya kazi asili mia moja.. na ukionekana mjuaji, unajua haki zako nakwambia wenyewe tu wanaanza kukutafutia kisa ili uondolewe kazini.

Mimi ni mmoja wapo, japo kwa sasa nina kazi nyingine ila kiukweli serikali imulike sekta binafsi upande wa ajira.

Madudu ni mengi na makubwa sana
 
Yapo kama.
1. Malipo ya nyuma ya kazi zilizofanywa kama hajalipwa
2.severance pay
3.transport allowance
4.likizo iliyokuwa due kama hipo.
5.rightful expectation
Rightfull expectations ndio nini mkuu.
 
mkataba wenu wa mwanzo wa kazi mpka mwisho wa kazi unakufunga......mkataba unaonesha haitakiwi uendelee kuwa kazini
...na VIP hivyo vipengele vya kutoa one month notice in case of terminating the contract,..na 2 month notice in case of redundancy mkuu.?
 
...na VIP hivyo vipengele vya kutoa one month notice in case of terminating the contract,..na 2 month notice in case of redundancy mkuu.?
hzo ni minor contract ambazo zipo ndani ya major contract inayosema tar fln mpka tar fln uwepo kazini.......so they are negligible
 
Habari kiongozi.
Mimi ni mwl ktk shule moja ya private hapa Dar es salaam.

Nina matatizo makubwa kazini, Wameniundia zengwe kuwa nimewapa mtihani wanafunzi,

Nikiwa nasahisha, wakanizuia kumalizia wakamalizia wao

Toka siku hyo wamenizuia kuingia shuleni

Na tayari wameshatafuta mtu mwingine

YOTE HAYA YANAFANYIKA
sijaitwa nikahojiwa juu ya tuhuma yangu
Wala sijaandika maelezo yoyote

JE
sheria ikoje ktk kumsimamisha na kumfukuza mwajiriwa. Nina miaka tisa (9) kazini

Pia hawajanipa hata barua ya kumsimamisha zaid ya mkuu wa shule kuwapa amri walinzi wa getini wasiniruhusu

Msaada plz

Natanguliza shukran

Una Muda gani toka timbwili hilo likukute?
Umeripoti kokote?
Miaka 9 walinzi wanakuzuia geti na bado hujalianzisha?
 
hzo ni minor contract ambazo zipo ndani ya major contract inayosema tar fln mpka tar fln uwepo kazini.......so they are negligible
...VIP walivyonipa hiyo notice mwezi wa NNE mkuu,..huoni kama ni automatic renew of contract
 
All in all ukiachishwa kazi kuwe na sababu au kusiwe na sababu lazima mwajiri akuite akutaarifu kinachojiri,akupe barua ya kuachishwa kazi inayoelezea kila kitu mlichojadiliana na pia benefits zako zote za msingi ziwe assured japo utasumbuliwa.
 
All in all ukiachishwa kazi kuwe na sababu au kusiwe na sababu lazima mwajiri akuite akutaarifu kinachojiri,akupe barua ya kuachishwa kazi inayoelezea kila kitu mlichojadiliana na pia benefits zako zote za msingi ziwe assured japo utasumbuliwa.
...kwenye hiyo barua ambayo subject ni" Notice for Accountant"...ndani ndio wameandika hawaendelea na mkataba sabb ya destructing of department.
....nimepewa just like a paper bila dispatch na sijawahi saini popote...na sizani kama wana nakala ya hiyo barua kwenye file
 
H
...kwenye hiyo barua ambayo subject ni" Notice for Accountant"...ndani ndio wameandika hawaendelea na mkataba sabb ya destructing of department.
....nimepewa just like a paper bila dispatch na sijawahi saini popote...na sizani kama wana nakala ya hiyo barua kwenye file
Hapo kuna walakin mkuu ngoja kuna nondo nitaweka hapa soon nipe 5minutes
 
KUACHISHA KAZI

Kuachisha kazi kwa ujumla maana yake ni kumalizika/kuvunjika kwa mkataba wa ajira kati ya muajiri na muajiriwa. Kwa maneno mengine ni kumalizika kwa mahusiano ya kiajira kati ya muajiri na muajiriwa.Kusitishwa kwa mahusiano hayo kunaweza kuanzishwa na upande wowote wa mkataba huo(muajiri au muajiriwa)

Katika kanuni za ajira na Mahusiano kazin(Kanuni za utendaji bora)za mwaka 2007,imeelezwa kuwa kuachishwa kazi ni pamoja na:

a. Kuachisha kazi chini ya sheria ya kimila ya Uingereza(Common Law)

b. Muajiri kusababisha ugumu wa muajiriwa kuendelea na ajira

c. Kushindwa kuongeza mkataba wa muda maalum kwa masharti yaleyale au yanayofana kama kulikuwa na matumaini ya kuongeza mkataba

d. Kushindwa kumruhusu mfanyakazi kurejea kazini baada ya likizo ya uzazi au ulezi

e. Kushindwa kumuajiri tena mfanyakazi pale ambapo muajiriamewaachisha kaziwafanyakazi kadhaa kwa sababu kama hiyo au zinazofanan na ametoa nafasi za ajira kwa baadhi ya wafanyakazi walioachishwa kazi tu


KUACHISHA KAZI KIHALALI

Katika sheria ya Kimila ya Uingereza(Common Law) kuachisha kazi kumeelezwa kuwa ni pamoja na

I. Kuachisha kazi kwa makubaliano-hapa ni pale ambapo muajiri na muajiriwa wamekubaliana kusitisha mahusiano yao ya kiajira Kwa mfano kama mkataba wa ajira ni wa mwaka mmoja na muda huo umekwisha hapo mkataba utakuwa umefikia kikomo

II. Ajira kukoma yenyewe-hapa ni pale ambapo mkataba wa ajira unakuwa umesitishwa katika mazingira kama kifo au kumalizika kwa shughuli ya muajiri

III. Kuachishwa kazi kunakofanywa na muajiri-muajiri pia anaweza kusitisha mkataba wa ajira lakin itampasa kwanza kuzingatia na kufuata taratibu za kisheria.

Katika Kanuni za Ajira na Mahusiano Kazini(Kanuni za Utendaji Bora)za mwakwa 2007 Kanuni ya 7(1)inasema ku”pale ambapo muajiri anafanya ajira kushindwa kuvumilika ambapo pia inaweza kusababisha muajiriwa ajiuzulu,kujiuzulu huko kutakuwa sawa na kuacha kazi kwa kulazimika”


Sheria ya ajira na mahusiano kazini na kanuni zake ,pia imeeleza kuwa ili kuachisha kazikuwe ni halali basi ni lazima kuwe na sababu halali na ya haki(valid and fair reason) na utaratibu wa haki(fair procedure)uwe umefuatwa.Muajiri anapaswa kuwa na sababu halali na awe amefuata utaratibu wa haki katika kumuachisha kazi muajiriwa.


Taratibu za kuachisha kazi zinatofautiana kulingana na sababu inayopelekea kuachisha kazi,lakini taratibu zote hizo ni lazima zimpe muajiriwa nafasi ya kusikilizwa kabla ya uamuzi wa kumuachisha kazi.Bila kujali uzito wa kosa lililofanywa na muajiriwa ,bila kujali kuwa muajiri wake ana ushahidi wa kutosha,ni lazima sheria kufuata taratibu za kumuachisha kazi kama ilivyoelezwa katika sheria ya Ajira na Mahusiano kazini na 6. Ya mwaka 2004 na kanuni zake za mwaka 2007.


Kushindwa kufuata taratibu hizo kutamaanisha muajiriwa ameachishwa kazi bila kupewa nafasi ya kujitetea(summary dismissal)Kutompa muajiriwa nafasi ya kujitetea au kujieleza ni kumnyima haki yake ya kisheria.Kwa mujibu wa sheria za kazi kuachisha kazi kwa namna hii ni sawa na kuachisha kazi kusivyo halali(unfair termination)


Endapo itathibitika kuwa kuachisha kazi kulikofanywa na muajiri si halali inaweza kuamuriwa kuwa muajiri atekeleze moja ya mambo yafuatayo kwa mfanyakazi/muajiriwa husika


1. Kumrudisha muajiriwa kazini(reinstatement)hapa muajiriwa atarudishwa kazini na itahesabika alikuwepo kazini kutokea siku alipoachishwa kazi na atashahili kulipwa stahiki zake alizostahili kulipwa kwa kipindi chote tangu kuachishwa kwake.Pale ambapo amri ya kumrudisha muajiriwa kazini imetolewa na muajiri amashindwa kutekeleza amri hiyo,atapaswa kumlipa mfanyakazi huyo fidia ya mishahara ya miezi isiyopungua kumi na mbili(12) na stahiki nyingine alizostahili kulipwa tangu kuachishwa kwake

2. Kumuajiri upya mfanyakazi kwa mashari mapya yatakayoamuliwa na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi au Mahakama kuu kitengo cha kazi(Labour Court). Endapo mwajiri atashindwa kutekeleza amri hii,atalazamika kulipa fidia ya mishahara ya miezi isiyopungua kumi na mbili pamoja na stahiki nyingineambazo muajiriwa alistahili kulipwa tangu siku aliyoachishwa kazi isivyo halali.

3. Kumlipa mfanyakazi fidia ya mshahara wa miezi isiyopunguakumi na mbili.Pamoja na fidia hiyo,pia atalazimika kumlipa stahiki zake nyingine anazostahili kulipwa kwa mujibu wa sheria yoyote ile au makubaliano yoyote yaliyokuwepo kati ya muajiri na muajiriwa.
 
KUACHISHA KAZI

Kuachisha kazi kwa ujumla maana yake ni kumalizika/kuvunjika kwa mkataba wa ajira kati ya muajiri na muajiriwa. Kwa maneno mengine ni kumalizika kwa mahusiano ya kiajira kati ya muajiri na muajiriwa.Kusitishwa kwa mahusiano hayo kunaweza kuanzishwa na upande wowote wa mkataba huo(muajiri au muajiriwa)

Katika kanuni za ajira na Mahusiano kazin(Kanuni za utendaji bora)za mwaka 2007,imeelezwa kuwa kuachishwa kazi ni pamoja na:

a. Kuachisha kazi chini ya sheria ya kimila ya Uingereza(Common Law)

b. Muajiri kusababisha ugumu wa muajiriwa kuendelea na ajira

c. Kushindwa kuongeza mkataba wa muda maalum kwa masharti yaleyale au yanayofana kama kulikuwa na matumaini ya kuongeza mkataba

d. Kushindwa kumruhusu mfanyakazi kurejea kazini baada ya likizo ya uzazi au ulezi

e. Kushindwa kumuajiri tena mfanyakazi pale ambapo muajiriamewaachisha kaziwafanyakazi kadhaa kwa sababu kama hiyo au zinazofanan na ametoa nafasi za ajira kwa baadhi ya wafanyakazi walioachishwa kazi tu


KUACHISHA KAZI KIHALALI

Katika sheria ya Kimila ya Uingereza(Common Law) kuachisha kazi kumeelezwa kuwa ni pamoja na

I. Kuachisha kazi kwa makubaliano-hapa ni pale ambapo muajiri na muajiriwa wamekubaliana kusitisha mahusiano yao ya kiajira Kwa mfano kama mkataba wa ajira ni wa mwaka mmoja na muda huo umekwisha hapo mkataba utakuwa umefikia kikomo

II. Ajira kukoma yenyewe-hapa ni pale ambapo mkataba wa ajira unakuwa umesitishwa katika mazingira kama kifo au kumalizika kwa shughuli ya muajiri

III. Kuachishwa kazi kunakofanywa na muajiri-muajiri pia anaweza kusitisha mkataba wa ajira lakin itampasa kwanza kuzingatia na kufuata taratibu za kisheria.

Katika Kanuni za Ajira na Mahusiano Kazini(Kanuni za Utendaji Bora)za mwakwa 2007 Kanuni ya 7(1)inasema ku”pale ambapo muajiri anafanya ajira kushindwa kuvumilika ambapo pia inaweza kusababisha muajiriwa ajiuzulu,kujiuzulu huko kutakuwa sawa na kuacha kazi kwa kulazimika”


Sheria ya ajira na mahusiano kazini na kanuni zake ,pia imeeleza kuwa ili kuachisha kazikuwe ni halali basi ni lazima kuwe na sababu halali na ya haki(valid and fair reason) na utaratibu wa haki(fair procedure)uwe umefuatwa.Muajiri anapaswa kuwa na sababu halali na awe amefuata utaratibu wa haki katika kumuachisha kazi muajiriwa.


Taratibu za kuachisha kazi zinatofautiana kulingana na sababu inayopelekea kuachisha kazi,lakini taratibu zote hizo ni lazima zimpe muajiriwa nafasi ya kusikilizwa kabla ya uamuzi wa kumuachisha kazi.Bila kujali uzito wa kosa lililofanywa na muajiriwa ,bila kujali kuwa muajiri wake ana ushahidi wa kutosha,ni lazima sheria kufuata taratibu za kumuachisha kazi kama ilivyoelezwa katika sheria ya Ajira na Mahusiano kazini na 6. Ya mwaka 2004 na kanuni zake za mwaka 2007.


Kushindwa kufuata taratibu hizo kutamaanisha muajiriwa ameachishwa kazi bila kupewa nafasi ya kujitetea(summary dismissal)Kutompa muajiriwa nafasi ya kujitetea au kujieleza ni kumnyima haki yake ya kisheria.Kwa mujibu wa sheria za kazi kuachisha kazi kwa namna hii ni sawa na kuachisha kazi kusivyo halali(unfair termination)


Endapo itathibitika kuwa kuachisha kazi kulikofanywa na muajiri si halali inaweza kuamuriwa kuwa muajiri atekeleze moja ya mambo yafuatayo kwa mfanyakazi/muajiriwa husika


1. Kumrudisha muajiriwa kazini(reinstatement)hapa muajiriwa atarudishwa kazini na itahesabika alikuwepo kazini kutokea siku alipoachishwa kazi na atashahili kulipwa stahiki zake alizostahili kulipwa kwa kipindi chote tangu kuachishwa kwake.Pale ambapo amri ya kumrudisha muajiriwa kazini imetolewa na muajiri amashindwa kutekeleza amri hiyo,atapaswa kumlipa mfanyakazi huyo fidia ya mishahara ya miezi isiyopungua kumi na mbili(12) na stahiki nyingine alizostahili kulipwa tangu kuachishwa kwake

2. Kumuajiri upya mfanyakazi kwa mashari mapya yatakayoamuliwa na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi au Mahakama kuu kitengo cha kazi(Labour Court). Endapo mwajiri atashindwa kutekeleza amri hii,atalazamika kulipa fidia ya mishahara ya miezi isiyopungua kumi na mbili pamoja na stahiki nyingineambazo muajiriwa alistahili kulipwa tangu siku aliyoachishwa kazi isivyo halali.

3. Kumlipa mfanyakazi fidia ya mshahara wa miezi isiyopunguakumi na mbili.Pamoja na fidia hiyo,pia atalazimika kumlipa stahiki zake nyingine anazostahili kulipwa kwa mujibu wa sheria yoyote ile au makubaliano yoyote yaliyokuwepo kati ya muajiri na muajiriwa.
NIMEIELEWA VYEMA
 
Back
Top Bottom