Tanzania limekuwa taifa la wacheza kamari (Tanbet)

Kabla ya kuilaumu serikali tujilaumu sisi wananchi ngazi ya familia. Wazazi wako bize na kutafuta hela na kushindwa kuwafundisha watoto kwamba kamari ni mbaya. Kila mzazi angetimiza wajibu kusingekuwa na wateja wengi wa betting. Kamari zilikuwepo toka enzi na enzi. Nikiwa kijana mdogo pale Arusha karibu na soko kuu kama unaelekea St Thomas Hospital kulikuwa na sehemu zenye hizo mashine ila wateja walikuwa ni watu wazima na huwezi kukuta mafuriko ya watu. Ila kutokana na mmomonyoko wa maadili kuanzia ngazi ya familia ndo siku hizi kila kona kuna kamari.
 
Kamari inajenga uchumi. Haya mambk ya maadili hiyo ni dini lakini kama serikali inapaswa kuangalia kodi basi
 
Haya yote yamesababishwa na serikali ya kifisadi ya CCM pale inapoweka kamari kama chanzo chake kikuu cha kujipatia fedha. Inauma sana.
 
Haya yote yamesababishwa na serikali ya kifisadi ya CCM pale inapoweka kamari kama chanzo chake kikuu cha kujipatia fedha. Inauma sana.
Mlee mtoto wako katika njia impasayo. Kamari zilikuwepo enzi na enzi. Humu JF kuna nyuzi kibao za watu kutelekeza watoto. Je ni CCM pia imehusika?
 

 
Lazima atarudi tu, amini hilo
 
Itakua kaliwa sana. Lakini Uzi wake una uchambuzi mzuri sana
Wadau hawajanielewa kabisa mkuu. Afadhali wewe umengamua uchambuzi wangu. Tatizo watu wanakimbilia kucomment kabla ya kusoma uzi.
 
Mkuu nina wasiwasi bado hujaelewa maudhui ya huu uzi. Rudia tena kusoma. Hoja yangu ni zaidi ya hii unayodhania mkuu. Soma kwa utulivu utanielewa.
 
2013 to 2016

Ulikuwa uniambii kitu na hayo mabeting , lakini jambo la kushukuru sanaa 2016 mwishon nilipata mwendo mzuri sanaa na kuacha hayo mambo na kuanza mwanzo mpya aisee kamali sio nzuri wapendwa na kuacha pia sio rahisi kabsa yaani kama addicted wa pombe kumuachisha pombe ndio usawa wa kuacha kamali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…