Tanzania limekuwa taifa la wacheza kamari (Tanbet)

Kwa mujibu wa Statista, thamani ya soko la michezo ya kubahatisha Tanzania itakuwa dola 110.1 milioni (Sh260.4 bilioni), ifikapo mwaka 2027. Hali ikiwa hivyo, Serikali inapunguza fedha kwenye eneo la upishi wa vijana kuwa wataalamu.
Dah!... hatari kweli kweli...
 
Tanzania ina raia 60M+ na opportunity nyng asee nadhani kila mtu inabid afuate njia anayoamini inampa tonge la kila siku na maendeleo kwa ujumla
 
Mkuu pambana na maisha hizi harakat achana nazo,kamari zipo na zitaendelea kuwepo tena iyo miaka unayosema bila shaka utakua ushavuta lakini naamini kamari ndo zitazid kushamiri
 
Mkuu pambana na maisha hizi harakat achana nazo,kamari zipo na zitaendelea kuwepo tena iyo miaka unayosema bila shaka utakua ushavuta lakini naamini kamari ndo zitazid kushamiri
Mkuu achana na dhambi ya kamari ufike mbinguni
 
Dah!... hatari kweli kweli...
Hii n izaidi ya hatari mkuu. Taifa linaelekea kuzimu ndio maana serikali inapagawa inauza rasilimali za taifa kwa waarabu
 
Vijana waacheni wabeti na kama Kuna namna nyingine wasaidiwe!

Binafsi sijawahi beti ila na marafiki zangu wengi wanabeti Kila siku wanasuka mikeka kupata na kukosa wanajua wao, hv ndugu mwandishi unataka huyu kijana akafanye nini?

Twende pamoja
Graduates kibao wapo mtaani hawana mifumo rasmi ya kupata hela hapakuchi panakucha siku zinaenda kibishi kila siku mnatangaza fursa ni za kujitolea tu (internship) hapati hata mia

Kwenye kilimo hapagusiki huko kulihudumia ekari moja ni inatakiwa uwe na laki tatu na nusu plus ukivuna seke seke lake inalijua vzr sina haja ya kufafanua

Kila anapopagusa panataka awe na connection/ Mkono mrefu ndo asaidike Sasa atafanya nn si bora abeti tu Kwa mtaji wa buku?


Kwenye biashara hakusogeleki mfano mzuri jaribu wewe binafsi Kodi utakayotajiwa utashangaa ni 60% ya Ile hela uliyonayo utafanyaje? Wale jamaa wa tax assessment wanakatwa na dipi weldi 😒😒

We unashauri vijana wafanyeje? Kuna ambae uliwahi mkuta ana uraibu wa kamari ukajaribu kumsapoti apate kazi yeyote asogeze siku? Kama yupo vipi baada ya kumsapoti aliendelea?
 
Tanzania ina raia 60M+ na opportunity nyng asee nadhani kila mtu inabid afuate njia anayoamini inampa tonge la kila siku na maendeleo kwa ujumla
Lakini katika hizo njia utakazochagua jihadhari usichague kamari kwani itakufilisi ndani ya muda mfupi sana. Inashangaza badala ya serikali kukataza kamari, inawachochea vijana waingie. Hii nchi imerogwa wallah!
 
After 15 years from now inchi itakuwa na vijana wa hovyo sana
Miaka 15 mingi sana mkuu. Baada ya miaka 5 tu tutakuwa na taifa la mateja wa dawa za kulevya, kamari, ugolo na tumbaku na upumbavu mwingine mwingi tu!
 
Afadhali pombe au sigara mtu anaweza kuacha kwa urahisi mkuu. Kuacha kamari sio jambo jepesi.
 
Mkuu, kukosa kazi sio kisingizio cha kutopea kwenye uraibu wa kamari. Hata watu wenye staha na walioajiriwa wamepoteza muda na pesa nyingi sana kwenye kmari. Kwa ufupi, kamari ni janga la kitaifa. Kila mtanzania mwenye nia njema na nchi hii anapaswa kupiga vita kamari.
 
We ulikua unasikiliza TBC ili iweje
Niliisikiliza ili kukamilisha utafiti wangu wa redio zinazochezesha kamari. Sikuwahi kuamini kwamba hata redio inayojinasibu kuwa redio ya taifa nayo inachezesha kamari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…