Tanzania Military Intelligence vs TISS

Tanzania Military Intelligence vs TISS

Status
Not open for further replies.
Kifupi hivi vyombo vinafanya kazi kwa ukaribu na kwakushirikiana TISS ina idara nyingi kwa hapo ndo panakuja utofauti katika idara hizi sitazisema ila kifupi idara zote zinashirikiana kwa mfano nikama unavyoona Wizara ya Mambo ya Nje na Ikulu nikama mguu wakulia na wakushoto yote ni Miguu!
 
Sasa hii ya bosi mkubwa kama Jack Zoka kupelekwa Canada juwa balozi ni demotion au?
 
Wadau nadhani kwakuwa wote tumeshapata picha kuhusu hizi idara mbili. Sasa hebu tuangalie wamefaulu vipi ktk kazi zao. Nitoe mfano tu wa Marekani ambapo CIA na intelligence organisations zingine zimefanikiwa kuifikisha Marekani hapo ilipo na kuwa Taifa lenye nguvu na sauti zaidi hapa duniani.wamefanikiwa hata kuiangusha dola kubwa iliyokuwa Hasimu wake mkuu yaani USSR. Hata hivyo kuna sehemu idara hizo za kijasusi za USA zilifanya makosa hata kugharimu maisha ya watu. Mfano tukio la Sep 11.

Sasa kwa hapa kwetu, mtizamo wangu ni kwamba Hizi idara zetu zimefanya mengi makubwa sana hasa hali ya usalama na Amani iliyopo kwa miaka mingi sasa, umoja wa kitaifa na Jeshi lenye Nidhamu kubwa sana ambapo hata baadhi ya nchi zilishasikika zikitamani kuwa na Jeshi lenye nidhamu kama Tz. Kwasababu inaaminika kuwa ni mara chache sana kukuta nchi masikini ikawa na jeshi lenye nidhamu. Mifano ipo mingi sana. Sasa yote hii ni kazi ya idara zetu hizi.

Success ingine ya idara zetu hizi ni ushindi ktk vita ya kagera. Kuna msemo kuwa ukiwa na MI imara basi ni rahisi kushinda vita hata kama adui ana silaha kuliko zako. Hata hivyo pamoja na success ya zaidi ya 90% lakini pia kuna sehemu kulifanyika mistakes. Mfano:-

1. Kushindwa kuzuia mashambulizi kwenye ubalozi wa Marekani. Jukumu la Tiss

2. Mabomu ya gongo la mboto na mbagala. Jukumu la MI. Walipaswa ku fore see.

3. Kutoroka kwa kanali Seromba. Kinachodaiwa kuwa sio raia wa Tz na ni Mrwanda. Kama ni kweli basi Vetting ya kujiunga na Jeshi is questionable kwani hadi kufikia cheo hicho ni kwanini hakubainika. Yamkini kuna wengine wengi wamebaki bado. Na kama ni kweli alikuwa ni raia wa nchi jirani basi ujasusi wao ni wa hali ya juu kuzidi wa kwetu kwani wameweza kumuingiza mtu akiwa na umri mdogo hadi anapata vyeo vi kubwa karibia na retirement age.

INGAWA MENGI YALIYOFANYWA NA IDARA ZETU NI MAZURI NA YALIYOTUKUKA LAKINI WANATAKIWA KUWA MACHO ZAIDI

1: TISS kama Idara inapokea kila siku, kila wiki, kila mwezi na ata miaka yote threats mbali mbali zinazotishia usalama wa Taifa letu na usalama wa viongozi wa nchi, hivyo basi sometimes ni vigumu sana kuzichambua kila threats mpaka upate picha kamili kinachoendelea na kupata jawabu sababu information zinazokuja nyinginezo zinakuwa hazijakamilika toka kwa CI au Assets mbalimbali wanaoaminika na wasiohaminika wengineo ambao wanaotafuta pesa tu so for instance kama ukiweza ku-solve threats za kuaminika 100 na kwa bahati mbaya moja ukakosea baada ya miaka mingi then basi ujue bado Idara ipo vizuri zaidi unavyofikiria.


2: Kutokea kwa Mabomu ya Gongo la Mboto na Mbagala ni human error ambayo haiko related na intelligence gathering sema kama wangeshindwa kujua chanzo na kushauri nini kifanyike ku-prevent tukio kutokea then ungesema kuna uzembe na usije ukasema mbona ilitokea mara mbili? Watu wanashauri mambo mengi sana kila siku lakini hakuna anayefanyia kazi ushauri unaotolewa.


3: Kazi ya Counterintelligence ni ngumu sana sana kuliko unavyofikiria, inabidi uwe makini sana ku-deal na every situation that comes across...Kuangalia balozi zote na wafanyakazi wake, raia wageni, viongozi na wanasiasa, vyanzo vyote vya ulinzi na wafanyakazi wake, etc sio kazi ndogo sana. Unashangaa Tanzania kwa huyo Kanali cheo kidogo kabisa wakati Uingereza DG wa MI5 Sir Roger Hollis alikuwa DA wa KGB-Russia, Marekani walikuwa na intelligence analyst anaitwa Aldrich Hazen Ames alikuwa DA wa KGB-Russia, kama mifano ipo mingi tu naweza kukupa so hapo ndio ujue hii Kazi ni ngumu kuliko Kulima hekali 1 kwa jembe la mkono na ushukuru Mungu kila siku na unabidi upeleke pongezi kwa Idara.


Kwa ufupi tu kama siku ya leo imekwisha salama kwako na umeweza kula ugali wako na watoto wako salama na kesho utamka salama na nchi ipo na Amani basi endelea kuishukuru TISS kwa kila jambo wafanyalo na tujaribu kuacha siasa za vijiweni tu kuponda somehow hii Idara.
 
Inasemekana FFU kulinda ikulu na misafara ya Rais iliwekwa na Nyerere lakini kabla ya tishio la uasi miaka ya sitini hadi sabini ulinzi ulikuwa chini ya JWTZ .....wakongwe akina Jasusi , joka Kuu watatusaidia.....inasemekana kutumia FFU ni kuongeza complication in case jeshi likiasi ........Wakongwe wanaweza kutusaidia

cc Phillemon Mikael
 
Last edited by a moderator:
Sasa ndugu kama wanaweza shauri na viongozi wasifuate ushauri wao why should we have them? If we know this guys are toothless....sasa umadhubut wao uko wapi kama taifa linaendelea kuangamia? I realy appreciate to some extent military inteligence but not TISS...

...then CoveOps zinatumika. Na Kama unadhani hawana meno basi jipange wewe na wenzako mtake kupindua nchi na hapo ndipo utakapoijua Idara ina meno au haina meno!
 
nadhani MI ndo wale wanapiga kozi Ngerengere -Morogoro na TISS wengi huwa wanachukuliwa mavyuoni na sanasana JKT. hawa jamaa wako njema.. watz wengi tunawajua wale wa kitengo cha PSU na ndo maana tunaidharau hii idara ya Wizara ya mambo ya ndani but wanafanya kazi ya ukweli na amani yetu ni matokeo ya kazi yao nzuri
 
Okay,sasa hao wahamiaji haram inakuaje hukamatiwa let say Dodoma au Mbeya na hawakamatiwi wanakoingilia?

mkuu hawa wanaofanya hii kazi ni watu kama wewe.. hawaoti from nowhere bali taarifa kutoka kwetu pia zinawasaidia katika utendaji wao. usalama wako unaanza na wewe.. mfano ni kwa Marekani ambao wako imara sana kiusalama lakini mbona idara zake zilishindwa ku detect tukio la Sept 11???
 
mkuu hawa wanaofanya hii kazi ni watu kama wewe.. hawaoti from nowhere bali taarifa kutoka kwetu pia zinawasaidia katika utendaji wao. usalama wako unaanza na wewe.. mfano ni kwa Marekani ambao wako imara sana kiusalama lakini mbona idara zake zilishindwa ku detect tukio la Sept 11???

Behind the scene, shambulizi la sept 11 kwenye jengo la biashara WTO lilifanywa na bush mwenyewe, mchezo ulipangwa na CIA na MOSSAD, usiniulize kwanini walijilipua wenyewe.
 
Too general!!!

mkuu hawa TISS wana mafunzo yao na pia huwa wanafanya mafunzo na idara nyingine za kiusalama kama Polisi, JWTZ, MAGEREZA ndio maana nakwambia hawa jamaa wana mafunzo magumu
 
TISS ndo wana mafunzo magumu mkuu ingawa na JWTZ nao mmh.. wanatisha

duh hizi porojo sasa.hivi training za maafisa wa tiss unaweza kuzilinganisha na stages za mafunzo wanazopitia makomandoo wa JWTZ.?!
 
duh hizi porojo sasa.hivi training za maafisa wa tiss unaweza kuzilinganisha na stages za mafunzo wanazopitia makomandoo wa JWTZ.?!

mkuu nadhani ungejaribu kufanya follow up kabla ya kuongea.. kwenye hao makomandoo wa JWTZ.. TISS wana watu wao waliowaweka. kila idara na sio za kiusalama tu zina watu wa TISS kama hujui. wanawapenyeza ili kujua kinachofanyika na kama mambo yanaenenda yanavyopaswa. wewe ndo mpiga porojo katika hili
 
mkuu hawa wanaofanya hii kazi ni watu kama wewe.. hawaoti from nowhere bali taarifa kutoka kwetu pia zinawasaidia katika utendaji wao. usalama wako unaanza na wewe.. mfano ni kwa Marekani ambao wako imara sana kiusalama lakini mbona idara zake zilishindwa ku detect tukio la Sept 11???
Justification at work,waliofanya uchunguz walibain kuwa vyombo vya usalama vinahusishwa na biashara ya kusafirisha wahamiaji haramu.Kuhusu Marekani hapo The Intelligent amefafanua
 
Last edited by a moderator:
mkuu hawa TISS wana mafunzo yao na pia huwa wanafanya mafunzo na idara nyingine za kiusalama kama Polisi, JWTZ, MAGEREZA ndio maana nakwambia hawa jamaa wana mafunzo magumu
Magumu au yametawanyika kwa usawa wa mahitaji na kutegemea wapi agent anaenda kufanyia operations zake???!!!

"All weather does not necessarily means extreme weather conditions"!!!!

Anyway
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom