Tanzania Motorbike Road Trip - Tanga | Safari ya Tanga

Tanzania Motorbike Road Trip - Tanga | Safari ya Tanga

Maswali Mazuri sana.

1. Kuhusu Mafuta.. Tank langu la Mafuta ni lita 4.8.. wakati nipo Dar niliweka mafuta ya elfu 12000 ambayo nilipata full Tank.. pia ilibeba kidumu cha lita 5 ambacho hicho niliweka mafuta ya elfu 14 ambayo lita kama 4 hivi.

Mafuta yaliyo kwenye tank la pikipiki nimetembea nayo mpaka Mkata (niliposimama chai) nikajaza tena yaliyo kwenye kidumu lita 4.. lita 4 hiyo ikanifikisha hadi muheza ambako kwenye dumu niliweka elfu 13000 na kwenye pikipiki niliweka elfu 9.

Mafuta hayo toka hapo muheza yalinifikisha mpaka kiwanda cha cement kile ndipo nikachukua ya kwenye dumu ambayo niliingiza kwenye pikipki kama lita 2 hivi hivyo mpaka nafika TANGA nilikuwa na Mafuta ya kutosha kwenye pikipiki na kwenye Dumu ambayo niliyatumia kesho yake kwenda Amboni Cave

NB. Sikupenda niishiwe mafuta njiani ndo nijaze.. hivyo nilikuwa nikitembea kilomita kadhaa nasimama najaza

(Kuna mtu aliniambia usisubili mafuta yaishe sababu utakuwa unahalibu kableta (sijui nimepatia jina) ile ya kuvuta mafuta wakati upo safari ndefu

PIKIPIKI YANGU KWENYE SWALA LA MAFUTA INANUSA TU ILA HOFU YANGU NDO ILIYOPELEKEA NITEMBEE NA KIDUMU BUT BILA KUDUMU NINGEFIKA BILA WASIWASI NA MAFUTA (NDO SAFARI YANGU YA KWANZA)
Safi sana. Umeelezea vizuri mno. Asante kwa ku share safari yako.

Vipi kuhusu upepo njiani, haukuwa kero??
 
Kwa hapo Dar es Salaam unaweza jua Honda xr 125cc yaweza kua bei gani? Iwapo Kuna duka linauza new bike
Sijui bei yake XR, ila xl 125 inakuwaga arround 6.9M kama saba tu.
Xr125 na Xl125 hazitatofautiana sana nahisi.
 
Nilinunua kariakoo ilikuwa 95000.. yeah kazuri sana.. humo niliweka:
1. Mswaki
2. Sabuni
3. Nguo za kuvaa
4. Shuka la kimasai (ili nilibeba endapo ikitokea itilafu ya kunifanya nilale polini)
5. Koti la Mvua
6. Sendo/Ndala za kushindia
7. Baadhi ya Documents ya pikipiki
8. Maji na Biskuti

Vyote vilikaa humo.. sema uwe mzuri kwenye kuvipanga, ukipanga vibaya unaweza kuona Truck dogo kumbe ni kubwa sana
Essentials
 
Na mm nina mpango nikirudi home IRINGA niende mbeya nina boxer BM 150 mdomo wa bata....hiyoo itakuwa from IRINGA twn......munogage ukooo
 
Kwa kukazia zaidi, chukua Honda Ace 125cc au Yamaha ybr 125. Hizi zote ni imara, mafuta zinatumia kidogo pia huchoki kuendesha na zina afya zaidi. Kama ni mpenzi wa 5 speed ni vema ukachukua hii Yamaha ybr 125 gearbox yake ni 5 speed.
Sawa Mkuu najichanga hapa nitanunua hiyo Yamaha ybr
 
Mkuu hivi ndio wewe kuna uzi ulisema unaishi chalinze na kufanya kazi dar mkuu? Kwenda na pikipiki hadi chalinze kila siku ni risk na gharam za mafuta bora kupanga mjini.

Mi pia natumia pikipiki sana kwenye mizunguko yangu mjini ila sijawahi kutoka nayo hata bagamoyo tu
Hahaha mkuu uoga huo.. Bagamoyo hapo karibu tembea ata ufanye utalii wa ndani tu
 
Sio mm mkuu ...
Upo sahihi umbali mrefu huo kwa pikipiki ni risk sana...

Chalinze nilienda mwezi uliopita... ila bagamoyo nishaenda sana kama mara 5 ivi....
Hivi mkisema risk ni nini? Mimi kiukweli kusafiri kwangu na pikipiki sijaona risk yoyote sasa sijui nyie mnasema risk gani?

Nachojua Risk ni wewe na uendeshaji wako only that.. nyie mnasema risk gani hiyo?
 
Hivi mkisema risk ni nini? Mimi kiukweli kusafiri kwangu na pikipiki sijaona risk yoyote sasa sijui nyie mnasema risk gani?

Nachojua Risk ni wewe na uendeshaji wako only that.. nyie mnasema risk gani hiyo?
Mkuu risk zile njia zenye traffic kubwa wakati mwingine wenye magari hawaheshimu pikipiki. Unaweza kuwq upo upande wako kabisa lakin akakuletea hukohuko sasa kidogo unakuwa mwangalifu na ndio hapo inakuwa risk.

Mfano imewahi nitokea kwenye mapishano ya morogoro road pale jangwani ilipo yard ya mwendokasi. Mimi natoka fire naenda magomeni jamaa yupo na corolla anatoka magomeni akatishe kwenda jangwani kule ilipo jengo la Yanga. Sasa kikawaida ilipaswa asuburi nipite kabla yeye hajakunja kuja kuingia barabara yangu.

Licha ya kumpa warning kwa kuwasha taa na kupiga horn lakin nikastuka huyu hapa tayari kashaingia. Nikifunga brake kali lakin haikuzuiwa kuanguka japo sikuu hata kidogo naye hakuumia. Nilivunja indicator ya pembeni.

Mara nyingine ilikuwa barabara ya bandari mi natoka Kigamboni jamaa atoka bandari ndani aingie barabarani same mistake anaforce aingie kama nyoka tu.
 
Mkuu risk zile njia zenye traffic kubwa wakati mwingine wenye magari hawaheshimu pikipiki. Unaweza kuwq upo upande wako kabisa lakin akakuletea hukohuko sasa kidogo unakuwa mwangalifu na ndio hapo inakuwa risk.

Mfano imewahi nitokea kwenye mapishano ya morogoro road pale jangwani ilipo yard ya mwendokasi. Mimi natoka fire naenda magomeni jamaa yupo na corolla anatoka magomeni akatishe kwenda jangwani kule ilipo jengo la Yanga. Sasa kikawaida ilipaswa asuburi nipite kabla yeye hajakunja kuja kuingia barabara yangu.

Licha ya kumpa warning kwa kuwasha taa na kupiga horn lakin nikastuka huyu hapa tayari kashaingia. Nikifunga brake kali lakin haikuzuiwa kuanguka japo sikuu hata kidogo naye hakuumia. Nilivunja indicator ya pembeni.

Mara nyingine ilikuwa barabara ya bandari mi natoka Kigamboni jamaa atoka bandari ndani aingie barabarani same mistake anaforce aingie kama nyoka tu.
Uh pole sana Mkuu na Mungu Mwema kwa kuwa ulipona Salama..

Siku zote napokaribia katika makutano huwa napunguza mwendo ata kama gari hakuna (kutokana na uwezo wangu wa kuona) hivyo ni muhimu sana kwenye makutano yoyote upunguze mwendo na kumbuka kumpa kipaumbele anayetoka Mkono wako wa kulia.

Hii ya kipaumbele wa kulia kwako ni better zaidi sababu itakufanya uwe salama barabarani na kisheria
 
Nilivyokuwa Tanga Nikaenda Mapango ya Amboni (Amboni Cave) pia nikaenda Makumbusho ya Tanga.

Naomba nieleweke sifanyi Biashara ila najaribu kuwaonyesha watu Pikipiki ni Usafiri Mzuri na Salama kuliko ata Gari (Endapo utakuwa Makini na Kuzingatia Sheria za Barabarani)

NB: Nimefanya kile nakipenda kwenye Moyo wangu

 
Back
Top Bottom