Tanzania Premier League: Kuna ulazima wa klabu moja wapo (Simba au Yanga) iondoke Dar na kuhamia Arusha au Mwanza ili kuongeza ladha ya mchezo wa soka

Tanzania Premier League: Kuna ulazima wa klabu moja wapo (Simba au Yanga) iondoke Dar na kuhamia Arusha au Mwanza ili kuongeza ladha ya mchezo wa soka

Inter, juve, Madrid, Barcelona na nyinginezo zote zinakuwa pale zilipoanzishwa, utaanzaje kuhamisha Sima au Yanga kwenye makao makuu yake.
Nani atalipa gharama za kuwaweka nje ya Dar kuanzia wachezaji hadi watumishi.
Nakubaliana na yule aliyekwambia hujui chochote kuhusu mpira.
 
Kwani lazima mechi ya Yanga (ikiwa nyumbani) na Mwadui FC ichezwe Dar? Kwani haiwezi kuchezwa katika mkoa ambao haujafanikiwa kupeleka timu ligi kuu?
Hii itakua sio fair kwa yanga au nini maana ya mechi ya nyumbani na mechi ya ugenini? Yani Mwadui akiwa mwenyeji acheze kwake ila Yanga mechi yake ihamishwe au unataka kuaminisha nn sijaelewa.

Mfumo wa mpira wa miguu ulimwenguni kote kwenye ligi kuna mechi za nyumbani na za ugenini kipi haswa special kwa simba au yanga mpaka wasiwe na home game?
 
Inter, juve, Madrid, Barcelona na nyinginezo zote zinakuwa pale zilipoanzishwa, utaanzaje kuhamisha Sima au Yanga kwenye makao makuu yake.
Nani atalipa gharama za kuwaweka nje ya Dar kuanzia wachezaji hadi watumishi.
Nakubaliana na yule aliyekwambia hujui chochote kuhusu mpira.
Kuwahamisha sio tatizo kama wakiridhia na wakiamua hivyo, Gharama sio sababu kama pesa zipo...mbona serikali wakiwemo watumishi wake wananahamia Dodoma?

Sema tu hakuna timu hapo itakubali kirahisi
 
Kuwahamisha sio tatizo kama wakiridhia na wakiamua hivyo, Gharama sio sababu kama pesa zipo...mbona serikali wakiwemo watumishi wake wananahamia Dodoma?

Sema tu hakuna timu hapo itakubali kirahisi
Sio kila kitu ni siasa, sababu ya serikali kuhamia dodoma ni kuwa katikati ya nchi ili kuweza kutoa huduma kirahisi.

Ila kwa maendeleo ya sasa ya sayansi na teknologia hizo sababu zilikuwa zimepitwa na wakati.

Huwezi kuiondotoa team kwenye base fun yake sasa hivi Simba wana viwanja vya maxoezi Bunju pia wana eneo wanaloweza kujenga viwanja huko, yanga wana eneo kigamboni kwa kifupi ni hoja isiyo na mashiko na siyo hoja ya mtu anayefatilia mpira.
 
Kabla ya kujiuliza ya Simba na Yanga kuhama Dar, jiulize pia kwanini hatuna uwanja mzuri kama wa taifa nje ya Dar? hata wa kuingiza tuu watu elfu 30. Mbona timu ya taifa pia kila siku inacheza Dar tuu? yakiwezekana hayo basi hata kuhama simba au yanga Dar itawezekana
 
Wakati Azam inaanzishwa ningejua kiwango walichopanga kukiwekeza kwenye mpira ninhewashauri waweke mkoani....hapa namaanisha wangetengeneza mashabiki wao wengi kuliko pale dar ambapo watu wanaweza kama jibu siyo A basi lazima iwe ni B
 
Simba hawezi kuhama Dar kumbuka ameshaanza uwekezaji wa Viwanja na hostel
 
Yanga na Simba zote mbili zilianzishwa na Muzungu, kwa kifupi kama Muzungu hana mkono hakuna kitu kinafanikiwa hapa kwetu, kulingana na uzoefu wangu, na siyo Yanga na Simba tu hata angalia Coco Beach ndiyo Beach pekee ya maana Dar Mji uliojengwa ukingoni mwa Bahari na Coco ilitengwa na Mzungu, huko kwingine kote watu wamejenga kwenye fukwe, kwa nini watu watoke Mbagala na sehemu nyingine za Dar waende Coco beach kufwata ufukwe wakati huko kote Bahari ipo karibu?
 
Yanga na Simba zote mbili zilianzishwa na Muzungu, kwa kifupi kama Muzungu hana mkono hakuna kitu kinafanikiwa hapa kwetu, kulingana na uzoefu wangu, na siyo Yanga na Simba tu hata angalia Coco Beach ndiyo Beach pekee ya maana Dar Mji uliojengwa ukingoni mwa Bahari na Coco ilitengwa na Mzungu, huko kwingine kote watu wamejenga kwenye fukwe, kwa nini watu watoke Mbagala na sehemu nyingine za Dar waende Coco beach kufwata ufukwe wakati huko kote Bahari ipo karibu?
Umeshaenda beach za kigamboni
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa humu jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania mimi binafsi ninadhani;

Kuna umuhimu wa klabu moja wapo kubwa (Simba au Yanga) kuondoka Dar na kuhamia majiji mengine makubwa kama Arusha au Mwanza ili kuongeza ladha ya mchezo wa soka katika Tanzania Premier League.

View attachment 1628699

Kama serikali imeweza kutoka Dar na kuhamia Dodoma ili kuiacha Dar ipumue kutoka katika msongamano wa magari, kelele, watu kwanini hivi vilabu vishindwe? Mbona vilabu vya Barcelona na Real Madrid vipo majiji tofauti huko nchini Spain lakini wakiwa wanacheza uwanjani siku hiyo dunia nzima inasisimuka?

Kuna ulazima gani wa vilabu hivi vyote kuwa jiji moja kubwa, maarufu na la kibiashara mpaka sasa ilhali mashabiki wao wapo nchi nzima? Kwanini kusiwe tu na ofisi ndogo ya timu moja wapo kati ya simba au yanga kisha ofisi kuu pamoja na wachezaji wote wakahamia Mwanza au Arusha?

Kuna siku moja mwaka jana wa 2019 niliwahi kuwaza kwamba, kwanini kila mkoa usiwe na mashindano yake ya mchujo wa ndani kisha ukatoa timu moja tu itakayoshiriki ligi kuu ya Tanzania ili kuleta picha ya utaifa?

Lakini kabla sijawasilisha wazo hilo hapa kuna jambo likaniambia moyoni, itakuwaje kwa mkoa wa Dar ambao ndio kitovu cha soccer la hapa bongo kwa maana ndio mkoa unaobeba vilabu viwili vikubwa vinavyofahamika Afrika na duniani (Simba na Yanga)?

We need to counterbalance na kuongeza ladha ya mchezo wa soccer. Kwanini mechi ya Simba na Yanga iwe "big match" na "derby" kwa wakati mmoja?

Mbona Inter na Juventus zikicheza inakuwa ni big match lakini sio Derby?

Mbona kuna baadhi ya mechi za La Liga zinachezwa nje ya Spain lengo likiwa kuwapa ladha watu wengine nje ya nchi yao kwa maana ligi yao sasa ni super brand.

Kwani lazima mechi zote za nyumbani za Simba na Yanga zichezwe Dar? Kwanini mechi zingine za nyumbani za miamba hiyo miwili zisichezwe katika mikoa iliyoshindwa kuingiza timu katika ligi kuu ya soka ya Tanzania bara ili kuwapa ladha mashabiki ya mikoa hiyo?

View attachment 1628700

SWALI: Bado kuna ulazima gani wa vilabu hivi vikubwa viwili kuendelea kuweka makazi yao makuu katika jiji moja la Dar ilhali wana mashabiki nchi nzima?

SOMA PIA>>> https://www.jamiiforums.com/threads...dgar-tenga-tunakwama-wapi-kama-taifa.1750502/

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Mashabiki wa YANGA ambao ni CCM wao ndio wahamie CHAO , kuna uwanja mkubwa unajengwa huko , mpira utakuwa na ladha.
 
Mkuu, ina maana wewe haujiamini bila mzungu?...

Siyo swala la mimi, ni swala na uhaliasia na ukweli uliopo, huko Mikoani unakokuongelea kulikuwa na Timu nzuri tu, Mwanza kulikuwa na timu hata Tanga nao walikuwa na African sports na Coastal union, Iringa, Songea kote huko sasa ziko wapi, isitoshe hata hizi Yanga na Simba naweza kwenda mbali kusema kwamba zinanawili na kushamili sababu ya Wahindi, ukiondaoa akina Mo, Manji Azam & co. siajabu hakuna kitu kitabakia na ndio maana Mo ni kama Mungu kwa baadhi ya watu, ...
 
Back
Top Bottom