Tanzania: Serikali yapiga marufuku watoto kukaa bweni (boarding) kuanzia darasa la nne kushuka chini

Tanzania: Serikali yapiga marufuku watoto kukaa bweni (boarding) kuanzia darasa la nne kushuka chini

Analalamika utadhani huwa wanashikiwa bunduki kuwapeleka watoto boarding.
Tatizo ni wazazi kutowapenda watoto wao.
Watz tunaiga wazungu ila wazungu hawapeleki watoto boarding

Wazungu wamafanya kazi muda mrefu kuliko sisi ila familia ni muhimu sana kwao
 
Nliwahi kwenda visitation day ya mtoto wa mtu darasa la 5 ye alikua boarding..nkakutana na wengne kama miaka mitatu kiumri yani tufanye yupo baby class au middle class..halafu kawekwa boarding..nkashangaa!!

Ila naelewa ni changamoto za maisha na malezi tu.usiombee ukose mda wa kuwa free halafu una mtoto hana msaidizi
Boarding mtoto wa miaka mitatu hii hapana.

Ndio shida ya Tanzania tamaa za watu wachache zinataka kuwaaribia na wengine.

Boarding school ni kuanzia miaka 7 darasa la kwanza. Shule nyingi makini utakuta wanafanya hivyo na kuna usimamizi mzuri na ada zake pia juu kidogo.

Sasa naona kuna watu wachache wanataka kuwaaribia wengine kwa sababu demand ni kubwa.

Ingefaa wizara kuimarisha usimamizi wake na kutoa adhabu kali kwa shule ambazo zinakiuka sheria kwa kuchukua chekechea. Mfano ukibainika unafanya mambo ndivyo sivyo, sheria iruhusu wizara ya elimu kuchukua uongozi wa hiyo shule kwa muda, mwenye shule jela na baada ya muda serikali itafute mnunuzi kama ilikuwa private iuzwe, hela ukipatikana kama kuna madeni ya bank yalipwe biashara iishie hapo.

Haya mambo yanataka ubunifu lakini sio habari za samaki mmoja akioza wote awafai. Matatizo yanayosababishwa na watu wachache sio sahihi kutunga sera zinazowaumiza watu wote, wakati wengine wanaendesha shule zao vizuri tu.
 
Tatizo ni wazazi kutowapenda watoto wao.
Watz tunaiga wazungu ila wazungu hawapeleki watoto boarding

Wazungu wamafanya kazi muda mrefu kuliko sisi ila familia ni muhimu sana kwao
Aliekwambia wazungu awapeleki watoto boarding nani asilimia kubwa ya viongozi wakuu ni zao la boarding schools. Na wenyewe watoto zao wanapeleka huko huko, bado kuna watoto wa wafalme kuanzia primary.

Rish Sunak, David Cameron, Boris Johnson, Theresa May, Prince William, Harry wote hao boarding school. Hao ni maarufu tu hiyo civil service ukipekuwa huko kwao utakuta asilimia kubwa ni boarding school alumni’s.

Boarding school aliyosoma Fatma Karume uingereza hada yake ni kufuru na wazazi wanaanza kuomba miaka tano kabla mtoto ajafikia umri wa kuanza; hela wanazo na nafasi kupata sio guarantee. Boarding schools nyingi nchi za wenzetu zina ushindani mkubwa kweli kupata nafasi ni shule za watoto wa matajiri tu.
 
Walianza Kenya mwaka jana kufuta shule za bweni kwa primary schools...nikajisemea mwakani ama miaka saba ijayo itakuja Tanzania..safari hii naona tumekuwa fast kuact sijui labda kuna mkubwa kaumizwa na jambo ama hali imekuwa tete sana.

Ila Tanzania bado km kawaida tunalainisha mambo wamesema mwisho grade 4 au uwe na kibali maalum, ambapo kiuhalisia sababu maalumu zipo ndio maana wazazi wakawapeleka...kwahio zitaendelea kuwepo

Kiukweli nyakati zimebadilika...mzazi anatakiwa kuwa karibu sana na watoto below 18yrs bila hivyo tutalia sana baadae...maana changamoto ni nyingi, akili ni changa kuhimili hata addiction zingine zimeletwa wazazi tunachemka kuzihimili sembuse mtoto lakini sasa tunafanyaje na shule zenye walimu wazuri ni private na nyingi ni boarding schools..

Nikiangalia upande wa pili ndugu zetu wa rangi za mtume wanaacha wife home anatunza watoto, wao wanachakarika...sisi tunachakarika wote ili kuweza kukeep status fulani ya maisha.

Kwa single parents maana wengine ni kwa kudra za mwenyezi Mungu wengine ni changamoto za nyakati...wanatakiwa kufanya nini maana mahangaiko ya kutafuta pesa nyumbani uangalizi wa watoto ni finyu...na je sasa hv akirudishiwa mtoto nyumbani atajiadjust vipi.

Ama tunajiendekeza, kutafuta pesa sikuhizi hakuna limit ya muda...zamani mzazi akitoka kazini saa kumi yupo home.

Mtoto kashatoka tuition anakutana na mzazi home, sikuhizi mpaka analala hajamuona mzazi sijui ni foleni, ama order zimezidi emails za kutuma ni nyingi, ama utandawazi umekua demand ni kubwa inapelekea mzazi kuwork overtime...

Anyway ni jambo la kufikirisha...mizani sijui tutaubalance vp
 
Kwani mzazi kalazimishwa kupeleka boarding au ni kiherehere chake?
Mtoto Ana haki ya kuishi na kulelewa na wazazi ,huyu mtoto ktk umri huu hawezi kufanya maamuzi yoyote mtoto anarudi kutoka likizo kanyooka shingo na we mzazi umekazana unajisifu kwamba shule Fulani watoto wanafundishwa hatari eti kisa kakonda,huko shule hata hujui mwanao Kala Nini matokeo yake mtoto akirudia likizo mapenzi yote yamehamia kwa matroni na patroni
 
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imekumbusha kuwa hairuhusiwi huduma ya bweni kutolewa kwa wanafunzi wa elimu ya awali na darasa la kwanza hadi la nne....
Hii ni taarifa njema sana kwa wazazi haiwezekani mtoto aende bweni akiwa na miaka miwili tu huu ni uonevu kwa watoto.

Tangazo liende mbali zaidi kwa kupiga marufuku watoto wote wa primary school kukaa bweni.

Waende mbali zaidi kwa kupiga marufuku home works kwa watoto wa Nursery mpaka darasa la nne.

Wazuie below 7 years kuamka saa kumi usiku kwenda shule atleast waende shule saa mbili warudi saa sita.
 
Uamuzi huu makini umekuja kwa kuchelewa sana! Ni pia tunaomba boarding ipigwe marufuku kabisa kwa primary na kusiwe na excuse yoyote wala cha vibali!

Wenye Shule wengi wana njaa wako tayari kupokea pesa za mashoga!

Ninapongeza sana hatua hii, tuwe serious tuokoe Taifa hili.
 
kama ni kweli, WAKO SAHIHI, na ikiwezekana iwe marufuku shule bweni shule ya msingi mpaka sekondari.. bweni ianzie form six na hivi vyuo vya kati.. Vyuo vyote ambavyo wanasoma vijana baada tu ya kumaliza shule ya msingi navyo bweni iwe marufuku.

Hakuna mzazi anaependa kukaa mbali na mtoto wake..changamoto shule nzuri nyingi ni private na nyingi ni boarding schools...
 
Hata hizo za karibu shule zinalazimisha mtoto akiwa std 4 na 7 akae kwa ulazima boarding. Mimi niliwagomea wakanambia uwe una uwezo wa kumpeleka mtoto saa 12 asubuhi au nimuhamishe nikawaambia fresh tu kwakuwa siko mbali na shule akawa anawahi. Wanafosi kutaka ada za boarding kiulazima.
Mimi sikubali mwanangu below standard 6.kuwa boarding. Wengi miongoni mwetu hawajui kuwa values za Mlezi znatakiwa kuaimparted kwa mtoto toka akiwa mdogo. Mzazi ni key factor ya Akili na utu wa mtoto mpaka uzeeni. Boarding at low ages ni ujuha tu.
 
Swala hapa sio shule za boarding ndizo zinazopelekea mmomonyoko wa maadili. Hili swala ni Pana sana... Swala la maadili ni Pana sana.

Je tabia ya uchokoraa watoto wanajifunzia bording school.?
Je tabia ulevi na kutumia madawa ya kulevya wanajifunzia boarding. ?

Je tabia ya kutukana matusi yote ya nguon wanajifunzia boarding?
Je tabia ya udokozi na wizi wanajifunzia boarding?

Je tabia ya ulawiti na ushoga wanajifunzia boarding?

Hizo tabia zote hapo juu 98% watoto wanajifunzia mitaan na majumban huo ndo ukweli
Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo. Maamuzi ni yako. Basi.
 
mshatengeneza vichoko kibaaaaao ndio mwashtukia eeh, haya pumbaf zenu wakati wanaanzisha hizo boarding za vitoto mlikuwa wapi? maana wengine hawana hata chembe ya sababu za kupeleka watoto huko ni uvivu tu uliopitiliza na kujitia uzungu.
 
Hao Wazazi wanaopeleka watoto wa 2 yrs Boarding huwa wanalazimishwa au ni matakwa yao?
Hata kama ni matakwa yao huo ni uonevu kwa watoto.

Kumbuka watoto ni Mali ya umma wewe kazi yako ni kuzaa na kulea tu.
 
Back
Top Bottom