Tanzania Tulikuwa salama zaidi Mikononi mwa Ujamaa kuliko Tulivyo sasa Mikononi mwa Ubepari/Ubeberu

Tanzania Tulikuwa salama zaidi Mikononi mwa Ujamaa kuliko Tulivyo sasa Mikononi mwa Ubepari/Ubeberu

Mto hoja wewe ni Mwamba sana,tumerudi nyuma mara 1000 na sababu kuu ni moja veranda vyote vilivyojengwa na kufanya kazi katika kuishi sera ya ubepari vilibinafisihwa na wajanja wachache wakanufaika na badaye vilikufa-na matatizo ya kiuchumi kama kukosekana kwa ajili yakaanzia hapo.
Nashukuru sana Mkuu.
Nakumbuka miaka ya 1990 hivi sehemu ambazo zilikuwa na viwanda vidogo na vile vya kati vilikuwa zimechangamka sana kulinganisha na sasa hivi. Wale waliokulia sehemu zenye Ginery (viwanda vya kuchakata mazao yatokanayo na pamba ikiwemo mafuta ya pamba), wanaweza kushuhudia hili. Viwanda alivyojenga Mwl. vilisaidia sana nchi kutokuwa na matumizi makubwa sana ya fedha za kigeni katika kuagiza bidhaa toka nje ya nchi. Nchi yetu ilijitegemea kwa mambo mengi madogo madogo tofauti na ilivyo sasa. Tulizalisha mafuta ya kula, sabuni, nguo (Mwatex, Mutex), hapa hapa kwetu.
Maisha enzi hizo yalikuwa na "ladha" tofauti na ilivyo sasa.
 
China wamefanya hivyo na wamepiga hatua.

Mambo mengi hutegemea political will ili yaende.

Sisi hatuna viongozi wa aina ya China na Russia.

Yaani viongozi mabeberu lakini wazalendo, hao hatuna.
China ili fanya mabadiliko kadhaa ya kisera kwa ukomunisti wao naweza ita mabadiliko makubwa.

Kwa kiasi kikubwa ukomunisti wa mwanzo wa China na huu wa sasa wenye sifa za kichina una mabadiliko kadhaa.

Nyerere aligoma kufanya mabadiliko kwenye fikra zake kuhusu ujamaa wake ndio maana aling'atuka.
 
Ndiyo Mkuu.
Waafrika wengi kwa asili tulikuwa wajamaa
Kwa sababu tulikuwa tunaishi kimakundi jamii ndogo ndogo.

Unafikiri jamii kubwa kama taifa linaweza ishi mfumo wa kale bila mabadiliko ya usasa ?
 
Unataka turudi enzi za jumapili
Mwisho kutumia magari binafsi
Ni saa 12 jioni....[emoji1]

Ova
 
China wamefanya hivyo na wamepiga hatua.

Mambo mengi hutegemea political will ili yaende.

Sisi hatuna viongozi wa aina ya China na Russia.

Yaani viongozi mabeberu lakini wazalendo, hao hatuna.
Russia haina mfumo wa ujamaa wala ukomunisti kuanguka kwa U.S.S.R kuliangusha kila kitu
 
Wapo waliodhani furaha ya maisha ni kujilimbikizia mimali miiingiii !
Wakafaulu kujilimbikizia lakini wamekuja kugundua kumbe mali huwa haileti furaha ile waliofikiria wataipata wakiwa na mimali mingi !!

Ndicho kilichotutoa kwenye reli !!
Tamaa ya mimali mingi binafsi !!
Maisha ni yale yale,exactly unaweza kuwa na mimali mingi lakini ukawa unaishi maisha yasiyokuwa na furaha

Ova
 
Nathubutu kusema wewe Pascal Mayalla ni "genius ". Una uwezo mkubwa sana wa kuchambua na kupembua mambo.
Nina imani siku moja utatufaa sana sehemu mojawapo serikalini endapo tukipata viongozi wazalendo.
Asante sana, kwa umri wangu niliofikia, ni over and above kuteuliwa!. Mtu kulitumikia taifa na kuwatumikia Watanzania, sio lazima uteuliwe, haya maandiko yangu ya "Kwa Maslahi ya Taifa", ninayoandika humu na kwenye magazeti ni huduma tosha kwa Taifa na kwa Watanzania, and soon, kipindi kitaingia kwenye mainstream media
View: https://youtu.be/b67jqx0GWd8?si=dJMLlehgMKg5Ua5M na kitakuwa moto kama kile kipindi changu cha Kiti Moto
P
 
Kabisa kabisa ! Sisi wengine tulikuwepo wakati ule na sasa pia bado tupo we knew and we know the whole truth !!
Hatujalishwa matango pori sisi !!
Kukaa foleni ugawaji kusubiria,bidhaa
Sukari nk [emoji1]

Ova
 
Mkuu ulizoandika hapa ni propaganda,ukweli ni kuwa kuanzia miaka ya 1970's USA alianzisha mgogoro wa kiuchumi kupitia uhaba wa mafuta wenye lengo la kuua Sera ya ujamaa Duniani ili kuendeleza ukiranja wake wa Dunia ili apate uungaji mkono na kudidimiza Russia na China.
Vita baridi vimekuwepo toka kutamatika kwa vita vya pili na vilikuwa vya pande mbili U.S.A VS U.S.S.R, Ubepari Vs Ukomunisti.

U.S.S.R walipambana kuangusha ubepari sehemu yoyote duniani na U.S.A walipambana kusimika ubepari sehemu yoyote duniani.

U.S.A alitumia ubabe wa kiuchumi na kijeshi kunyong'onyesha wakomunisti sehemu yoyote duniani na Russia alitumia pesa na silaha kufadhili mapinduzi ya wakomunisti dhidi ya ubepari sehemu mbalimbali duniani.

Vita baridi vilikuwa vya pande mbili U.S.A na U.S.S.R sio upande mmoja pekee
 
Wewe ndio huna akili na ikiwezekana una matope kabisa,badlands ya kusema athali za ujamaa katika kipindi chake wewe unaleta athali za ujamaa baada ya mabeberu kuwapiga pini juu ya kuendesha Nchi kwa sera ya Ujamaa.
Kwa hio unadhani tukianza ujamaa saizi hatutapigwa pini?
Kama unapenda sana ujamaa hamia North Korea
 
Watu wengi wanamlaumu Nyerere na kuponda ujamaa wakidhani USA anauchukia ujamaa.
Ujamaa ni usoshalist ambao upo Israel ambao wana kibbutzim na Moshav.
Sweden ni wajamaa. Ujerumani ni wajamaa na ndio maana wana mpaka chama cha kijamaa (SDU cha akina Gerhard Shroder)
Japan ni wajamaa.

Na fuatilia mataifa yenye ujamaa, hakuna umasikini wala hakuna tajiri sana kama Elon Musk ila unashangaa taifa lenye uchumi mkubwa Ulaya ni wajamaa.
Hata timu kubwa ya kandanda kama Beyern Minchen inaendeshwa kijamaa.

Nyerere alikosa watu ambao walikuwa falsafa ya kujenga uchumi as kijamaa. Bahati mbaya alimpa Kawawa kuongoza jahazi wakati akiwa hajui model ya ujamaa inafanya vip kazi.
Ujamaa unatendeka vipi kwenye hizo nchi ulizo taja ?

Na tafsiri ya ujamaa kwa Nyerere ilikuwa ipi ?
 
Nashukuru sana Mkuu.
Nakumbuka miaka ya 1990 hivi sehemu ambazo zilikuwa na viwanda vidogo na vile vya kati vilikuwa zimechangamka sana kulinganisha na sasa hivi. Wale waliokulia sehemu zenye Ginery (viwanda vya kuchakata mazao yatokanayo na pamba ikiwemo mafuta ya pamba), wanaweza kushuhudia hili. Viwanda alivyojenga Mwl. vilisaidia sana nchi kutokuwa na matumizi makubwa sana ya fedha za kigeni katika kuagiza bidhaa toka nje ya nchi. Nchi yetu ilijitegemea kwa mambo mengi madogo madogo tofauti na ilivyo sasa. Tulizalisha mafuta ya kula, sabuni, nguo (Mwatex, Mutex), hapa hapa kwetu.
Maisha enzi hizo yalikuwa na "ladha" tofauti na ilivyo sasa.
Ulisoma ripoti ya mwanzo baada ya kuanza utekelezaji wa Azimio la Arusha matokeo yake yalikuwa yapi ?
 
Mkuu ulizoandika hapa ni propaganda,ukweli ni kuwa kuanzia miaka ya 1970's USA alianzisha mgogoro wa kiuchumi kupitia uhaba wa mafuta wenye lengo la kuua Sera ya ujamaa Duniani ili kuendeleza ukiranja wake wa Dunia ili apate uungaji mkono na kudidimiza Russia na China.
Kufeli kwa ujamaa kunaanzia mbali sana kabla ya kufika kwenye USA na washikaji zake,

Uzalisha ndani ya nchi tu ulikuwa mdogo,
Tulishindwa kuzalisha Sabuni, sukari, mafuta na hata chumvi ya kutosha wakati tuna bahari kubwa, na hapo USA alitutesa? Mwinyi anadai UDA ilikuwa inakufa kabisa, ufanisi ulikuwa chini ya sifuri, napo USA ? Nyerere alipiga marufuku TV na computer 💻 kwa raia wake wasipate kujua yanayoendelea nje, na pia wasipate kufunguka kifikra, nayo tulaumu USA,
USA alikuja tu kupiga msumari wa mwisho kwenye jeneza, ila ujamaa ulijizika wenyewe, hata USA asingeingilia, ujamaa ulikuwa unafeli, sera kama vijiji vya ujamaa, maduka ya ushirika, ni sera ambazo no way huku duniani zitafanikiwa, hata ufanyaje hutoboi


Ujamaa unafeli kwa sababu unajengwa kwenye misingi ya kuleana watu wavivu na wenye nguvu wote kuwakandamiza
 
Amani iwe nanyi nyote.
Kwa wale wazee wenzangu mtakubaliana na mimi kwamba Tanzania ingekuwa mbali zaidi kimaendeleo endapo ingeendelea na mfumo wa Ujamaa chini ya chama kimoja kuliko ilivyo sasa.

Uchumi wetu ulianza kuyumba mara tu awamu ya pili chini ya Mzee Ruksa, Alhaji Ali Hassani Mwinyi ilipoingia madarakani na kuusaliti Ujamaa wa Hayati Mwl. JKN.

Hadi kufikia mwaka 1987, uchumi wa Tanzania ulikuwa unaongoza kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati. Hii ina maana uchumi wetu ulikuwa mkubwa kuliko hata wa Kenya ambayo ndiyo kinara kwa kuwa na uchumi mkubwa katika ukanda huu kwa sasa!

Miaka ya 1990 tulipokubaliana na mambo ya kipuuzi kama nchi, tukapoteana kabisa na hali yetu haijatengamaa mpaka kesho. Fedha yetu inazidi kuporomoka mwaka hadi mwaka huku kukiwa na pengo kubwa sana kati ya wenye nacho na wasionacho.

Hivyo ushauri wangu ni serikali kufanya kila linalowezekana kuturudisha katika mfumo wetu wa Ujamaa; Sera inayotutofautisha sisi na majirani zetu. Hii itasaidia kuleta ustawi kwa wote na kutuondolea kero ya kuwa na viongozi wezi na vibaka waliojificha kwa mavazi ya uongozi.
Asalaam Aleykum.
...1980 uchumi ulianza kwenda Kombo ....mara kwanza JKN aliomba kutoka 1983.....wapambe kina Butiku wakagoma....1985 akasema siombi tena ushauri akatoka....alishaona ujamaa sio njia pekee tena kumiliki na kukuza uchumi...kama tulivyolaririshwa.....wewe unachosema hukielewii
 
Back
Top Bottom