Tanzania Tulikuwa salama zaidi Mikononi mwa Ujamaa kuliko Tulivyo sasa Mikononi mwa Ubepari/Ubeberu

Tanzania Tulikuwa salama zaidi Mikononi mwa Ujamaa kuliko Tulivyo sasa Mikononi mwa Ubepari/Ubeberu

Amani iwe nanyi nyote.
Kwa wale wazee wenzangu mtakubaliana na mimi kwamba Tanzania ingekuwa mbali zaidi kimaendeleo endapo ingeendelea na mfumo wa Ujamaa chini ya chama kimoja kuliko ilivyo sasa.

Uchumi wetu ulianza kuyumba mara tu awamu ya pili chini ya Mzee Ruksa, Alhaji Ali Hassani Mwinyi ilipoingia madarakani na kuusaliti Ujamaa wa Hayati Mwl. JKN.

Hadi kufikia mwaka 1987, uchumi wa Tanzania ulikuwa unaongoza kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati. Hii ina maana uchumi wetu ulikuwa mkubwa kuliko hata wa Kenya ambayo ndiyo kinara kwa kuwa na uchumi mkubwa katika ukanda huu kwa sasa!

Miaka ya 1990 tulipokubaliana na mambo ya kipuuzi kama nchi, tukapoteana kabisa na hali yetu haijatengamaa mpaka kesho. Fedha yetu inazidi kuporomoka mwaka hadi mwaka huku kukiwa na pengo kubwa sana kati ya wenye nacho na wasionacho.

Hivyo ushauri wangu ni serikali kufanya kila linalowezekana kuturudisha katika mfumo wetu wa Ujamaa; Sera inayotutofautisha sisi na majirani zetu. Hii itasaidia kuleta ustawi kwa wote na kutuondolea kero ya kuwa na viongozi wezi na vibaka waliojificha kwa mavazi ya uongozi.
Asalaam Aleykum.
Ujamaa/Ukomunisti ni LAANA kubwa sana hapa duniani.
Chini ya Sera, Fikra na Falsafa ya Ujamaa/Ukomunisti, inaamini kwamba Raia wote ktk nchi ni MATEKA wa Mwenyekiti. Katika msingi huu, kamwe raia hamuwezi kuwa na maendeleo na wala hamuwezi kuishi kwa furaha na amani, badala yake raia wataishi kama wapo jehanamu.
 
...1980 uchumi ulianza kwenda Kombo ....mara kwanza JKN aliomba kutoka 1983.....wapambe kina Butiku wakagoma....1985 akasema siombi tena ushauri akatoka....alishaona ujamaa sio njia pekee tena kumiliki na kukuza uchumi...kama tulivyolaririshwa.....wewe unachosema hukielewii
Mwalimu alikataa kushusha thamani ya shilingi ya Tanzania kama alivyotakiwa kufanya na IMF na World Bank ili Nchi ikopeshwe pesa !
Hivyo akaamua ni bora ang’atuke kuliko ageuke jiwe kwa kukubali masharti ya wakubwa wa Dunia !!
 
Watu wengi wanamlaumu Nyerere na kuponda ujamaa wakidhani USA anauchukia ujamaa.
Ujamaa ni usoshalist ambao upo Israel ambao wana kibbutzim na Moshav.
Sweden ni wajamaa. Ujerumani ni wajamaa na ndio maana wana mpaka chama cha kijamaa (SDU cha akina Gerhard Shroder)
Japan ni wajamaa.

Na fuatilia mataifa yenye ujamaa, hakuna umasikini wala hakuna tajiri sana kama Elon Musk ila unashangaa taifa lenye uchumi mkubwa Ulaya ni wajamaa.
Hata timu kubwa ya kandanda kama Beyern Minchen inaendeshwa kijamaa.

Nyerere alikosa watu ambao walikuwa falsafa ya kujenga uchumi as kijamaa. Bahati mbaya alimpa Kawawa kuongoza jahazi wakati akiwa hajui model ya ujamaa inafanya vip kazi.
Kama hata wasaidizi wake wa karibu hawakuuelewa huo ujamaa hata raia pia ilikuwa ni haki vile vile kutomuelewa.
 
Ujamaa unatendeka vipi kwenye hizo nchi ulizo taja ?

Na tafsiri ya ujamaa kwa Nyerere ilikuwa ipi ?
Namna bora kabisa ya utafiti ni participant observation. Ukiweza fika Japan au Slovenia au Ujerumani/Israel/Sweden; ongea nao, ishi nao, ona namna usoshalist ulivyo.
Sio kila kitu utaelewa kwa google au vitabu. Kuona na kuishi ni kupata real experience ya nini kinaendelea.
 
Mkuu tunashukuru sana kwa bandiko hili lililosheheni "madini" tupu. Binafsi huwa navutiwa sana na nyuzi zako pamoja na michango yako kwa ujumla ukiachilia michache ambayo kwa kweli binafsi huwa nafikiria kuna watu huwa wanatumia account yako! Huyu aliyetoa "madini" haya ndo Pascal Mayala original.
😁😁😁😁
Ubarikiwe sana Mkuu.
Kumbe ulikuwa unawaza Kama Mimi👇.
Kuna mda huyu bro anazinguaga kinyama.
Kiufupi huwa tupo smart,ila ila ninapowaza kuhusu siasa za chama chake na kufumbia baadhi ya Mambo ya hovyo na kusifia baadhi ya vitu ambavyo ni ukakasi kwa watu wengine huwa naumia Sana.
 
Namna bora kabisa ya utafiti ni participant observation. Ukiweza fika Japan au Slovenia au Ujerumani/Israel/Sweden; ongea nao, ishi nao, ona namna usoshalist ulivyo.
Sio kila kitu utaelewa kwa google au vitabu. Kuona na kuishi ni kupata real experience ya nini kinaendelea.
Umeshindwa kuelezea
 
Laiti kama siku moja nikawa kwenye nafasi ya kufanya maamuzi nchi hii, nitahakikisha nafanya kila linalowezekana kuirudisha hii nchi kwenye msitari. Tanzania ni nchi kubwa na tajiri sana na inapaswa kuwa hivyo hata kwa hali ya maisha ya wananchi wote pia na siyo kwa wachache tu.
Uzuri ni kwamba you will never be. Utabaki kuwa rais wa keyboard.
 
Ujamaa uko kinyume na asili ya binadamu ndiyo maana kote duniani umeshindikana ku impelement.

Ujamaa ni kugawana umasikini miongoni mwa jamii., kufanya matajiri wawe masikini na masikini wawe masikini zaidi
 
Laiti kama siku moja nikawa kwenye nafasi ya kufanya maamuzi nchi hii, nitahakikisha nafanya kila linalowezekana kuirudisha hii nchi kwenye msitari. Tanzania ni nchi kubwa na tajiri sana na inapaswa kuwa hivyo hata kwa hali ya maisha ya wananchi wote pia na siyo kwa wachache tu.
Mimi nawaza tu,mahali pa kuanzia ni kusafisha wasomi wanasiasa kwa damu na moto.
Hawa tuliowaamini na kuwapa dhamana ya kutawala na wakatumia fursa hii kutuuza kwa matajiri wahuni wa ndani na nje.Wakatulazimisha tuwe na elimu inayotufanya watumwa wa wanasiasa na matajiri.
Nchi ikishatakaswa,ndipo tunaanza upya na akili mpya kama vile ndio kwanza tumepata uhuru
 
Kuna Mambo mazuri ya ujamaa na mabaya, hata ubepari una Mambo mazuri na yasiyofaa. Tatizo ni pale tulipovunja azimio la Arusha na kuwaruhusu viongozi kuwa wafanyabiashara. Hapo Kila kiongozi akiingia anawaza namna ya kupata Mali na njia rahisi ya kutajirika ni kupitia siasa.
 
Amani iwe nanyi nyote.
Kwa wale wazee wenzangu mtakubaliana na mimi kwamba Tanzania ingekuwa mbali zaidi kimaendeleo endapo ingeendelea na mfumo wa Ujamaa chini ya chama kimoja kuliko ilivyo sasa.

Uchumi wetu ulianza kuyumba mara tu awamu ya pili chini ya Mzee Ruksa, Alhaji Ali Hassani Mwinyi ilipoingia madarakani na kuusaliti Ujamaa wa Hayati Mwl. JKN.

Hadi kufikia mwaka 1987, uchumi wa Tanzania ulikuwa unaongoza kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati. Hii ina maana uchumi wetu ulikuwa mkubwa kuliko hata wa Kenya ambayo ndiyo kinara kwa kuwa na uchumi mkubwa katika ukanda huu kwa sasa!

Miaka ya 1990 tulipokubaliana na mambo ya kipuuzi kama nchi, tukapoteana kabisa na hali yetu haijatengamaa mpaka kesho. Fedha yetu inazidi kuporomoka mwaka hadi mwaka huku kukiwa na pengo kubwa sana kati ya wenye nacho na wasionacho.

Hivyo ushauri wangu ni serikali kufanya kila linalowezekana kuturudisha katika mfumo wetu wa Ujamaa; Sera inayotutofautisha sisi na majirani zetu. Hii itasaidia kuleta ustawi kwa wote na kutuondolea kero ya kuwa na viongozi wezi na vibaka waliojificha kwa mavazi ya uongozi.
Asalaam Aleykum.
Ujamaa umeshakufa toka miaka ya tisini baada ya kujunjika USSR na ukuta wa berlin. Nchi zilizokuwa namba moja katika ujamaa(China na Russia) leo hii ndo zinazozalisha mabilionea wa kibepari. Kosa letu ni bado tupo kijamaa ambapo serikali inapewa mamlaka kubwa. Lakini hao viongozi wa serikali hawana vigezo na sifa za kupewa haya mamlaka makubwa ya nchi. Tunatakiwa tuige nchi zilizoendelea kwa kuzipa vigezo kampuni na sekta binafsi. Tukiwapa sekta binafsi kipaumbele kwa kuwapa masharti ya kuwa na mazingira mazuri ya kazi. Na kutoa ajira kwa kiasi fulani tutafika mbali sana. Hii nchi magazeti yamejaa siasa, burudani na michezo. Tanzania iwape wawekezaji mazingira yaliyo bora kuliko. Unawapa tu masharti kuajiri watu 10000, halafu halipi hata senti ya kodi. Wewe kama serikali unapata hela kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii. Unakuta katika nchi yetu tuna mabilionea wa dola wameajiri watu bila bima ya afya wala mikataba na bado wanapata upendeleo wa kodi. System haitakiwi kumpa kipaumbele raisi na viongozi wa serikali. Mfumo inabidi upendelee kampuni na sekta binafsi. Huku ujerumani miji ambayo viwanda vipyo viwanda ndo vinasimamia maendeleo kwa asilimia kuda. Ukifika makao makuu ya Audi katika mji wa Ingolstadt. Audi ndo imejenga Uwanja wa mipira, Mall kubwa ya Westpark, Arena ya michezo mbali mbali. Pia Audi inandaa matamasha mbali mbali wanamuziki wanakuja kwa udhamini wao. Ukiwapa kipaumbele viongozi wa serikali katika media wanatumia hela za kodi ambazo ni za kwako wewe mwananchi. Lakini unapoipa kipaumbele sekta binafsi hawawezi kukuangusha maana wanalazimika kuhakikisha kuwa huduma muhimu zinapatikana ili kuimarisha uzalishaji wao. Tungekuwa na sekta binafsi imara haya mafuriko ya Hanang makampuni mengi yangefika na ku solve matatizo. Lakini serikali inafika pale kufanya PR badala ya kusolve. Na hata kama wakitaka ku solve haya matatizo kuna maofisa wanataka kupiga hela na sio kusaidia. Huu ni mtazamo wangu kutokana na nilichoexperience.
 
Amani iwe nanyi nyote.
Kwa wale wazee wenzangu mtakubaliana na mimi kwamba Tanzania ingekuwa mbali zaidi kimaendeleo endapo ingeendelea na mfumo wa Ujamaa chini ya chama kimoja kuliko ilivyo sasa.

Uchumi wetu ulianza kuyumba mara tu awamu ya pili chini ya Mzee Ruksa, Alhaji Ali Hassani Mwinyi ilipoingia madarakani na kuusaliti Ujamaa wa Hayati Mwl. JKN.

Hadi kufikia mwaka 1987, uchumi wa Tanzania ulikuwa unaongoza kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati. Hii ina maana uchumi wetu ulikuwa mkubwa kuliko hata wa Kenya ambayo ndiyo kinara kwa kuwa na uchumi mkubwa katika ukanda huu kwa sasa!

Miaka ya 1990 tulipokubaliana na mambo ya kipuuzi kama nchi, tukapoteana kabisa na hali yetu haijatengamaa mpaka kesho. Fedha yetu inazidi kuporomoka mwaka hadi mwaka huku kukiwa na pengo kubwa sana kati ya wenye nacho na wasionacho.

Hivyo ushauri wangu ni serikali kufanya kila linalowezekana kuturudisha katika mfumo wetu wa Ujamaa; Sera inayotutofautisha sisi na majirani zetu. Hii itasaidia kuleta ustawi kwa wote na kutuondolea kero ya kuwa na viongozi wezi na vibaka waliojificha kwa mavazi ya uongozi.
Asalaam Aleykum.
UJAMAA NI MUHIMU SAANA
 
Uchumi wa kibepari sidhani kama unazuia serikali kutekeleza majukumu yake ya kuleta maendeleo ya nchi, ujamaa ni umasikini na kwa kiasi kikubwa ndio unaotuchelewesha, hata hizo nchi zilizoendelea kwa ujamaa kama China na Urusi hazina ujamaa huo tunaoutaka sisi
 
Amani iwe nanyi nyote.
Kwa wale wazee wenzangu mtakubaliana na mimi kwamba Tanzania ingekuwa mbali zaidi kimaendeleo endapo ingeendelea na mfumo wa Ujamaa chini ya chama kimoja kuliko ilivyo sasa.

Uchumi wetu ulianza kuyumba mara tu awamu ya pili chini ya Mzee Ruksa, Alhaji Ali Hassani Mwinyi ilipoingia madarakani na kuusaliti Ujamaa wa Hayati Mwl. JKN.

Hadi kufikia mwaka 1987, uchumi wa Tanzania ulikuwa unaongoza kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati. Hii ina maana uchumi wetu ulikuwa mkubwa kuliko hata wa Kenya ambayo ndiyo kinara kwa kuwa na uchumi mkubwa katika ukanda huu kwa sasa!

Miaka ya 1990 tulipokubaliana na mambo ya kipuuzi kama nchi, tukapoteana kabisa na hali yetu haijatengamaa mpaka kesho. Fedha yetu inazidi kuporomoka mwaka hadi mwaka huku kukiwa na pengo kubwa sana kati ya wenye nacho na wasionacho.

Hivyo ushauri wangu ni serikali kufanya kila linalowezekana kuturudisha katika mfumo wetu wa Ujamaa; Sera inayotutofautisha sisi na majirani zetu. Hii itasaidia kuleta ustawi kwa wote na kutuondolea kero ya kuwa na viongozi wezi na vibaka waliojificha kwa mavazi ya uongozi.
Asalaam Aleykum.
Yaani uturudishe kwenye ujamaa??? Hv unajua hata wachina wenyewe ujamaa umebakia kwenye makaratasi??? Mpk mchonga anaachia madaraka ni kutokana na kufeli kwa siasa za ujamaa
 
Amani iwe nanyi nyote.
Kwa wale wazee wenzangu mtakubaliana na mimi kwamba Tanzania ingekuwa mbali zaidi kimaendeleo endapo ingeendelea na mfumo wa Ujamaa chini ya chama kimoja kuliko ilivyo sasa.

Uchumi wetu ulianza kuyumba mara tu awamu ya pili chini ya Mzee Ruksa, Alhaji Ali Hassani Mwinyi ilipoingia madarakani na kuusaliti Ujamaa wa Hayati Mwl. JKN.

Hadi kufikia mwaka 1987, uchumi wa Tanzania ulikuwa unaongoza kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati. Hii ina maana uchumi wetu ulikuwa mkubwa kuliko hata wa Kenya ambayo ndiyo kinara kwa kuwa na uchumi mkubwa katika ukanda huu kwa sasa!

Miaka ya 1990 tulipokubaliana na mambo ya kipuuzi kama nchi, tukapoteana kabisa na hali yetu haijatengamaa mpaka kesho. Fedha yetu inazidi kuporomoka mwaka hadi mwaka huku kukiwa na pengo kubwa sana kati ya wenye nacho na wasionacho.

Hivyo ushauri wangu ni serikali kufanya kila linalowezekana kuturudisha katika mfumo wetu wa Ujamaa; Sera inayotutofautisha sisi na majirani zetu. Hii itasaidia kuleta ustawi kwa wote na kutuondolea kero ya kuwa na viongozi wezi na vibaka waliojificha kwa mavazi ya uongozi.
Asalaam Aleykum.
Ni ngumu Sana kumchomoa Mtakatifu Nyerere kwenye hii laana ya dhulma, yeye ndie alieasisi chama hichi kisha akawepo hadi kinapevuka
 
Back
Top Bottom