Tanzania tuna protocol za ovyo kabisa kwa Viongozi wetu

Tanzania tuna protocol za ovyo kabisa kwa Viongozi wetu

Yaani kiongozi anashuka kwenye gari anazungukwa na minders zaidi ya hamsini wengine wananing'inia kwenye milango, hadi kiongozi anaenda kukaa jukwaani kaambatana na minders zaidi ya 20 wanamzunguka hadi anakaa na bado kuna wanamsimamia kwa nyuma, kwa hatari gani aliyokuwa nayo kiongozi wa nchi masikini kama Tanzania hadi awe na ulinzi mkubwa kuliko kiongozi wa marekani au uingereza aliyekuwa na bifu kubwa na makundi kibao ya ugadi duniani?viongozi mpaka ikaja kuwa normal kwa viongozi kuzungukwa na wapambe wengi kupita uhitaji.
Jaribu kufuatilia vizuri ili ujue ni yapi yaliyokuwa yakimpata yule aliyepita kabla ya huyu, ambayo wewe ulikuwa hutangaziwi, halafu ndiyo uendelee na hizi criticisms zako. Unajua tena watu tukishakula halafu tukashiba!
 
Usimsahau na Kiranga
Ila niliwahi Kumuliza Head Of Psu Wa Sasa Wambura, Why Mnakuwa na tited security Sana Kwa Wakuu Wa Nchi, Akasema Wanataka Wao [emoji1][emoji1][emoji1]
Kwa nchi kama Marekani, rais kulindwa na walinzi wengi, hususan wanaoonekana waziwazi wameshika silaha kubwa za moto, ni suala la aibu.

Viongozi wanataka kuonesha picha ya kwamba Marekani ni nchi ya demokrasia, viongozi wana imani sana na usalama wao bila ya ulinzi mkali, wanapendwa na watu.

Hii dhana ina tija kwa kiwango fulani, lakini ikizidishwa ina madhara yake. Mfano mmoja ni mauaji ya rais John F. Kennedy, yaliyowezekana kufanyika kirahisi kwa sababu rais alikuwa kwenye gari ya wazi, kwa sababu alitaka kuwaona wananchi na wananchi wamuone, bila ya ulinzi mkubwa sana.Inasemekana walinzi wake walimshauri asipande gari la wazi, lakini rais Kennedy alikataa, akiamini hakuna tatizo la kiusalama.

Kwa kawaida marais wa Marekani wanahusisha ulinzi mkubwa, hususan wa silaha nzito zinazoonekana wazi, kuwa ni tabia za tawala za kijeshi, za kidikteta, zisizo na demokrasia, ambazo hazijiamini na zinapenda kutisha wananchi.

Binafsi sikupendelea muonekano wa kijeshi ulioanza kuingia serikalini kipindi cha Magufuli, kiasi cha kwamba si tu ulinzi wa rais ulikuwa kijeshi zaidi na walinzi kubeba silaha kubwa za moto, bali pia hata rais mwenyewe, ambaye si mtawala wa kijeshi, alipenda kuvaa magwanda ya kijeshi.

Sijawahi kumuona rais mwingine yeyote wa Tanzania kavaa magwanda ya jeshi bila kuwa vitani. Hata Kikwete ambaye alikuwa mwanajeshi.

Kuna picha chache tu za Nyerere amevaa kijeshi, hususan kimgambo, hususan wakati wa vita vya Kagera au operesheni maalum za kijeshi.

Marais walielewa kanuni ya "civilian leadership/ control of the military".

Uongozi wa kidemokrasia wa kiraia unaongoza jeshi, na taswira inayotolewa na uongozi inatakiwa kuwa ya uongozi wa kiraia.

Si wa kijeshi.

 
Lakini hata Rais wa Marekani huwa analindwa na askari wenye mabunduki makubwa.

Ushawahi kuushuhudia msafara wa Rais wa Marekani?

Kama umewahi, basi huwezi shindwa kuwaona jamaa wa CAT na magwanda yao pamoja na mabunduki yao.

Juzi tu nimetoka kuushuhudia hapa….na jamaa walikuwepo kamili gado….kikosi kizima!

81E298AB-4BC6-4490-B7AF-3C66FD6BB7D2.jpeg
 
Lakini hata Rais wa Marekani huwa analindwa na askari wenye mabunduki makubwa.

Ushawahi kuushuhudia msafara wa Rais wa Marekani?

Kama umewahi, basi huwezi shindwa kuwaona jamaa wa CAT na magwanda yao pamoja na mabunduki yao.

Juzi tu nimetoka kuushuhudia hapa….na jamaa walikuwepo kamili gado….kikosi kizima!

View attachment 1770389
Hata Marekani bado haijafaulu mtihani wa kuwa nchi yenye demokrasia na maelewano mema na muonekano usio wa kijeshi.
I'm sure Ulaya kuna nchi zimeizidi Marekani katika hili.

Waziri Mkuu wa Uholanzi kulikuwa na wakati alikuwa anapenda kuendesha baiskeli kwenda kazini.Msafara wa Waziri Mkuu unakuwa wa baiskeli badala ya magari.

Na kwa kweli wenzetu hao (Marekani) historia yao inaweza ku justify hayo mambo, ukichukulia assasinations na assasination attempts za public figures zilivyotamalaki kuanzia Kennedy mpaka Reagan kwa Marais.

Ila habari za rais kuvaa magwanda ya jeshi wamejitahidi kuziepuka kwa kiasi kikubwa, ukiacha vile vi jacket vyao vya kirais vya military.


2020_07_16_100298_1594884840._large.jpg
 
Wazungu huwa wanatucheka Sana , tupo bado Zama za WW2 , kuna mtu alijitengenezea ulinzi wa mabunduki kila angle , lakni Wana wakamtupia kirusi cha COVID huku wanakula [emoji897]kirusi kikamaliza mchezo ......
Watu kitu gani wewe mtumwa wa fikra

Sent from my HRY-LX1T using JamiiForums mobile app
 
Kiafrika afrika msafara mkubwa hautumiki kama sehemu ya Ulinzi bali as a Prestige.
 
Yule alikuwa analindwa hadi na malaika, bomb detector ila wapi kazimika kama mshumaaa.

Posho posho acha wamlinde njaa mbaya, kama nyarandu karudi CCM wao ni nani wasimlinde raisi
 
Hili ndilo nlitaka kuwakumbusha wenzangu pia humu.

Inaonekana upeo wa wengi wetu ni mdogo kwenye masuala ya Utawala.

..mbona nyerere hakulindwa kama hawa wa sasa hivi?

..wakati wa nyerere nchi ilikuwa ktk tishio kubwa la kiusalama.

..Kuna wakati manowari za makaburu wa afrika kusini zilifika mpaka pwani ya Dsm.

..pia kulikuwa na majaribio matatu ya kumpindua Nyerere.

..pamoja na hali hiyo Nyerere hakuwahi kuwa na ulinzi unaotisha wenye silaha nzito kama tunavyoshuhudia sasa hivi.
 
Ndio tofauti ya developed/rich countries na developing/poor countries. Ukiona marais wa Ulaya na Marekani wanatembea kama vile wapo wenyewe usije ukadhani hawana ulinzi. Actually wana ulinzi mkali kuliko hawa wa kwetu.
 
Usimsahau na Kiranga
Ila niliwahi Kumuliza Head Of Psu Wa Sasa Wambura, Why Mnakuwa na tited security Sana Kwa Wakuu Wa Nchi, Akasema Wanataka Wao [emoji1][emoji1][emoji1]
Ha ha ha Jamiiforums ipo juu kileleni. Hebu tupia picha ya Wambura tumuone.
 
Kwa nchi hii ambayo baadhi ya watu wanafurahia kifo cha mwingine huwezi ukachukulia poa tu, hujui Leo au kesho watafanyaje.
Huu Uzi ungesomeka 'Tanzania inawatu wa ajabu kweli kufurahia vifo vya viongozi wao'
Ktk mazingira kama haya kwa nini nisiwe hata na walinzi 800.
Nani alifurahi? Hebu ona chozi hilo
FB_IMG_16178723178620316.jpg
 
..mbona nyerere hakulindwa kama hawa wa sasa hivi?

..wakati wa nyerere nchi ilikuwa ktk tishio kubwa la kiusalama.

..Kuna wakati manowari za makaburu wa afrika kusini zilifika mpaka pwani ya Dsm.

..pia kulikuwa na majaribio matatu ya kumpindua Nyerere.

..pamoja na hali hiyo Nyerere hakuwahi kuwa na ulinzi unaotisha wenye silaha nzito kama tunavyoshuhudia sasa hivi.
Ulinzi wa viongozi wa dunia wa enzi za Nyerere unataka kuulinganisha na ulinzi wa viongozi wa zama hizi?

Kama ni hivyo basi tulinganishe ulinzi wa Abraham Lincoln na ulinzi wa Julius Nyerere, siyo?

Absurd!
 
Nchi ulizotaja zinatechnologia kubwa sana za ulinzi kiasi kwamba sio lazima kuwa karibu sana na muheshimiwa ili kumlinda, Analindwa kwa mbali sana, Kwa sisi ndo hivyo technologia ni ndogo so akili za kawaida na training tu ndo zinatumika so lazima wawe karibu sana
 
CCM na viongozi wao wapo na wasiwasi masaa 24, maov yao wanayowafanyia wananchi yanawatia hofu wenyewe, nahasa hao TISS ni watu wa ovyo sana
 
Tuachane na mambo ya ulinzi wa Rais....hayatuhusu sisi,wako wahusika.
 
Ulinzi wa viongozi wa dunia wa enzi za Nyerere unataka kuulinganisha na ulinzi wa viongozi wa zama hizi?

Kama ni hivyo basi tulinganishe ulinzi wa Abraham Lincoln na ulinzi wa Julius Nyerere, siyo?

Absurd!

..mfano uliotumia kutetea hoja yako sio mzuri.

..kuna miaka 100+ kati ya Uraisi wa Abraham Lincoln na Julius Nyerere.

..ulinzi wa Jpm ulikuwa mkubwa, wa aina yake, na Watz hatukuuzoea kwa viongozi wakuu

..kulikuwa mpaka na helikopta ya doria kama sehemu ya msafara wa bwana mkubwa.

..zaidi, msafara ulijumuisha na ambulance.
 
Back
Top Bottom