Tanzania tuna protocol za ovyo kabisa kwa Viongozi wetu

Tanzania tuna protocol za ovyo kabisa kwa Viongozi wetu

Ulinzi wa viongozi wa dunia wa enzi za Nyerere unataka kuulinganisha na ulinzi wa viongozi wa zama hizi?

Kama ni hivyo basi tulinganishe ulinzi wa Abraham Lincoln na ulinzi wa Julius Nyerere, siyo?

Absurd!
Unasema Hitler hakulindwa kama meko? Joseph Stalin pia hakuwa na ulinzi kama meko?
 
Nchi ulizotaja zinatechnologia kubwa sana za ulinzi kiasi kwamba sio lazima kuwa karibu sana na muheshimiwa ili kumlinda, Analindwa kwa mbali sana, Kwa sisi ndo hivyo technologia ni ndogo so akili za kawaida na training tu ndo zinatumika so lazima wawe karibu sana
Mnaongea pumba wakati mnaona msafara umejaa migari yenye mitambo ya ki teknolojia na maelikopta juu alafu ooh tekinolojia tekinolojia mavi
 
Tuachane na mambo ya ulinzi wa Rais....hayatuhusu sisi,wako wahusika.
Hayakuhusu wewe sisi tunalipa kodi alafu of tuna watoto hatutaki waone mabunduki kama kuna vita.
 
Ambulance na helikopta mbona ni mambo yaliyo standard katika zama hizi kuhusiana na ulinzi wa viongozi…

Ukuaji wa teknolojia unaenda sambamba na threaths pia.

Kumbuka kuwa mtu anayetaka kumdhuru Rais anahitaji kuwa sawa mara moja tu ili atimize azma yake!

Ila ulinzi wa Rais unapaswa uwe sawa mara zote. Siku wakikosea ndo Rais anaweza kudhurika.

Kuna ubaya gani ulinzi wa Rais kuwa imara?

Yaani ulinzi ukiwa imara, mnalalamika.

Siku ikitokea Rais kawa assassinated, mtaanza kuuhoji ulinzi wake!

Hamna jema nyie.
Ambulance ya nini wakati msafara una daktari na una vingora, hivi raisi ni nani mbona mnamfanya kama tofauti na raia waliompa ajira.
 
Hao viongozi uliowataja wana ulinzi mkubwa sana na "haulinganishiki" na ulinzi wa viongozi wetu. Hapo unapoona anashuka kwenye ndege bila ulinzi wa askari unaoweza kuutambua ni sehemu isiyohitaji ulinzi wa namna hiyo, ni kama hapa kwetua rais akiwa ikulu, huwezi kuona ulinzi wa namna ile, tofauti na akiwa ktk mkusanyiko mkubwa wa watu, na mfumo huo upo duniani kote. Tukumbuke kuwa namna tunavyolinda viongozi wetu ni taaluma, ambayo wataalamu wetu wamejifunza na wakabobea. Tazama picha nilizo ambatanisha uone hata Hao uliowataja .View attachment 1770558View attachment 1770559
Wapi kuna mibunduki ya wa kunja sura
 
Kwa nchi hii ambayo baadhi ya watu wanafurahia kifo cha mwingine huwezi ukachukulia poa tu, hujui Leo au kesho watafanyaje.
Huu Uzi ungesomeka 'Tanzania inawatu wa ajabu kweli kufurahia vifo vya viongozi wao'
Ktk mazingira kama haya kwa nini nisiwe hata na walinzi 800.
Ukiona raia ambaye wewe mwenyewe Kiongozi unamuita mnyonge, halafu anakuja kufurahia kifo chako, jua wewe kiongozi ulikuwa na walakini mkubwa.
Ni watu mafedhuli tu, ambao binadamu wengine hufurahia wakifa.
 
Hehehehe!!! Viongozi wetu Afrika bana, sema usichokijua kwa wenzetu kule Ulaya unapomuona kiongozi anatembea na wapambe wachache jua eneo lote huwa limewekwa ulinzi wa hali ya juu, kule kwenye maghorofa juu huwa kuna snipers SWAT team, pia drones zinachezea kwa mbali, na satellite zinaangaza, yaani eneo lote linapigwa kurunzi balaa.
Wewe kwa macho yako ya Kiafrika unawaona hao wachache ila mchezo unachezwa kivingine.
Tatizo unaangalia sana tv series za hollywood
 
Acheni chuki kwa mama yetu.mbona katika utawala uliopita hamkusema ulinziulivyokuwa mkubwa?
 
Matako nimeongelea nzi wanaomzunguka kiongozi sijaongelea gharama matako
Kama umeshindwa elewa nilichoandika ngoja nigongelee msumari kabisa kuwa wewe ni mmoja wa watu wale wakawaida wasiotumia akil zao..pole sana kaka
 
Kumbe unajua kuwa wenzetu wanatumia akili zaidi kuliko kujazana watu mia kwenye kiongozi sasa mbona huna akili ya kuelewa mleta hoja?
Nawewe huna akili pia sabab unaifananisha Tz na kina biden..hiv unajua security ya rais unapomwona tu huwa ina tumia mamilion ya walipa kodi kias gan.....
 
Marekani gani unaizungumzia? Hii ambayo marais wawo bush na obama walipokuja hapa kwetu walikuwa na walinzi zaidi ya 200 na wengine wakapanda hadi juu ya paa laikulu yetu?
Inawezekana walipo kuja marais wa US hapa TZ mleta mada alikuwa mwanafunzi wa darasa la tatu A akiwapiga wenzake na zile ndege za karatasi wakati Mwalimu anaandika ubaoni.
 
Nawewe huna akili pia sabab unaifananisha Tz na kina biden..hiv unajua security ya rais unapomwona tu huwa ina tumia mamilion ya walipa kodi kias gan.....
Unakimbilia kwenye gharama, sijaongelea gharama na huwezi compare tz na us kwa gharama. Nimesema wale utitiri wanaoonekana na raisi wengine na mibunduki. Ungemjua Fidel Castro hakuwa na hela ila alikuwa na ulinzi mkali wa intelijensia na hakuwa na mabunduki. Pia nyerere hakuwa na mabunduki ila alikuwa na mashushushu wa kutosha huo ndiyo ulinzi wa akili siyo mijitu imejazana na mibunduki hadharani inakimbia kimbia hovyo, migari yenye antenna, helikopta, wanajeshi, gari mia mbili, ambulance, gari la mgahawa, gari la matangazo na dj, Gari lenye spika, gari la mahawara, upuuzi mtupu.
 
Inawezekana walipo kuja marais wa US hapa TZ mleta mada alikuwa mwanafunzi wa darasa la tatu A akiwapiga wenzake na zile ndege za karatasi wakati Mwalimu anaandika ubaoni.
Ile ni foreign trip acha ushamba tena Tanzania ndiyo ilijipendekeza zaidi.
 
Inawezekana vyombo vyetu vya ulinzi ni dhaifu sana kiutaalam, ndiyo maana wanafanya mambo ambayo kwa hakika yanaashiria upungufu mkubwa wa uwezo wa kupanga, kufikiri na kutenda.

Wasichokijua ni kuwa nguvu bila akili na maarifa, ni upuuzi mtupu. Pundamilia pamoja na ukubwa wake kumzidi simba, analiwa na simba kwa sababu simba anatumia akili, pundamilia anatumia nguvu.
 
Ile ni foreign trip acha ushamba tena Tanzania ndiyo ilijipendekeza zaidi.
Kuwa foreign trip ndio mpaka wapande kule juu ikulu?. Teknolojia inayotumiwa kwa ajili ya ulinzi wa viongozi wa mataifa tajiri ni kubwa mno sisi bado tunaelekea huko.

Kumbuka kuwa tulivamiwa na magaidi kule Rufiji na Mkuranga na wakashungulikiwa ipasavyo tofauti na wanavyowalea kule Nigeria na Chad.

Ni lazima ilikuwa Hayati JPM awe na ulinzi mkali. Hata huyu wa sasa anahitaji ulinzi mkubwa kwa aina hiyo ya mataifa yetu ya afrika yalivyo na urahisi wa kuingiliwa na magaidi pamoja na vikundi vya kivita vyenye kufadhiliwa na mbinu za kibeberu.
 
Nchi za Ulaya zina njia zingine za kisiasa zaidi ambazo zinaweza kutumika eneo la tukio na walinzi wa kawaida wakakaa pembeni,sisi kuna uwezekano mkubwa kua hatuna zaidi ya kutegemea ulinzi wa watu

Kila nchi jamani ina mambo yake,msiwe mnalinganisha nchi hii na nyingine maana huu ni kama uvivu wa kufikiri
 
Nchi za Ulaya zina njia zingine za kisiasa zaidi ambazo zinaweza kutumika eneo la tukio na walinzi wa kawaida wakakaa pembeni,sisi kuna uwezekano mkubwa kua hatuna zaidi ya kutegemea ulinzi wa watu

Kila nchi jamani ina mambo yake,msiwe mnalinganisha nchi hii na nyingine maana huu ni kama uvivu wa kufikiri
Unajiongelesha kama vile huoni yale magari yenye vifaa vya kisasa yenye mi antenna. Sasa kushika magobole hadharani ndiyo ulinzi? Kwani wakificha bastola viuoni kuna shida? Mibunduki mikubwa hadharani ni viashiria tosha vya udikteta.
 
Wanapenda misifa tu sidhani Kama Kuna mwenye uthubutu wa kuhatarisha usalama wa Samia.

Kuna Yule sista mvaa miwani mikubwa imeziba uso wote [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]huwa ananifurahisha Sana [emoji1787]yaani mrembo anaweka uso mbuzi utadhani anabifu na mumewe[emoji1787][emoji1787]

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom