Tanzania tuna protocol za ovyo kabisa kwa Viongozi wetu

Tanzania tuna protocol za ovyo kabisa kwa Viongozi wetu

Mkuu bado hatujawa Wazuri upande wa Screening na Mass Gathering controlling huwezi amini kuna watu wanapata enough closer na watawala huku wakiwa na vifaa vya hatari, Kumzonga zonga ni kama kumguard ivi ila hata mimi sipendi vile lakini kwa mazingira yetu acha tu iwe ivo kwa sasa huku waki advance kufanya Screening kwa hadhira, Rais wa Marekani usiseme ana ulinzi mdogo hapana yupo na kundi kubwa la watu wasionekana
 
Mkuu bado hatujawa Wazuri upande wa Screening na Mass Gathering controlling huwezi amini kuna watu wanapata enough closer na watawala huku wakiwa na vifaa vya hatari, Kumzonga zonga ni kama kumguard ivi ila hata mimi sipendi vile lakini kwa mazingira yetu acha tu iwe ivo kwa sasa huku waki advance kufanya Screening kwa hadhira, Rais wa Marekani usiseme ana ulinzi mdogo hapana yupo na kundi kubwa la watu wasionekana
Nyerere alikua na uwezo huo ila unasema sasa hivi bado hatuna uwezo huo? Au unajisemea wewe? Taasisi ina miaka 60 bado unasema haina uwezo au kuna mtu alijaza watu wake akawapa maagizo badala ya kufuata ushauri wao yeye ndiyo anawashauri wao.
 
Nyerere alikua na uwezo huo ila unasema sasa hivi bado hatuna uwezo huo? Au unajisemea wewe? Taasisi ina miaka 60 bado unasema haina uwezo au kuna mtu alijaza watu wake akawapa maagizo badala ya kufuata ushauri wao yeye ndiyo anawashauri wao.
Kipindi cha Nyerere na sasa ivi ni tofauti sana kwa sasa threat ni kubwa sana afu pia kumbuka idara inaweza kuwa na mipango hii lakini kuna vitu kama dharura mfano misiba, Barack obama ali hutubia kwenye msiba wa nelson mandela akiwa ndani ya Bullet proof Box yote hii ikimaanisha hawakuwa well prepared kutokana na nature ya tukio
 
Mzee ulinzi hauko ivo, Marekani hajaamua tu kukuonesha ni kiasi gani anamlinda Rais wake ukiona behind the scene utashangaa sana
Kumbe hatuelewani nimeongelea ile mijitu inayomzonga zonga rais na kumpumulia kwa nyuma mingine kushoto na mibunduki ya kivita
 
Nyerere alitawala nchi yenye population gani?
Mwinyi alitawala population gani?
Mkapa nae?

Kama nakumbuka vizuri, wale jamaa wa Rufiji hawakuwepo kipindi cha hao wazee, walianza lini?

Hivi karibuni ndo tumeanza kupata teknolojia pia, hata rada, achilia za kijeshi, alinunua mkapa. Ben alinunua ndege ya masafa marefu kwa matumizi ya raisi, kabla ya hapo walikuwa wanaingia kwenye commercial airlines.

Itoshe kusema, kadiri mshahara unavyoongezeka ndivyo matumizi yanavyoongezeka.

Una point nzuri lakini kuingiza population katika mada hii umepotoka. Haya, katika uongozi wa watu hao nchi haikuwa kuwa na wakazi waliopungua milioni 10. Unataka kusema kuwa na population ndogo inamaanisha kutokuwepo kwa watu watano wanaoweza kuua Rais? Zanziba mpaka leo iko chini ya wakazi milioni tano lakini Rais Karume aliuawa miaka 49 iliyopita!

Tuseme hivi, Afrika kuna tabia ya kupoka madaraka kwa mtutu wa bunduki. Iwe ni vikundi vya kigaidi au vyombo vya ulinzi. Kwangu ndio sababu kubwa ya ulinzi kuwa ulivo, japo ni kweli kama ulivyosema - technolojia ya kung’amua hatari bado ni ya chini sana au haipo kabisa. Bado mabavu yanahitaji ili kufanya mambo mengi Afrika.
 
Una point nzuri lakini kuingiza population katika mada hii umepotoka. Haya, katika uongozi wa watu hao nchi haikuwa kuwa na wakazi waliopungua milioni 10. Unataka kusema kuwa na population ndogo inamaanisha kutokuwepo kwa watu watano wanaoweza kuua Rais? Zanziba mpaka leo iko chini ya wakazi milioni tano lakini Rais Karume aliuawa miaka 49 iliyopita!

Tuseme hivi, Afrika kuna tabia ya kupoka madaraka kwa mtutu wa bunduki. Iwe ni vikundi vya kigaidi au vyombo vya ulinzi. Kwangu ndio sababu kubwa ya ulinzi kuwa ulivo, japo ni kweli kama ulivyosema - technolojia ya kung’amua hatari bado ni ya chini sana au haipo kabisa. Bado mabavu yanahitaji ili kufanya mambo mengi Afrika.
Kwenye population nilimaanisha, ni rahisi kulinda mzingo ule ule wenye watu wachache kuliko watu wengi
 
Nadhani hoja kubwa si ulinzi imara, ni ulinzi wa kitaalamu. Hao Marais wa Marekani ambako waliopita wengi wameuawa kuna 'intelligence' ya maana kwanza kabla kiongozi hajafika na wakati akiwa katika eneo

Nyerere alikuwa katika hatari kubwa sana nyakati za ukombozi ukizingatia akina Mondlane waliuawa hapa nchini

Ulinzi wa Nyerere ulikuwa wa kisayansi kiasi kwamba hakuwa anazungukwa na maaskari na bunduki bali usalama ulishapitiwa kabla na baada ya kufika eneo. Utakumbuka'' intelligence'' yetu ilivyokuwa nyakati hizi

Inashangaza sana , sijui kwanini alikuwa na ulinzi wa namna ile.

Ulinzi wa kuzungukwa na mabunduki na makundi ya watu ni wa karne ya 18. Ni ulinzi wa kijima sana.
Anwar Saadat aliuawa katikati ya kundi la Walinzi. Ndivyo ilivyokuwa kwa viongozi wengi miaka ya nyuma

Zama za teknolojia matumizi ya akili ni muhimu sana kuliko uwepo wa makundi yenye mibunduki

Jamaa alikuwa ana exaggerate kila kitu , alitaka tu kuonekana ni mtu special sana duniani.
Hakukuwa na sababu ya Helikopta ikiwa alisimama hovyo barabarani na kuhutubia.

Katika vitu vinavyokera ni Protokali ya kuhutubia. JPM alibadilisha namna kiongozi anavyotoa hotuba

Siku hizi kila anayesimama anaanza kuwatambua wageni waliopo. Ni makosa makubwa sana

Viongozi waliopo wanatambuliwa mara moja wakati wa kuanza kwa shughuli.
Viongozi wanaofuata wanamtambua mgeni rasmi kwa kumu address 'Mh Rais' au VP au PM

Rais anatambulishwa uwepo wa viongozi, si kazi ya Rais kuwatambua kwasababu walishatambuliwa

Nyerere, Mwinyi, Mkapa walianza hotuba kwa kutambua mwenyeji wa shughuli.
Hakuna sababu ya kusoma majina ya kila kiongozi katika jukwaa kuu

Halafu Rais atambue viongozi wakuu kwa makundi.
Mfano akimtambua waziri mkuu tayari ameshtambua uwepo wa Mawaziri.
Ukimtambua CDF umeshatambua vyombo vya ulinzi na usalama. Hakuna sababu ya kutambua TISS,Polisi n.k.

Wanaoandaa hotuba ya Rais waliangalie hili. Rais anatambua mwenyeji kisha viongozi kwa ujumla wao na wananchi. Si kazi ya Rais kutaja kila mtu aliyekuwepo. Hili alianzisha JPM na sasa linaendelea bila kujua kuna tatizo

Pascal Mayalla
Kila kitu tuna mlaumu Magufuli watanzania tuache chuki zisizo na msingi kisa mtu ulikuwa umpendi fulani. Maswala ya ulinzi hayako chini ya Rais. Rais uwa hana mamlaka ya kujiwekea ulinzi. Hivyo kusema Magufuli alitaka aonekane special ni kumzushia tu. Kitengo cha ulinzi wa Rais ndiyo chenye jukumu kubwa kuhakikisha ulinzi na usalama wa Rais.
Mwl. Nyerere alishawahi kukataa mara kwa mara ulinzi wake pale Butiama. Mara nyingi alisema ahitaji ulinzi nyumabani kwake, lakini bado aliwekewa ulinzi, na wakati mwingine yeye bila kujua. Nakumbuka hata Kikwete hakupenda kuzongwa na walinzi wake lakini halikuwa hana namna.
Ma Rais wetu wengi walio pita walikuwa hawana maadui wengi katika jamii yetu. Na hawajahi kutishiwa maisha kabla ya wao kuwa marais. Tukiondoa Nyerere, ambaye alikuwa na maadui wengi wa nje. Mbali ya Ulinzi wa Nyerere, yule bwana alijiamini sana. Kuna wakati akili ikimtuma anabadili njia aliyopangiwa kupita, au muda mwingine, anagoma kufanya jambo fulani. Kuna mama mmoja, alipatwa na mabaya baada ya kujaribu kwenda nyumbani kwake Butiama na kuingia sehemu akiwa na nia mbaya. Alipatwa na kilicho mpata. Hivyo Nyerere pia kutokana na mila na matambiko ya kichifu alikuwa na nguvu za ulinzi huo. Ndo maana alikuwa huru sana.
Kikwete alikuwa mtu wa watu na alijichanganya toka hajawa Rais. Alijenga urafiki na watu wa tofauti. Hivyo hii ilimjengea kutokuwa na maadui wengi.
Magufuli alikuwa na maadui toka alipokuwa waziri, kutokana na majukumu yake alisimamia kile alichokiamini, na bila kupindisha. Hii ilimjengea maadui wengi. Akiwa waziri alishawahi kupewa sumu, na alikimbizwa ujerumani kwa matibabu.
Alikuwa waziri pekee mbali na waziri mkuu aliepewa ulinzi maalum. Na huu ulinzi uliamliwa na Rais Mkapa mara baada ya kuwa amepewa sumu.
Watu wenye fedha na wenye mamlaka hawakumpenda Magufuli toka yuko waziri. Hii ilitokana na misimamo na utendaji wake kazi usio pinda pinda. Mara baada ya kuwa Rais alijiongezea maadui na hasa kutoka nje. Ni kwasababu ya misimamo yake ya kiuchumi katika uwekezaji. Kivyovyote vile ulinzi ilibidi uimarishwe juu yake. Walinzi wengi kumzunguka ni mbinu tu za kiulinzi. Hivyo ulinzi hakuutaka yeye bali ilibidi iwe hivyo.

Sikwamba Marais wa marekani hawana ulinzi wa kuzingirwa. Tazama Obama alivyokuwa akitoka nje kwenye matembezi walinzi kibao. Hata wanapokuja ziara huku Africa eneo zima linatawaliwa na walinzi hadi katika Magorofa.
Japo mnasifia Marekani lakini ni nchi ambayo Marais wanne (4) waliuwawa wakiwa madarakani. Pia Marais wawili walijeruhiwa wakiwa madarakani.
Kama Rais Kennedy angekuwa kazongwa sniper yule angepata wakati mgumu wa kumlenga na kumuuwa. Hivyo kujazana ni mbinu tu ya kiusalama. Kumbuka Bush alishawahi kutupiwa kiatu wakati akitoa hotuba. Mwinyi wakati akihutubia waislamu alishawahi kuzabwa kofi, Kikwete akiwa kwenye kampeni Mwanza alishawahi kuvamiwa na kutaka kupigwa mweleka. Mie sioni tatizo akipewa ulinzi wa hivyo wa kurundikana hii umchanganya adui au mtu mwenye nia mbaya.

Watanzania tunapenda kujidharau hasa hiki kizazi cha sasa. Tanzania kiulinzi tuko imara, haijarishi teknolojia, ila tunambinu zetu. Wakati wa Iddi Amini mataifa mengi yaliamini Tanzania itapigwa, kwani Iddi Amini alikuwa na siraha nzito na za kisasa kwa wakati huo, na alisaidiwa na Ghadaffi, lakini japo Tanzania hatukuwa na siraha nzito, tulishinda vita kwa ari na mori wa nguvu. Na Tanzania iliogopeka. Walijiuliza kivipi tulishinda. Wakati huo Meja jenelari Mayunga, Mwita Marwa na wengineo waliijua siri.
Hivyo tusidharau mbinu za kiusalama za kibongo.
 
Tanzania tunafanya kazi kwa kutumia nguvu

Rais Magufuli aliyelindwa kama Mungu yuko wapi? Tulinde afya, tumlinde rais kwa ndani sio kwa nje.

Hatuna mifumo wa taasisi imara

Tukiwaambia tunahitaji katiba mnabisha nchi inahitaji katiba itakayoweka miongozo ya kila jambo linalofanyika katika nchi na kutengeneza mifumo imara ya kiuongozi.
Yani huwezi tu kujenga hoja kwenye kila mjadala unaohusu selikali bila kumnanga marehemu.
Kumbuka tu kuwa mifumo ya ki usalama wa kiongozi unategemeana pia na mazingira,nyakati na technology pia.
JPM amekuwa na maadui toka akiwa waziri na ndiomana alishwahi kupewa sumu.
Misimamo yake ya kuvuruga mipango ya mabepari na wafanyabiashara kharamu lazima umjengee maadui wengi.
Swala la usalama wake haamui yeye ila taasisi husika.
Na unaposema Rais JPM alilindwa kama Mungu na leo yupo wapi,unamaana gani?Inamaana Magufuli ndio Rais wa kwanza kuwa na ulinzi mkali Africa au Duniani?au ni chuki zenu tu zilizolemaza akili?
Kifo chake hakihusiani na shambulizi lolote la kiusalama.Mimi nijuavyo alikuwa na tatizo la kiafya.
Screenshot_.png
 
Yaani kiingozi na msafara wa magari mia anasimama kijijini ambapo watu hawana hata manati ila sasa kazungukwa na mabunduki ya kivita zaidi ya hamsini anahutubia wanyonge unajiuliza anawaogopea nini wanyonge hawa? Angalau basi angewaamuru jamaa wafiche silaha ndani aongee na wanyonge wake kwanza duh?
Mo dewji alipotekwa mlipiga kelele na kuhoji yeye kutokuwa na ulinzi,sasa leo unamzungumzia Rais wa nchi utafikiri ni mtu wa kawaida sana,vaa viatu vyake kwanza ndio uhoji mambo mazito kama hayo.
 
Siku jf watu wakianza kuangalia vitu "in a positive way" nitakuwa kiama kimebakiza wiki!
Watu wengi hapa ni wa vijiweni tu, ambao wana negative minds; hivyo maisha yao yote yana negative outcomes. Ndiyo maanaa hawaeishi kulalamika, yaani hata kulaumu maiti kwa vitu ambavyo maiti hiyo haikuhusika.
 
Hao wakina Biden na Eliza wanalindwa na zaidi ya hao watu wanaowalinda viongozi wa Africa.

Nadhani tunakurupuka sana, anapokuwepo raisi wa US au malkia, mzingo mkubwa unakuwa kwenye rada ya kiulinzi, thermal image inafanya kazi muda wote, snipers, SS, CIA, MI6, FBI, NSA, na technology za hali ya juu kulikagua eneo lote.

Hatuna hiyo teknology, hatuna huo uwezo, angalau basi apate ulinzi wa bodyshield.
UJINGA ni kipaji na Magufuli alikuwa nacho, sasa ukiongeza na kiburi chake ndiyo akawa HAYAWANI. Maana tayari kwa kipindi chake Tanzania ilikuwa inahesabika kama nchi ya 5 Afrika yenye Kiongozi mwenye ulinzi mkali.
 
sas
Mzee ulinzi hauko ivo, Marekani hajaamua tu kukuonesha ni kiasi gani anamlinda Rais wake ukiona behind the scene utashangaa sana
Ni kweli kabisa kama Obama alipokuja Tanzania alikuwa na msafara wa watu 800 ina maana wote wale walikuwa wafanya biashara tu?
 
UJINGA ni kipaji na Magufuli alikuwa nacho, sasa ukiongeza na kiburi chake ndiyo akawa HAYAWANI. Maana tayari kwa kipindi chake Tanzania ilikuwa inahesabika kama nchi ya 5 Afrika yenye Kiongozi mwenye ulinzi mkali.
Kuwa na ulinzi mkali ni ujinga au udhaifu? Ukweli kwamba alikuwa raisi wa nchi ya Tz, alikuzidi mbali mno, hata alama za nyayo zake usingeweza kuziona, achilia mbali kuzikaribia.

Hivyo kama unafikiri alikuwa ni MJINGA na HAYAWANI, fikiria nafasi yako wewe kwenye hiyo hierarchy ya UJINGA na UHAYAWANI.
 
Back
Top Bottom