Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Duh! Hizi ni kama mbata za uso hizi.Pole brother! Siku hizi umekuwa wa watu sio wa issues. Unajadili watu badala ya masuala. Watu wanakufa kaka, achana na hiyo. Jadili issues. Issues hazifi
Hulka yake haimruhusu kufokea. Kama jana amekaripia bila kufokea. Watu hawakatai kusahihishwa au kukaripiwa. Walichokuwa wanalalamikia ni kufokewa hadharani. Mheshimiwa nae akianza kufokea watu hadharani tutamshangaa na watu watamuuliza kulikoni?Ngoja awafokee tuone mtakavyomshukia hadi namuonea huruma...
Ya mwisho? Unajuaje ilikuwa ya mwisho wakati Rais amesema alishaonywa mara tatu hivi? Unajuaje kama angepigwa bit ya nne, ya tano na kuendelea? Rais leo kamwambia kwa utulivu tu kuwa anapwaya na asipojirekebisha ataondolewa kwenye hiyo nafasi. Bila kufokewa. Lakini Jaffo anajua bit ya tano ya tano haitakuja. Ni ama awajibike vizuri zaidi au nafasi atapewa mwingine. Bila kufokewa.Duh.. ni kazi kweli kweli... mbona Jaffo alishapigwa bit ya mwisho na Magu hivi majuzi tu... ila kichwa cha habari chahusika
Hata kipindi cha maombolezo hakijaisha tayari mnaombea upinzani wajitoe kwenye uchaguzi wa 2025? Mheshimiwa Rais hajasema bayana kuwa mikutano ya hadhara ya kisiasa inaruhusiwa, hajafanya mabiliko yeyote kwenye Tume ya Uchaguzi, hajazungumzia Katiba Mpya, hajazungumzia specifically watu waliokuwa na kesi za kubambikwa, hajazungumzia uhuru wa vyombo vya habari, hajazungumzia uhuru wa kupata na kutafuta taarifa, hajazungumzia wasichana wanaopata mimba wakiwa shuleni, hajazungumzia mikataba, hajazungumzia yaliyo mpata Lissu ( Kama Rais), hajazungumziwa uendeshwaji wa Bunge ikiwa pamoja na wale wabunge wakuteuliwa wa "Chadema", hajazungumzia Covid na mambo mengine mengi tu ambayo wapinzani wamekuwa wakiyahoji.Kwa mshangilio huo,inawezekana hata 2025 wasishiriki uchaguzi mkuu. Watamuacha mama Samia apite
Bado Wana Imani kubwa Sana na ccm
Umesema kweli. Nadhani ndoto za kuwa hatakosolewa kwa sababu ni mwanamke au anaongea kwa upole zitabakia kuwa ndoto tu. Na sidhani kama hata yeye mwenyeww atafurahia kuzungukwa na "praise team" peke yake. Ataona kama ni dharau fulani.Mkuu hii ndio makala yenyewe au ni sehemu ya makala? Angalau kwa hotuba ya leo SSH sio JPM hata kwenye matamshi mfano tutaongeza wigo,tu(ni)
Ni kweli SSH ni ccm kama alivokuwa JPM ila kumsifia leo haimaanishi hatokosolewa kesho!
Na ndio maana watu walishangaa uwekezaji mkubwa kwenye industry inayopumulia mashine. Kununua Dreamliner kabla ya kupata uhakika wa kuweza kusafiri kwenda nje na kama hata hao abiria wapo. Na hiyo hasara ya 60 bilioni ina walakin hasa ukizingatia hali ya Corona duniani na gharama za uendeshaji wa hizo ndege ambazo sio mpya tena.Fanya utafiti kidogo juu ya hali ya aviation industry duniani kabla hujaihukumu ATCL. Airlines zote zinapumulia machine!
mweeh.. sasa kwani siyo maneno ya kweli? mbona wapo na walishajipambanua hadharani?Nimetamani sana kulisoma na kulimaliza hili andiko lako, lakini haya maneno uloanza nayo yameonyesha kuna walakini.
"Wale ndugu zetu waliombea, waliongojea, na hata waliosubiria Magufuli afariki akiwa madarakani"