Kwa muendelezo wa posti hapo juu - HAYATI MWALIMU mpaka umauti unamkuta alikuwa tayari ameshasambaza SERENGETI kwa nchi zote za KIAFRIKA. Hawa SERENGETI yaani CHUI walikuwa ni wake kwa waume na wenye sifa ya kuolewa na kuoa.
Hii yote ilifanyika kwa nia ya kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na mataifa mbali mbali dhidi ya CHAMA CHA MAPINDUZI na TANZANIA [emoji1241] kwa ujumla.
Vile vile hawa watu wa mataifa mengine ya AFRIKA na hata nje ya AFRIKA nao walifanya hivyo hivyo kwa upande wa TANZANIA [emoji1241] kwa kukubali kuja na kuishi TANZANIA [emoji1241] ikiwa ni pamoja na kuoa au kuolewa na WATANZANIA. Hiki kitendo kwa lugha ya kiingereza wanaita ni "INTERMARRIAGE".
Sasa CHAMA CHA MAPINDUZI yaani CCM walijidhatiti kupitia mfumo huu wa mahusiano ya kijinsia, kiudugu na hata kidiplomasia dhidi ya mataifa mengine. Kwahiyo CHAMA CHA MAPINDUZI yaani CCM kimejiimalisha na kujidhatiti sana kupitia sera ya mambo ya nje.
Ndio maana inakuwa ni vigumu kwa VYAMA VYA UPINZANI kukubalika ndani ya nchi na hata nje ya nchi, kwa sababu CHAMA CHA MAPINDUZI yaani CCM wao walijiimarisha sana kupitia UTU yaani HUMANITY kwa kuwa na kauli mbiu inayosema "BINADAMU WOTE NI SAWA NA KILA MTU ANASTAHILI HESHIMA".
Na mpaka sasa hivi kuna watu wanaendelea kunufaika na uwepo wa CHAMA CHA MAPINDUZI yaani CCM kuendelea kuwepo madarakani. Kwahiyo inakuwa ni vigumu kwa VYAMA VYA UPINZANI kuweza kukubalika, kuwa na nguvu ya ushawishi na hata kushinda UCHAGUZI.
Kwahiyo VYAMA VYA UPINZANI kama vinataka kuleta mabadiliko ya kweli ni lazima wategue mitego yote iliyofanywa na CHAMA CHA MAPINDUZI yaani CCM, tofauti na hapo watakuwa wanapaka rangi upepo.
Na hawa VYAMA VYA UPINZANI wala wasitegemee taasisi za dini, kwa sababu hizi taasisi za dini hazina madhara yoyote zaidi ya kufanya maombi na sala. Hizi taasisi za dini zote zilishadhibitiwa, kwahiyo hazina madhara kwa watawala yaani CHAMA CHA MAPINDUZI.
Na watu wenye madhara ambao walikuwa wanaweza kuitingisha CCM ni MWASHITA yaani SIMBA pekee yao, wengine ni SAMBULA MATE tu yaani ni WATU WASIOJIWEZA yaani ni WATU WANAOHITAJI MSAADA.
Na wala msitegemee MWASHITA yaani SIMBA watakuja kuitingisha CCM, kwa sababu wao ndio wanaokula na kufurahia keki ya taifa. Hawa MWASHITA yaani SIMBA ndio jamii yenye uchumi mkubwa inayonufaika na uwepo wa CHAMA CHA MAPINDUZI madarakani.
Jamii nyingine zisipoamka, zitaendelea kuwa ni jamii za kuajiriwa na kufanya biashara ndogo ndogo, yaani "PETTY TRADE".
Hiyo ndio SIASA YA TANZANIA! Hiyo ndio HALI HALISI YA TANZANIA! Na hiyo ndio CCM aliyoiacha HAYATI MWALIMU!