Tanzania ya sasa ni ile aliyoona Oscar Kambona, Mwalimu Nyerere alikosea sana

Tanzania ya sasa ni ile aliyoona Oscar Kambona, Mwalimu Nyerere alikosea sana

Mkuu Yoda Unataka mkuu wetu ale BAN?


Sijaona jambo lolote baya kwake, Hakuna kejeli wala lugha ya matusi katika machapisho yake, Sasa mnatakaje ale BAN?


Huoni kama utaifishaji na ujamaa wakati wa HAYATI MWALIMU na KAMBONA ndo umezaa jamii hizo mbili anazoongelea Charles Mandela?


Mnataka sisi na wanetu na wana wa vizazi vyetu vijavyo turithi nini au tujivunie nini lakini?


Mashujaa wanapigwa mawe na historia nayo inapigwa mawe, Je, Mnataka tujivunie urithi aina gani, au ule wa bia tamu?


Au tuigeuze mitandao hii ya kijamii iwe sehemu ya kutazama picha na video za ajabu ndo mtafurahi?


Kila jema tunalojifunza mnalipiga mawe, Mnataka Taifa hili liwe la watu wa aina gani lakini?


Au mnataka vijana wote wawe mchele mchele ndo furaha yenu ikamilike?
Ngoja kuna jambo fulani nitawaeleza kwa LUGHA YA STAHA ili mfahamu kinagaubaga kuhusu OSCAR SALATHIEL KAMBONA na HAYATI MWALIMU na kutokuwepo kwa JAMII YA MWASHITA yaani SIMBA 🦁[ hata vizazi vyao havipo ndani ya CCM ] ndani ya CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️.

Hii ilikuwa ni FUNDISHO kwa VIJANA na WANASIASA wa kipindi kile na hata kwa kipindi hiki itakuwa ni FUNDISHO kwa VIJANA wanaotafuta fursa na WANASIASA wanaochipukia.
 
Ngoja kuna jambo fulani nitawaeleza kwa LUGHA YA STAHA ili mfahamu kinagaubaga kuhusu OSCAR SALATHIEL KAMBONA na HAYATI MWALIMU na kutokuwepo kwa JAMII YA MWASHITA yaani SIMBA 🦁[ hata vizazi vyao havipo ndani ya CCM ] ndani ya CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️.

Hii ilikuwa ni FUNDISHO kwa VIJANA na WANASIASA wa kipindi kile na hata kwa kipindi hiki itakuwa ni FUNDISHO kwa VIJANA wanaotafuta fursa na WANASIASA wanaochipukia.
Nakumbuka kuna mahal ulisema jamii ya simba ilipewa baadh ya mikoa na mfano tanga na baadh ya mikoa mingine. Sasa inakuaje tena miziz yao haipo ccm?au sikuelewa
 
Nakumbuka kuna mahal ulisema jamii ya simba ilipewa baadh ya mikoa na mfano tanga na baadh ya mikoa mingine. Sasa inakuaje tena miziz yao haipo ccm?au sikuelewa
Ndio! Pamoja na makubaliano yaliyofanyika baina ya hizi JAMII MBILI za MWASHITA yaani SIMBA 🦁 na SERENGETI yaani CHUI, lakini wale MWASHITA yaani SIMBA 🦁 yaani wale waliokuwa wafanyakazi wa VYAMA VYA USHIRIKA vya NCU, SHIRECU na WETCU waligoma kujiunga na CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️ na kuamua kusimamia MASILAHI YA TAIFA tu, ambayo ni MASILAHI YA NCHI YA TANZANIA 🇹🇿 na sio MASILAHI YA CHAMA TAWALA ambacho ni CCM ⚒️.

Kwa kufanya hivyo, wale waliokuwa wafanyakazi wa VYAMA VYA USHIRIKA vya NCU, SHIRECU na WETCU walikuja na AZIMIO la kuanzisha CHAMA CHA KISIASA kilichokwenda kwa jina la CHAMA CHA WANANCHI - CUF ☀️.

Kwahiyo hawa MWASHITA yaani SIMBA 🦁 pamoja na wenyeji wengine wa hii MIKOA MITATU [ 3 ] ya MWANZA, SHINYANGA NA TABORA waliogoma kujiunga na CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️, walijiunga na MWASHITA yaani SIMBA 🦁 na kufanyika kuwa ni sehemu ya MWASHITA yaani SIMBA 🦁.

Sasa hawa JAMII YA MWASHITA yaani SIMBA 🦁 [ pamoja na vizazi vyao ] kuna sababu zilizowafanya kugoma kujiunga na CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️.

Sababu hizo nitawaeleza baadae kwenye habari ya OSCAR SALATHIEL KAMBONA na HAYATI MWALIMU mwenyewe mpaka ikafikia hatua ya hawa JAMII YA MWASHITA yaani SIMBA 🦁 kutojiunga na CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️.

Sasa hivi, yaani kwa wakati huu hakuna aliyekuwa mfanyakazi wa VYAMA VYA USHIRIKA vya NCU, SHIRECU na WETCU ambaye yupo ndani ya CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️. Hata vizazi vyao hakuna ndani ya CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️!!
 
Nakumbuka kuna mahal ulisema jamii ya simba ilipewa baadh ya mikoa na mfano tanga na baadh ya mikoa mingine. Sasa inakuaje tena miziz yao haipo ccm?au sikuelewa
Hata yule aliyekuwa RAIS WA AWAMU YA TANO [5] WA COLLEGE OF HUMANITIES & SOCIAL SCIENCES [ CoHSS ] pale UDOM kwa mwaka wa 2012/13 ni KIONGOZI pekee wa SERIKALI YA WANAFUNZI kutoka COLLEGE OF HUMANITIES & SOCIAL SCIENCES [ CoHSS ] ambaye hakufanikiwa kujiunga na CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️. Wengine wote waliotangulia walifanikiwa kujiunga na CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️.

Yule aliyekuwa RAIS WA AWAMU YA TANO [5] ni kizazi cha MWASHITA yaani SIMBA 🦁 yaani wale waliokuwa wafanyakazi wa VYAMA VYA USHIRIKA vya NCU, SHIRECU na WETCU.

Kwahiyo yeye hakufanikiwa kujiunga na CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️ kwa sababu ni MWIKO kwa kizazi cha MWASHITA yaani SIMBA 🦁 kujiunga na CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️.
 
Nakumbuka kuna mahal ulisema jamii ya simba ilipewa baadh ya mikoa na mfano tanga na baadh ya mikoa mingine. Sasa inakuaje tena miziz yao haipo ccm?au sikuelewa
Na yule aliyekuwa RAIS WA AWAMU YA TANO [ 5 ] WA COLLEGE OF HUMANITIES & SOCIAL SCIENCES kwa mwaka 2012/13 pale UDOM ndio MTOTO wa MISTER ABILITY aliyeimbwa kwenye ile nyimbo iliyotungwa na RADIO, RABADABA na WEASEL.



Sasa kwenye ile SERIKALI YA AWAMU YA TATU YA TANZANIA 🇹🇿 iliyokuwa inaongozwa na MISTER CLEAN ambaye ndiye HAYATI BENJAMIN WILLIAM MKAPA alifanikiwa kumteua MISTER ZERO kuwa WAZIRI MKUU baada ya huyo MISTER ABILITY kugomea nafasi ya uteuzi ya UWAZIRI MKUU.
 
Nakumbuka kuna mahal ulisema jamii ya simba ilipewa baadh ya mikoa na mfano tanga na baadh ya mikoa mingine. Sasa inakuaje tena miziz yao haipo ccm?au sikuelewa
Na hawa VIONGOZI wa MIKOA MITATU [3] YA MWANZA, SHINYANGA NA TABORA wakiwemo WABUNGE NA MADIWANI wa CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️ wote ni WALALA HOI au kwa jina lingine wanaitwa ni HOHE-HAHE ambao wanakuwa BRAINWASHED kwanza, kabla ya kupewa nafasi yoyote ndani ya CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️.

Yaani ni WATU ambao hawana nguvu yoyote, iwe ni nguvu ya KISIASA au hata nguvu ya KIUCHUMI, hawana!!

Ndio maana WABUNGE wa hii MIKOA MITATU [3] ya MWANZA, SHINYANGA NA TABORA huwa wanaenda BUNGENI kama wanaenda SOKONI.
 
Na hawa VIONGOZI wa MIKOA MITATU [3] YA MWANZA, SHINYANGA NA TABORA wakiwemo WABUNGE NA MADIWANI wa CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️ wote ni WALALA HOI au kwa jina lingine wanaitwa ni HOHE-HAHE ambao wanakuwa BRAINWASHED kwanza, kabla ya kupewa nafasi yoyote ndani ya CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️.

Yaani ni WATU ambao hawana nguvu yoyote, iwe ni nguvu ya KISIASA au hata nguvu ya KIUCHUMI, hawana!!

Ndio maana WABUNGE wa hii MIKOA MITATU [3] ya MWANZA, SHINYANGA NA TABORA huwa wanaenda BUNGENI kama wanaenda SOKONI.
Hahahaha.kama wanaenda sokon.mandela bna.
 
Shukrani sana, Mkuu Charles Mandela!

-5903306723446336694_121.jpg

Haya ndio matumizi sahihi ya MITANDAO YA KIJAMII na mkitumia MITANDAO YA KIJAMII vizuri mtafahamu mambo mengi sana.
 
Usikae kimya ,mkuu huu uzi miaka 10+ijayo itakua n funzo kubwa kwa watu wengi.hapa ndo umuhimu wa mitandao unaonekana.

IMG_20211215_105753.jpg

OSCAR SALATHIEL KAMBONA - mwanafunzi, rafiki wa karibu na baadae ADUI mkubwa wa HAYATI MWALIMU.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni MWAMBA wa chama cha TANU na SERIKALI YA TANZANIA 🇹🇿 kwa ujumla.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni MWANASIASA namba mbili kwa ushawishi baada ya HAYATI MWALIMU.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alizaliwa mkoa wa RUVUMA mwaka 1928, baba yake alikuwa ni MCHUNGAJI wa KANISA LA ANGLIKANI na mmoja kati ya wachungaji wa kwanza wa KIAFRIKA nchini TANZANIA 🇹🇿.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alianza kwa kufundishwa chini ya MTI na shule ya awali alisoma shule ya MTAKATIFU BARNABASI huko kwao na baadae aliendelea na masomo ya SEKONDARI katika shule ya ALLIANCE iliyopo DODOMA.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni mwanafunzi mwenye uwezo mkubwa darasani, kwa vile baba yake alikuwa hana uwezo wa kulipa ADA YA SHULE, OSCAR alitumia mbinu ya kujifunza na kuweza kusali kwa LUGHA YA KIINGEREZA 🇬🇧 na kumshawishi ASKOFU - MUINGEREZA amlipie ADA YA SHULE.

Baadae alimaliza SHULE YA SEKONDARI YA ALLIANCE na kufaulu kwenda SEKONDARI YA JUU katika SHULE YA WAVULANA YA TABORA, huko sasa ndipo alipokutana na HAYATI MWALIMU.

Wakati huo HAYATI MWALIMU alikuwa tayari ni MWALIMU na alikuwa anafundisha SHULE YA KIKATOLIKI YA MTAKATIFU MARIA iliyopo TABORA MJINI.

Basi baada ya kumaliza SHULE YA SEKONDARI YA JUU katika SHULE YA SEKONDARI YA WAVULANA YA TABORA, alipata ufadhili wa kujiunga na CHUO KIKUU CHA MAKERERE kilichopo nchini UGANDA 🇺🇬.

Baada ya masomo ya CHUO KIKUU, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alifanikiwa kuchukua SHAHADA YA UALIMU na alirudi DODOMA kufundisha SHULE YA SEKONDARI YA ALLIANCE, shule aliyosoma.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alivyokuwa SHULE YA SEKONDARI YA ALLIANCE alipanda vyeo mpaka kufikia kuwa MWALIMU MKUU kwa kipindi kifupi tu.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuja kukutana na HAYATI MWALIMU kwa mara ya pili mwaka 1954, kwenye mkutano wa TAIFA WA WAALIMU uliofanyika DAR ES SALAAM baadae mwaka 1955, akajiunga na TANU iliyokuwa imezaliwa mwaka 1954.

IMG_20211215_105719.jpg

Kipindi hicho TANU ilikuwa haina PESA ZA KUTOSHA, kwahiyo OSCAR SALATHIEL KAMBONA alifanya kazi kwa kujitolea na kwa bidii ya hali ya juu.

Alizunguka nchi nzima kuonana na machifu na wanavijiji na kwa kipindi cha mwaka mmoja alifanikiwa kuongeza wanachama wengi sana ndani ya CHAMA CHA TANU.

Mwaka 1957, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alipata UFADHILI WA MASOMO na kwenda kusoma UINGEREZA 🇬🇧, na wakati mmoja HAYATI MWALIMU akiwa UINGEREZA 🇬🇧 kwenye harakati za UHURU alilala chumba cha OSCAR KAMBONA alipokuwa chuoni.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alifunga NDOA na MISS TANGANYIKA - FLORA MORIYO mwaka 1960 na alisimamiwa na HAYATI MWALIMU mwenyewe.

3034331_2725964_msemaukweli255_20210328_105433_0.jpg

Akiwa KATIBU MKUU WA TANU kwa kushirikiana na HAYATI MWALIMU mwenyewe, waliongoza TANGANYIKA kupata UHURU, mwaka 1961.

IMG_20211215_105921.jpg

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni KIONGOZI MCHESHI na alikuwa anakubalika sana na WAZEE WA DAR ES SALAAM na watu wengi walidhani baada ya HAYATI MWALIMU kumaliza wakati wake basi OSCAR SALATHIEL KAMBONA atakuwa ni RAIS ajaye.

Umaarufu wake uliongezeka mwaka 1964, wakati JESHI LA TANZANIA 🇹🇿 lilipotaka kufanya MAPINDUZI, OSCAR SALATHIEL KAMBONA kama WAZIRI WA ULINZI alienda JESHINI na kuwatuliza ASKARI wa wakati huo. Huku RAIS HAYATI MWALIMU na MAKAMU wake, RASHID MFAUME KAWAWA walichukuliwa na kupelekwa mafichoni na WATU WA USALAMA.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alienda JESHINI akaongea na ASKARI, akasikiliza matakwa yao na kufanya usuluhishi. Madai yalikuwa ni kupandishwa mishahara na nafasi za JESHI zilizokuwa zinashikiliwa na WAZUNGU wapewe WAZAWA yaani WATANZANIA WEUSI.

Ijapokuwa kulikuwa na uvumi ya kwamba baadhi ya WAKUBWA WA SERIKALI, VYAMA VYA WAFANYAKAZI walipanga njama na JESHI ili wampindue HAYATI MWALIMU.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni maarufu sana JESHINI, walimuamini na wakatulia. Cha kushangaza ni kwamba - MAJESHI YA KENYA 🇰🇪 NA UGANDA 🇺🇬 pia na wao walifanya migomo kama hiyo, siku mbili baadae na madai yalikuwa ni yale yale.

Ndani ya BARAZA LA MAWAZIRI - OSCAR SALATHIEL KAMBONA ndio alikuwa ni mtu anayeweza kubishana na HAYATI MWALIMU na kupingana kwa hoja! Wengine waliwahi kusema kuwa OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa anaona analingana na HAYATI MWALIMU kwa hadhi.

Na mtu mwingine aliyeweza kufanya hivyo alikuwa ni ABDALLAH FUNDIKIRA aliyekuwa WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA kwa wakati huo, tena ni kwa sababu alisoma na HAYATI MWALIMU katika CHUO KIKUU CHA MAKERERE nchini UGANDA 🇺🇬.

ABDALLAH FUNDIKIRA alijiuzuru nafasi yake ya UWAZIRI baada ya kupishana kauli na HAYATI MWALIMU. [ Itaendelea.. ]
 
OSCAR SALATHIEL KAMBONA - mwanafunzi, rafiki wa karibu na baadae ADUI mkubwa wa HAYATI MWALIMU.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni MWAMBA wa chama cha TANU na SERIKALI YA TANZANIA 🇹🇿 kwa ujumla.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni MWANASIASA namba mbili kwa ushawishi baada ya HAYATI MWALIMU.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alizaliwa mkoa wa RUVUMA mwaka 1928, baba yake alikuwa ni MCHUNGAJI wa KANISA LA ANGLIKANI na mmoja kati ya wachungaji wa kwanza wa KIAFRIKA nchini TANZANIA 🇹🇿.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alianza kwa kufundishwa chini ya MTI na shule ya awali alisoma shule ya MTAKATIFU BARNABASI huko kwao na baadae aliendelea na masomo ya SEKONDARI katika shule ya ALLIANCE iliyopo DODOMA.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni mwanafunzi mwenye uwezo mkubwa darasani, kwa vile baba yake alikuwa hana uwezo wa kulipa ADA YA SHULE, OSCAR alitumia mbinu ya kujifunza na kuweza kusali kwa LUGHA YA KIINGEREZA 🇬🇧 na kumshawishi ASKOFU - MUINGEREZA amlipie ADA YA SHULE.

Baadae alimaliza SHULE YA SEKONDARI YA ALLIANCE na kufaulu kwenda SEKONDARI YA JUU katika SHULE YA WAVULANA YA TABORA, huko sasa ndipo alipokutana na HAYATI MWALIMU.

Wakati huo HAYATI MWALIMU alikuwa tayari ni MWALIMU na alikuwa anafundisha SHULE YA KIKATOLIKI YA MTAKATIFU MARIA iliyopo TABORA MJINI.

Basi baada ya kumaliza SHULE YA SEKONDARI YA JUU katika SHULE YA SEKONDARI YA WAVULANA YA TABORA, alipata ufadhili wa kujiunga na CHUO KIKUU CHA MAKERERE kilichopo nchini UGANDA 🇺🇬.

Baada ya masomo ya CHUO KIKUU, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alifanikiwa kuchukua SHAHADA YA UALIMU na alirudi DODOMA kufundisha SHULE YA SEKONDARI YA ALLIANCE, shule aliyosoma.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alivyokuwa SHULE YA SEKONDARI YA ALLIANCE alipanda vyeo mpaka kufikia kuwa MWALIMU MKUU kwa kipindi kifupi tu.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuja kukutana na HAYATI MWALIMU kwa mara ya pili mwaka 1954, kwenye mkutano wa TAIFA WA WAALIMU uliofanyika DAR ES SALAAM baadae mwaka 1955, akajiunga na TANU iliyokuwa imezaliwa mwaka 1954.

Kipindi hicho TANU ilikuwa haina PESA ZA KUTOSHA, kwahiyo OSCAR SALATHIEL KAMBONA alifanya kazi kwa kujitolea na kwa bidii ya hali ya juu.

Alizunguka nchi nzima kuonana na machifu na wanavijiji na kwa kipindi cha mwaka mmoja alifanikiwa kuongeza wanachama wengi sana ndani ya CHAMA CHA TANU.

Mwaka 1957, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alipata UFADHILI WA MASOMO na kwenda kusoma UINGEREZA 🇬🇧, na wakati mmoja HAYATI MWALIMU akiwa UINGEREZA 🇬🇧 kwenye harakati za UHURU alilala chumba cha OSCAR KAMBONA alipokuwa chuoni.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alifunga NDOA na MISS TANGANYIKA - FLORA MORIYO mwaka 1960 na alisimamiwa na HAYATI MWALIMU mwenyewe.


Akiwa KATIBU MKUU WA TANU kwa kushirikiana na HAYATI MWALIMU mwenyewe, waliongoza TANGANYIKA kupata UHURU, mwaka 1961.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni KIONGOZI MCHESHI na alikuwa anakubalika sana na WAZEE WA DAR ES SALAAM na watu wengi walidhani baada ya HAYATI MWALIMU kumaliza wakati wake basi OSCAR SALATHIEL KAMBONA atakuwa ni RAIS ajaye.

Umaarufu wake uliongezeka mwaka 1964, wakati JESHI LA TANZANIA 🇹🇿 lilipotaka kufanya MAPINDUZI, OSCAR SALATHIEL KAMBONA kama WAZIRI WA ULINZI alienda JESHINI na kuwatuliza ASKARI wa wakati huo. Huku RAIS HAYATI MWALIMU na MAKAMU wake, RASHID MFAUME KAWAWA walichukuliwa na kupelekwa mafichoni na WATU WA USALAMA.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alienda JESHINI akaongea na ASKARI, akasikiliza matakwa yao na kufanya usuluhishi. Madai yalikuwa ni kupandishwa mishahara na nafasi za JESHI zilizokuwa zinashikiliwa na WAZUNGU wapewe WAZAWA yaani WATANZANIA WEUSI.

Ijapokuwa kulikuwa na uvumi ya kwamba baadhi ya WAKUBWA WA SERIKALI, VYAMA VYA WAFANYAKAZI walipanga njama na JESHI ili wampindue HAYATI MWALIMU.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni maarufu sana JESHINI, walimuamini na wakatulia. Cha kushangaza ni kwamba - MAJESHI YA KENYA 🇰🇪 NA UGANDA 🇺🇬 pia na wao walifanya migomo kama hiyo, siku mbili baadae na madai yalikuwa ni yale yale.

Ndani ya BARAZA LA MAWAZIRI - OSCAR SALATHIEL KAMBONA ndio alikuwa ni mtu anayeweza kubishana na HAYATI MWALIMU na kupingana kwa hoja! Wengine waliwahi kusema kuwa OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa anaona analingana na HAYATI MWALIMU kwa hadhi.

Na mtu mwingine aliyeweza kufanya hivyo alikuwa ni ABDALLAH FUNDIKIRA aliyekuwa WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA kwa wakati huo, tena ni kwa sababu alisoma na HAYATI MWALIMU katika CHUO KIKUU CHA MAKERERE nchini UGANDA 🇺🇬.

ABDALLAH FUNDIKIRA alijiuzuru nafasi yake ya UWAZIRI baada ya kupishana kauli na HAYATI MWALIMU. [ Itaendelea.. ]
Nipo seat ya mbele
 
Kwa miaka ile ya uhuru, ujamaa ulikuwa ni essential sana kwa jamii yetu kwasababu taifa lilikuwa ni changa na hatukuwa sawa.

Ujamaa ulileta hali ya usawa na umoja katika kujenga taifa. Tukawa na lugha moja ya kiswahili na leo unaona faida yake unakwenda mkoa wowote na kuongea na watanzania wenzako bila pressure.

Pia kwa nyakati zile kulikuwa na baadhi ya watanzania walishaanza elements za matabaka, watu kama wachagga walikuwa na mifumo ya uchief akina mangi ambao waliamini ndio top position na waliiheshimu but Hayati baba wa taifa alifanya jitihada sana kukemea watu kujiona sio sehemu ya umoja wa taifa imagine leo bila kuwapo umoja wa taifa, kungekuwa na jamii zinawadominate wengine kwa ubabe na kuhodhi rasilimali kisheria kabisa bila kupingwa. Ila leo hapa ukiongea huo upuuzi kwanza kila mtu atakuona Takataka.

Kwahiyo ninyi watoto wa kizazi hiki cha sasa mkiwa mnaambiwa haya mastory ya ajabu ajabu ya sijui nani alifanya nini tumieni na akili zenu kuangalia kipi kinatija kipi hakina.

Sasa mfano unataka kwenye historia tuwaongelee wazee waliokuwa wanataka kumpindua nyerere kama akina bibi titi akina nani sijui yule aliyefia kigamboni ambao wao sera yao wamebeba maneno ya udini ndani yake kuwa waislaam ndio waligombania uhuru wa taifa hili.... Sasa unajiuliza huyu mtu anataka kila mtu aishi kwa misingi ya dini anayoiamini yeye au tumualeweje?!

So ni ubinafsi. Unapomuongelea nyerere hebu jaribu kwanza kumjua. Yule mzee alichofanya ni kutuwekea misingi bora sana ya jamii, sera ya ujamaa kwa nyakati zile ilikuwa muhimu sana katika kutuimarisha kama taifa changa lililotoka katika usimamizi wa wakoloni, sasa tungelianza hili taifa na sera za kibaguzi za kabila fulani liwe juu ya makabila mengine si ajabu leo katiba ungesema wasukuma, wachagga au wahaya au wahehe, au wazanaki, au wagogo ndio jamii teule ambayo inatakiwa kuwa katika uongozi. Au basi katiba ingesema dini ya usislam ndio dini ya taifa wengine nyie ni makafiri mtasali kwa maelekezo ya viongozi wa dini ya kiislam.

Haya yote nyerere aliyazima mapema sana. Na hao watu ambao unasikia walifutwa katika vitabu vya history sio kwasababu hawakuwa na mchango katika mapambano na harakati za uhuru, ila walikuwa na ajenda zao binafsi na za kimakundi.

Nitakupa mifano, wakati nyerere anakwenda kudai uhuru wa Tanzania nzima, kuna chifu sijui mangi nani yule alienda kudai uhuru wa wachaga tu baaasi, yaani kilimanjaro nadhani na Arusha kuwe ni taifa huru wasihusiane na jamii zingine, sasa huu ufala wewe unataka uandikwe katika history.

Kuna wapigania uhuru walitaka mpindua nyerere na kuanza harakati binafsi wao wakataka nyaraka za uhuru zitambue Tanzania ni jamii ya kiislam kama vile kule Sudan, somali, wakati kwa miaka ile karibu 90% ya watanzania hawapo katika Imani moja wala uislam. Sasa unataka vitabu vya history viwaongelee wapuuzi kama hawa hata kama walikuwa na harakati?!

Nyerere hata anafariki tazama maisha yake na familia yake, hivi unaweza fananisha na familia za akina mwinyi, mkapa, kikwete, na huyu wa sasa, hivi hata wanafanania.... Tazama walivyojiweka mbali na siasa za sasa. Tazama namna hawajihusishi na maswala ya uongozi au kuwa kiherehere.

Hivi mfano hili taifa lingekuwa Baba wa taifa ni kikwete, hivi 90% ya watendaji wa serikali si wangekuwa wakerewe, na katika noti hata ridhiwani angewekwa kama mtoto wa taifa. Maana sio kwa tamaa zao.

So, as much as tutamsema huyu mzee lakini, tukubali ana mema yake na ametufikisha hapa kwa wema tu sio hila wala nia mbaya. Na tunamsingi mzuri sana wa kujipanga na kuwa taifa bora afrika.

Huyu wa sasa anakosea kuleta sera za kijamaa za miaka ile nyakati hizi ambapo haziendani na nyakati hizi za mifumo ya uchumi ya soko huria.

Na tusipende kutumia neno uchumi wa kibepari bali tuseme uchumi wa soko huria.....

Tuendelee kuheshimu n akuenzi mema ya Baba wa taifa mwalimu J. K. Nyerere, na tujitahidi kuondoa huu mfumo wa ujamaa wa kifukara tujenge ujamaa wa kisasa wa soko huria ambapo tutashare mitaji, mbinu, ili tupambane na mataifa jiarani katika kuwa super economy wa afrika.
[emoji122][emoji122][emoji122]
 
Sifa kubwa ya Mwalimu Nyerere tofauti na hao wengine akiwemo Kambona ni kutoigaiga mambo, Bali aliamini kuwa matatizo ya mwafrika yataondokana na mwafrika kuishi Kama desturi yake yani kwa asili mwafrika amekuwa akiishi kijamaa...yeye alisema maendeleo ni kazi na si mikopo Kama ilivyo sasa...Kuna watu humu ni mablind supporter wa capitalism...lakini ukweli ni kwamba hata ubepari haujasaidia nchi za Afrika, ni mfumo uliopelekea nchi nyingi maskini kuwa na madeni makubwa yasiyoweza kulipika na wizi wa rasilimali...china si wakujifananisha nao, eti waliacha ujamaa na kufuata ubepari...china haijawahi kusema kuwa waliacha mfumo fulani wakaenda mfumo mwingine halafu ndo wakafanikiwa, maendeleo ya china mzizi wake ni ujamaa...ujamaa haukatazi kufanya biashara, Ila unaweka control kubwa Sana katika biashara kiasi kwamba msipokuwa na dira nzuri hamuwezi kutoboa...Ila mkijipanga vizuri mnakuwa thabiti zaidi kuliko mfumo wa kibepari ambao ni more fragile na unategemea zaidi external factors kuliko hali ya kiuchumi ya ndani...China kilichokuwa kinamkwamisha ni kutokuwa member wa World Trade Organization miaka ya nyuma...ivo kuathiri uwezo wake wa kufanya biashara...sababu kuu ya kufeli kwa ujamaa kwa nchi nyingi zilizofwata mfumo huo ni vikwazo....na kufaulu kwa ubepari ni mikopo kutoka taasisi za mabepari...na mikopo hii ilichochea rushwa, urasimu, ukiritimba na hatimaye umaskini...kwa kuwa mingi haikutumika kwa kazi mahsusi...Bali iliishia kwa wachache...halafu hawa wanaokuja kwetu na kujinasibu kuwa ni mabepari ni gia tu hiyo...ili waweze kutuibia vizuri lakini terms wanazoingia wao kwa wao wazungu zina elementi nyingi za kisoshalisti...sema hawaziiti majina hayo, kaangalie faida za kuwa mwanachama eu...na jinsi wanavyolimit free trade na nchi zisizo wanachama...tatizo la nchi za Afrika ni zaidi ya aina ya mfumo unaotumika kutawala...unaanzia kwenye nafasi ya mwafrika katika dunia ya leo...yani Kama wakikaa wenye nguvu duniani ni kipi mwafrika ataleta mezani, wao wakimwona kiongozi wa kiafrika katika mikutano yao wanajua kaja kuomba misaada, sasa namna iyo hamuwezi kutoboa...
Factos
 
OSCAR SALATHIEL KAMBONA - mwanafunzi, rafiki wa karibu na baadae ADUI mkubwa wa HAYATI MWALIMU.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni MWAMBA wa chama cha TANU na SERIKALI YA TANZANIA 🇹🇿 kwa ujumla.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni MWANASIASA namba mbili kwa ushawishi baada ya HAYATI MWALIMU.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alizaliwa mkoa wa RUVUMA mwaka 1928, baba yake alikuwa ni MCHUNGAJI wa KANISA LA ANGLIKANI na mmoja kati ya wachungaji wa kwanza wa KIAFRIKA nchini TANZANIA 🇹🇿.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alianza kwa kufundishwa chini ya MTI na shule ya awali alisoma shule ya MTAKATIFU BARNABASI huko kwao na baadae aliendelea na masomo ya SEKONDARI katika shule ya ALLIANCE iliyopo DODOMA.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni mwanafunzi mwenye uwezo mkubwa darasani, kwa vile baba yake alikuwa hana uwezo wa kulipa ADA YA SHULE, OSCAR alitumia mbinu ya kujifunza na kuweza kusali kwa LUGHA YA KIINGEREZA 🇬🇧 na kumshawishi ASKOFU - MUINGEREZA amlipie ADA YA SHULE.

Baadae alimaliza SHULE YA SEKONDARI YA ALLIANCE na kufaulu kwenda SEKONDARI YA JUU katika SHULE YA WAVULANA YA TABORA, huko sasa ndipo alipokutana na HAYATI MWALIMU.

Wakati huo HAYATI MWALIMU alikuwa tayari ni MWALIMU na alikuwa anafundisha SHULE YA KIKATOLIKI YA MTAKATIFU MARIA iliyopo TABORA MJINI.

Basi baada ya kumaliza SHULE YA SEKONDARI YA JUU katika SHULE YA SEKONDARI YA WAVULANA YA TABORA, alipata ufadhili wa kujiunga na CHUO KIKUU CHA MAKERERE kilichopo nchini UGANDA 🇺🇬.

Baada ya masomo ya CHUO KIKUU, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alifanikiwa kuchukua SHAHADA YA UALIMU na alirudi DODOMA kufundisha SHULE YA SEKONDARI YA ALLIANCE, shule aliyosoma.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alivyokuwa SHULE YA SEKONDARI YA ALLIANCE alipanda vyeo mpaka kufikia kuwa MWALIMU MKUU kwa kipindi kifupi tu.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuja kukutana na HAYATI MWALIMU kwa mara ya pili mwaka 1954, kwenye mkutano wa TAIFA WA WAALIMU uliofanyika DAR ES SALAAM baadae mwaka 1955, akajiunga na TANU iliyokuwa imezaliwa mwaka 1954.

Kipindi hicho TANU ilikuwa haina PESA ZA KUTOSHA, kwahiyo OSCAR SALATHIEL KAMBONA alifanya kazi kwa kujitolea na kwa bidii ya hali ya juu.

Alizunguka nchi nzima kuonana na machifu na wanavijiji na kwa kipindi cha mwaka mmoja alifanikiwa kuongeza wanachama wengi sana ndani ya CHAMA CHA TANU.

Mwaka 1957, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alipata UFADHILI WA MASOMO na kwenda kusoma UINGEREZA 🇬🇧, na wakati mmoja HAYATI MWALIMU akiwa UINGEREZA 🇬🇧 kwenye harakati za UHURU alilala chumba cha OSCAR KAMBONA alipokuwa chuoni.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alifunga NDOA na MISS TANGANYIKA - FLORA MORIYO mwaka 1960 na alisimamiwa na HAYATI MWALIMU mwenyewe.

Akiwa KATIBU MKUU WA TANU kwa kushirikiana na HAYATI MWALIMU mwenyewe, waliongoza TANGANYIKA kupata UHURU, mwaka 1961.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni KIONGOZI MCHESHI na alikuwa anakubalika sana na WAZEE WA DAR ES SALAAM na watu wengi walidhani baada ya HAYATI MWALIMU kumaliza wakati wake basi OSCAR SALATHIEL KAMBONA atakuwa ni RAIS ajaye.

Umaarufu wake uliongezeka mwaka 1964, wakati JESHI LA TANZANIA 🇹🇿 lilipotaka kufanya MAPINDUZI, OSCAR SALATHIEL KAMBONA kama WAZIRI WA ULINZI alienda JESHINI na kuwatuliza ASKARI wa wakati huo. Huku RAIS HAYATI MWALIMU na MAKAMU wake, RASHID MFAUME KAWAWA walichukuliwa na kupelekwa mafichoni na WATU WA USALAMA.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alienda JESHINI akaongea na ASKARI, akasikiliza matakwa yao na kufanya usuluhishi. Madai yalikuwa ni kupandishwa mishahara na nafasi za JESHI zilizokuwa zinashikiliwa na WAZUNGU wapewe WAZAWA yaani WATANZANIA WEUSI.

Ijapokuwa kulikuwa na uvumi ya kwamba baadhi ya WAKUBWA WA SERIKALI, VYAMA VYA WAFANYAKAZI walipanga njama na JESHI ili wampindue HAYATI MWALIMU.

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa ni maarufu sana JESHINI, walimuamini na wakatulia. Cha kushangaza ni kwamba - MAJESHI YA KENYA 🇰🇪 NA UGANDA 🇺🇬 pia na wao walifanya migomo kama hiyo, siku mbili baadae na madai yalikuwa ni yale yale.

Ndani ya BARAZA LA MAWAZIRI - OSCAR SALATHIEL KAMBONA ndio alikuwa ni mtu anayeweza kubishana na HAYATI MWALIMU na kupingana kwa hoja! Wengine waliwahi kusema kuwa OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa anaona analingana na HAYATI MWALIMU kwa hadhi.

Na mtu mwingine aliyeweza kufanya hivyo alikuwa ni ABDALLAH FUNDIKIRA aliyekuwa WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA kwa wakati huo, tena ni kwa sababu alisoma na HAYATI MWALIMU katika CHUO KIKUU CHA MAKERERE nchini UGANDA 🇺🇬.

ABDALLAH FUNDIKIRA alijiuzuru nafasi yake ya UWAZIRI baada ya kupishana kauli na HAYATI MWALIMU. [ Itaendelea.. ]
[ Inaendelea kutoka posti namba 910 ]

IMG_20211215_105733.jpg

Vile vile kwa mwaka 1965, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alipishana kauli na HAYATI MWALIMU kwa mara ya kwanza, ni baada ya TANZANIA 🇹🇿 kuwa NCHI ya CHAMA kimoja.

Japo OSCAR SALATHIEL KAMBONA alipitisha hoja kama WAZIRI lakini hakuafiki mabadiliko hayo kwa madai ya kwamba - SERIKALI ikijisahau hakutakuwa na namna ya kuikumbusha na inaweza ikapelekea TANZANIA 🇹🇿 kuwa ni NCHI ya KIDIKTETA.

Baadae tena, mwaka 1967 wakati wa AZIMIO LA ARUSHA - OSCAR SALATHIEL KAMBONA alipingana na HAYATI MWALIMU kwenye suala la UJAMAA. Yeye, yaani OSCAR SALATHIEL KAMBONA alisema hivi - "Ni lazima UJAMAA ujaribiwe kwanza kwa sehemu chache za TANZANIA 🇹🇿 kuona kama unafaa au haufai na baada ya hapo kama utazaa matunda, ndipo UJAMAA utumike kwa nchi nzima".

Baada ya mabishano ya FARAGHA ya muda mrefu baina ya OSCAR SALATHIEL KAMBONA na HAYATI MWALIMU, akisaidiwa na RASHID MFAUME KAWAWA, hilo AZIMIO lilipita bila kupingwa.

Na wakati mwingine OSCAR SALATHIEL KAMBONA alinukuliwa akisema ya kuwa - "RASHID MFAUME KAWAWA anaendeshwa na HAYATI MWALIMU na hana maamuzi yake".

Basi baada ya hapo, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alijiuzulu nafasi zake zote za CHAMA na SERIKALI huku akisema kuwa, sababu za kiafya ndio zimepelekea achukue uamuzi huo.


IMG_20211215_110021.jpg


Kuna taarifa zilikuwa zinasema ya kwamba, baada ya kujiuzulu kwa OSCAR SALATHIEL KAMBONA aliambiwa kuwa kuna mpango wa kumkamata na kumtia ndani, hivyo tarehe 26/07/1967 alijikusanya yeye na mkwewe na watoto wake na kuendesha gari mpaka NAIROBI - KENYA 🇰🇪 ambapo alipanda ndege na kuelekea UINGEREZA 🇬🇧.

Lakini pia, kuna taarifa zinazosema kuwa IDARA YA USALAMA WA TAIFA ilikuwa inajua OSCAR SALATHIEL KAMBONA anatoroka, ila ilimwacha aondoke ili kuepusha vurugu.

Huku nyuma kulikuwa na maneno ya kwamba OSCAR SALATHIEL KAMBONA ameondoka na PESA nyingi sana lakini OSCAR SALATHIEL KAMBONA alivyokuwa UINGEREZA 🇬🇧 alikanusha vikali na kuomba SERIKALI YA TANZANIA 🇹🇿 iwasiliane na SERIKALI YA KENYA 🇰🇪 ili kupata uhakika lakini SERIKALI YA TANZANIA 🇹🇿 haikufanya hivyo.

Kutokana na matukio yale, hotuba ya HAYATI MWALIMU ya mwaka 1969 kwenye sherehe ya SIKU YA MAPINDUZI, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikejeliwa na kuimbwa na WANAFUNZI WA SHULE pamoja na MAJESHI ya NCHI nzima. Nyimbo nyingi za kumkejeli OSCAR SALATHIEL KAMBONA zilitungwa MASHULENI pamoja na MAJESHINI.

Mwaka 1969, OSCAR SALATHIEL KAMBONA na wenzake saba [ 7 ] akiwemo BIBI TITI MOHAMMED walishitakiwa kwa kosa la UHAINI, ikidaiwa walikuwa wamepanga njama za kufanya MAPINDUZI dhidi ya SERIKALI ya HAYATI MWALIMU. Kwenye ile kesi kuna watu ambao walifungwa miaka kumi [ 10 ], wengine walifungwa MAISHA ila OSCAR SALATHIEL KAMBONA kwa sababu hakuwepo TANZANIA 🇹🇿, yeye MAISHA yaliendelea kama kawaida.

Lakini pamoja na haya yote, OSCAR SALATHIEL KAMBONA huwa anafananishwa na MWANASIASA KIJANA kutoka nchi ya KENYA 🇰🇪 aliyekuwa anaitwa TOM MBOYA.



Masaibu, matukio ya kisiasa na mambo waliyoyapitia hawa WANASIASA wawili karibia wote wanafanana.



Na baada ya kuanzishwa kwa MFUMO WA VYAMA VINGI mwaka 1992, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alitangaza kurudi TANZANIA 🇹🇿 kwa masharti ya SERIKALI isije ikamkamata.

Baada ya kurudi TANZANIA 🇹🇿, OSCAR SALATHIEL KAMBONA aliitisha mkutano mkubwa wa KISIASA kwenye UWANJA WA JANGWANI - DAR ES SALAAM, ukiwa na malengo ya kuwaeleza WATANZANIA kilichomfanya kuwa mkimbizi na uchafu wa VIONGOZI WAKUBWA WA SERIKALI.

Kwenye ule mkutano alisema HAYATI MWALIMU ni MTUSI wa RWANDA 🇷🇼! RASHID MFAUME KAWAWA na HAYATI BENJAMIN MKAPA ni watu wa MSUMBIJI 🇲🇿 na huku JOHN MALECELA ni MKONGOMANI 🇨🇩.

Pia alidai HAYATI MWALIMU na RASHID MFAUME KAWAWA wameficha PESA nyingi sana ULAYA 🇪🇺. Kwa kuwa OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa hana ushahidi, basi watu wengi walimpotezea na umaarufu wake ulianza kupungua tangu siku ile.

Baadae OSCAR SALATHIEL KAMBONA alianzisha CHAMA CHA KISIASA cha TADEA ambacho hakikufanya vizuri KITAIFA. Na kipindi hicho alikuta hii JAMII ya MWASHITA yaani SIMBA 🦁 yaani wale wenyeji wa hii MIKOA MITATU [ 3 ] ya MWANZA, SHINYANGA NA TABORA walikuwa tayari wameshaanza kujijenga KIUCHUMI na KISIASA kupitia CHAMA CHA WANANCHI - CUF ☀️.

Mwaka 1997, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alifariki dunia nchini UINGEREZA 🇬🇧 na walifuatana na ndugu yake OTIMI SALATHIEL KAMBONA. Huku kwa miaka michache ya baadae mtoto wake wa kwanza, pia alifariki kwa mazingira ya kutatanisha nchini UINGEREZA 🇬🇧. Hali hii ilileta sintofahamu kubwa sana kwa WATANZANIA.

Mwili wa OSCAR SALATHIEL KAMBONA ulirudishwa TANZANIA 🇹🇿 na kupokelewa na aliyekuwa WAZIRI WA MAMBO YA NJE kwa wakati huo na RAIS WA AWAMU YA NNE [ 4 ], Ndugu JAKAYA MRISHO KIKWETE.

Licha ya kuwahi kuwa marafiki wakubwa, HAYATI MWALIMU hakuhudhuria MSIBA wa OSCAR SALATHIEL KAMBONA. [ Itaendelea.. ]
 
Wakati BW. SALATHIEL anatofautiana kimtazamo na HAYATI MWALIMU kwa nini alichagua kupata hifadhi UINGEREZA na si kwingineko?

IMG_20211215_105955.jpg

OSCAR SALATHIEL KAMBONA alichagua kupata hifadhi nchini UINGEREZA 🇬🇧 kwa sababu ya mafungamano makubwa na KANISA LA ANGLIKANI.

KANISA LA ANGLIKANI lina mafungamano makubwa na TAIFA LA UINGEREZA 🇬🇧, yaani kwa lugha nyingine tunaweza kusema hivi - KANISA LA ANGLIKANI ni KANISA LA UINGEREZA 🇬🇧 kulingana na historia ya KANISA.

Kwahiyo kwa upande wa OSCAR SALATHIEL KAMBONA ilikuwa ni nafuu kwake kwenda UINGEREZA 🇬🇧 kutokana na BABA MZAZI kuwa MCHUNGAJI au MTUMISHI wa KANISA LA ANGLIKANI lenye mafungamano makubwa na TAIFA LA UINGEREZA 🇬🇧.
 
OSCAR SALATHIEL KAMBONA alichagua kupata hifadhi nchini UINGEREZA [emoji636] kwa sababu ya mafungamano makubwa na KANISA LA ANGLIKANI.

KANISA LA ANGLIKANI lina mafungamano makubwa na TAIFA LA UINGEREZA [emoji636], yaani kwa lugha nyingine tunaweza kusema hivi - KANISA LA ANGLIKANI ni KANISA LA UINGEREZA [emoji636] kulingana na historia ya KANISA.

Kwahiyo kwa upande wa OSCAR SALATHIEL KAMBONA ilikuwa ni nafuu kwake kwenda UINGEREZA [emoji636] kutokana na BABA MZAZI kuwa MCHUNGAJI au MTUMISHI wa KANISA LA ANGLIKANI lenye mafungamano makubwa na TAIFA LA UINGEREZA [emoji636].
Mkuu samahani unaweza elezea hapa katika fikra za kimapinduzi alizo kuwa nazo OK na JkN nani alikuwa sahihi kulingana na nyakati hizo?

Pia Kuna tetesi kwamba rais wa awamu ya tatu alikuwa na mchango mkubwa Sana katika kuwagombanisha watu hawa je ni kweli?
 
Mkuu samahani unaweza elezea hapa katika fikra za kimapinduzi alizo kuwa nazo OK na JkN nani alikuwa sahihi kulingana na nyakati hizo?
OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa na FIKRA ZA KIMAGHARIBI yaani FIKRA ZA KIBEPARI na HAYATI MWALIMU alikuwa ni muumini wa FIKRA ZA KIJAMAA.

Lakini wale WANAZUONI waliowashuhudia hawa WATU wawili yaani HAYATI MWALIMU na OSCAR SALATHIEL KAMBONA walikuwa wanasema hivi - "Aliyekutangulia, amekutangulia tu!" au kuna msemo mwingine huwa wanasema hivi - "Mwanafunzi bora hawezi kuwa kama MWALIMU wake, hata awe mzuri vipi!"

Kwahiyo pamoja na OSCAR SALATHIEL KAMBONA kuwa na mazuri yake lakini HAYATI MWALIMU alionekana kuwa ni bora, kwa sababu ndio aliyemkaribisha OSCAR SALATHIEL KAMBONA ndani ya CHAMA CHA TANU.
Pia Kuna tetesi kwamba rais wa awamu ya tatu alikuwa na mchango mkubwa Sana katika kuwagombanisha watu hawa je ni kweli?
Hapana, SIO KWELI! Kwa sababu WANASIASA wenye umri na rika la HAYATI BENJAMIN WILLIAM MKAPA ambaye ndiye aliyekuwa anaitwa MISTER CLEAN walikuta mapokeo, nyaraka na historia ya OSCAR SALATHIEL KAMBONA, na hakuna cha ziada zaidi ya hapo.

Sema kilichokuja kuharibu ni MAWASILIANO YA FAKSI baina ya OSCAR SALATHIEL KAMBONA na aliyekuwa SPIKA MSTAAFU ADAM SAPI MKWAWA na hata baada ya kurudi TANZANIA 🇹🇿, huyo OSCAR SALATHIEL KAMBONA aliongeza maadui kwa kuwataja RASHID MFAUME KAWAWA na HAYATI BENJAMIN WILLIAM MKAPA kuwa ni WATU wenye asili ya MSUMBIJI 🇲🇿 na JOHN MALECELA kuwa ni MTU mwenye asili ya KONGO 🇨🇩.

Kwahiyo, HAYATI BENJAMIN WILLIAM MKAPA alivyofanikiwa kuingia IKULU alikuwa tayari ana ORODHA YA MAJINA YA WANASIASA ambao walikuwa wanatakiwa kushikishwa ADABU, miongoni mwa MAJINA hayo ni ADAM SAPI MKWAWA na OSCAR SALATHIEL KAMBONA.

Mwaka 1996, alinukuliwa HAYATI BENJAMIN WILLIAM MKAPA akisema hivi - "Hizo milioni thelathini [ 30,000,000 ] alizobakiza ADAM SAPI MKWAWA ndio zitamtosha kulea mpaka wajukuu zake". Na kilichofuata ni historia, sote tunatambua kilichompata ADAM SAPI MKWAWA na familia yake, sasa hivi wote wanaomba omba misaada kwenye vituo vya televisheni huko 😂😂

Halafu cha ajabu na cha kushangaza, kuna TAASISI ambazo zinatumia JINA LA "MKWAWA" na hazinufaishi familia ya MKWAWA 🙏🏽🇹🇿🙏🏽

Baada ya miaka miwili yaani mwaka 1997, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alifariki dunia akiwa LONDON - UINGEREZA 🇬🇧 na huo ndio ulikuwa mwisho wa habari za OSCAR SALATHIEL KAMBONA.

Sasa wale MWASHITA yaani SIMBA 🦁 yaani wale waliokuwa wafanyakazi wa vyama vya ushirika vya NCU, SHIRECU na WETCU waliona na kushuhudia yote haya yakifanyika na wakaja na AZIMIO LA PAMOJA la kutoshiriki siasa za CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️,yaani wao na vizazi vyao.

Baada ya hapo, hawa MWASHITA yaani SIMBA 🦁 yaani wale waliokuwa wafanyakazi wa vyama vya ushirika vya NCU, SHIRECU na WETCU wakiongozwa na MISTER ABILITY waliamua kupitisha maazimio ya pamoja ya kutoshiriki SIASA ZA CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM ⚒️, yaani wao na vizazi vyao.
 
[ Inaendelea kutoka posti namba 910 ]

Vile vile kwa mwaka 1965, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alipishana kauli na HAYATI MWALIMU kwa mara ya kwanza, ni baada ya TANZANIA 🇹🇿 kuwa NCHI ya CHAMA kimoja.

Japo OSCAR SALATHIEL KAMBONA alipitisha hoja kama WAZIRI lakini hakuafiki mabadiliko hayo kwa madai ya kwamba - SERIKALI ikijisahau hakutakuwa na namna ya kuikumbusha na inaweza ikapelekea TANZANIA 🇹🇿 kuwa ni NCHI ya KIDIKTETA.

Baadae tena, mwaka 1967 wakati wa AZIMIO LA ARUSHA - OSCAR SALATHIEL KAMBONA alipingana na HAYATI MWALIMU kwenye suala la UJAMAA. Yeye, yaani OSCAR SALATHIEL KAMBONA alisema hivi - "Ni lazima UJAMAA ujaribiwe kwanza kwa sehemu chache za TANZANIA 🇹🇿 kuona kama unafaa au haufai na baada ya hapo kama utazaa matunda, ndipo UJAMAA utumike kwa nchi nzima".

Baada ya mabishano ya FARAGHA ya muda mrefu baina ya OSCAR SALATHIEL KAMBONA na HAYATI MWALIMU, akisaidiwa na RASHID MFAUME KAWAWA, hilo AZIMIO lilipita bila kupingwa.

Na wakati mwingine OSCAR SALATHIEL KAMBONA alinukuliwa akisema ya kuwa - "RASHID MFAUME KAWAWA anaendeshwa na HAYATI MWALIMU na hana maamuzi yake".

Basi baada ya hapo, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alijiuzulu nafasi zake zote za CHAMA na SERIKALI huku akisema kuwa, sababu za kiafya ndio zimepelekea achukue uamuzi huo.


Kuna taarifa zilikuwa zinasema ya kwamba, baada ya kujiuzulu kwa OSCAR SALATHIEL KAMBONA aliambiwa kuwa kuna mpango wa kumkamata na kumtia ndani, hivyo tarehe 26/07/1967 alijikusanya yeye na mkwewe na watoto wake na kuendesha gari mpaka NAIROBI - KENYA 🇰🇪 ambapo alipanda ndege na kuelekea UINGEREZA 🇬🇧.

Lakini pia, kuna taarifa zinazosema kuwa IDARA YA USALAMA WA TAIFA ilikuwa inajua OSCAR SALATHIEL KAMBONA anatoroka, ila ilimwacha aondoke ili kuepusha vurugu.

Huku nyuma kulikuwa na maneno ya kwamba OSCAR SALATHIEL KAMBONA ameondoka na PESA nyingi sana lakini OSCAR SALATHIEL KAMBONA alivyokuwa UINGEREZA 🇬🇧 alikanusha vikali na kuomba SERIKALI YA TANZANIA 🇹🇿 iwasiliane na SERIKALI YA KENYA 🇰🇪 ili kupata uhakika lakini SERIKALI YA TANZANIA 🇹🇿 haikufanya hivyo.

Kutokana na matukio yale, hotuba ya HAYATI MWALIMU ya mwaka 1969 kwenye sherehe ya SIKU YA MAPINDUZI, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikejeliwa na kuimbwa na WANAFUNZI WA SHULE pamoja na MAJESHI ya NCHI nzima. Nyimbo nyingi za kumkejeli OSCAR SALATHIEL KAMBONA zilitungwa MASHULENI pamoja na MAJESHINI.

Mwaka 1969, OSCAR SALATHIEL KAMBONA na wenzake saba [ 7 ] akiwemo BIBI TITI MOHAMMED walishitakiwa kwa kosa la UHAINI, ikidaiwa walikuwa wamepanga njama za kufanya MAPINDUZI dhidi ya SERIKALI ya HAYATI MWALIMU. Kwenye ile kesi kuna watu ambao walifungwa miaka kumi [ 10 ], wengine walifungwa MAISHA ila OSCAR SALATHIEL KAMBONA kwa sababu hakuwepo TANZANIA 🇹🇿, yeye MAISHA yaliendelea kama kawaida.

Lakini pamoja na haya yote, OSCAR SALATHIEL KAMBONA huwa anafananishwa na MWANASIASA KIJANA kutoka nchi ya KENYA 🇰🇪 aliyekuwa anaitwa TOM MBOYA.



Masaibu, matukio ya kisiasa na mambo waliyoyapitia hawa WANASIASA wawili karibia wote wanafanana.

Na baada ya kuanzishwa kwa MFUMO WA VYAMA VINGI mwaka 1992, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alitangaza kurudi TANZANIA 🇹🇿 kwa masharti ya SERIKALI isije ikamkamata.

Baada ya kurudi TANZANIA 🇹🇿, OSCAR SALATHIEL KAMBONA aliitisha mkutano mkubwa wa KISIASA kwenye UWANJA WA JANGWANI - DAR ES SALAAM, ukiwa na malengo ya kuwaeleza WATANZANIA kilichomfanya kuwa mkimbizi na uchafu wa VIONGOZI WAKUBWA WA SERIKALI.

Kwenye ule mkutano alisema HAYATI MWALIMU ni MTUSI wa RWANDA 🇷🇼! RASHID MFAUME KAWAWA na HAYATI BENJAMIN MKAPA ni watu wa MSUMBIJI 🇲🇿 na huku JOHN MALECELA ni MKONGOMANI 🇨🇩.

Pia alidai HAYATI MWALIMU na RASHID MFAUME KAWAWA wameficha PESA nyingi sana ULAYA 🇪🇺. Kwa kuwa OSCAR SALATHIEL KAMBONA alikuwa hana ushahidi, basi watu wengi walimpotezea na umaarufu wake ulianza kupungua tangu siku ile.

Baadae OSCAR SALATHIEL KAMBONA alianzisha CHAMA CHA KISIASA cha TADEA ambacho hakikufanya vizuri KITAIFA. Na kipindi hicho alikuta hii JAMII ya MWASHITA yaani SIMBA 🦁 yaani wale wenyeji wa hii MIKOA MITATU [ 3 ] ya MWANZA, SHINYANGA NA TABORA walikuwa tayari wameshaanza kujijenga KIUCHUMI na KISIASA kupitia CHAMA CHA WANANCHI - CUF ☀️.

Mwaka 1997, OSCAR SALATHIEL KAMBONA alifariki dunia nchini UINGEREZA 🇬🇧 na walifuatana na ndugu yake OTIMI SALATHIEL KAMBONA. Huku kwa miaka michache ya baadae mtoto wake wa kwanza, pia alifariki kwa mazingira ya kutatanisha nchini UINGEREZA 🇬🇧. Hali hii ilileta sintofahamu kubwa sana kwa WATANZANIA.

Mwili wa OSCAR SALATHIEL KAMBONA ulirudishwa TANZANIA 🇹🇿 na kupokelewa na aliyekuwa WAZIRI WA MAMBO YA NJE kwa wakati huo na RAIS WA AWAMU YA NNE [ 4 ], Ndugu JAKAYA MRISHO KIKWETE.

Licha ya kuwahi kuwa marafiki wakubwa, HAYATI MWALIMU hakuhudhuria MSIBA wa OSCAR SALATHIEL KAMBONA. [ Itaendelea.. ]

Mkuu tunasubir uendelee hapa.
Alafu mister ability n nan?hii code nimeisahau.
 
Back
Top Bottom