Charles Mandela
JF-Expert Member
- Dec 9, 2011
- 2,752
- 2,282
Eeh! Wale waliokuwa wafanyakazi wa VYAMA VIKUU VYA USHIRIKA VYA MWANZA [NCU], SHINYANGA [SHIRECU] na TABORA [WETCU] yaani MWASHITA walikuwa wana hela, haijapata kutokea mpaka leo.basi mwashita si aanzishe dola yake tuu, mapesa yote hayo
Kuna kipindi fulani cha miaka ya tisini [1990's] hadi elfu mbili [2000's], TANZANIA iliwahi kuwa na BALOZI NCHI YA KANADA aliyekuwa anaitwa MAMA CHIPUNGAHELO.
Huyu MAMA CHIPUNGAHELO aliwahi pia kuwa MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM. Sasa kipindi fulani akiwa BALOZI WA TANZANIA kwa upande wa TAIFA LA KANADA alikuwa anawasifia sana wafanyakazi wa CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA CHA MKOA WA KAGERA [KCU].
Wale waliokuwa wafanyakazi wa CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA CHA MKOA WA KAGERA [KCU] walikuwa wamewekeza sana kwenye MAJENGO, hadi KANADA walikuwa wameshawekeza na hawa wengine wa VYAMA VIKUU VYA USHIRIKA VYA MWANZA [NCU], SHINYANGA [SHIRECU] na TABORA [WETCU] walikuwa wanawekeza kwenye SEKTA YA USAFIRISHAJI WA ABIRIA NA MIZIGO.
Ilifikia hatua mmoja wa wafanyakazi wa CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA CHA MKOA WA KAGERA [KCU] alinunua LORI moja aina ya MERCEDES BENZ, halafu akaipeleka SHINYANGA MJINI. Pale SHINYANGA MJINI ilikuwa inatembea tembea tu.
Pembeni ya bodi ilikuwa imechorwa MIKUNGUU YA NDIZI na upande wa mbele kwenye bodi ilikuwa imeandikwa "NINSIMAKATONDA" maana yake ni "TUNAMSHUKURU MUNGU" kwa LUGHA YA KIHAYA. Hilo LORI lipo hadi leo na limepaki kule kwenye zile gereji za UWANJA WA KAMBARAGE. Ilikuwa ni MERCEDES BENZ yenye kichwa cha rangi ya kijani na bodi ya rangi nyeupe.
Sasa wale waliokuwa wafanyakazi wa VYAMA VIKUU VYA USHIRIKA VYA MWANZA, SHINYANGA na TABORA yaani MWASHITA walivyosikia hivyo walifanya KUFURU, ikiwa pamoja na kununua na kumiliki KIWANDA CHA SUKARI CHA KAGERA na waliwekeza sana kwenye MAJENGO, SEKTA YA VIWANDA pamoja na SEKTA YA USAFIRISHAJI.