Tanzania yapokea mkopo wa trilioni 1.2 kutoka Benki ya Dunia. Kuboresha tabia nchi, usalama na barabara

Tanzania yapokea mkopo wa trilioni 1.2 kutoka Benki ya Dunia. Kuboresha tabia nchi, usalama na barabara

Benki ya Dunia imeipa Serikali ya Tanzania trilioni 1.2 kwaajili ya tabia nchi, barabara na viwanja vya ndege.

Nadhani sasa ni muda wa kuondoa tozo au kuambiwa siku ya ukomo.

Kiuchumi mkopo unakwenda kusisimua mzunguko wa fedha hasa kama sehemu kubwa ya hizi tenda yatapewa makampuni ya hapa nchini, pesa zitatembelea mifuko ya wananchi na shughuli za uzalishaji zitaongezeka kupokea pesa za wananchi hawa. Hasara yake, tunaandika deni jipya katika madeni ya Serikali.
======


Tanzania imepokea mkopo wa masharti nafuu wa Sh1.2 trilioni utakaofungua milango ya kuboresha usalama, ustahimilivu wa tabianchi, uwezo wa barabara za ndani na viwanja vya ndege vya Mikoa.

Taarifa iliyotolewa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Benki ya Dunia (IDA) leo Mei 27, imesema mkopo huo utaiwezesha Tanzania kufanikisha maeneo hayo chini ya Mradi wa Ushirikiano wa Usafiri Tanzania (TanTIP) utakaowezesha pia taasisi husika katika kupanga na kusimamia sekta hiyo.

Imesema ufadhili huo utasaidia uboreshaji na ukarabati wa barabara zenye urefu wa kilomita 500, zikiwemo za Mtwara-Mingoyo-Masasi (kilomita 201), Lusahunga-Rusumo (kilomita 92), Songea-Rutukila (kilomita 111) na Iringa-Msembe (kilomita 104), huku ikishughulikia hali ya hewa ili kuongeza ustahimilivu wa barabara.
Baada ya serikali kupata huu mkopo tuwe tunaambiwa kabisa kuwa tumefikia deni kiasi gani hadi hapo?Maana imezoeleka hapa kwetu,mikopo inageuzwa kuwa mapato ya ndani na mapato ya ndani yanakuwa kwa akili ya kuinufaisha CCM na serikali zake.Haiwezekani miradi iliyotekelezwa kwa fedha za mikopo tuambiwe ni CCM imetekeleza kwa sababu kukopa siyo ilani wala umahiri.Unakopa kwa sababu huna mbinu nyingine/as the last option.
Pia nchi yetu lazima ijikite katika miradi,shughuli zinazowezekana kwa mapato yetu.Fedha za mikopo zielekezwe katika miradi ambayo sisi kama nchi hatuwezi kuifanya.
 
Benki ya Dunia imeipa Serikali ya Tanzania trilioni 1.2 kwaajili ya tabia nchi, barabara na viwanja vya ndege.


Tabia ya nchi ni vitu kama vipi....????? na ni vinahitaji mikopo kweli....na vitarudishaje mkopo huo...

Waswahili wengi huwa tunashindwa kulipa madeni kwasababu tunatumia hela za mikopo kwa mambo yasiyotupa uwezo wa kuzirudisha...

That's why Yaaani Baba kuumwa Jipu tu,, watoto wanadai urithi
 
MOTHERF-VCK ,Holy trinity(IMF ,WORLD BANK & WTO)....Poverty Trap!!
 
Safi sana Mama Samia. Muangalie na mkoa wa Pwani.

Barabara ya Kisarawe inahitaji lami lakini pia barabara ya kuunganisha makao makuu ya mkoa - Kibaha na wilaya zake hakuna.

Ajabu Jakaya hakuliona hili licha ya kutoka mkoa husika.
Aliiona msoga? We Huoni DSM to msoga full Lami.
 
Unafuu wa maisha uwepo basi kama mche wa sabuni ulishindikana kununulika kwa 2,000 saivi hiyo hela unapata nusu mche poor organization in Ministry which deals with Industry sector
 
Huko ndiko kuupiga mwingi!! Sawa tuendelee kumshangilia, nyama ziko chini tutazikuta!
 
trilioni 1.2 kwaajili ya tabia nchi, barabara na viwanja vya ndege.
Eti barabara, hivi ni vichekesho,
Kuna barabara kariakoo zimejengwa kwa gharama kweli ila zimekuwa ni maegesho ya magari(parking)na kukusanya 500 kwa saa, yaani badala zitumike kwa makusudio basi zimekuwa ni parking yaani hovyo kabisa
Na malori yamejazana humo yaani haziwezi kudumu hata miaka miwili na huu ni ubadhirifu wa hela na uhujumu uchumi
Yaani kwa ufupi zinaenda kubugiwa tu
 
Sina tatizo na mama Samia kupata pesa hizi za "mikopo" zinazowezesha baadhi ya vitu ndani. Kama kweli hizi pesa zikitumika vizuri, viwanja vya ndege vikajengwa, barabara zenye ubora zikajengwa, na miradi mingine mingine yenye kuboresha sura ya nchi, hili ndilo kila mtanzania analitaka.

Tatizo la msingi nililonalo ni "agenda behind" zinazosukuma mama "awezeshwe" namna hii na wale tuliozoea kuwaita mabeberu, hawa wanaoshikilia uchumi wa dunia. Agenda iliyo nyuma ni hawa hawa "mabeberu" kutaka kuuaminisha umma wa Tanzania kwamba "mnaona? mkicheza vizuri na sisi mtapata wepesi katika mambo yenu. Yule jamaa yenu aliyejimwambafy na mamiradi makubwa makubwa kama ya reli za kisasa, umeme wa kutosheleza, maviwanja ya ndege ya kisasa, madaraja marefu marefu, mlimkubali sana kwa sababu ya mamiradi kama hayo. Lakini huyu mama rais wenu mpya asiye na shida na sisi tutamsaidia kufanya hayo hata bila ya yeye kutupigia kelele kwamba tunaiba madini yenu".

Hawa jamaa ni plotters balaa. Bila Magufuli kufurukuta na kuwapigia makelele wala tusingefika hata hapa.
 
Pesa za kulipia nyongeza ya mishahara hiyo sisi tulio deep tunajua
 
Back
Top Bottom