Tanzania, Zanzibar zasaini Hati ya Makubaliano Sekta ya Madini
CHETU CHETU, CHAO CHAO

Huyu mama inaelekea moyoni mwake ana hasira na huu muungano, anaamini Tanganyika inaikalia Zanzibar. Sasa kashika madaraka kaamua kutukomesha.
Haswa.

Huyu ni katika kundi lile lile la OMO, ila kwa vile ni muigizaji mzuri, kama alivyoonyesha akiwa chini ya Magufuli, Kikwete na udhaifu wake wa akili hakuweza kumtambua huyu na kumleta ndani ya serikali.

Sasa anafanya kila kitu kuamsha hisia za waTanganyika ili muungano uvunjike; na kwa mwendo huu anaokwenda nao atafanikiwa sana.
 
Kuna habari njema, SSH anaua muungano na hadi sasa amefanikiwa sana. Watanganyika wanayaona haya na ndiyo maana ikitokea kama la Bandari wanakuwa wakali sana!
Hii ndiyo kazi kubwa inayofanyika.
Sasa sina shaka tena, naomba tu ifanikiwe, tena kwa haraka.
 
Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko ameshuhudia utiaji saini wa Hati ya Makubaliano kati ya Wizara ya Madini ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wizara ya Maji, Nishati na Madini ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Makubaliano hayo ni mwendelezo wa ushirikiano uliopo baina ya wizara hizo mbili zilizopo katika upande wa Muungano ikiwa ni maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa Februari, 2023 jijini Arusha ya kushirikiana kwa lengo la kufanya madini yaliyopo katika maeneo husika yaweza kuleta manufaa kwa pande zote mbili.
images (76).jpeg


Tanzania ni nini Tanzania imetokana na Muunganiko wa nchi mbili zenye mamlaka kamili Tanganyika na zanzibar.

Hayo sio maneno yangu jamanini nisije nikaambiwa nina nia mbaya na muungano ni maneno ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977 Sehemu ya kwanza ibara ya 1 na 2 ikisomwa pamoja na sheri ya Kutangaza Jamhuri ya Muungano Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 na pia Nyongezqa yake Eneo la Jamhuri ya Muungano Sheria ya 1984 Na.15 ib.6
ntanukuu kidogo..
1.Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano.
2.-(1) Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo.

Huenda labda nitoe kidgo Muhtasari ili nielewe kilichoandikwa hapo juu historia ndogo kidgo ili nielewe zaidi
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliundwa Aprili 26, 1964 ikiwa ni Muungano wa Mataifa mawili huru ya Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ambapo Jamhuri hizi mbili ziliingia mkataba wa Muungano mnamo mwaka 1964 na kuanzishwa Dola ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kabla ya Serikari ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kulikuwa na nchi mbili huru zilizokuwa zikijitegemea:

Jamhuri ya Tanganyika iliyoundwa mwaka 1962 baada ya kupata uhuru tarehe 9 Desemba, 1961
na
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar iliyoundwa kufuatia Mapinduzi ya Januari 12, mwaka 1964.

Kila nchi ilikuwa na mamlaka yake (sovereign) ikiwa na eneo na mipaka, Katiba na Serikali yake, na iliendesha shughuli zake kwa kujitegemea kiuitawala.

Sasa Tuone kwenye Swala hili walilotia SIGN NASHANGAA NI KWANINI WAKATI NI MOJA YA SWALA LILILOPO KWENYE KATIBA KAMA SWALA LA MUUNGANO BADO LIWEKEWE TENA SAINI KWA SABABU MOJA YA MASWALA YA MUUNGANO 22 MADINI NA NISHATI LIPO NA HALINA HAJA YA MAKUBALIANO NA KINGINE KWANINI TUNAKUWA WAOGA KUTUMIA JINA LA TANGANYIKA WAKATI TUNATUMIA JINA LA ZANZIBAR PEKE YAKE
 
Zipo Taarifa kwamba Tanzania na Zanzibar zimesaini Makubaliano kwenye sekta ya madini .

Sasa mimi kwa akili yangu ndogo sijaelewa chochote , Aliyeelewa anisaidie mimi na wengine wenye akili ndogo kama yangu .

Natanguliza shukrani

Screenshot_2023-07-20-15-53-04-1.jpg
 
Changu ni changu chako ni chetu[emoji56][emoji56][emoji56]
 
Sasa itabidi tuweke utaratibu wa namna hiyo kwa kila mkoa.
Nimeuliza wapi makubaliano ya 'Tanzania na Kigoma' kuhusu kilimo cha Mawese?
Wapi makubaliano ya Tanzania na Mwanza kuhusu dhahabu na Almasi?
Wapi makubaliano ya Tanzania na Rukwa kuhusu Mahindi?
Huu ni ujinga wa kipekee kabisa.
SSH ameamua liwalo na liwe, na kafanikiwa sana si kuutikisa muungano bali kuuvunjilia mbali
So far kule Kisonge wanashangaa kama huyu ni 'mwenzetu au ni Mwenzao'
Hawa watu kazi imewashinda kila mahali.
Hawa wanaosaini ni matumbo tu hakuna anayejali mtoto wake na kijukuu kitaku na amali gani.
Tunawajua, ni VP , PM na Speaker. Halafu wapambe wao mawaziri. Siku Tanganyika ikirudi hatutaki kuwasikia
Mafao yenu mtayapata Tanzania !
Sina shaka hilo nalo waziri kapewa kama agizo toka kwa Samia, ili kuipa uzito mkubwa Zanzibar, ionekane kuwa na hadhi sawa na serikali ya Tanzania.
Kuna waziri mmoja mwanamana aliondolewa kwasababu tu alishauri jambo kinyume na 'maagizo' kutoka juu
Watu hawayaoni matendo haya na kuyaelewa vizuri, ili wayape uzito unaostahili.
Bandari imesaidia sana kuwaonyesha Watanganyika matundu mengi, hata hili linaonekana kwasababu kila anachokifanya SSH watu wanakifuatilia. Unakumbuka bill za umeme zimefutwa kwa maagizo ! Makamba alitenda tu lakini maagizo yalitoka juu. Kwamba Wazanzibar walipiwe bill za umeme na mama ntilie wa Ilala! sad
Matukio yote haya ni alama za Samia kuutengeneza muungano uwe wanavyoutaka wao, Zanzibar.
Na ndicho kinaendelea. Zile kero 20 za Wazanzibar kazimaliza yeye na Rais Mwinyi. Think about that

Na mijitu ya Tanganyika ipo inakenua tu meno (nawazungumzia viongozi waliomo ndani ya CCM,mawaziri na mibunge).
Tunawaona na tuna majina yao, ipo siku tutawauliza kuhusu haya. Ipo siku watoto wao wataogopa kunasabishwa na majina ya baba zao kwasababu majina tu yatakuwa ''sumu''
Zanzibar, kupitia kwa Samia sasa hivi inatengeneza muundo wa muungano wanaoutaka wao bila ya kuwashirikisha walioungana nao.
Hawa wanaamrishwa kutekeleza tu!
Bila kuwashirikisha waliobeba muungano kwa gharama kubwa. Samia anachofanya ni kuwapa tu wanachotaka bila kuwawajibisha. Sasa hivi mizigo inaingia bure Zanzibar inaletwa bara, halafu Mtanganyika anatozwa kodi kwasababu hakuna mapato. Zanzibar ni uchochoro wa kupitishia bidhaa tu kuja bara. Hiyo ni kazi yake na amefanikiwa

SSH amemaliza kero ya Muungano kwa kuua. Ahsante
 
Mafuta sio madini ?....maana huitwa dhahabu nyeusi....yakipatikana huko Zenji huenda yakajumuishwa kwenye hayo makubaliano ?

Nguruvi3 Kalamu Pascal Mayalla zitto junior

..Znz walifanya jitihada kubwa mpaka wakaondoa mafuta kwenye masuala ya muungano.

..Sasa sidhani kama kuna uwezekano wa wao kurudisha mafuta yao kwenye mikono ya muungano.
 
Halafu kwenye vikao vya maamūzi yeyote ya makubaliano!; Wajumbe wa Zanzibar lazima wawe.2 Sababu mzanzibar lazima aiwakilishe Zanzibar ktkTanzania na Tanzania zanzibar ni Mbia! Mjumbe wa Tanzania ni m.1!
 
..Zanzibar hawana hata sehemu ya kuchimba mchanga, halafu Tanganyika inasaini nao mkataba wa mashirikiano ktk sekta ya madini?
Na ndiyo lengo. Baada ya kusikia watu wakihoji juu ya mchanga unaosombwa kila siku. Kwa kifupi cha Tanganyika ni cha wote, lakini cha zanzibar ni cha zanzibar tu.

Mkataba huo unaipa Tanganyika wajibu, na haki ni kwa mtoto mpendwa.
 
Kusema kweli watanganyika wote ni majuha tuu kwa hichi kinachoendelea. Watanganyika wote ni mafala nyie mkiongozwa na mimi.
 
Yaani Muungano Una Kero, Sasa Hamjamaliza Kutatua Mnasaini Mipya Ili Kukwamisha Kuuvunja Endapo Muda Utafika, Mwaka Wa Kiislam Imekuwa Rasmi Mapumziko
 
..Znz walifanya jitihada kubwa mpaka wakaondoa mafuta kwenye masuala ya muungano.

..Sasa sidhani kama kuna uwezekano wa wao kurudisha mafuta yao kwenye mikono ya muungano.
Hapa ndipo utauona unafiki wa Kizanzibar. Kwa hili kwavile wanajua huo ni mchongo wa kuchukua mapato ya madini ya Tanganyika hutawasikia. Hawawezi kusema kwasababu ya 'umimi', kwamba chetu ni chao pia chao ni chao
 
Na ndiyo lengo. Baada ya kusikia watu wakihoji juu ya mchanga unaosombwa kila siku. Kwa kifupi cha Tanganyika ni cha wote, lakini cha zanzibar ni cha zanzibar tu.

Mkataba huo unaipa Tanganyika wajibu, na haki ni kwa mtoto mpendwa.
Hii ni njia ya kupata uhalali wa kutumia rasilimali za Tanganyika kule Zanzibar. Kwamba sasa Rais SSH anaweza kuagiza zichotwe tu na kupelekwa Zanzibar kwasababu tuna makubaliano

Hivi kama sisi ni nchi moja tunawezaje kuwa na mkataba?

Pascal Mayalla nadhani unaelewa maana ya kile unachotetea kwamba 'Hatuna elimu ya Uraia'' sasa hili vipi
 
Back
Top Bottom