Umelogwa wewe
 
Tanganyika ni wilaya ndani ya nchi ya Tanzania, haiwezi kuingia makubaliano binafsi na nchi nyingine.
Nikawazaaaa nikashindwa kujiuliza, ni lini Tanganyika nao watasaini mkataba au Makubaliano...
 
Kwahiyo walioko CCM wanamwelewa Nyerere na hata wapinzani waliohamia ghafla CCM hapo awali hawakumwelewa Nyerere ila baada ya kuhamia CCM ghafla wakamwelewa.

Mathalani EL alipohamia CCM uelewa wake kwa Nyerere ulifutika na aliporudi uelewa wake ukawa restored? Eti au MAALIM alipohamia CCM uelewa wake kwa JKN ulifutika mazima!

Haya kama hawamwelewi tueleze wataka wamwelewe Kwa misingi ipi? Yani jambo Gani wapaswa wapinzani kumuelewa Nyerere ambalo hawamwelewi, mpaka utoe kauli hiyo uliyoitoa?

Je kama Leo serikali Ya Tanzania imesaini mkataba na serikali ya Zanzibar ni lini serikali Ya Tanzania itasaini mkataba na Serikali (unknown) ya Tanganyika ambayo ni sehemu ya Muungano?
Ogopa nchi ikiwa na wajinga wengi wanaweza kuchagua Rais wa nchi, rejea alichosema Profesa wa majalalani kwamba Kuna kitu kimeonesha UJInga wa viongozi walio wengi
 
Tanganyika ni wilaya ndani ya nchi ya Tanzania, haiwezi kuingia makubaliano binafsi na nchi nyingine.
Ficha UJInga basi wangesema angalau wizara mbili zimesaini makubaliano au basi Rais ameamua katika kutatua mambo au kero za Muungano, Secta ya madini imeingizwa kwenye mambo ya Muungano na itakua na waziri anayeshughulikia mambo yote ya madini Kwa pande zote mbili. Kama ilivyo wizara ya Mammbo ya ndani au wizara ya ulinzi na Jeshi la kujenga taifa
 
Kwa sasa siamini chochote kinachosainiwa na Selikari hii labda waweke wazi hayo makubaliano na miongozo nisome mwenyewe
 
Samahani, this is not for you! Umewapunguza wangapi?? Pumbavu kweli wewe
Huu ni ushauri kwenu CHADEMA naamini wewe ni mwanaCHADEMA, msidharau wazee. Jaribuni kuwaweka wazee karibu ili mpate kuijua historia ya nchi yetu vizuri.

Hili la kutumia hekima na busara za wazee linaifaidisha sana CCM, wanapata kuyajua mengi. Hususani hili suala la Muungano.

CHADEMA kuwa ni chama Cha vijana ni hasara kwao, viongozi wote wa CHADEMA wamezaliwa baada ya uhuru na Muungano isipokuwa Mbowe kama sikosei. Hii sio nzuri ndio maana wanaonekana kupuyangapuyanga kwenye historia ya nchi yetu.

Mkitumia wazee mtaondokana na dhana ya wengi kwamba CHADEMA ni chama Cha kiharakati. Harakati zinazotakiwa Sasa ni ujenzi wa Taifa, Sasa harakati zenu za kisiasa zinawaeudisha nyuma mara oooh! Tunarudisha Tanganyika ,mara oooh ukombozi wa pili wa mtanzania kutoka Kwa mkoloni mweusi, hayo yote mnapoteza Muda.

Tanganyika is no more.
 
Walifanya hivyo walipodhani kuwa wana mafuta. Lakini mpaka sasa hayajapatikana ya kuweza kuvunwa. Sitashangaa wakidai kuwa mafuta/gesi asilia zirudishwe kwenye Muungano ili wafaidike na yaliyopatikana Tanganyika.

Amandla...

..hata yasiporudishwa wana mrija wa kufyonza kwasababu mafuta yaliyoko Tanganyika ni ya serikali ya muungano.
 
Hapo ndio ccm walipotufukisha. Chochote watakacho wazanzibari huku Tanganyika wanavaa koti la muungano. Hata uongozi wanapata huku Tanganyika lakini sio kinyume chake. Wana bunge lao ambalo mtanganganyika hatii pua, ila wao kwenye bunge letu wapo! Hiyo ndio maana unasikia muungano wetu ni wa kipekee duniani.

Magufuli alitusaidia kudhibitisha kuwa katiba yetu imepitwa na wakati, na ni wakati wa katiba mpya. Na sasa Samia kutudhibitishia kuwa muungano wa serikali 2 ni wa kufanyiwa marekebisho makubwa, aidha serikali 3, ama moja.
 
Madini sio mambo ya muungano, mleta mada aliulizia kuhusu 'Tanganyika' ambayo ni wilaya tu ndani ya mkoa wa Katavi lini itaingia makubaliano na Zanzibar kitu ambacho hakiwezekani.

Muungano wenu upo 'ki-chama' zaidi (Ccm) , ndio maana lazima waendelee kunga'nga'nia madaraka maana ni wao tu watakaoweza kuendelea na huu muundo wake.
 
Kweli wazanzibar wako kuvuna vya Tanganganyika ndio maana wametulia kimyaa hata kero za muungano hawazioni tena.
 
Relax relax relax!
 

Tanganyika ni nchi ya maiti hai, siku tukizinduka chini ya huu ukondoo tuliovikwa na CCM ndio tutapata mwelekeo.
 
Nyerere hakuwa akili kubwa
Ndio maana alikosa kupinduliwa mara kadhaa.

Nyerere alikuwa ni muota ndoto wa mchana na Kuna mtaalamu aliwahi kumuelezea hivyo.

Kifupi katupa dhahama ambayo tusipoikabili Sasa basi baadae itatupasa
 
Wewe ni kiazi mviringo!
 
Nikawazaaaa nikashindwa kujiuliza, ni lini Tanganyika nao watasaini mkataba au Makubaliano yoyote tu na serikali ya Tanzania??[emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa ccm ni dhambi kuitaja Tanganyika. Ukiitaja tu Tanganyika wanasema unataka kuvunja muungano.
Ndio maana ninasema SSH amesaidia sana. Hivi kwa haya yanayotkea bado kuna CCM asiyeelewa kwamba Tanganyika inahitajika, tena jana si kesho. Hawa CCM Tanganyika hawana akili kiwango hiki

Kuna Mbunge mmoja tu amebaki kuwa na heshima zake, Ali Kessy. Huyu alisimama na Tanganyika akiwaeleza wazi wazi pale Bungeni. Wazanzibar walimchukia lakini alikuwa mkweli kwao. Leo maneno yake ynasimama na kumheshimisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…