TANZIA: Producer Joshua Magawa "Pancho Latino" wa B hitz records afariki dunia

TANZIA: Producer Joshua Magawa "Pancho Latino" wa B hitz records afariki dunia

Nimekuwa nkitamani kufika kwenye hivi visiwa ambavyo vijana wengi wa Dar es Salaam wamekuwa wakienda wikiendi,hili linafanya nijifikirie mara mbili aise

Kuna watu wangu wa karibu walienda huko, wakati wa kurudi kukawa kama na upepo mkali pia walichelewa giza likawa limeingia!!

Walilia kwenye hivyo vidude sijui ngalawa au mashua, nimewapokea macho mekunduuu na mmoja alirudi na malaria tukamkimbiza hospitali akalazwa wiki nzima yuko hoi sasa sijui alingatwa na mbu saa ngapi huko.

Toka niliposikia hizo story mie wala habari nako sina!! Nitapambana na tochi za traffic to Bagamoyoooo naogelea maji ya ugoko au kama hamu ya kisiwani imenishika sana basi Kigamboni pananitosha 😀😀😀

RIP Pancho, alipangalo Mola wanadamu hatuwezi kulitengua. Tangulia, tunakufuata ni swala la muda tu.
 
Neno moja nikwamba.

Vijana, Kiburi cha uzima kisikufanye ukajisahau.


Niiv tunajisahau sana, ila mazeee Watu wanakata sanaaaaaa
 
Kinachowaua waogeleaji wazuri kwenye maji....ni njaa kama wamekwama mbali na makazi!!!...

Mawimbi makubwa yanayochosha mwili.....

Na kushikwa na misuli Yaani ndio baharia anakufa huku anajiona!!!....usiombe ushikwe na msuli ndani ya maji....unaweza kufa hata kwenye kina kifupi cha maji!!.,,,,

Na hili tatizo huwapata waogeleaji wanaokaa muda mrefu mbali na maji!!!...
mwaka 2014 mwezi 12 nilinusurika kufa maji msasani beach baada ya maji kurudi nilikuwa mbali kidogo na ukingo wa bahari.nilitumia maarifa na nguvu zangu zote kujiokoa nilikuwa nimevaa vest na boxer cha ajabu ile vest na boxer niliiziona nzito na sijui nilizivua vipi na kubaki uchi nilipiga miguu mpaka msuli wa mguu moja wa kushoto ukanishika niliishiwa nguvu nikiwa naelekea chini huku nimisha kubali kifo bahati nzuri ile nimegota chini nayasikia maji utosini nikaenda mbele kidogo ndipo yakanifikia machoni.
tokea mwaka 2014 sijawahi kurudi baharini tena wala kusogelea maji yoyote kwa ajili ya kuogelea-bahari sasa naiona kama kituo cha polisi.
 
Back
Top Bottom