Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 15,819
- 33,255
- Thread starter
-
- #121
Ukiona mtu anasema mitano tena ujue tayari Ccm waneshachukua akili yake. Huwezi kumpigia kura Magufuli aendelee kuwa Raisi wa Tanzania kama umepewa akili timamu na Mungu.π’π’π’ Nafikiria MITANO TENA halafu vile namna vyuma vitatunyonga tukufe dah!
Usifanye uamuzi kwa hasira,fanya ukiwa umetulia. Huyo unayempigia debe unadhani atatuajiri wote?! Uongo,hata Nchi zilizoendelea haziwezi kuajiri raia wake wote! Kodi wanalipa ili kupata mapato ya serikali, afya, elimu pia wanachangia. Uamuzi wa hasira siyo wa busara!TAREHE 28/10/2020: SIKU YA KUWEKA HISTORIA KUU TANZANIA.
Amani iwe nanyi watu wa Mungu!
Kwa kipindi cha miaka 59 tangu uhuru, Tanzania imekuwa ikiongozwa na Chama cha mapinduzi. Katika miaka hii yote watanzania wamepitia mengi sana ila kila siku maisha ya watanzania yamezidi kuwa ya kuogofya na ya kusikitisha. Umasikini umekuwa donda kuu la watanzania na mbaya zaidi katika kipindi hicho chote, watanzania wamekuwa wakishuhudia wanasiasa wakizidi kujineemisha kwa pesa zao za kodi na mbaya zaidi wamekuwa wakiwafanya watanzania kuwa ombaomba na watumwa kwenye nchi yao.
Tofauti na miaka ya maraisi waliopita ambao pamoja na kujineemisha binafsi ila angalau walijitahidi kuheshimu utu wa mtanzania kwa kumuheshimu na kutomnyanyasa Ila katika kipindi cha miaka 5 watanzania wameshuhudia unyanyasaji mkubwa wa haki zao kutoka kwa watu waliojionesha kwao kuwa watu wazuri kumbe walikuwa chui waliojivika ngozi ya Kondoo!!
Mungu si Athumani alimuokoa mtoto wake Tundu Antiphas Lissu kwenye jaribio la mauaji hapo tarehe 7 mwezi wa 9 mwaka 2017 akiwa amepanga historia kuu iandikwe hapa Tanzania hapo tarehe 28/10/2020. Kwa hiyo ewe mtanzania usikose kuwa sehemu ya historia hii kuu inayoenda kuandikwa hapo tarehe 28/10/2020.
Kwa nini Tarehe 28/10/2020 ni siku ya watanzania kuandika Historia kuu juu ya nchi yao?
1. Kama wewe ni mzazi uliyemsomesha mtoto wako kwa shida hadi akamaliza chuo na hadi leo hajapata ajira, basi tarehe 28/10/2020 nenda kapige kura kuonesha kuwa CCM haistahili kabisa kuendelea kutawala nchi hii kwa sababu mfumo wao na sera zao umefanya mwanao akose ajira. Tarehe hiyo mchague Tundu Antiphas Lissu kuweka historia mpya Tanzania.
2. Kama wewe ni mtanzania uliyefanya kazi katika maisha yako ili uje kuishi vizuri, ila CCM wamefilisi mifuko ya pensheni na kufanya upate pensheni kidogo na kuishi kwa tabu, basi Tarehe 28/10/2020 nenda kaandike historia mpya kwa kuiadhibu CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu
3. Kama wewe ni kijana uliyesoma kwa shida huku ukiingia mkataba na serikali wa kukukata asilimia 6 mpaka 7 ya mshahara ukipata ajira, ila CCM ya awamu ya tano imekufanya ukatwe asilimia 15 basi nenda kaandike historia tarehe 28/10/2020 kwa kuikataa na kuiadhibu CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu.
4. Kama Wewe ni Mtanzania ambaye gharama za matibabu zimekuwa kubwa na umekuwa ukipata shida ya gharama za matibabu kwa miaka yote basi tarehe 28/10/2020 nenda kaiadhibu CCM kwa kuinyima kura na uandike historia kwa kumchagua Tundu Antiphas Lissu!
5. Kama Wewe ni mfanyakazi ambaye kwa miaka 5 hukupata haki yako ya kuongezwa mshahara na mwaka huu umeona bima ya afya ikiondoa baadhi ya dawa kwenye mfumo wa bima huku gharama ya maisha ikizidi kupanda basi kaandike historia kuu tarehe 28/10/2020 kwa kuinyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu
6. Kama wewe ni mzazi uliyepata shida kumsomesha mtoto wako private na amefika chuo amenyimwa mkopo kwa kusomeshwa private elimu ya chini basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia Kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu
7. Kama wewe ulikuwa mfanyakazi uliyeajiliwa sehemu ila Sera za Awamu ya tano ya CCM zikafanya upoteze ajira yako kwa kampuni kufirisika basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu
8. Kama wewe ni mfanyabiashara uliyeangaika kupata mtaji ikiwemo kukopa, ila kodi za tra na mnyanyaso ya tra yamekufanya ufunge biashara au ufirisike basi tarehe 28/10/2020 Kawe sehemu ya historia kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu
9. Kama Wewe ni mkulima uliyekuwa ukiuza mazao yako vizuri bila shida ila sera za Chama cha mapinduzi zikakupiga marufuku kuuza mazao nje na kupelekea ukafirisika na kupata hasara basi Kawe sehemu ya historia kuu hapo tarehe 28/10/2020 kwa kuwanyima kura CCM na kumpa kura Tundu Antiphas Lissu.
10. Kama wewe ni kijana ambayo umekuwa ukihangaika bila ajira kwa sababu ya sera mbovu za kiuchumi za Chama cha mapinduzi basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia kuu katika nchi yetu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu.
Ewe mtanzania, kumbuka sehemu pekee ya wewe kueleza hisia zako juu ya mwanasiasa yeyote au Sera zozote zinazokuathili kimaisha na kiuchumi ni kwenye Sanduku la Kura. Hivyo Tarehe 28/10/2020 nenda Kawe sehemu ya Historia kuu inayoenda kuandikwa ya kuweka utawala mpya hapa Tanzania kwa maslahi mapana ya nchi yetu na watu wake
Ukipiga kura, usiache kulinda kura maana kura yako ina thamani sana
Share na mwenzako!
Hapana hawezi kutuajili wote Ila ataweka mazingira mazuri ya sekta binafsi kuja kwa wingi nchini Tanzania na kuajili watu wengi kuliko huyu magufuli wako ambaye ameharibu ukuaji wa sekta binafsi na kufanya wawekezaji kukimbia na maelfu ya watu kupoteza na kukosa ajiraUsifanye uamuzi kwa hasira,fanya ukiwa umetulia. Huyo unayempigia debe unadhani atatuajiri wote?! Uongo,hata Nchi zilizoendelea haziwezi kuajiri raia wake wote! Kodi wanalipa ili kupata mapato ya serikali, afya, elimu pia wanachangia. Uamuzi wa hasira siyo wa busara!
Katika kipindi cha mitano ya awali ya JP amejenga misingi ya ukuaji wa uchumi, mitano ya sasa itatumia misingi hiyo kuleta ukuaji wa uchumi na ustawi wa jamii.Hapana hawezi kutuajili wote Ila ataweka mazingira mazuri ya sekta binafsi kuja kwa wingi nchini Tanzania na kuajili watu wengi kuliko huyu magufuli wako ambaye ameharibu ukuaji wa sekta binafsi na kufanya wawekezaji kukimbia na maelfu ya watu kupoteza na kukosa ajira
Usihofu,umemaliza mlima sasa ni kuteremka, tano kwa JPM.π’π’π’ Nafikiria MITANO TENA halafu vile namna vyuma vitatunyonga tukufe dah!
TAREHE 28/10/2020: SIKU YA KUWEKA HISTORIA KUU TANZANIA.
Amani iwe nanyi watu wa Mungu!
Kwa kipindi cha miaka 59 tangu uhuru, Tanzania imekuwa ikiongozwa na Chama cha mapinduzi. Katika miaka hii yote watanzania wamepitia mengi sana ila kila siku maisha ya watanzania yamezidi kuwa ya kuogofya na ya kusikitisha. Umasikini umekuwa donda kuu la watanzania na mbaya zaidi katika kipindi hicho chote, watanzania wamekuwa wakishuhudia wanasiasa wakizidi kujineemisha kwa pesa zao za kodi na mbaya zaidi wamekuwa wakiwafanya watanzania kuwa ombaomba na watumwa kwenye nchi yao.
Tofauti na miaka ya maraisi waliopita ambao pamoja na kujineemisha binafsi ila angalau walijitahidi kuheshimu utu wa mtanzania kwa kumuheshimu na kutomnyanyasa Ila katika kipindi cha miaka 5 watanzania wameshuhudia unyanyasaji mkubwa wa haki zao kutoka kwa watu waliojionesha kwao kuwa watu wazuri kumbe walikuwa chui waliojivika ngozi ya Kondoo!!
Mungu si Athumani alimuokoa mtoto wake Tundu Antiphas Lissu kwenye jaribio la mauaji hapo tarehe 7 mwezi wa 9 mwaka 2017 akiwa amepanga historia kuu iandikwe hapa Tanzania hapo tarehe 28/10/2020. Kwa hiyo ewe mtanzania usikose kuwa sehemu ya historia hii kuu inayoenda kuandikwa hapo tarehe 28/10/2020.
Kwa nini Tarehe 28/10/2020 ni siku ya watanzania kuandika Historia kuu juu ya nchi yao?
1. Kama wewe ni mzazi uliyemsomesha mtoto wako kwa shida hadi akamaliza chuo na hadi leo hajapata ajira, basi tarehe 28/10/2020 nenda kapige kura kuonesha kuwa CCM haistahili kabisa kuendelea kutawala nchi hii kwa sababu mfumo wao na sera zao umefanya mwanao akose ajira. Tarehe hiyo mchague Tundu Antiphas Lissu kuweka historia mpya Tanzania.
2. Kama wewe ni mtanzania uliyefanya kazi katika maisha yako ili uje kuishi vizuri, ila CCM wamefilisi mifuko ya pensheni na kufanya upate pensheni kidogo na kuishi kwa tabu, basi Tarehe 28/10/2020 nenda kaandike historia mpya kwa kuiadhibu CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu
3. Kama wewe ni kijana uliyesoma kwa shida huku ukiingia mkataba na serikali wa kukukata asilimia 6 mpaka 7 ya mshahara ukipata ajira, ila CCM ya awamu ya tano imekufanya ukatwe asilimia 15 basi nenda kaandike historia tarehe 28/10/2020 kwa kuikataa na kuiadhibu CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu.
4. Kama Wewe ni Mtanzania ambaye gharama za matibabu zimekuwa kubwa na umekuwa ukipata shida ya gharama za matibabu kwa miaka yote basi tarehe 28/10/2020 nenda kaiadhibu CCM kwa kuinyima kura na uandike historia kwa kumchagua Tundu Antiphas Lissu!
5. Kama Wewe ni mfanyakazi ambaye kwa miaka 5 hukupata haki yako ya kuongezwa mshahara na mwaka huu umeona bima ya afya ikiondoa baadhi ya dawa kwenye mfumo wa bima huku gharama ya maisha ikizidi kupanda basi kaandike historia kuu tarehe 28/10/2020 kwa kuinyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu
6. Kama wewe ni mzazi uliyepata shida kumsomesha mtoto wako private na amefika chuo amenyimwa mkopo kwa kusomeshwa private elimu ya chini basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia Kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu
7. Kama wewe ulikuwa mfanyakazi uliyeajiliwa sehemu ila Sera za Awamu ya tano ya CCM zikafanya upoteze ajira yako kwa kampuni kufirisika basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu
8. Kama wewe ni mfanyabiashara uliyeangaika kupata mtaji ikiwemo kukopa, ila kodi za tra na mnyanyaso ya tra yamekufanya ufunge biashara au ufirisike basi tarehe 28/10/2020 Kawe sehemu ya historia kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu
9. Kama Wewe ni mkulima uliyekuwa ukiuza mazao yako vizuri bila shida ila sera za Chama cha mapinduzi zikakupiga marufuku kuuza mazao nje na kupelekea ukafirisika na kupata hasara basi Kawe sehemu ya historia kuu hapo tarehe 28/10/2020 kwa kuwanyima kura CCM na kumpa kura Tundu Antiphas Lissu.
10. Kama wewe ni kijana ambayo umekuwa ukihangaika bila ajira kwa sababu ya sera mbovu za kiuchumi za Chama cha mapinduzi basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia kuu katika nchi yetu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu.
Ewe mtanzania, kumbuka sehemu pekee ya wewe kueleza hisia zako juu ya mwanasiasa yeyote au Sera zozote zinazokuathili kimaisha na kiuchumi ni kwenye Sanduku la Kura. Hivyo Tarehe 28/10/2020 nenda Kawe sehemu ya Historia kuu inayoenda kuandikwa ya kuweka utawala mpya hapa Tanzania kwa maslahi mapana ya nchi yetu na watu wake
Ukipiga kura, usiache kulinda kura maana kura yako ina thamani sana
Share na mwenzako!
Wapiga kura huwa hawaamui wa kuwa madarakani, bali wahesabu kura.
Mpaka kwa akili yako ya ukilaza umeona nimeandika kitu basi ujue huyo Magufuli wako hapaswi kuendelea kuwa Raisi hata kwa dakika 10 zaidi. Nakushauri na wewe fanya maamuzi magumu manaake najua hapo ulipo huna ajira ya kudumu wala huna uhakika wa pensheni endapo ikitokea umeezeka.umejitahidi kuandika sana lakini ushindi haukwepeki kwa JPM: wewe ruka lala amka lia cheka
Msingi upi aliojenga wa ukuaji uchumi??? Kuzuia wahaya wasiuze kahawa nje ya nchi na kuwa masikini??? Kupora korosho kusini na kusababisha umasikini mkubwa??? Au kuteka watu, kuua na kubambikia watu makesi???Katika kipindi cha mitano ya awali ya JP amejenga misingi ya ukuaji wa uchumi, mitano ya sasa itatumia misingi hiyo kuleta ukuaji wa uchumi na ustawi wa jamii.
Safi sana. Hamasisha pia ndugu zako, jamaa na marafiki wakampigie kura Lissu hapo kesho. Waambie pia wasikae mbali na vituo vya kura kusubiri matokeoKesho nitaenda kibaha nikitokea chanika kumpigia tundu lisu
Amina. Lazima tarehe 28/10/2020 tutaiweka kama siku kuu ili kuashiria ukombozi wa Taifa letu na mwanzo mpya wa maendeleo ya nchi yetu.Sote kwa pamoja tukamchague Lissu kwa kishindo, Tuifagie kabisa CCM na kero zake za kufukarika wananchi! Tarehe 28.10.2020 itakuwa ikiadhimishwa kama tarehe ya ukombozi wetu kila mwaka!
Kuteremka kivipi wakati hata kwenye kampeni hakuna sera mahususi za ajira, pensheni, kuboresha maisha ya wananchi??? Yeye anaongelea ndege tuUsihofu,umemaliza mlima sasa ni kuteremka, tano kwa JPM.
Inawezekana jich lako limeona hayo ambayo mimi siwezi kuyathibitisha! Lakini ninaona miradi ya kimkakati kama usafirishaji (ndege, barabara, viwanja, reli), umeme wa uhakika, formalization ya biashara, vituo vya kutolea huduma za jamii kama afya, elimu, kuingia uchumi wa kati, hisa kwenye madini, masoko ya ndani ya madini, kuboresha ushirika, uwezo wa Serikali kujitegemea kimapato, raslimali watu nk.Msingi upi aliojenga wa ukuaji uchumi??? Kuzuia wahaya wasiuze kahawa nje ya nchi na kuwa masikini??? Kupora korosho kusini na kusababisha umasikini mkubwa??? Au kuteka watu, kuua na kubambikia watu makesi???
Mradi wa ndege una business plan ipi ya kutengeneza faida??? Ndege zetu zinasafiri wapi na wapi???Inawezekana jich lako limeona hayo ambayo mimi siwezi kuyathibitisha! Lakini ninaona miradi ya kimkakati kama usafirishaji (ndege, barabara, viwanja, reli), umeme wa uhakika, formalization ya biashara, vituo vya kutolea huduma za jamii kama afya, elimu, kuingia uchumi wa kati, hisa kwenye madini, masoko ya ndani ya madini, kuboresha ushirika, uwezo wa Serikali kujitegemea kimapato, raslimali watu nk.
Amina, na Mungu atutangulie katika kufanikisha hili. Abariki na afanikishe hili kwa Jina la YesuNi siku ya mapinduzi ya kweli ya kumwondoa Mkoloni mweusi kuitawala nchi yetu ki mabavu.