Uchaguzi 2020 Tarehe 28/10/2020: Siku ya kuweka Historia kuu Tanzania

Uchaguzi 2020 Tarehe 28/10/2020: Siku ya kuweka Historia kuu Tanzania

TAREHE 28/10/2020: SIKU YA KUWEKA HISTORIA KUU TANZANIA.

Amani iwe nanyi watu wa Mungu!

Kwa kipindi cha miaka 59 tangu uhuru, Tanzania imekuwa ikiongozwa na Chama cha mapinduzi. Katika miaka hii yote watanzania wamepitia mengi sana ila kila siku maisha ya watanzania yamezidi kuwa ya kuogofya na ya kusikitisha. Umasikini umekuwa donda kuu la watanzania na mbaya zaidi katika kipindi hicho chote, watanzania wamekuwa wakishuhudia wanasiasa wakizidi kujineemisha kwa pesa zao za kodi na mbaya zaidi wamekuwa wakiwafanya watanzania kuwa ombaomba na watumwa kwenye nchi yao.

Tofauti na miaka ya maraisi waliopita ambao pamoja na kujineemisha binafsi ila angalau walijitahidi kuheshimu utu wa mtanzania kwa kumuheshimu na kutomnyanyasa Ila katika kipindi cha miaka 5 watanzania wameshuhudia unyanyasaji mkubwa wa haki zao kutoka kwa watu waliojionesha kwao kuwa watu wazuri kumbe walikuwa chui waliojivika ngozi ya Kondoo!!

Mungu si Athumani alimuokoa mtoto wake Tundu Antiphas Lissu kwenye jaribio la mauaji hapo tarehe 7 mwezi wa 9 mwaka 2017 akiwa amepanga historia kuu iandikwe hapa Tanzania hapo tarehe 28/10/2020. Kwa hiyo ewe mtanzania usikose kuwa sehemu ya historia hii kuu inayoenda kuandikwa hapo tarehe 28/10/2020.

Kwa nini Tarehe 28/10/2020 ni siku ya watanzania kuandika Historia kuu juu ya nchi yao?

1. Kama wewe ni mzazi uliyemsomesha mtoto wako kwa shida hadi akamaliza chuo na hadi leo hajapata ajira, basi tarehe 28/10/2020 nenda kapige kura kuonesha kuwa CCM haistahili kabisa kuendelea kutawala nchi hii kwa sababu mfumo wao na sera zao umefanya mwanao akose ajira. Tarehe hiyo mchague Tundu Antiphas Lissu kuweka historia mpya Tanzania.

2. Kama wewe ni mtanzania uliyefanya kazi katika maisha yako ili uje kuishi vizuri, ila CCM wamefilisi mifuko ya pensheni na kufanya upate pensheni kidogo na kuishi kwa tabu, basi Tarehe 28/10/2020 nenda kaandike historia mpya kwa kuiadhibu CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

3. Kama wewe ni kijana uliyesoma kwa shida huku ukiingia mkataba na serikali wa kukukata asilimia 6 mpaka 7 ya mshahara ukipata ajira, ila CCM ya awamu ya tano imekufanya ukatwe asilimia 15 basi nenda kaandike historia tarehe 28/10/2020 kwa kuikataa na kuiadhibu CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu.

4. Kama Wewe ni Mtanzania ambaye gharama za matibabu zimekuwa kubwa na umekuwa ukipata shida ya gharama za matibabu kwa miaka yote basi tarehe 28/10/2020 nenda kaiadhibu CCM kwa kuinyima kura na uandike historia kwa kumchagua Tundu Antiphas Lissu!

5. Kama Wewe ni mfanyakazi ambaye kwa miaka 5 hukupata haki yako ya kuongezwa mshahara na mwaka huu umeona bima ya afya ikiondoa baadhi ya dawa kwenye mfumo wa bima huku gharama ya maisha ikizidi kupanda basi kaandike historia kuu tarehe 28/10/2020 kwa kuinyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

6. Kama wewe ni mzazi uliyepata shida kumsomesha mtoto wako private na amefika chuo amenyimwa mkopo kwa kusomeshwa private elimu ya chini basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia Kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

7. Kama wewe ulikuwa mfanyakazi uliyeajiliwa sehemu ila Sera za Awamu ya tano ya CCM zikafanya upoteze ajira yako kwa kampuni kufirisika basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

8. Kama wewe ni mfanyabiashara uliyeangaika kupata mtaji ikiwemo kukopa, ila kodi za tra na mnyanyaso ya tra yamekufanya ufunge biashara au ufirisike basi tarehe 28/10/2020 Kawe sehemu ya historia kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

9. Kama Wewe ni mkulima uliyekuwa ukiuza mazao yako vizuri bila shida ila sera za Chama cha mapinduzi zikakupiga marufuku kuuza mazao nje na kupelekea ukafirisika na kupata hasara basi Kawe sehemu ya historia kuu hapo tarehe 28/10/2020 kwa kuwanyima kura CCM na kumpa kura Tundu Antiphas Lissu.

10. Kama wewe ni kijana ambayo umekuwa ukihangaika bila ajira kwa sababu ya sera mbovu za kiuchumi za Chama cha mapinduzi basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia kuu katika nchi yetu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu.

Ewe mtanzania, kumbuka sehemu pekee ya wewe kueleza hisia zako juu ya mwanasiasa yeyote au Sera zozote zinazokuathili kimaisha na kiuchumi ni kwenye Sanduku la Kura. Hivyo Tarehe 28/10/2020 nenda Kawe sehemu ya Historia kuu inayoenda kuandikwa ya kuweka utawala mpya hapa Tanzania kwa maslahi mapana ya nchi yetu na watu wake

Ukipiga kura, usiache kulinda kura maana kura yako ina thamani sana

Share na mwenzako!
Umenena vyema Lord Denning!
 
Mradi wa ndege una business plan ipi ya kutengeneza faida??? Ndege zetu zinasafiri wapi na wapi???

Barabara kajenga barabara ngapi magufuli??? Au fly-over ya mfugale ambayo mvua ya masaa 5 tu inasababisha ifurike maji???

Masoko ya madini yamefanya nini cha ziada??? Au unasikiliza takwimu zao za kupika izo na unaziamini???

Ushirika gani umeboreshwa??? Huo ambao haujalipa pamba kanda ya ziwa??? Huo ulioshindwa kwenye korosho na mbaazi??? Au huo uliofeli kwenye tumbaku na kahawa na wakulima wamekuwa wasikini wa kutupwa???

Unasema serikali inajitegemea kimapato, kivipi???? Wakati kila siku tunaona katibu mkuu wizara ya fedha akipokea fedha za misaada kutoka kwa wazungu???
Kujitegemea ni mchakato na hatujajitegemea kwa asilimia 100, ila tumeanza hatua kwa hatua kukusa mapato ya ndani, kuziba mianya ya uvujaji wa mapato, kuimarisha makusanyo, utegemezi wa wahisani kwenye bajeti umepungua,uchaguzi huu tumeugharimia kwa asilimia 100, ujenzi wa meli kadhaa na vivuko, madaraja, barabara , huduma za jamii.
 
Mpaka kwa akili yako ya ukilaza umeona nimeandika kitu basi ujue huyo Magufuli wako hapaswi kuendelea kuwa Raisi hata kwa dakika 10 zaidi. Nakushauri na wewe fanya maamuzi magumu manaake najua hapo ulipo huna ajira ya kudumu wala huna uhakika wa pensheni endapo ikitokea umeezeka.

Nenda kapige kura kesho, kura ya ukombozi na mchague Tundu Antiphas Lissu kuwa Raisi wa Jamhuri ya Tanzania 2020-2025 ili aweke mfumo bora wa kukuhakikishia maisha bora wewe na uzao wako!!

ukipiga kura yako usiondoke bila kuilinda

hahhaa aiseee mm kura lazima nipige, lazima nihakikishe kwenye ushindi wa jpm na mm nakua mmoja wapo
 
Iye pole sana, ninaona una hasira, Nchi hii ni yetu hatutaijenga kwa hasira bali kwa Busara kubwa na utulivu,wala tusifanye majaribio. Ninakushauri chagua maendeleo usichague maneno! Umeuliza maswali mengi sana nitayajibu hata kwa hatua. Naanza na Idadi ya Flyovers msikilize Mwenezi kwenye vidio iliyoambatishwa.
Busara gani unayotumia kujenga nchi??? Kujenga uwanja wa kimataifa Chatto wakati kuna maelfu ya shule wanafunzi wanakaa chini na hawana hata vitabu??? Wakati kuna maeneo wanakunnywa maji ya tope???

Maendeleo gani unayosema tuchague??? Mipango miji tu mmeashindwa kufanya nchi imejaa squatters!

Hivi unaona ni busara kujenga flyover inayojaa maji kwa mfugale alafu jangwani mmejenga kituo na barabara kwenye Mkondo wa maji??
 
Kujitegemea ni mchakato na hatujajitegemea kwa asilimia 100, ila tumeanza hatua kwa hatua kukusa mapato ya ndani, kuziba mianya ya uvujaji wa mapato, kuimarisha makusanyo, utegemezi wa wahisani kwenye bajeti umepungua,uchaguzi huu tumeugharimia kwa asilimia 100, ujenzi wa meli kadhaa na vivuko, madaraja, barabara , huduma za jamii.
Hivi unajua unaongea na watu wenye upeo wa namna gani??? Hizo data zenu za kupika ishieni kuzitumia kudanganyana kwenye korido zenu za Lumumba huko!! Ni mapato gani ya ndani yamekua??? Kama korosho huuzi nje, Mbaazi huuzi nje, biashara zinafungwa na makampuni ya wawekezaji yanakimbia na watu wanapoteza kazi. Sasa unaweza kusemaje??

Kwani kugharamia uchaguzi kuna gharama gani??? Bil 300 nayo ni hela???
 
hahhaa aiseee mm kura lazima nipige, lazima nihakikishe kwenye ushindi wa jpm na mm nakua mmoja wapo
Kama unajali kweli hii nchi na vizazi vijavyo huwezi kuwa na msimamo wa kumpigia kura magufuli
 
Tano tena kwa JPM, kazi iendelee!
Ukisema tano tena jua ni tano tena za mateso, kukosa ajira kwa vijana, kuuliwa kwa sekta binafsi, kuondolewa kwa dawa nyingi kwenye Bima ya afya na kukosa kwa pensheni kwa wastaafu wetu
 
Kama unajali kweli hii nchi na vizazi vijavyo huwezi kuwa na msimamo wa kumpigia kura magufuli

yaaani mm nkampigie mtu mwenye mdomo mchafu na kuvunja sheria? kwanza kaniblock twitter baada ya kutoa maoni yngu kuhusu magufuli, hapo hajashika nchi tu kashaanza kublock watu, kule youtube ndo kabisaaa chadema channel wamfunga comments
 
TAREHE 28/10/2020: SIKU YA KUWEKA HISTORIA KUU TANZANIA.

Amani iwe nanyi watu wa Mungu!

Kwa kipindi cha miaka 59 tangu uhuru, Tanzania imekuwa ikiongozwa na Chama cha mapinduzi. Katika miaka hii yote watanzania wamepitia mengi sana ila kila siku maisha ya watanzania yamezidi kuwa ya kuogofya na ya kusikitisha. Umasikini umekuwa donda kuu la watanzania na mbaya zaidi katika kipindi hicho chote, watanzania wamekuwa wakishuhudia wanasiasa wakizidi kujineemisha kwa pesa zao za kodi na mbaya zaidi wamekuwa wakiwafanya watanzania kuwa ombaomba na watumwa kwenye nchi yao.

Tofauti na miaka ya maraisi waliopita ambao pamoja na kujineemisha binafsi ila angalau walijitahidi kuheshimu utu wa mtanzania kwa kumuheshimu na kutomnyanyasa Ila katika kipindi cha miaka 5 watanzania wameshuhudia unyanyasaji mkubwa wa haki zao kutoka kwa watu waliojionesha kwao kuwa watu wazuri kumbe walikuwa chui waliojivika ngozi ya Kondoo!!

Mungu si Athumani alimuokoa mtoto wake Tundu Antiphas Lissu kwenye jaribio la mauaji hapo tarehe 7 mwezi wa 9 mwaka 2017 akiwa amepanga historia kuu iandikwe hapa Tanzania hapo tarehe 28/10/2020. Kwa hiyo ewe mtanzania usikose kuwa sehemu ya historia hii kuu inayoenda kuandikwa hapo tarehe 28/10/2020.

Kwa nini Tarehe 28/10/2020 ni siku ya watanzania kuandika Historia kuu juu ya nchi yao?

1. Kama wewe ni mzazi uliyemsomesha mtoto wako kwa shida hadi akamaliza chuo na hadi leo hajapata ajira, basi tarehe 28/10/2020 nenda kapige kura kuonesha kuwa CCM haistahili kabisa kuendelea kutawala nchi hii kwa sababu mfumo wao na sera zao umefanya mwanao akose ajira. Tarehe hiyo mchague Tundu Antiphas Lissu kuweka historia mpya Tanzania.

2. Kama wewe ni mtanzania uliyefanya kazi katika maisha yako ili uje kuishi vizuri, ila CCM wamefilisi mifuko ya pensheni na kufanya upate pensheni kidogo na kuishi kwa tabu, basi Tarehe 28/10/2020 nenda kaandike historia mpya kwa kuiadhibu CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

3. Kama wewe ni kijana uliyesoma kwa shida huku ukiingia mkataba na serikali wa kukukata asilimia 6 mpaka 7 ya mshahara ukipata ajira, ila CCM ya awamu ya tano imekufanya ukatwe asilimia 15 basi nenda kaandike historia tarehe 28/10/2020 kwa kuikataa na kuiadhibu CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu.

4. Kama Wewe ni Mtanzania ambaye gharama za matibabu zimekuwa kubwa na umekuwa ukipata shida ya gharama za matibabu kwa miaka yote basi tarehe 28/10/2020 nenda kaiadhibu CCM kwa kuinyima kura na uandike historia kwa kumchagua Tundu Antiphas Lissu!

5. Kama Wewe ni mfanyakazi ambaye kwa miaka 5 hukupata haki yako ya kuongezwa mshahara na mwaka huu umeona bima ya afya ikiondoa baadhi ya dawa kwenye mfumo wa bima huku gharama ya maisha ikizidi kupanda basi kaandike historia kuu tarehe 28/10/2020 kwa kuinyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

6. Kama wewe ni mzazi uliyepata shida kumsomesha mtoto wako private na amefika chuo amenyimwa mkopo kwa kusomeshwa private elimu ya chini basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia Kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

7. Kama wewe ulikuwa mfanyakazi uliyeajiliwa sehemu ila Sera za Awamu ya tano ya CCM zikafanya upoteze ajira yako kwa kampuni kufirisika basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

8. Kama wewe ni mfanyabiashara uliyeangaika kupata mtaji ikiwemo kukopa, ila kodi za tra na mnyanyaso ya tra yamekufanya ufunge biashara au ufirisike basi tarehe 28/10/2020 Kawe sehemu ya historia kuu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu

9. Kama Wewe ni mkulima uliyekuwa ukiuza mazao yako vizuri bila shida ila sera za Chama cha mapinduzi zikakupiga marufuku kuuza mazao nje na kupelekea ukafirisika na kupata hasara basi Kawe sehemu ya historia kuu hapo tarehe 28/10/2020 kwa kuwanyima kura CCM na kumpa kura Tundu Antiphas Lissu.

10. Kama wewe ni kijana ambayo umekuwa ukihangaika bila ajira kwa sababu ya sera mbovu za kiuchumi za Chama cha mapinduzi basi tarehe 28/10/2020 kaandike historia kuu katika nchi yetu kwa kuwanyima kura CCM na kumchagua Tundu Antiphas Lissu.

Ewe mtanzania, kumbuka sehemu pekee ya wewe kueleza hisia zako juu ya mwanasiasa yeyote au Sera zozote zinazokuathili kimaisha na kiuchumi ni kwenye Sanduku la Kura. Hivyo Tarehe 28/10/2020 nenda Kawe sehemu ya Historia kuu inayoenda kuandikwa ya kuweka utawala mpya hapa Tanzania kwa maslahi mapana ya nchi yetu na watu wake

Ukipiga kura, usiache kulinda kura maana kura yako ina thamani sana

Share na mwenzako!
Usipumbazwe na propaganda mfu za Mawakala wa Mabeberu, ambao wameshaahidiwa pepo na mabwana zao. Nyerere alitutoa katika ukoloni wa kisiasa. Ni jukumu la kizazi hiki kupigania uhuru wa kiuchumi na wa kujitegemea bila kuathiriwa na ukoloni mambo leo unaotaka kupoka na kujimilikisha njia zetu za uchumi, kwa kupitia mawakala wao!

Miaka mitano mingine kwa Jemedari si jambo la hiari. Ni jambo la lazima ili kulinda utaifa, utamaduni, amani na utulivu kwa maslahi yetu na ya ya Taifa kwa ujumla.
 
Usipumbazwe na propaganda mfu za Mawakala wa Mabeberu, ambao wameshaahidiwa pepo na mabwana zao. Nyerere alitutoa katika ukoloni wa kisiasa. Ni jukumu la kizazi hiki kupigania uhuru wa kiuchumi na wa kujitegemea bila kuathiriwa na ukoloni mambo leo unaotaka kupoka na kujimilikisha njia zetu za uchumi, kwa kupitia mawakala wao!

Miaka mitano mingine kwa Jemedari si jambo la hiari. Ni jambo la lazima ili kulinda utaifa, utamaduni, amani na utulivu kwa maslahi yetu na ya ya Taifa kwa ujumla.
Mawakala wa Mabeberu ni kina nani??? Embu fafanua??
 
Ukisema tano tena jua ni tano tena za mateso, kukosa ajira kwa vijana, kuuliwa kwa sekta binafsi, kuondolewa kwa dawa nyingi kwenye Bima ya afya na kukosa kwa pensheni kwa wastaafu wetu
Usihofu, mimi ninaamini ni tano ya amani tele, JPM ana aminika akiahidi anatekeleza! Naomba unifafanulie kidogo kuhusu dawa kuondolewa bima ya afya naona unairudia sana!
 
Busara gani unayotumia kujenga nchi??? Kujenga uwanja wa kimataifa Chatto wakati kuna maelfu ya shule wanafunzi wanakaa chini na hawana hata vitabu??? Wakati kuna maeneo wanakunnywa maji ya tope???

Maendeleo gani unayosema tuchague??? Mipango miji tu mmeashindwa kufanya nchi imejaa squatters!

Hivi unaona ni busara kujenga flyover inayojaa maji kwa mfugale alafu jangwani mmejenga kituo na barabara kwenye Mkondo wa maji??
Naomba ukumbuke pia Chato ni sehemu ya Tanzania, hivyo inayohaki ya kujengwa na kuendelezwa kama sehemu zingine! Usisahau kuna utalii mkubwa wa Burigi, jirani na Geita, ni eneo la kimkakati kukuza uchumi.
 
Back
Top Bottom