Tatizo la Corona: Wa kulaumiwa ni Serikali kwa asilimia 100%

Tatizo la Corona: Wa kulaumiwa ni Serikali kwa asilimia 100%

Huyu ngoma ikipamba moto ataturuka tu kuwa nilimwambia mfunge na kusali hamkusikia
Japo wananchi ni waumini wa madhehebu mbalimbali lakini kikatiba serikali haina dini.
Hawajachaguliwa kuongoza nchi sababu ya dini zao.
Ukisikia mtu anashindwa kufanya kazi yake au majukumu yake kitaifa,akitumia kigezo cha kusali tu.ujue ameishiwa maarifa anahitaji masada.
Kwani Mungu atamsaidia yule mwenye juhudi na maarifa ya kujikwamua yeye mwenyewe.
 
Mimi walinishangaza pale walipowarudisha wanafunzi wa mashuleni na vyuoni nyumbani huku wakiendelea kuruhusu watu waingie na kutoka mipakani...unaziba huku kule kuko wazi..mnhhh
morning madam akeeeeeeeeeeeeee.....swalamaaaaaaaaaaaaaa
 
Sasa wakifa kwani nani anadhulika? Hizi akili mi za watu kama wewe mkuu. Eti watu wakifa hauna hata huruma! Hooeless kabisa. Afe mama yako pia usiwe na huruma.

Kama wenyewe hawajihurumii? Yaani kifo kinaumiza sana mioyo ila watanzania ni wazembe, hawajui haki zao, ni Zero kabisa kabisa. Yaani ni mazamwamwa . Ukisoma comments ndo utaona aibu aisee. Wala sifichi, watakaokufa na corona tanzania hawatoumiza moyo kama watakaofariki Uganda. Tanzania wazembe.
 
Na ukiwaza mbali zaidi kuna wengine makwao uko nje wamesha funga hamna kutoka na Kuingia unaweza ukaona ni jinsi gani wenzetu wako serious sio walio athirika sana wala Walio athirika kidogo

Njoo uku sasa kwetu..Dah aise ni uzembe mpaka natamani Kulia unamkimbilia Mungu wakati mwenyewe haupo serious hujafanya chochote kujisaidia Mungu akusaidie nini? Ukute watanzania wengine walivyo vilaza wanasubiri Miujiza Tutaisha nakwambia
Kuna wakati inakuwa vigumu kuelewa viongozi wetu wanatumia nini kufikiri. Unakataa kuzuia wageni kuingia nchini mwako eti kwa kuhofia kukosa watalii ambao wameelemewa na corona huko kwao?
 
Badala ya sisi wananchi kuona ni namna gani tuweze kujikinga mmoja mmoja na kuzingatia maelekezo ya wataalamu, ndo kwanza tunaanza kulaumu serkali kanakwamba serikali ndo walio uleta ugonjwa ,na pia hata hiyo lockdown unayoitaka wewe au unayotaka kuiga kutoka kwa wenzetu jarbu kuangalia na mazingira yao na yetu ulinganishe sio kila kitu successful kwao na uku kitakuwa successful hali ya uchumi mbaya wananchi maskini asilimia kubwa ya watu wanategemea kipato cha kila siku kuilisha familiya na serikali haina pesa yakusema kuwalisha watu kama ikiamua lockdown afu na lockdown yenyewe ni hadi lini ?? Na huku hata dawa haijulikani itapakina lini ??
Watu watakaa lockdown hadi lini ?? Marekani walipitisha bajeti ya dollar tirrioni we una hiyo pesa ?? Mi nadhani watu wangezingatia haya

Kwanza ,kuvaa mask kwa kila MTU kila wakati pamoja na gloves.

Pili,Kuwa na sanitizers ya kujisafisha kila Mara.

Tatu,Kuepuka misongamano isiyo na lazima mfano huna haja ya kuenda k.koo kama bidhaa huska unaweza ipata mtaani kwako.

Nne,Kuripoti mapema kituo cha afya pale unapohisi joto kupanda na dalili kama mafua.

Tano,Kuepuka kuzurura mitaani bila sababu ya msingi.

Sita,Kujiziba pale tunapo piga chafya.

Saba,Kujitahidi kukaaa mbali na watu wengine kwa mita kadhaa.

Nane,Kuzingatia na Kuepuka kujishika maeneo ya mdomoni,puani na machoni kabla ya kunawa

Mwisho ,Watu mnalaumu serikali na huku hata kujikinga wenyewe mnapuuzia,afu asilimia kubwa ya wanaotaka lockdown ni watumishi wa serikali maana mnajua mshahara wenu upo pale pale ,vipi kama mkiambiwa mkatwe nusu ya mishahara kwaajili ya lockdown mtakubali ili hiyo pesa isaidie wale wasiojiweza ?

Nobody.
 
Hadi sasa, ukiacha Zanzibar ambako wagonjwa bado wanaongezeka, Tanzania bara, kwa kiasi kikubwa umedhibitiwa. Sababu kubwa ya kudhibitiwa ni wananchi kuzingatia ushauri wa wataalamu, na usimamizi makini wa Serikali. Baadhi ya Mikoa imwxhukua hatua zaidi ya kuhakikisha vyombo vya usafiri na maeneo ya mikusanyiko ya watu km hospitali, masoko, nk yanapuliziwa dawa.

Wanapuliza dawa? Hii siyo fursa ya wakubwa mkuu?

Nasikia kila basi si chini ya 8,000/= kupulizwa kwa siku. Hao wenye mabasi hiyo pesa kila siku wakati wasafiri wanahamasishwa kubakia nyumbani unajiuliza wanaipata wapi?

Nasikia wanalazimishwa kuwa na sanitizer za wasafiri pia kwa gharama ya hao hao wenye mabasi.

Corona imekuwa fursa, imekuwa kufa kufaana.
 
Tahadhari gani unazungumzia bara wakati leo makanisani watu walijazana na tbc inarusha

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
Anayehudhuria ibada kwenye nyumba hizo atambue kuwa anafanya hivyo kwa dhamira ya imani yake bika kulazimishwa. Lakini ajue kuwa anajihatarisha kama hatachukua hatua stahiki za kujikinga
 
Sio kweli wanaougua ni wengi mloganzila kumejaa walikua wanaingia mpaka wagonjwa 50 per day wewe unasema umedhibitiwa

Sent using Jamii Forums mobile app

Tupo ushahidi wa taarifa yako hiyo kuhusu Mloganzila.

Ila, tambua kuwa Mlonganzila ni hosoitali ya rufaa ya Taifa hivyo hupokea wagonjwa muda wote kwa sababu ina nafasi kubwa. Km Chumba cha wagonjwa mahtuti (ICU) kina uwezo wa kulaza wagonjwa wengi kuliko hospitali yoyote nchini.
 
Wewe mtu unaongea ukiwa nchi gani!! Unadiriki kusema umethibitiwa, kweli!?? Hii "exponential growth" huioni, ama mwenzetu unaongea ukiwa usingizini, hata habari za takwimu zitolewazo na Wizara kabisa huzijui!!! Wenzako wameona Mloganzila haitoshi, wameichukua na Amani, halafu unasema imethibitiwa!! Kwa usalama wako tu, ondoa hili wazo na chukua hatua...wagonjwa ni wengi mtaani.
Wewe ndio watoa taarifa ya uzushi. Hospitali zilizoteuliwa mkoani Dsm ni kwa ajili ya vipimo vya awali vya COVID-19 ili kuongeza uwezo wa upimaji. Mgonjwa akithibitishwa anapelekwa Mloganzira kwa matibabu.
 
Tatizo la Corona wa kulaumiwa ni serikali kwa asilimia 100% nitawalaani mpaka kaburini

Nina sababu ya kusema serikali ndo ya kulaumiwa kwa sababu zifuatazo

KWANZA kabisa kipindi mwezi wa pili na wa tatu Corona ilivyoanza kuwa serious ninyi mliendelea kuwapokea watalii na wachina tena bila kificho mkisema kuwa hamtaki kupoteza mapato na watalii kwa sababu ya Corona

PILI ni kwamba mliendelea kuruhusu wageni na safari zikiendelea bila kujali watu wetu watakaoambukizwa mkijimwambafai kwamba mmejizatiti kwa kuwapima watu Airports

TATU mlikua mnaidharau Corona Rais na Makonda walikua wakidharau Corona wakiita kuwa ni kaugonjwa kadogo tu hako na kasiwatishe watanzania huku mkisema ni kaugonjwa kadogo mngekua basi hata mmejiandaa kufanya tafiti ya dawa za asili na kuandaa mazingira ya kukabiliana na Corona. Halafu sasa hivi mnasema tuombe my dear government maombi hayatosaidia chochote mungu hadhihakiwi na wala hapendi unafiki!

NNE hamkufunga mipaka hata mpaka sasa sidhani kama mmefunga sijui mnataka tufe wote?

TANO mliwapa wanasiasa nafasi mkaingiza siasa kwenye ugonjwa mara polepole aite wapinzani Corona mara makonda atoe matamko ya hovyo hovyo sasa hivi mambo yamekua magumu mnasema tuombe maombi hayatosaidia chochote kile nawaambia maana mlikufuru mkasema korona ni kaugonjwa kadogo sana.Mmesahau suala la bashite kumtangaza mtoto wa mbowe kuwa ana Corona na kwamba ni mungu kaleta Corona kwa familia ya Mbowe

SITA hili ni kosa kubwa sana mlificha data za ugonjwa wa Corona sijui mlikua mnamaanisha nini mfano tu mdogo kulipotiwa Corona Zanzibar na mgonjwa mkabisha lakini baadae ikaja kuonekana ni kweli,mlificha sana na sasa mmeona hali ni mbaya hadi waziri anakiri alikua anaficha ficha lakini sasa ameamua kuwa muwazi mmepika data na mnaendelea kuficha maana watu wanakufa wengine ni ndugu zetu kabisa na tena wanakufa kwa Corona mnawazika lakini cha ajabu hairipotiwi

Sasa hivi mmeona hali ni mbaya Mloganzila imejaa ndio mnakumbuka shuka kumekucha watu wameathirika wengi mnoo Corona inatembea mtaani kama nzi mmekumbuka shuka kumekucha watanzania wengi wanaenda kupoteza maisha kwasababu ya uzembe wenu

Wa kulaumiwa ni serikali ya awamu ya tano kwa asilimia 100 na nitawalaani mpaka kaburini
Ibada nazo hazija simamishwa mpaka leo
 
Ibada nazo hazija simamishwa mpaka leo
Kumbuka tu kwamba uhai wako uko mikononi mwako unapofanya maamuzi na kuyatekeleza. Uliingia duniani peke yako na utataitoka mwenyewe tu.
 
Back
Top Bottom