Asinywe maji wakati anakaribia kulala nyingine apande juu ya mti akojoeJamani kuna dogo mvulana yuko form one ana miaka 15, ni mdogo wangu, ana shida ya kukojoa kitandani, tumejaribu sana hospitali lakini ni mzima kabisa, ila ndo hivyo dogo kwa wiki mara 2 au mara tatu anakojoa.
Naombeni mnishauri au mniambie dawa yake ni nini.
Daaaah! mkuu huwa nikikumbuka nabaki kumshukuru tu Mungu maana nlkuaga nawaza sana kama ntakuja kupona na kuwa kama wengine ila kwa nguvu zake mola nilipona bana.Kweli kabisa, tatizo hilo huwa linaondoa confidence yote. Hongera kwa kupona.
Hapana. Hilo jina nimejiita kuweka utofauti. Ila nilikuwa nalimwaga kweli kweli. Asubuhi mshua kama anaoteshwa vile. Lazma aje ahahakikishe chumbani kwangu. Nikizingua tu, ananitoa uchi uchi mpaka nje kuchezea bakoraaa.Ndio maana ukajipa na hilo jina [emoji1] [emoji1] [emoji1]
Duh! Sijui unawaza nini! Inabidi tuyaheshimu mawazo yako japo ni abusive na detrimental kwa mtoto. Angekuwa mdogo wako ungefanya hivyo?!!Hyo anatakiwa mumpe tatizo la kisaikolojia la KUZOMEWA na watoto wenzake tena unawaandaa wanakuwa wengii mtaani litamuathiri atakuwa na hofu wakati wa kulala na atasoma udhaifu wake mimi uncle wangu amepona
Tatizo halijakukuta vizuriDuh! Sijui unawaza nini! Inabidi tuyaheshimu mawazo yako japo ni abusive na detrimental kwa mtoto. Angekuwa mdogo wako ungefanya hivyo?!!
sasa pm ya kazi gani wakati hili ni tatizo la watu wengi hapa ila wamekaa kimyaNi pm mkuu kuna dawa ajaribu mm mwenyewe nili acha nikiwa na miaka 26 kiukweli ina umiza saana. Kuna dawa rahisi tu
Umeniacha nimecheka ile mbay [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]sasa pm ya kazi gani wakati hili ni tatizo la watu wengi hapa ila wamekaa kimya
Ni kweli hili tatizo watu wengi wanalo. Hata nyumbani kuna binti wa miaka 14 ana tatizo kama hilo. Na linamtesa kwa kweli kwa sababu kila siku inabidi atoe godoro kuanika. Awe wazi ili liwasaidie wengi.sasa pm ya kazi gani wakati hili ni tatizo la watu wengi hapa ila wamekaa kimya
Habari wanajamvi mambo vipi, no mara chache naandika nyuzi huku jf katika hili naomba tumsaidie.
Nina mdogo wetu mmoja wa kwetu huko mkoani kwa sasa yupo Kibaha hapa ana tatizo kukojoa kitandani na ni mtu mzima ana miaka 28 kwa sasa namnukuu "Kaka tatizo hili ninalo muda mrefu toka nipo mdogo mpaka sasa na nina elimu ya chuo kikuu nimeishi kwa wasi wasi sana mara.nyingi nimekorofishana na.watu nilowahi kaa mabweni ya mtaani ilinibidi.nipange chumba cha peke yangu ili niondokane na.aibu hyo.japo si mara zote lkn jambo hili ni la aibu sana sana,"" hayo ni machache waungwana dogo aliongea kwa uchungu akilia pia anasema amehangaika sana sana kutafuta tiba bado tatizo liko palepale akaongeza kuwa imebidi aishi kwa unyonge sana sana. Kama mtu.anajua mtu ama hospitali inayoweza kutibu hlo tatizo pm namba zenu nitampatia awatafute jamani. msaada wenu hata kuoa dogo anaogopa siku za usoni maana ni aibu sana. Nawasilisha asante
Duh! sio mchezo kabisaTafuta ule mpira wa maji mrefu na hakikisha kila siku usiku anapoenda kulala basi unauchukua na kumchomeka nao huyo Kijana katika Lidudu lake kisha ule mpira unaukunjua ili uwe mrefu na unauelekezea nje au bustanini kabisa ili usiku pale anapokuwa anajikojolea ule mkojo usipotee tu bure na badala yake moja kwa moja uende kumwagilia ama Maua ya hapo Kwenu au Shamba. Lichukulieni hilo tatizo lake kama Fursa kuelekea katika Kilimo biashara na hapo hata gharama ya kununua Mbolea ( Samadi ) mtakuwa mmeikoa.