Tatizo la Mabaka, Mba na Fungus (Fangasi) sugu na kuwashwa sehemu za siri kwa wanaume na wanawake- Fahamu chanzo, Dalili na Matibabu yake

jamani wandugu heshima kwenu

naombeni kujua madhara yatokanayo na fangasi za muda mrefu kama miaka 10 hivi katika sehemu za siri kwa mwanamke japokuwa keshapata tiba na kupona tayari. Je kuna madhara yoyote yatokanayo na ugonjwa huo. Jamani natanguliza shukrani zangu kwenu
 

Attachments

  • GOD.jpg
    13.2 KB · Views: 133
heshima kwenu wana jamvi,

nanapenda kuuliza jamani kama kuna madhara yoyote yatokanayo na fangasi ya muda mrefu kama miaka 10 hivi katika sehemu za siri za mwanamke. Kwa anayejua tafadhali naombeni mnijuze ijapokuwa ameshishapata matibabu na kupona.


Natanguliza shukurani zangu za dhati
 
Mkuu hapa singoji kitu vitungu swaumninavyo ndani fastar natengeneza kesho ntachek fangas wangu wapoje namiaka sita nasumbuliwa na fangasi miguuni baada ya sikutano ndo ntakuja kutoa tarifa rasmi
 
Sikubaliani kabisa na maneno yalisemwa kuwa una uwezekano wa kuugua figo. Nilishaandika siku za nyuma jamvini juu ya wachangiaji kuacha tabia ya kurukia mambo ambayo hawana utaalamu nayo hasa wakati inahusu afya. Nikurudi kwa huyu aliyekuwa na shida, ni vigumu kukupa jibu la moja kwa moja, kwani maelezo yako hayatoshelezi. Kuna tofauti katika aina tofauti za maambukizi. Kama una fungus kwenye ngozi (superficial fungal infection) hakuna madhara kama umetibiwa ukapona. Kama umepata fungus ya ndani (vaginal candidasis kwa wanawake). Matibabu huwa yanaleta mafanikio mazuri kabisa. Complication pekee ni maumivu wakati wa tendo la ndoa ambayo nayo yanaisha baada ya muda fulani. Kumbuka kuwa candida wapo kwa wanawake wengi na ni mojawapo ya kinga (normal microflora). Mwisho, kama umepona endelea na maisha mazuri usiwe na hofu.
 
Nashukuru kwa ufafanuzi wa kitaalam mkuu. Wataalam kama nyinyi mnatakiwa muwe mnapita hapa jukwaani mara kwa mara ilikutoa ushauri sahihi kwa wadau.
 
hahaha nilikomesha amoeba kwa kutumiia njia hii. yaani kuna kipindi amoeba walikuwa wananitesha nikinywa dawa baada ya muda naumwa tena na dawa zenyewe za Amiba kama unavyoziju zinachafua. Aah nikajisemea ya nini kuhangaika nikatengeneza juisi ya vitunguu Swaumu yaani niliviponda kama punje thelathini nikachanganya na ndimu/limao mbili kisha nikailaza usiku wote. Kesho yake nikaanza kuitumia kama robo glass kutwa mara mbili kwa siku kama tatu.

Baada ya hapo sikusumbuliwa tena na amoeba labda niwe mzembe kwa kula vichafu. Ingawa mmh vitunguu vilikuwa vikali siku ya kwanza nilivyokunywa asubuhi tu nilivyoamka bila kula chochote wee huo mchemsho kama nusu saa hivi baada ya hapo kama masaa mawilii niliharisha na choo nikakisikia ni harufu ya vitunguu swaumu tu.

Ila tahadhari usiweke kwenye chombo cha chuma hasa mchanganyiko huo unapokuwa umechanganya na asali maana hufanya sumu.
 
Ahsante mkuu kwa kutoa ushuhuda wako wa dawa hii.Kwa yeyote mwingine atakayepona asisite kuja kusema hapa ili watu wengine wasioamini wapate kuamini na kuitumia dawa hii.
 
wapo wengine tuna vidonda vya tumbo, haitasumbua? MziziMkavu saidia hapa pia
 
Last edited by a moderator:
mkuu nisaidie dawa hiyo iliyomsaidia mwenzetu

Nashukuru kwa ufafanuzi wa kitaalam mkuu. Wataalam kama nyinyi mnatakiwa muwe mnapita hapa jukwaani mara kwa mara ilikutoa ushauri sahihi kwa wadau.
 





mkuu nashukuru sana kwa maelezo yako yenye kutia moyo na kuleta matumaini mapya, napenda kukuuliza tu kuwa hizo fangasi kwa mwanamke haziwezi leta madhara kwenye viungo vya uzazi japokuwa nilishapona tayari? Maana mimi bado cjazaa.
 

Salam,
Ndugu Fungas kwa wanawake ni tatizo ambalo husababishwa na mambo mbali mbali kama unadhifu , uambukizo, madhara sehemu nyengine ya mwili, mfano sukari...nk sasa wewe sijui ni sabau gani ulipata fungus, hata hivyo si rahisi kusema kama kuna tatizo ama hapana kwa sababu maradhi yeyote hayakosi athari, kwa mfano michubuko , vidonda, kuziba au kukaliana baadhi ya ngozi au mirija nk...(adhesion) ila hutegemea mda (duration), kiwango (Sevearity of illness) na madhara mengine (complications) the early the diagnosis and treatment the good the prognosis.
USHAURI
Kwa hapa jamvini si rahisi kupata jawabu sahihi ni bora katafute Daktari wa kina mama umwelezee kwa urefu jinsi ya ulivyoumwa na kutibiwa na nini shaka yako mfano, kupata uja uzito, atakufanyia vipimo na kukueleza kama umeathirika au hapana na atakujibu masuala yako kwa uhakika, hili ni suala linahitajinuzito unao stahili. :smiling:
 
mkuu nashukuru sana kwa maelezo yako yenye kutia moyo na kuleta matumaini mapya, napenda kukuuliza tu kuwa hizo fangasi kwa mwanamke haziwezi leta madhara kwenye viungo vya uzazi japokuwa nilishapona tayari? Maana mimi bado cjazaa.

vagina candidiasis haina long term side effects kwa mwanamke kama ilivyo bacterial infection. Anoyance ya kuwashwa na harufu mbaya unapokuwa na uambukizo na disharge zinazotokea ndo shida kubwa. Wanawake wengi wanaokuwa wajawazito huwa wanakuwa na hili tatizo na wanaendelea kuzaa. Make sure unakuwa msafi lakini usifanye doching!
 
Baosita ubarikiwe sanaaaa mkuu nimepona kabisa fangas sina tena nimesumbuka nazo miaka 6 mpaka ilifika najichoma na maji ya moto ndo nilale. Azantesna mkuu

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…