Tatizo la Maji na Ukame: Lawama zangu zote ni kwa Waziri Lukuvi na Waziri wa Mazingira

Hakuna gharama yeyote mimi haya ndio mambo yangu, chimba kisima chako mimi nakuletea kimashine cha kutoa hizo chumvi hapo hapo nyumbani kwako.
Desalination project ya kunywesha watu Milioni 7 kwa jiji kama la Dar Hakuna gharama?
 
Hapana usimuonee Lukuvi hata kidogo !
Kama population ya waTanzania inaongezeka kwa kasi ya ajabu, Juzi kati tuu tulikuwa mil20, gafla ndani ya miaka10 tumekuwa mil60! Option rahisi aliyo kuwa nayo lukuvi kama waziri ilikuwa kubadilisha matumizi ya ardhi ili ku accommodate hili ongezeko na hiki ndicho kinacho fanyika duniani kote.

kubadilisha matumizi ya ardhi kutoka mapori ya akiba au mashamba na kuwa makazi ya watu si jambo la ajabu
 
Kwani inahitaji Rais kwenda ziara sehemu ili ajue Kuna Tatizo?
 
Sisi tuchakachuwe ya Ziwa Victoria, Tanganyika, Nyasa, Rukwa, Natron, Eyasi watu wapata maji, wala hatuhitaji kwenda baharini.
Kwa Wakazi wa Morogoro, Pwani na Dar wakachukue maji wapi?
 
Itaje iyo mito ya Iringa inayotiririsha maji mwaka mzima
 
Kwa hiyo lukuvi na waziri wa mazingira ndo wamezuia mvua, aisee.....
 
Tatizo la ungezeko la watu kupita kiasi nalo siwezi kulikataa Ila kuhusu wavamizi wa ardhi mikoa ya Morogoro, Pwani, Rukwa, Katavi, Kigoma na Tabora hapa Lukuvi anastahili lawama kwa kuliendeleza hili kwa kuwarasimisha.

Kwa nini wanaondoka kwao? Kama Tatizo ni Malisho kwa nini wasiwekeze kwenye kuwapa teknolojia ya ufugaji wa kisasa wa kibiashara?

Mtu mmoja ana ng’ombe 1000 tena anawafuga kizamani malisho atapata wapi?
 
Kweli kabisa, unafiki umezidi.
 

Kwani Ruvu, Rufiji, Ruvuma, Pangani, nk inamwaga cubic million ngapi za maji yasiyo na chumvi baharini?

Kwani maji ya maziwa Victoria, Tanganyika, Nyasa, Rukwa nk yana chumvi?



Si mseme tu vipaumbele vyenu ni maslahi yenu yakiwamo Madege mnayotanua nayo nyie?
 
Kwanza Unajua uhusiano kati ya mvua na mazingira hasa Miti? Au hata iyo elimu hauna?
Tupe huo uhusiano maana mimi elimu sina, mwaka jana na mwaka juzi mvua zilisababisha mafuriko kuna nini kilichobadilika ili ionekane mwaka huu lukuvi ndo kazuia mvua......twende kazi.
 
Reactions: PNC
Water desalination, very expensive
 
Unafikiri kwa nini watu wanaenda kujenga au kufanya shughuli zao kwenye vyanzo vya maji?
Sababu kibwa ni ulegevu uongozi katika ngazi mbalimbali. Kuna watu watasema ni kwa sababu ya umaskini, lakini siyo kweli. Maskini wapo Duniani kote. Uharibifu wa mazingira umamwathiri zaidi maskini kuliko tajiri. Hivyo kumwacha maskini aharibu mazingira ni sawa kumjengea kaburi mgonjwa badala ya kumpa matibabu.
 
Nakubaliana na wewe 100%. misitu na mapori mengi yameharibiwa kisiasa katika awamu ya tano chini ya Jiwe. Maeneo ya hifadhi yamegawiwa kwa watu, eti binadamu ni muhimu kuliko tembo lakini tukasahau kuwa mapori na misitu ndio uhai wetu wenyewe. Pia kuna kauli ya hatari sana inaendeshwa na viongozi wa kisiasa ambao pia ni viongozi wa serikali, eti wale ambao hawajayaendeleza maeneo yao wananyangánywa. Hii siyo haki, eneo la mtu hata kama ni pori na msitu liendelee kuwa mali yake na siyo lazima kufyeka misitu na mapori eti ndio kuendelezwa kama kigezo cha umiliki. Hii siyo sawa hata kidogo.
 
Unadhani vyanzo vya maji vitaendelea kuwepo Kama Mazingira yanaharibiwa?
Tanzania atuna tatizo la maji,tunatatizo la uongozi mbovu, Uwezi kuwa na ziwa kubwa la pili duniani, alafu ukakosa maji, kwani sh ngapi kuvuta maji toka Victoria mpaka dar?kuna ziwa nyasa ziwa Tanganyika manyara,mito ndio usiseme,waka Nchi kama Misri na Hisiopia zinategemea mto nile hatujawai kusikia habari hii ya upungufu wa maji,tuna viongozi wazembe tu,wanawaza misaada ya Wazungu baada ya kutumia raslimali tulizopewa mwenyezi Mungu.
 
Asante!
 
Kwaiyo Wewe unaona watu wakose mahali pa kuishi kisa mazingira, mbona Marekani, China,na Nchi za Ulaya hatuoni mapoli?na hatuoni shida ya maji na umeme! Wazungu wanawadanganya tu eti mtunze mapoli wakati wao wanafanya maendeleo, Sisi huku tunaambiwa kufuga mapoli uku wakiwapa viela kidogo ambavo vinaishia katika midomo ya viongozi.
 
Hujitambui wewe dogo.
Juzi kati maana yake nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…