Tazama jinsi Samia alivyomzidi akili Magufuli kwenye uchumi

Tazama jinsi Samia alivyomzidi akili Magufuli kwenye uchumi

Kuna wakati unasoma comments hapa unabaki kushangaa tu.Mkuu hapa wewe changia ukijua unajibizana na watu mwisho wa siku wanakwenda kureport nini wamefanya kwa siku hiyo kusifia ili wapate mkate wa kupeleka mezani kwa familia zao.
Mambo ya kusifia ili upate teuzi yalikuwa kipindi cha jiwe mzee, ndio maana akina Katambi, Jerry Muro, Makonda wakapewa vyeo kwa kutukana upinzani
Hapa tunakuja na facts
 
Kuna wakati unasoma comments hapa unabaki kushangaa tu.Mkuu hapa wewe changia ukijua unajibizana na watu mwisho wa siku wanakwenda kureport nini wamefanya kwa siku hiyo kusifia ili wapate mkate wa kupeleka mezani kwa familia zao.
Shida mtu akishakua chawa anakua hata akili anaipoteza, wengi wanatumia makalio kufikiri.
 
Uchumi umepowa sana aise...na hii siyo kwa Tanzania Bali ni karibia nchi zote zilizokuwa zinaendelea kwa maana ya third country's na hii imesababishwa zaidi na ugonjwa wa Corrina,pili Vita ya Ukaraine na Russia ndo ikaja kutonesha zaidi vidonda vya kiuchumi vilivyokuwa vikikauka taratibu.
Mwisho wa siku maisha yamekuwa haghali sana sana.
 
Magufuli alikuwa hana akili kabisa linapokuja suala la uchumi
 
USD ndio kimbilio la watu wengi kipindi cha crisis, so huwa inapanda sababu ndio hela inayokuwa kwenye demand kubwa kipindi cha majanga

So USD imepanda dhidi ya shilingi yetu si kwa sababu shilingi yetu imeporomoka bali ni kutokana na crisis iliyopo duniani inafanya watu wengi kukimbilia kunununua USD

Ukitaka kulinganisha hela ya nchi yako linganisha na regional currencies kama UGX, Kshs,
Kshs ndio hela imara zaidi kwenye ukanda wetu
Wrong

USD ni Pesa ambayo tunapokea pale tunapouza bidhaa nje, au tunapo pokea misaada.

Endapo tusipouza nje bidhaa nyingi ila twanunua nyingi maana yake twatumia Dollar yetu. Ili kufanya regulation BOT huongeza rate ili ununuzi upungue.

Tanzania hupata dollar nyingi kwenye dhahabu na Utalii, ikifuatia na mazao ya kilimo.

Ila hutumia nyingi zaidi kwenye kuagiza Mafuta ya Kula, na Petroleum products zingine.

Ili fedha yetu iende juu yatakiwa tuuze bidhaa nyingi nje ya Tanzania.
 
Maharage kilo 3500 huko.. Sijui shilingi 1 ya kenya kuwa 18 ya tz ina msaada gani katika hili.

Naomba wachumi wanijibu.
 
Sisi wabongo ni wazee wa mapambio kila awamu...

Ni juzi juzi tu hapa JPM akiwa hai, pambio kuu lilikuwa ni uchumi wa chini wa kati, sifa kemkem...

Sasa hayo yote yamesahaulika, marehemu anapigwa madongo na mama anapambwa kama ilivyokuwa kwa JPM...
Hiii ndio tanzania kakaaa[emoji3]
Wengine tumebaki kuwa wapenzi watizamaji tuu
 
Wrong

USD ni Pesa ambayo tunapokea pale tunapouza bidhaa nje, au tunapo pokea misaada.

Endapo tusipouza nje bidhaa nyingi ila twanunua nyingi maana yake twatumia Dollar yetu. Ili kufanya regulation BOT huongeza rate ili ununuzi upungue.

Tanzania hupata dollar nyingi kwenye dhahabu na Utalii, ikifuatia na mazao ya kilimo.

Ila hutumia nyingi zaidi kwenye kuagiza Mafuta ya Kula, na Petroleum products zingine.

Ili fedha yetu iende juu yatakiwa tuuze bidhaa nyingi nje ya Tanzania.
Mimi nafahamu yote hayo, ila thamani ya dola vs Shilingi inaathiriwa na factor nyingi zaidi ya export na imports zetu
Mfano federal reserve rate, benki kuu ya Marekani ikipandisha interest rates, huwa inapandisha value ya dollars vs other currencies

Kukiwa na crisis duniani mfano vita au mlipuko wa magonjwa, dollar huwa inapanda pia vs other currencies

Jaribu ku Google kwa nini value ya dollar imepanda sana mwaka jana dhidi ya major currencies nyingine
 
Maharage kilo 3500 huko.. Sijui shilingi 1 ya kenya kuwa 18 ya tz ina msaada gani katika hili.

Naomba wachumi wanijibu.
Kama huwezi kununua maharage kalime utajirike
Vyakula vimepanda sababu ya ukame na sio Tanzania tu
 
Mkuu mfumuko wa bei hatuhitaji takwimu ambazo mimi na wewe tunaweza tusijue zimepatikanaje.

Tuangalie tu uhalisia wa bidhaa sokoni.
Mafuta ya kula chini ya JPM yalikuwa 5000 kwa lita hivi sasa ni 8500 hiyo ni kiashiria cha inflation,

Maharage chini ya JPM yalikuwa 1600-2000 ila kwa sasa kwa bei ya leo sokoni ni 4000.

Mbolea chini ya JPM ilikuwa 60000 mfuko wa kila 50 Urea leo hii ni 120000 bila Ruzuku.

Bati chini ya JPM ilikuwa 240000-270000 kwa Bando sasa ni 400000+.

Sabuni mchi wa Sabuni tulinunua kwa 1500 bei ya juu sasa ni 3500.

Chumvi kwa miaka 7 mfululizo tulinunua mfuko wa 20kg kwa 6000-7000 sasa ni 12000.

Hebu nieleze hii control ya inflation wewe unaiona wapi ???
Kaka ..

Chawa humpenda mtu mchafu na sio msafii..
Huo ndio uhalisia..

Chawa gang ni wengi mnoo[emoji1][emoji1]
 
Back
Top Bottom