TB Joshua hakuwahi kubatizwa wala kumpokea Yesu! Nimeshangaa sana

Nimeshakwambia kauli ya "inawezekana" ni kauli dhaifu haihitaji hata kupinga, sioni sababu ya kubishana katika hili.

Umeshindwa kuonesha ni vp huyo Mungu anahusika au kuwajibik na huu ulimwengu sasa utasemaje nimekimbia?
 
Nimeshakwambia kauli ya "inawezekana" ni kauli dhaifu haihitaji hata kupinga, sioni sababu ya kubishana katika hili.

Umeshindwa kuonesha ni vp huyo Mungu anahusika au kuwajibik na huu ulimwengu sasa utasemaje nimekimbia?
Kwa mara ya nne.

Unaelewa "mutual exclusivity" ni nini?

Mbona hujibu hili swali?
 
Nature ni asili ya ulimwengu.AU
Ulimwengu kabla mwanadamu hajatia ustaarabu wake.

Hapa mwanadamu kaikuta nature na yeye ndio anahangaika kuijua nature.
ITAFUTE nature ukiipata nature ndio unaweza kuhitimisha kama mungu yupo au hayupo.
Kwa sasa hivi huwezi kupinga kwa sababu huna tafiti yoyote wala majibu yoyote sahihi ya kisayansi zaidi ya ubishi.
UNADHANI wale wanaofanya utafiti ili kujua 'the mother of all atom' ni wajinga
 
Unajua maana ya kuokoka vzr,nyie ndio mmepelekwa na wake zenu church tena wake wenyewe wameshagongwa na hao manabii uchwara hvy mnaenda kuchorwa tu na kupuuzwa mkifika mnapewa vyeo mnakuwa wazee wa kunufaisha wanaume wenzenu,mnagongewa na mnawachangia utajiri,hakuna zaidi ya makanisa haya: SDA sabato, Lutheran, Anglican,AIC,TAG,RC, mengine mbwembwe tu
Kama hujaokoka hupaswi kujadili habari na Mtumishi huyu. Kwanza haikuhusu Wanaohusika nae wamenyamaza
 
Hujawahi kuthibitisha na kamwe hutaweza kuthibitisha kutokuwepo kwa Mungu.
Hivi hiyo level ya specifity wewe ndiyo hunayo kabisa kwani mada ya uzi ni nyingine na wewe umekuja na hoja nyingine kabisa.
Tuwe ndani ya mada kwenye kuchangia au tuwe tunapita kimya kimya.
 
Wewe ushajua mpaka yatakayotokea wakati ujao?

Kutabiri yatakayotokea wakati ujao nakko ni mada ya uzi huu?

You are an ignoble imbecile.
 
Ni rahisi sana kuthibitisha uwepo wa Mungu. Kuwapo kwako wewe ni uthibitisho tosha kwamba Mungu yupo. Kama Mungu hayupo wewe ungetoka wapi?

Sio kweli kwamba kuna mambo mabaya yanatokea duniani. Linaweza kuwa jambo baya kwako lakini likawa faida kwa viumbe wengine. Mungu ameweka mtindo wa maisha ya kutegemeana katika mazingira tunayoishi.Mungu hakuumba binadamu peke yake tu ili aishi, bali pia aliumba na viumbe wengine ili waishi.

Kwa mfano; simba anapomkamata binadamu na kumla haina maana kuwa Mungu hayupo. Mungu alimuumba simba ale nyama akiwamo na binadamu.

Chunguza kwa makini, kila jambo unaloliona kama baya kwa binadamu, linakuwa faida kwa viumbe wengine. Ili binadamu aishi ni lazima na viumbe wengine waishi.
 
Kuwepo kwangu kunathibitishaje Mungu yupo?

Mungu alishindwa kuumba ulimwengu huu uwe ambao Simba hamuui mtu na mtu hamuui Simba?
 
Mungu alimjua nabii Yeremia tangu tumboni mwa mama yake na kumfanya kuwa nabii wa mataifa.....kwa nini isiwe kwa TB Joshua? nawaza tu...
 
Kuwepo kwangu kunathibitishaje Mungu yupo?

Mungu alishindwa kuumba ulimwengu huu uwe ambao Simba hamuui mtu na mtu hamuui Simba?
Kuwapo kwako kunathibitisha uwepo wa Mungu kwa sababu bila ya Mungu wewe usingekuwapao. Je una njia yoyote ya kuthibitisha uwepo wako bila kumhusisha Mungu? Kama ipo thibitisha.

Mungu hakushindwa kuumba ulimwengu uwe kwa jinsi unavyotaka wewe, bali haukuwa mpango wake. Mungu hapangiwi cha kufanya. Mpango wa Mungu ulikuwa ni kujenga mfumo wa ikolojia kwa viumbe wake. Ni mpango wa Mungu pia unapomchinja ng'ombe kwa ajili ya kitoweo wakati wa sherehe za kuzaliwa kwako. Hata tunapokufa, pia ni faida kwa viumbe wanaokula mili yetu.

Nasisitiza: MUNGU YUPO.
 
Kuwapo kwangu kunathibitisha kwamba kuna process iliyofanya niwepo, hujathibitisha kwamba process hiyo ina uhusiano wowote na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote.

Zaidi, nimeeleza kwamba, uwepo wa Mungu huyo na uwepo wa ulimwengu ambao mabaya yanawezekana kuwepo ni vitu viwili vinavyopingana ambavyo haviwezi kuwapo pamoja.

Ni vitu viwili vilivyyo "mutually exclusive".

Vitu vilivyo mutually exclusive maana yake ni kwamba, kikiwepo kimoja, kingine hakiwezi kuwepo.

Kama shilingi ya Nyerere yenye kichwa na mwenge, ikiangukia kichwa, maana yake haijaangukia mwenge,

Ikiangukia mwenge, maana yake haijaangukia kichwa.

Sasa, uwepo wa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, unawezekana tu ikiwa dunia inayoruhusu mabaya haiwezekani kuwepo.

Tunaona dunia inayowezekana kuwa na mabaya ipo.

Hivyo, Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Hizi habari si kuhusu dunia ninayoitaka mimi.

Hizi ni habari za kuhusiana na logical consistency.

Hujathibitisha ni vipi kuwapo kwangu kunathibitisha Mungu yupo.

Hujaondoa contradiction ya "the problem of evil".

Tatizo nakueleza kuhusu "mutual exclusivity", "the problem of evil" na "logical consistency" sina hakika kama unaelewa hayo mambo ni nini.
 
Unaweza kuuthibitisha huo mfumo uliokufanya uwepo bila Mungu kuhusika?
 
Unaweza kuuthibitisha huo mfumo uliokufanya uwepo bila Mungu kuhusika?
Naweza kuthibitisha Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hahusiki kwenye uwepo wangu hapa bila hata kuthibitisha huo mfumo ulionifanya niwepo ni upi.

Naweza kujua kwamba Washington DC, USA si mji mkuu wa Chad, Central Africa, bila hata kujua mji mkuu wa Chad, Central Africa, ni mji gani.

Kama ninavyoweza kuthibitisha kwamba, mwanamme mwenye miaka 60 leo hawezi kuwa na mama mzazi binti mwenye miaka 5 leo.

Yani nakuambia hivi.

Ukiniwekea baba ana miaka 60 leo hapa, ukaniwekea na binti mdogo ana miaka 5 leo hapa.

Ukasema kwamba, huyu binti mwenye miaka 5 leo, ndiye mama mzazi aliyemzaa huyu baba mwenye miaka 60, naweza kukukatalia kwamba huyu binti wa miaka 5 leo, hawezi kuwa mama mzazi wa huyu baba wa miaka 60 leo.

Kwa sababu huyu baba kazaliwa miaka 60 iliyopita, huyu binti kazaliwa miaka 5 iliyopita.

Wakati huyu baba anazaliwa, huyu binti alikuwa hajazaliwa bado, alizaliwa miaka 55 baadaye.

Na hapo, hata kama simjui mama halisi wa huyu Baba wa miaka 60, nitajua tu kwamba huyu binti wa miaka 5 si mama mzazi wa huyu baba wa miaka 60.

Unachofanya hapa, ni sawa na kuniletea binti wa miaka 5 na Baba wa miaka 60.

Unasema huyu binti wa miaka 5 ndiye mama mzazi wa huyu Baba wa miaka 60.

Nakwambia hilo haliwezekani, kimantiki haiwezekani binti wa miaka 5 leo awe mama mzazi wa Baba wa miaka 60 leo.

Unaniuliza swali.

Kama huyu binti si mama mzazi wa huyu Baba, huyu Baba mama yake mzazi ni nani?

Sihitaji kujua mama mzazi wa huyu Baba wa miaka 60 ili kujua kwamba binti wa miaka 5 hawezi kuwa mama mzazi wa Baba wa miaka 60.

Kwa sababu binti wa miaka 5 kuwa mama mzazi wa Baba wa miak 60 ni contradiction.

Sihitaji kujua kilichoniweka hapa ni nini ili kujua kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hahusiki katika mchakato wa kuniweka hapa.

Kwa sababu uwepo wa Mungu huyo pamoja na dunia ambayo inaruhusu mabaya ni contradiction sawasawa na binti wa miaka 5 leo kuwa mama mazazi wa kumzaa Baba aliye na miaka 60 leo
 
Kuwepo kwangu kunathibitishaje Mungu yupo?

Mungu alishindwa kuumba ulimwengu huu uwe ambao Simba hamuui mtu na mtu hamuui Simba?
Ndo ujiuze ata mtume alilogwa vipi na yesu alisulubiwa vp wakati walikuwa mitume wa Mungu?
 
Ndo ujiuze ata mtume alilogwa vipi na yesu alisulubiwa vp wakati walikuwa mitume wa Mungu?
Hujathibitisha Mungu yupo.

Umeelewa habari ya mutual exclusivity ya uwepo wa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote na ulimwengu wenye problem of evil?

Tunajadiliana kwenye level moja au tumepishana kiasi hatuwezi kuelewana?
 
Ingependeza zaidi uthibitishe kwanza mfumo uliokufanya uwepo hapa duniani bila kumhusisha Mungu, badala ya kutoa mifano ya USA na binti wa miaka 5 kuwa na mtoto wa miaka 60. Thibitisha kwanza, kisha toa mifano. Kazi ya mifano ni kunogeshe tu maelezo ya urhibisho wa jambo.

Thibitisha kwanza tafadhali.
 
Umeelewa mantiki ya huo mfano?

Mtu A akisema mama yako mzazi ni binti wa miaka mitano, mtu mwingine B akabisha na kusema binti wa miaka mitano hawezi kuwa mama yako mzazi, wewe utabisha na kumwambia mtu B ingependeza aseme Mama yako mzazi ni nani kabla ya kusema binti wa miaka mitano hawezi kuwa Mama yako mzazi?

Unaelewa ndicho unachofanya hapa?

Unaelewa naweza kuju jibu fulani si sahihi hata kabla ya kujua jibu sahihi ni lipi?

Unaelewa kwamba naweza kujua binti wa miaka mitano haw3mezi kuwa mama yako mzazi, hata kama simjui mama yako mzazi ni nani?

Unaelewa nikijua Washington DC ni mji ulio Marekani, na ili mji uwe mji mkuu wa nchi ni lazima uwe ndani ya nchi hiyo, mtu akiniambia Washington DC ni mji mkuu wa nchi ya Chad, naweza kujua Washington DC si mji mkuu wa Chad bila ya kujua mji mkuu wa Chad ni mji gani?

Unaelewq kwamba mimi nakuambia Washington DC si mji mkuu wa Chad, kwa sababu Washington DC ni mji ambao uko Marekani, si Chad. Wewe unanilazimisha nitaje mji mkuu wa Chad.

Hata kama sijui mji mkuu wa Chad, hilo haliondoi ukweli kwamba Washington DC si mji mkuu wa Chad, kwa sababu Washington DC uko Marekani.

Kwa hiyo, kama tunatafuta mji mkuu wa Chad, na tunafanya "elimination method" kuitoa miji yote ambayo haipo Chad, Washington DC tunautoa. Haupo Chad. Hauwezi kuwa mji mkuu wa Chad.

Habari ya Mungu kuwepo ina cintradiction. Inatolewa kwa elimination method. Huko kwingine sijakwambia najua nini kimeniweka, na kutokujua huko hakunizuii kujua kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na uoendo wote hayupo.

Kama vile kutokujua mji mkuu wa Chad ni mji gani hakunizuii kujua kwamba Washington DC, mji uliopo Marekani, si mji mkuu wa Chad.

Unakubali kwamba sihitaji kujua jibu sahihi ili kujua kwamba jibu fulani si sahihi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…