TBC MPYA: Ushauri, Maoni na Mapendekezo ya ubora wa vipindi (Television Content)

TBC MPYA: Ushauri, Maoni na Mapendekezo ya ubora wa vipindi (Television Content)

inakera sana hasa kuonyesha mambo ya ccm muda wote, yani mtabaki mnaangalia wenyewe
 
1.Kila muda wanatangaza mambo ya richama rireeee pendwa sana...hapo wanakera sana,

2.Kila muda Jamal kashoggy akiingia ubalozini...Mara majasusi wakitoka...mnakera sana.

3.Rangi mbayaaaaa kama rangi za enzi za ujima Wa kutumia ulimbombo na ulindi.

4Sauti kama zile za kwenye movie ikifika sehemu ya jini au mganga kutoa maagizo yake.

5.Watangazji ni zaid ya wahenga....yaani ni senior citizens (wahenga waandamizi), tafuteni vijana kama kina Tunda, Mobeto, Mimi mars, DJ zero DJ sinyorita, b12, , etc ..mtapata watazamaji.

Kwa Leo naishia hapo , ntarudi
 
Acheni kutumika na chama. Nchi hii ina vyama vingi lakini cha ajabu mnarusha sana tena live matangazo ya chama.Ondoeni kipindi cha chereko, hawavumi, uchumi wa viwanda na vyote mnavyoona havina msisimko kwa jamii. Mkitumika kwa usawa bila kujali chama na ilani nawahakikishia Mungu atawabariki mno
 
huwa nakerwa saut za watangazaj kuwa kama moja hv . haifurashi hata kusikiliza . af hawaongei fastafasta msikilize mtu kama salim kikeke ..saut ina base hv .anasoma taarifa akiwa huru..sasa hapa tbc mtu hapepes hata macho kma mdori vile.
 
Kati ya kipindi mliniudhi ni wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo uliopita hasa monduli mlikuwa mnaonyesha CCM tu, taarifa ya habari kwenu ni habari za ccm na serikali tu, mnaboa kwelim
Vipindi vingine havina mvuto kwa mfano safari ya dodoma, tunatekeleza, this week in perspective, chereko, tafakuri baada ya habar n.k
 
Ndugu WanaJF,

Kumekuwepo na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi na hata hapa JF kuhusiana na changamoto ya vipindi vya Televisheni ya Taifa (TBC1). Malalamiko hayo yameegemea zaidi katika eneo la ubora wa vipindi na ubunifu.

Kwa bahati nzuri, Mkurugenzi pamoja na Watendaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) ni wadau wakubwa wa JamiiForums na huwa wanafuatilia taarifa na mijadala mbalimbali inayoendelea hapa. Hivyo tukiitumia vyema nafasi hii, tutawasaidia kuboresha maeneo ambayo yanatakiwa kurekebishwa kwa haraka.

Naomba tutumie uzi huu kutoa maoni, ushauri na mapendekezo kuhusu aina ya vipindi na ubunifu ambao ukitumiwa utasaidia kuifanya televisheni hii ya taifa kuvutia kutazamwa na kufurahiwa.

Tumeshalalamika sana. Sasa ni wakati wa kuchukua hatua na kutaja suluhu kwa mifano ili kuimaliza changamoto hii kabisa.

Karibuni sana.
Ni vizur pia mkawa mnajiunga na BBC ile SAA 3 usku kulko kuleta mavipind ya ziara za katbu wa ccm au katbu mwenez ,yaan kuna cku nataman niipusue hii TV kwa mavipind yenu ,afu mbaya zaid no dstv hivyo ITV ,channel ten ,star sion kabsa ,yaan napita kwenye jarbu kubwa sana la kuvumilia kuangalia TBC muda wote huo..Mungu aniepushe na kutoa lugha za laana
 
Ni vizur pia mkawa mnajiunga na BBC ile SAA 3 usku kulko kuleta mavipind ya ziara za katbu wa ccm au katbu mwenez ,yaan kuna cku nataman niipusue hii TV kwa mavipind yenu ,afu mbaya zaid no dstv hivyo ITV ,channel ten ,star sion kabsa ,yaan napita kwenye jarbu kubwa sana la kuvumilia kuangalia TBC muda wote huo..Mungu aniepushe na kutoa lugha za laana
Amen
 
Mmekua TV la CCM halafu mtegemee kuwaangalia niwaambie tu ukweli Hakuna mtu ataangalia litibiccm lelu kwani Hakuna tofauti Kama kusikiliza radio uhuru mie Sitaki kufanya jinai kwakuangalia litiv la maccm hata mkifungia TV zote hapa nchini
 
ondoeni vipindi vyote muweke docomentary za wanyama tu maana hawana chama
 
anza kwa kufuta ule ujinga awavumi lakin wamo..
ndo ntajua mnaskilza af niwashauli kukwepa u-kada

Umenifurahishaaa ile kitu ni mbaya ahaina kichwa wala miguu muda wote ni kusifia serikali jaaamaa analetaga cjui stori gan fyeka hiyo kitu nashanaga kabisa CEO wa TBC naye kalidhika kabisa kutupa ule upupu
 
Nchi inaongelea maadili ya Taifa letu yanapotea,
Nyie kama chombo cha Taifa mnacheza video za bongo fleva Wadada wamevaa vichupi sasa hayo maadili yanayo piganiwa ni maadili gani?

Kama TBC ni chombo cha Taifa cha kupasha habari
Anzisheni vipindi vya mtaa kwa mtaa nchi nzima
Badala ya wale wa vyombo binafsi kupiga singeli mtaa kwa mtaa na kuaribu maadili yetu huko mtaani

Nyie njooni kivingine huku mitaani kwetu na kupigania maadili
Mfano leo TBC ipo mwembe yanga temeke
Mada ni wananchi wanasemaje kuhusu mmomonyoko wa maadili ya Taifa wananchi wanapewa mic wanafunguka wanatoa maoni yao na kero zao
Ilo lifanyike nchi nzima .
 
Asanteni sana kwa mnaoendelea kutoa ushauri elekezi wa nini kifanyike..

Ambao bado mpo kwenye upande wa lawama bila kushauri cha kufanya niwaombe mjielekeze kwenye kutoa mawazo ya kujenga ili tupate matokeo tunayoyatamani.

Ni matumaini yangu uongozi wa TBC utapita hapa kuyachukua na kuyafanyia kazi.

Shukrani.
 
Pendekezo langu: Muajirini chakubanga awe anasoma habari kila siku. Pia fungueni tawi lenu pale lumumba kwenye jengo la ccm.
Mtafanikiwa saaaana.🙄🙄
 
TUNAOMBA MJIFUNZE KWA ITV NA MFANYE KUZUDI WAO NA WAANDISHI WASIINGILIWE NA MAMLAKA YOYOTE KATIKA KAZI YAO
MAANA WAMESOMA WAMEAJILIWA WAMEAMINIWA

😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡

PIA TUNAOMBA VIPINDI VYA LIVE VIWE NA KIPAUMBELE KAMA KENYA HAPO HII INAONGEZA LADHA YA WATAZAMAJI
MAANA VIPINDI VINGI VINAVYOPENDWA NA WATU NI VILE VINAVYOENDA LIVE
 
Acheni kutumika kisiasa! Tunashindwa kuwelewa kama nyie ni Television ya Taifa au tawi la chama?
Ubora wa picha ni sifuri kabisa!
Nchi hii imejaa vijana zaidi ya 70% nyie asilimia 80 ya vipindi vyenu ni vya kizee!
Mnashindwa hata kuonesha mechi ya Taifa stars mmekalia ziara za viongozi wa chama wakitembelea matawi sijui kigoma gani huko!
Mmetangaza kufunga mitambo mipya ya kisasa na picha ndo kabisa zimerudi zile za kiwango cha chini kabisa!
Subirini na wengine wanakuja na mjiandae kwa POVU ZAIDI
Nadhani umepotoka ndugu yangu,kati ya stesheni zenye vipindi vya kufundisha katika Taifa hili,Tbc wanaongoza kwa kuwa na vipindi vya ubunifu wa hali ya juu,hongereni sana Tbc.
 
Asanteni sana kwa mnaoendelea kutoa ushauri elekezi wa nini kifanyike..

Ambao bado mpo kwenye upande wa lawama bila kushauri cha kufanya niwaombe mjielekeze kwenye kutoa mawazo ya kujenga ili tupate matokeo tunayoyatamani.

Ni matumaini yangu uongozi wa TBC utapita hapa kuyachukua na kuyafanyia kazi.

Shukrani.
Mkuu mbona wakati wa Tido TBC ilibadilika sana Ikaanza kupendwa...Alivyoondoka imerudi kulekule ilipotoka.

Hapa tutapoteza muda kushauri wakati tatizo linajulikana.
 
Back
Top Bottom