TBC MPYA: Ushauri, Maoni na Mapendekezo ya ubora wa vipindi (Television Content)

TBC MPYA: Ushauri, Maoni na Mapendekezo ya ubora wa vipindi (Television Content)

1.Acheni u ccm unawezaje kurusha ziara,mikutano ya ccm halafu bunge usionyeshe live?
2.Mbona habari za vyama,viongozi wa upinzani hamzionyeshi?
3.Kuwe na taarifa ya habari za uchunguzi wa kero za wananchi siyo kuonyesha mikutano ya viongozi.
4.Taarifa za Habari ziwe kwa kiingereza na kiswahili.
5.Mipira michezo jitahidini sana kuonyesha live
6.Kuwe na vipindi vya kilimo cha kisasa teknolojia mpya uzalishaji katika viwanda kero zao

Asante mkuu. Angalau wewe umetoa ushauri elekezi kuanzia namba 3 na kuendelea. Hiki ndicho nilichokilenga. Tutaje ideas kama hivyo. Asante.
 
TBC mpaka iwe mpya sio rahisi.
1. Mwandaaji na aina ya vipindi ni vya kizee mno. Ubunifu ni zero.
2. Mnavaa kama madereva na sio watangazaji. Mnekukula mmenenepeana haswa wanawake ni vipipa. Hao rudisha nyuma kuandaa na kuongoza vipindi. Eleweni kutangaza kwenye tv ni zaidi ya kazi ya PR. Muonekano ndio branding. Get people with best voice and appearence plus brains. WAPO TELE.
3. Hamjaweza tumia teknologia ipasavyo. Quality ya video zenu inasikitisha. TV ya Taifa? No way. Mnashindwaje na madogo kama ayo, itv nk ?
4. Wekeni channels tofauti. Say TBC 1 huko wekeni watu wa serikali na programme za kuisifu serikali. Fine. TBC 2 ya biashara na programme zilizochangamka za vijana, kisasa, nk
TBC 3 say International hii ni ya utalii na kwa kiingereza. Huko unaiuza Tanzania duniani na sera ya viwanda na ipatikane free duniani kote na balozi zetu na airport zote na portal zote kubwa. Weka vivutio, mahoteli, mbuga, na quality ya picha iwe ya kimataifa.
5. Hiyo serikali mtandao ionekane kimataifa. Mambo ya passport, viza, uwekezaji na fursa. Wawepo watu wanaojua lugha na sio kiingereza cha kihaya.[emoji2][emoji1]

Asante kwa maoni. Namba 2, 4 na 5 ni mawazo elekezi. Hayo mengine ni malalamiko na kejeli ambazo nashauri tujaribu kuziepuka kwa sababu zinaficha ushauri.
 
1. Mimi kuanzia kimuonekano, rangi zenu sio nzuri. Yaani hata nikiiangalia tbc ktk king'amuzi cha dstv bado muonekano haivutii.
2. Jaribuni kuvuta watu kwa kuonyesha vipindi vya michezo hasa mpira wa miguu na mieleka. Ikiwezekana wwe tena sio mechi za zamani na pia ligi tofauti kama za Tz, uk, spain, italy etc.
3. Habari kwa upande wa watangazaji wanaume mmajitahidi, wanaume wamechangamka wanapotangaza habari. Wanawake wengi wamezubaa maana unakuta mtangazaji mwanaume anajaribu kumu-engage mtangazaji mwanamke kwenye mazungumzo ya kuchangamsha habari ila unakuta mwitikio ni mbovu. Wamezubaa wengi.
3. Kingine nafikiri kinawaangusha ila hamna namna ya kukizuia ni KUAJIRI vyeti badala ya vipaji. Ni bahati mbaya ila hamna namna. Kuna vijana wana vipaji na ubunifu wa hali ya juu ktk mambo ya journalism ila vyeti ndio 'taizo'.
4. Watengenezaji wenu wa documentaries za hapa kwetu wawe na ubunifu. Documentaries zimezubaa ma kupooza.

Kwa hiyo, Anzeni na muonekano wa tv yenu. Kweli Rangi imepooza sana. Hamna ule uHD.

Nawapa pongezi pia kwa kuwa na nia ya kutaka kubadilika na kuomba mawazo ya watu. Kwa ujumla, mjikite ktk quality amd contents ya vipindi na muonekano wenu.
Mnajitahidi.

Natamani wachangiaji wote tungeenda hivi. Huku ndiko kuelekeza cha kufanya. Unatoa ushauri ambao unajadilika na unaweza kufanyika.

Kuna watu humu wana mawazo mazuri ila wanashindwa kuyatoa na kuishia kulalamika sijui kwanini.

Tujitahidi kutaja suluhu wakuu. Kama una ideas ambazo unaona ni workable, zitaje tu. Huenda ukaikuta imefanyiwa kazi.
 
Hapo naomba kutofautiana na wewe. Kwa Rais aliepo madarakani swala ni kujenga hoja baada ya kujitathmini. Taasisi kama TBC imezeeka kimuundo na kimfumo. Kwa kutizama tu vipindi vyao unajua jinsi wanavyoplan. In incremental. Ya mwaka ujao ni ya mwaka jana badilisha hapa na pale ...maisha yasonge. TBC inahitaji total overthaul. Unapotafuta mkuu wa taasisi na vitengo unatafuta mtu mwenye vision na uwezo wa kusimamia vision. Nani asieikumbuka National Housing ilivyobadilika baada ya kupata viongozi sahihi? CRDB Je, nk. Taasisi zimekuwa tamu mpaka watu wameanza kupigana vikumbo kwa fitna.
Tubadili mbinu jinsi ya kutafuta CEOs na waachwe watekeleze vision zao. Political interference iwe pia tamed.
Utamlaumu Rais kama kweli anaingilia kazi nzuri. Lakini kama kazi ni mbaya unamtegemea akae kimya?
Tuwasaidie TBC kwa kuwaeleza njia na mbinu sahihi za kupitia watoke hapo walipo maana kweli wana hali mbaya.
Its too sad to see our cash cow being mismanaged.
Ng'ombe huyo alipaswa kutoa lita 20 lakini anayoa lita 5 japo anakula majani yaleyale.

Sahihi kabisa. Asante kwa kujazia maarifa. Napenda kama wadau tuchukue hatua kwa kutoa mapendekezo na tusikubali kukwama kwenye malalamiko tu.
 
3. Mechi za Team ya taifa anzeni kuonyesha hyo ruzuku mnayopewa kaz yake nn unganeni hata na ZBC 2
4. Wekeni vipind vinavyoendana na dunia ya sasa sio kla siku vipind vya wazee tu unategemea nan ataangalia

3. Safi
4. Unaweza kutaja mifano? Pendekeza mfano wa kipindi mkuu.
 
Ongezeni ubora wa picha
Watangazaji wamezubaa pia badilisheni kuweni kama media nyingine nunueni vipaji toka station nyingine kama alivyofanya efm au clouds
Wekeni siasa pembeni na mfocus kwa wananchi kero na maoni yao
 
CEO: Naomba ushauri.

Mshauri: Punguza ukada.

CEO: Huo siyo ushauri, ni kulalamika.

Ushauri ni ushauri. Hata mtu akisema neno TBC lihamishwe litoke upande huu kwenda ule ndiyo ushauri wenyewe huo.

Mpaka sasa inaonyesha hiko kitu ndicho kinawakera na kuwapotezea viewers wengi. Mi ninachojua hata kama umeamua kusifia CCM kuna namna unaweza kuifanya hata watu wakapenda.

Tatizo ni wazee walioshikilia siti. Tugeeni kijiti vijana
 
Siku TBC watakapoweza kutofautisha kati ya Chama(CCM) na Serikali, naamini safari ya mabadiliko ya kweli itakuwa imeanza.
 
TBC mpaka iwe mpya sio rahisi.
1. Mwandaaji na aina ya vipindi ni vya kizee mno. Ubunifu ni zero.
2. Mnavaa kama madereva na sio watangazaji. Mnekukula mmenenepeana haswa wanawake ni vipipa. Hao rudisha nyuma kuandaa na kuongoza vipindi. Eleweni kutangaza kwenye tv ni zaidi ya kazi ya PR. Muonekano ndio branding. Get people with best voice and appearence plus brains. WAPO TELE.
3. Hamjaweza tumia teknologia ipasavyo. Quality ya video zenu inasikitisha. TV ya Taifa? No way. Mnashindwaje na madogo kama ayo, itv nk ?
4. Wekeni channels tofauti. Say TBC 1 huko wekeni watu wa serikali na programme za kuisifu serikali. Fine. TBC 2 ya biashara na programme zilizochangamka za vijana, kisasa, nk
TBC 3 say International hii ni ya utalii na kwa kiingereza. Huko unaiuza Tanzania duniani na sera ya viwanda na ipatikane free duniani kote na balozi zetu na airport zote na portal zote kubwa. Weka vivutio, mahoteli, mbuga, na quality ya picha iwe ya kimataifa.
5. Hiyo serikali mtandao ionekane kimataifa. Mambo ya passport, viza, uwekezaji na fursa. Wawepo watu wanaojua lugha na sio kiingereza cha kihaya.[emoji2][emoji1]
Constructive [emoji106]
 
Kuna yule mzee wa tafakuri, yeye kwenye kila tafakuri lazima amtaje mzalendo no.1 kwani amsipomtaja atafukuzwa kazi? Acheni kujipendekeza kupita kiasi.
 
Labda tupate uzoefu wa watu kama BBC, najua hatuwezi kuwa kama wao by 100%, but we can emulate a few things from them.

Kuna BBC One- Hii ni flagship channel
BBC Two- Kwa ajili ya habari za michezo na current affairs.
BBC Four Kwa ajili ya serious issues na documentary
BBC News- Habari zinazotokea na live coverage.
Zipo za bunge, international affairs, lugha zingine, watoto, art, nk. Wamegusa almost kila kitu.

Sisi muhimu ni Habari, Michezo, Home affairs, International affairs, Arts, Utalii, Watoto nk

Ubora wa mitambo ni kitu muhimu.

Go for talented, presentable and charming news anchors, tafuteni talents kama ambavyo mnaangalia vyeti.
 
Labda tupate uzoefu wa watu kama BBC, najua hatuwezi kuwa kama wao by 100%, but we can emulate a few things from them.

Kuna BBC One- Hii ni flagship channel
BBC Two- Kwa ajili ya habari za michezo na current affairs.
BBC Four Kwa ajili ya serious issues na documentary
BBC News- Habari zinazotokea na live coverage.
Zipo za bunge, international affairs, lugha zingine, watoto, art, nk. Wamegusa almost kila kitu.

Sisi muhimu ni Habari, Michezo, Home affairs, International affairs, Arts, Utalii, Watoto nk

Ubora wa mitambo ni kitu muhimu.

Go for talented, presentable and charming news anchors, tafuteni talents kama ambavyo mnaangalia vyeti.

Umeeleza vizuri sana mkuu pamoja na kushauri. Wewe ni miongoni mwa mlioelewa lengo la Uzi huu.

Asante kwa kutoa ushauri constructive..
 
Hivi orijino komedi bado ipo? Naombeni majibu leo nataka niangalie TBC baada ya kuiblock kwa miaka tisa.
 
Anzeni na kubadilisha mwonekano wenu kwanza..
 
Ushauri tu.
1. Ongezeni channel nyingine ziendane na hali halisi ya sasa. Nazi ziwe free ving'amuzi vyote.
2. TAARIFA ya habari ni muhimu sana. Mnapogusia,Siasa mubalance mambo, hapo ndipo mwaharibu kabisaaa, ndipo wengi mnapowakera watazamaji. Mnaegemea sana Chama tawala yaani HD mnaboa. Hadi aliyekuwa kwenye tukio hushangaa. Leteni wale wazungumzaji kwenye jambo muhimu wafafanue.
 
Subiri kidogo msemaji wa tBc, nikaangalie kwanza hiyo runinga ya taifa, ntakuja kutoa shauri, sikuwa na taarifa kama bado mpo hewani
 
1. Onyesheni bunge mubashara, kama mnaweza kuonyesha na kufuatlia ziara za rais wetu mubashara basi naamini hata bunge mubashara inawezekana.
2. Boresheni ubora wa picha zenu.
3. Kuweni "fair" kama mnaweza onyesha harakati/habari za CCM onyesheni basi na upinzani.
4. Binafsi sifurahishwi na kipindi cha chereko na kile kinachoonyesha kumbukumbu za vifo vya watu jina lake limenitoka.


Vipindi vyenu vingi vinajenga ukiacha hayo mapungufu yenu, kuna watu wametoa ushauri mpunguze vipindi vya kizee na kuongeza vya vijana ili hali hawajataja vipindi vya kizee ni vipi hivyo na vya vijana ni vipi. Wasiwasi wangu ni kuwa hivyo vipindi vya vijana wanavyovitaka ni muziki yaani bongoflava sijui naija/hiphop/kwaito n.k kama "channels" nyingi za kisasa zinavyofanya. Mimi nashauri hivi kuliko kuonyesha muziki usiokuwa na maadili ni heri tuendelee na hivyo vipindi wanavyoviita wao vya kizee.
Ni hayo tu.


Ficus
 
Bibi mzee hata ukimpaka wanja hapendezi, nimeangalia zaidi ya mara tatu sijaona mabadiliko yoyote. TBC tayari haina jipya, mkitaka kufufuka badilisheni mitizamo yenu, TBC ni televisheni ya taifa, lakini ipo chini ya chama kwa sasa. Matukio mengi ya wananchi wanayohitaji kuyaona hamuonyeshi, nyie ni vipindi vya ziara tu za viongozi wa CCM. Wapeni wananchi habari wanazozitaka hata kama nyie mnazichukia.

Hata hao wanasiasa mnaowatumia hawawaangalii, na ndio maana kila wakati simu zinapigwa clouds, mjue wengi hawana habari na nyie.

Rudi kwenye tamasha la URITHI WETU, clouds ndio ilicover kwa zaidi ya 80%, na ni tamasha la TAIFA, hamjajua tu ni kwa nini?
 
Back
Top Bottom