TBC1 yasitisha kuonesha baadhi ya Mikutano ya Bunge moja kwa moja (Bunge LIVE)

TBC1 yasitisha kuonesha baadhi ya Mikutano ya Bunge moja kwa moja (Bunge LIVE)

TBC sio Shirika la Biashara.

Linaendeshwa kwa kodi zetu....

Kama hiyo ni hoja ya msingi.....
Mbona waziri Nape hajasema kwamba hiyo bilioni 4 badala yake itaelekezwa kwenye shuguli zipi?
Kwasababu nina hakika tayari kurugenzi ya TBC tayari ilikua imekwisha tenga gawio la gharama hiyo ya kurusha matangazo ya bunge moja kwa moja toka Dodoma
 
Huu utawala unaweza kuwa mbovu kuliko wowote ule, na watu wamezidi kushabikia sana but timde will tell
 
Gharama za Kurusha Mikutano ya Bunge zinatokana na Kodi zetu wananchi, ni fedha zetu wananchi, Tuna haki ya kujua ni kwa namna gani wawakilishi wetu wanatuwakilisha bungeni na pia tunataka kujua kuwa Serikali yetu ina majibu gani juu ya matatizo yetu.
Hii hatua ambayo serikali inaichukua kuzuia sisi wananchi kufuatilia LIVE mambo yetu kupitia bunge letu, ni hatua ya KIDIKTETA, kinyume cha Utawala bora na kinaturudisha nyuma hatua kadhaa katika suala zima la Uwazi.
Ni ajabu serikali ya Magufuli imeanza kupiga hatua moja nyuma kwa kutaka kujipa power zaidi juu ya wananchi kwa kujaribu Kucontrol Information juu ya namna gani nchi hii inaendeshwa.
Ni matumaini yangu kuwa Wananchi hatutokubali kitendo hiki cha "Kioga" kilichofanywa na Wizara ya Habari.
SERIKALI INAOGOPA GHARAMA KWANI FEDHA SI NI KODI ZETU, NA TBC SI NI SHIRIKA LETU?.
Nadhani Nape Nnauye anataka kuiokoa zaidi CCM kuliko Tanzania, Nadhani pengine viatu vya uwaziri vimeanza kuwa vikubwa kwake!

Hii ni hatua ya Kisiasa tu na wala haina mantiki yoyote!
 
Gharama za Kurusha Mikutano ya Bunge zinatokana na Kodi zetu wananchi, ni fedha zetu wananchi, Tuna haki ya kujua ni kwa namna gani wawakilishi wetu wanatuwakilisha bungeni na pia tunataka kujua kuwa Serikali yetu ina majibu gani juu ya matatizo yetu.
Hii hatua ambayo serikali inaichukua kuzuia sisi wananchi kufuatilia LIVE mambo yetu kupitia bunge letu, ni hatua ya KIDIKTETA, kinyume cha Utawala bora na kinaturudisha nyuma hatua kadhaa katika suala zima la Uwazi.
Ni ajabu serikali ya Magufuli imeanza kupiga hatua moja nyuma kwa kutaka kujipa power zaidi juu ya wananchi kwa kujaribu Kucontrol Information juu ya namna gani nchi hii inaendeshwa.
Ni matumaini yangu kuwa Wananchi hatutokubali kitendo hiki cha "Kioga" kilichofanywa na Wizara ya Habari.
SERIKALI INAOGOPA GHARAMA KWANI FEDHA SI NI KODI ZETU, NA TBC SI NI SHIRIKA LETU?.

Hii ni hatua ya Kisiasa tu na wala haina mantiki yoyote!
Wanao shabikia hii Serikali watunze akiba ya maneno
 
Umemnukuu vibaya. Amesema hawatarusha baadhi ya matukio na si matukio yote
 
Zama za bunge live zimepita,tufanyeni kazi jamani,

kwahapa jf tunamtuma yerico nyerere aende dodoma atakuwa akituletea jf live
 
Wapinzani mtamkumbuka Kikwete. Aliwalea sana kama mayai
 
Kwani si wengine wote walikuwa wanapata feed kutoka tbc? Sio kwamba ndio maana hata star tv nao wameshindwa kurusha? Kwa maana hiyo hata itv wakipata si itakuwa hiyo hiyo edited version ya tbc? Unless watu bungeni warekodi wenyewe kwenye smartphone zao, je inawezekana?
hapanaaaaaaaaaaaaaa bhana eti wote wanapata tbc ngoja niingie mitamboni ntapata jibu saa hii
 
Uko sahihi mkuu lakini pia Kuna mihimili mitatu.kuna Bunge,mahakama,na SERIKALI.Hiyo TV ni mali ya Serikali sio ya bunge.Huwezi lazimisha mali za muhimili mwingine zitumikaje na muhimili mwingine.TBC hawalazimiki kisheria kurusha mijadala ya bunge.
Haiwajibiki ndio... na kwakuwa bunge ndio huipangia FBC bajeti ni vema kuanzia mwaka 2015/2016 wawapangie 0Tzs ya ruzuku ili wajiendeshe
 
yelewiiiiiiiiiiiiiiiii sasa tutarajie kuona harusi live kwa wingi


hivi itv star na wengine ambao wanajitegemea wanafanyaje aisee hii wizara ni jipu.. badala kufanya ubunifu wapate jinsi ya kutuonyesha jambo hili muhimu kwa taifa wanaleta longolongo piga chini muhusika
Hii wizara jipu kabisa na limeiva kabisa
 
Hii serikali ya Magufuli lenyewe Ni jipu. Hawataki likosolewe. Tv za majirani zetu wanashindana kuonyesha live matukio yote muhimu kwa maslahi ya watu wao,sisi ahh. Jamaa wanaonyesha hadi kesi za mahakani. Awamu hii wako too manual.
Hapa tutamkumbuka Kikwete,alikuwa mvumilivu Sana kwa wakosoaji wake,sio hawa wa sasa.
Sishangai Sana,maana waziri wa habari na michezo hajui hata TFF ni nini,inasimamia nini na wapi. Majipu kila kona
 
Tatizo siyo gharama amesema hivyo ili wavivu msilalamike lkn sababu hasa ni kwamba huu ni muda wa kazi na siyo wa kuangalia luninga, hivyo fanyeni kazi na Bunge mtaliona jioni baada ya kazi au wkend!
Sasa humu jamii forum saa hizi unafanya kazi? Ungesubiri hiyo saa tano usiku.
 
Cku zote viongoz wetu si watu wa kutatua matatizo ni watu wa kuyaahirisha tu, hii dunia ya sasa imebadirika huwez kuongoza kwa kuahirisha matatizo na ujanja ujanja, haya mambo athari zake huwa hazionekani hapo hapo huwa zinachukua muda, baadae mtakaa uchi tu lazima. Sasaiv ukizuia tv zisioneshe wabunge watarecord SOUND CLIPS watatuma kwenye social media tutapata ukweli tu japokuwa inaweza isiwe timely hizo recorded mtaangalia ninyi na wake zenu by the way hakuna mtu anaangalia tbc saiv

ndio aina ya viongozi wa serikali tulionao, hatufiki popote na hawa watu, tusipowaondoa ni kwamba tutaendelea kuula wa chuya kwenye hii dunia...
sijui ni kwanini hatuwezi kuwaondoa hawa watu jamani...
 
Back
Top Bottom