TBC1 yasitisha kuonesha baadhi ya Mikutano ya Bunge moja kwa moja (Bunge LIVE)

TBC1 yasitisha kuonesha baadhi ya Mikutano ya Bunge moja kwa moja (Bunge LIVE)

Mimi naona ni maamuzi ya busara sana tena sana maana kuna watu hakuna jambo la msingi lakini linaoneshwa live hivyo pesa inatumika bure tuu!
Pia kuonesha bunge live kulikuwa kuna changia vurugu bungeni maana kuna watu wanaligeuza bunge kama sehemu ya kujipatia umaarufu na wengine wanaona ndio sehemu ya kufanyia uhuni!

Sioni sababu ya msingi ya kuonesha bunge live ikiwa kuna kipindi jioni cha bungeni leo!

Mimi napendekeza hata TV binafsi zipigwe marufuku kuonesha bunge live na wafate maelekezo ya TBC na wawe wanachukua kupitia TBC!

Najua hili ni pigo kwa UKAWA kwani wamezoea kufanya vurugu wakijua wanaonekana live.....
Mungu saidia Tanzania. Huyu ni aina ya msomi wetu
 
Mimi naona ni maamuzi ya busara sana tena sana maana kuna watu hakuna jambo la msingi lakini linaoneshwa live hivyo pesa inatumika bure tuu!
Pia kuonesha bunge live kulikuwa kuna changia vurugu bungeni maana kuna watu wanaligeuza bunge kama sehemu ya kujipatia umaarufu na wengine wanaona ndio sehemu ya kufanyia uhuni!

Sioni sababu ya msingi ya kuonesha bunge live ikiwa kuna kipindi jioni cha bungeni leo!

Mimi napendekeza hata TV binafsi zipigwe marufuku kuonesha bunge live na wafate maelekezo ya TBC na wawe wanachukua kupitia TBC!

Najua hili ni pigo kwa UKAWA kwani wamezoea kufanya vurugu wakijua wanaonekana live.....
Kwani unadhani wananchi wanapenda vurugu?
 
TBC inaonesha Harusi live, lakini inashindwa kuonesha Bunge live. Hii inatokea Tanzania tu.
 
Nisawa mida hiyo ya asubh mie nakuwa kazin na jion kurudi..so naona jambo la msingi kurudiwa saa nne
 
Moja ya jambo la kusifiwa katika awamu ya nne ni uwazi na Uhuru Wa vyombo vya Habari ndio maana tulishuhudia serikali ilikuwa ikikosolewa kwa sababu wananchi walikuwa na taarifa za kutosha.
Tofauti na awamu ya tano inaonesha dalili ya kutotaka wananchi kupata taarifa.!
Hii ni ishara ya serikali isiyotaka kukosolewa..!
 
Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na
Michezo, Nape Moses Nnauye, amesema
Televisheni ya Taifa imeacha kurusha LIVE
kipindi cha Bunge kuanzia jana ili kubana
matumizi. Na itakuwa ikirekodi baadhi ya
matukio na kuonyesha usiku.

Kama mtanzania, unadhani unatendewa
haki?
 
Hii ni agenda ya CCM tangu bunge la 10 kwa hiyo wamepata pa kuanzia
 
Amna shida mim naona sawa tu kama wamedhamiria kufanya hivyo maana kuna tbcfm sio lazima. Uone ,cha msingi ni kusikia basi
 
Inahitajika sura isiyo na haya hata chembe ili kutetea huu ushenzi!!!
 
tuna haki ya kupata taarifa Na kwanini hizo gharama bunge hili la kumi Na moja Tu hiyo miaka mingine kulikuwa hakuna hasara?nape ajipime
 

Serikali imechukuwa uamuzi sahihi kabisa, ilikuwa inafikia wakati unakwenda ofisini kupata huduma wafanyakazi wamekodoa kwenye luninga wanaangalia Bunge, Nasema SAFI SANA NAPE!
Wewe ni bendera inayofuata upepo, kazi yako ni kuunga mkono kila jambo la CCM, liwe jema au baya haijalishi!
 
kama TBC HAWAWEZI KURUSHA,BASI ITV AU STARTV AU CHANNEL NYINGINE YENYE UWEZO WA KU.INCUR HIO WAPEWE WARUSHU FULU TIME-BY THE WAY KAMA SERIKALI INAKUSANYA KODI KWETU KAZI YA KODI KODI NI NINI?KWA NINI WANATAKA KUBANA KILA KITU-WAMEFUNGUA ACCOUNT YA FIXED DEPOSIT SEHEMU NN?HIZO HELA WANATAKA PELEKA WAPI?
 
Kati ya maeneo ambayo kikwete alifanikiwa ni kuweka Uhuru wa habari,
Kwa hili la tbc na utendaji kazi wa jpm inashanhaza!!!!
 
Ni sawa kabisa kutorusha live kwani huo ni muda Wa kazi na hapa ni kazi tu. Hivi kupambana na umasikini kutakuja kwa staili Kama hii ya KUSHINDA kwenye luninga saa za kazi???

Queen Esther

Je,Unadhani ni haki kwa serekali kukatiza matangazo ya moja kwa moja kwa shughuli za bunge?
Tutoe maoni yetu hapa serekali itayaona na kuyafanyia kazi.
Karibuni!
 
Back
Top Bottom