TBC1 yasitisha kuonesha baadhi ya Mikutano ya Bunge moja kwa moja (Bunge LIVE)

TBC1 yasitisha kuonesha baadhi ya Mikutano ya Bunge moja kwa moja (Bunge LIVE)

Kama serikali ina lengo na dhamira ya kweli ya kusafisha mwezi wa nchi hii kwanini wasituoneshe wabunge wetu wanavyochambua mambo bungeni na kama kuna dhamira ya kweli kwanini waogope kurusha bunge live unadhani ni woga wa kuanikwa na wabunge walioenda bungeni kuwatumikia wananchi na siyo kwa faida zao.
 
Ulishawahi kuona wabunge wanachambua mambo ya maana hata siku moja zaidi ya kuuza sura tu.
 
Nimesoma hii report ya Nape kuhusu utaratibu serikali ilioutumia wakuhamishia vipi vya bunge usiku nikacheka sana...

Hoja ya Nape ni kwamba eti watu wapate muda mzuri wa kushuhudia yaliyojiri mchana...

Namuuliza swali moja jepesi sana Nnauye hivi saa tano usiku ni sawa na saa tano asubuhi?

Pili je lisaa limoja linatosha kumpa mlipa kodi habari ilitumia masaa matano wakati ikiwa halisi?

Hivi kwani bunge ni kwaajili ya Nape magufuli au kwaajili ya waliowapa hayo madaraka?
 
KWA KAWAIDA VYOMBO VYOTE VVYA HABARI NDO UTUPASHA HABARI ZILIZOJIRI NA ZINAZOJIRI NA KWA ASILIMIA KUBWA WATANZANIA WENGI VIJIJINI NA MJINI WANAPATA HABARI ZILIZOJIRI KUPITIA TARIFA YA HABARI NA WANAFAAMU KINACHOENDELEA,
KUNA TATIZO GANI BUNGE KUONYESWA RECORDED KATIKA MUDA AMBAO WATU WANAPATA HABARI NJE YA MUDA WA KUANGAIKA ILI KUJIONGEZEA KIPATO MTU BINAFSI ILI KUONDOKANA NA UMAZIKINI WA MTU BINAFSI
 
Tatizo hajui kwamba yeye ni Serikali na hana nguvu kwenye Bunge.Awaachie wabunge waamue nini wafanye.Mbona ile TBC 2 ni full kukataa mauno na gharama zote inatoa Serikali. labda akamdanganye aliyempa uwaziri
 
weeee mbwa wa nape kale makombo yake tayari amekuwekea jalalani kwake mpuuzi wewe; unadhani kukataza watz kuangali wawakilishi ndo utafich a uovu na udhaifu wa serokali dikiteta kama hii?
 
hiv kumbe matusi yanaruhusiwa humu!! bila kuelimishana!!!! hii sasa sio JF!
 
KWA KAWAIDA VYOMBO VYOTE VVYA HABARI NDO UTUPASHA HABARI ZILIZOJIRI NA ZINAZOJIRI NA KWA ASILIMIA KUBWA WATANZANIA WENGI VIJIJINI NA MJINI WANAPATA HABARI ZILIZOJIRI KUPITIA TARIFA YA HABARI NA WANAFAAMU KINACHOENDELEA,
KUNA TATIZO GANI BUNGE KUONYESWA RECORDED KATIKA MUDA AMBAO WATU WANAPATA HABARI NJE YA MUDA WA KUANGAIKA ILI KUJIONGEZEA KIPATO MTU BINAFSI ILI KUONDOKANA NA UMAZIKINI WA MTU BINAFSI
kajifunze kuandika vizuri kwanza, umazikini ndio nini?
 
KWA KAWAIDA VYOMBO VYOTE VVYA HABARI NDO UTUPASHA HABARI ZILIZOJIRI NA ZINAZOJIRI NA KWA ASILIMIA KUBWA WATANZANIA WENGI VIJIJINI NA MJINI WANAPATA HABARI ZILIZOJIRI KUPITIA TARIFA YA HABARI NA WANAFAAMU KINACHOENDELEA,
KUNA TATIZO GANI BUNGE KUONYESWA RECORDED KATIKA MUDA AMBAO WATU WANAPATA HABARI NJE YA MUDA WA KUANGAIKA ILI KUJIONGEZEA KIPATO MTU BINAFSI ILI KUONDOKANA NA UMAZIKINI WA MTU BINAFSI

Ndugu usitake kunambia huelewi nini maana ya taarifa ya habari! Mpaka kuitwa "taarifa ya habari" maana yake ni yaliyokwisha tokea. Hii ni tofauti na "habari ya yanayotokea sasa".

Pia kumbuka kama wewe unahangaika mchana, sio kila mtu anahangaika mchana kama wewe. Wakati wewe umelala kuna wengine wameamka, ukiamka wengine wamelala. Kama haitoshi sio wote wameajiriwa kama wewe, wengine wamejiajiri au hawajapata kazi kabisa na wanahangaika.
 
ni ngumu sana kumuelimisha mwana lumumba kuliko ngamia kupenya kwenye tundu la sindano
 
Hoja ya kufanya kazi kujiongezea kipato ni ya kijinga sana, hili bunge limeanza lini kuoneshwa live, kabla ya hapo watanzania walikuwa na utajiri gani? Kwa nini TV zisizuiwe kurusha matangazo muda wa kazi? Acheni watu waone yanayojiri huko mnaficha nini?
 
Ndugu usitake kunambia huelewi nini maana ya taarifa ya habari! Mpaka kuitwa "taarifa ya habari" maana yake ni yaliyokwisha tokea. Hii ni tofauti na "habari ya yanayotokea sasa".

Pia kumbuka kama wewe unahangaika mchana, sio kila mtu anahangaika mchana kama wewe. Wakati wewe umelala kuna wengine wameamka, ukiamka wengine wamelala. Kama haitoshi sio wote wameajiriwa kama wewe, wengine wamejiajiri au hawajapata kazi kabisa na wanahangaika.

Kama ni hivyo si vituo vya habari vingekua vinazimwa usiku ili kwatu walale kwa kua mchana kutwa wamehangaika? Hii yote lengo lake ni kutetea bunge kutoonyeshwa moja kwa moja au ana hoja nyingine?
 
Mi nashindwa kuelewa..wapinzani ni kama watoto wa kambo hawaishi "kompleini"..nnachokiona hapo ni mabadiliko ya ratib,kwani kilivokuwa kinarushwa live mchana mlikua na nyie mnachangia kwa Njia ya simu?
 
iv wafuac wa ukawa ni kip kwanza mnajivunia! Mbon mnakoment matuc badil ya kujenga hoja? Jengen hoja achen hasira siasa haziendeshw kiivo nitukanen na me maana nyie
 
Sasa napata picha kama vile NAPE hatakaa muda mrefu kwenye nafasi aliyonayo hapo kwenye serikali ya Ngosha!
 
Mi nashindwa kuelewa..wapinzani ni kama watoto wa kambo hawaishi "kompleini"..nnachokiona hapo ni mabadiliko ya ratib,kwani kilivokuwa kinarushwa live mchana mlikua na nyie mnachangia kwa Njia ya simu?
Huwezi kurusha bunge zima la siku kwa saa moja tu. mabadiriko ya ratiba yaendane na muda halisi uliotumika. Musiedit hata second moja.
 
Rais ni mwanasayansi, wabunge wanapiga siasa, wanajua media zitawarusha, wanajua watapata wa kuwaunga mkono. Kila siku ukiwasikiliza wanasiasa unaweza kudhani kuwa kuna jambo la hatari sana linatarajiwa kutokea ndani ya siku chache zijazo. Mapinduzi makubwa ya elimu yanahitajika ili kuweza kuwaokoa hawa watoto wanaonza chekechea katika miaka hii ya karibuni, ili na wao wasiweze kuzama katika mtego huu wa kudanganywa na media zetu. Kila kitu kinaandikwa kishabiki, kila mtu anakuwa na mawazo ya kishabiki. Nawashauri wabunge waanze kujipanga ili tija yao iweze kuwarudisha tena ndani ya bunge lijalo. Lakini rais ni mwanasayansi mwenye dhamira njema na uwezo wa kufanya makubwa anao.
 
Katika kauli za Mawaziri, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye, ametangaza kwamba, Kuanzia tarehe 26 Januari mwaka 2016, TBC1 haitaonesha tena Mikutano ya bunge live kutokana na gharama za kuonesha live kufikia bilioni nne kwa mwaka.

Badala yake TBC1 watarekodi na kuonesha katika kipindi maalum usiku kuanzia saa nne hadi saa tano.

Hii itanyima wanchi fursa ya kuona kinachoendelea Bungeni.
=========



Mheshimiwa spika,
Naomba kutoa kauli ya serikali kuhusu TBC kutangaza moja kwa moja vikao vya majadiliano ya bunge. Mheshimiwa spika, shirika la utangazaji Tanzania, TBC lilianza kurusha moja kwa moja matangazo ya vikao vya bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania mwaka 2005. Kabla ya kuanza kurusha moja kwa moja, TBC wakati huo televisheni ya taifa ilikuwa inarekodi matukio yote ya bunge na kurusha usiku katika vipindi maalumu vilivyojulikana kama bungeni leo kwa maana ya yaliyojiri ndani ya bunge kwa siku husika.

Baada ya kuanza kwa utaratibu wa kuanza kurusha matangazo moja kwa moja mwaka 2005, gharama za kufanya kazi hio zimekua zikipanda kwa kasi hadi kufikia Tshs. bilioni 4.2 kwa mwaka kwa maana ya mikutano minne ya bunge.

Shirika limekuwa likigharamia kwa sehemu kubwa matangazo hayo kwa kutumia mapato yake yanayotokana na matangazo madogo madogo ya biashara, ifahamike kuwa asilimia 75 ni vipindi vingi vinavyolenga kutoa elimu kwa umma na asilimia 25 ni burudani.

Mheshimiwa spika, kutokana na hali hii, TBC imeona ni busara kubadilisha mfumo wa utangazaji wa shughuli za bunge ili kukabiliana na kupanda kwa gharama za uendeshaji, hivyo basi, TBC imeona ni busara kuanzia mkutano huu wa bunge iwe inarusha baadhi ya matangazo ya bunge moja kwa moja yaani live ikiwa ni njia ya kubana matumizi.

Chini ya utaratibu huu, TBC itahakikisha kuwa, baadhi ya matukio ya matukio ya bunge yatarushwa moja kwa moja na mengine kurekodiwa na kuandaliwa kipindi maalum kitakachoitwa leo katika bunge. Kipindi hiki kitakua na mambo yote muhimu yaliyojiri ndani ya bunge kwa siku husika. Kipindi hichi kitakuwa kinarushwa kuanzia saa nne usiku hadi saa tano usiku.

Na mheshimiwa spika kipindi hicho kimeanza jana na tayari baadhi ya wananchi wameonyesha kuridhishwa na utaratibu huu na kuwa na kipindi maalum usiku kikishughulikia shughuli za bunge, mheshimiwa spika, uamuzi huu utapunguza gharama za uendeshaji wa shirika na pia kupitia kipindi cha leo katika bunge, watanzania walio wengi watapata nafasi ya kufahamu yaliyojiri bungeni kwani wakati bunge linaendelea mijadala yake, watanzania walio wengi huwa wanakua na kazi za kiofisi au zingine za ujenzi wa taifa kwa mahali walipo.

Mheshimiwa spika nakushukuru.

Huyuu bwana ni katibu mwenezi wa chama, kila afanyacho anafikiria zaidi kipi kitakipa chama chake credit na anasahau kabisa kuwa hata katiba ya nchi inasema kila mtanzania ana haki ya kupata habari. Karne ya leo kuleta hoja kama hii bingeni ni aibu kwa nchi
 
Back
Top Bottom