TBT: Unakumbuka nini kuhusu mabomu ya Mbagala (2009) na Gongo la Mboto (2011)?

Tupe story kidogo aisee😁
Mpaka leo najiuliza wanaokimbia marathon mapafu yao yakoje? Niliongozana na baba aliyekuwa na kichanga cha approx chini ya miezi 3, hakijafunikwa chochote. Ikabidi nimpatie kanga niliyokuwa nayo amfunike. Namuuliza mamake yuko wapi, kosa, ndio kaanza kilio mke wangu..mke wangu...Ama, nikajiongezea mbio kunusuru ya kwangu...
 
poleni sana!
 
Ukahisi Diwali gani ipo Gongolamboto, hukujiuliza Wahindi gani waishi uko.
 
Ya mbagala nilikua nipo mkoani kipindi hicho nasoma...

Ila haya ya juzi ya gongo la mboto..

Picha linaanza siku hiyo mchana nilienda bwawani kuoga.. nikaibiwa nguo zangu.. kipindi hicho tunakaa kule mbande sehemu moja wanapaita kwa tinyango...

Kwa tinyango miaka hiyo kulikua kuna njia ya magaro yale ya mchanga (selela)..
Siku hiyo nimeibiwa nguo narudi hom mama alinichapa kinoma noma..
Nikasusa na kula kabisa.. siku hiyo mchana sikupata menu.

Imefika sa 12 tukaanza kusikia kwa mbaaaali milio ya mabomu..
Kwa mda huo tulikua hatuelewi kitu chochote kile...

Sa 2 juu ya alama ndio mambo yalianza changanya hapo mambo yakawa vururu valala..

Ila kufupisha story tulitembea kwa mguu kutoka mbande tukapita ndani ndani mpaka mwanambaya.... Moja kwa moja mpaka mkuranga...

Tukaridishwa kesho yake kwa msaada wa polisi...
 
Jeshi lolote lile duniani mlipuko kwenye ghala la silaha unaweza tokea.
Pia, Rwanda ni nchi yenye uwezo wa kawaida sana kijeshi wala sio wa kuwalinganisha na Tanzania kivita.
 
Nakumbuka wimbo wa diamond na mpoto
 
Ya mbagala nilikua Tosa boys, form 6,tuko domitory tunasikiliza radio hata Dar siijui na sijawah kufika

Ya Goms nilikua mwaka wa kwanza Ifm, niko hostel kigamboni majira ya saa 2 usiku sitakuja kusahau yanaitika kama yako kilometa chache yan wave unaisikia kabisa inavyokata upepo. Nikajiuliza sijui walio karibu inakuaje kama kigambon huku fery mpaka nyumba zinatikisika vivuko vikasimama kufanya kazi.
 
Sikuwepo ila kila nikitazama rejea za hayo matukio mawili kwenye madhara naona picha za unguided rockets na waandishi ndio wanaita jina la kiujumla kuwa ni mabomu. Roketi zenyewe naona nyingi zikizidi sana zitakuwa 220mm au hata ndogo 122mm.

Yawezekana mabomu ndio yalilipukia kambini na kuleta madhara makubwa ambayo hayakuonekana kwa public alafu mizinga ikaruka sehemu mbalimbali. Ila ilikuwa ni milipuko midogo sio missiles zile wala sio rockets kubwa kama 300mm.
 
Itoshe kusema uliyasikia kwa mbali hali ilikuwa hivyo, je watumiaji wakiwa field inakuwaje!! Vita mbaya sana tuendelee kudumisha amani yetu!!
True..hii kitu vita kilinifikirisha sana kipindi kile, sisi yalikuwa ya bahati mbaya. Imagine nchi ambazo hiyo milio ni 24/7!..
 
Tupe maelezo huu ulikuwaje mkuu
Ilikuwa mida ya saa saba kwenda Saa nane mchana nakumbuka tulikuwa darasani kipindi cha Physics mwalimu akiwa mzee mmoja anaitwa Nzohi.

Ghafla tukaanza kusikia vishindo na ngurumo kama radi, hakuna aliyeuliza kuna nini watu wote tulijikuta mlangoni tukigombania kutoka, kufika nje tukakutana na class ya PCB nao wanakuja mbio upande wa class za PCM kuuliza ni nini Hamna mwenye jibu but inaonekana matatizo yapo huko upande wa mbele ya shule.
Basi almost shule nzima ikaelekea upande wa bonden like kama unaenda kisarawe, sasa kuna makombora yakalipuka huko yakaja na kipande cha roof ya huko jeshini, yakaangukia huko pondi (bondeni) kwa waliosoma pugu wanapajua bondeni aka pond au kwa mama P njia ya kwenda kwa mkandawile.

Watu wote tukaanza kurudi mbio tena shulen, kufika nusu ya mlima tunakutana na rundo la wanajesh nao wanakimbia kuja huku bonden pond, aisee ilikuwa ni mshike mshike haswaa! Wananchi, wanajeshi kwa wanafunzi kila mtu na njia yake.

Madhara yalikuwa mengi kwenye mali na vifo!

Hayo Ndo nakumbuka kwa ufupi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…