TBT ya kibabe: Mabasi na vyombo vya usafiri Tanzania

TBT ya kibabe: Mabasi na vyombo vya usafiri Tanzania

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
1. TAWAQAL EXPRESS

1640251205752.jpg


Pichani ni basi la kampuni ya Tawaqal. Kampuni hii ilikuwa balaa. Njia ya Dar - Mbeya, Dar- Kyela, Dar - Tunduma na Dar - Songea.

Kampuni hii ilikuwa na madereva mahiri kwelikweli. Miongoni mwao alikuwepo GIRIKI.

Jamaa alitoka Dar saa 12 asubuhi akaingia Mbeya saa 7 mchana.

2. SHABAHA EXPRESS

263007996_408387751030329_6493633342006558773_n.jpg

Kampuni hii ilibamba sana miaka ya nyuma ikisafirisha abiria kati ya Dar na Arusha. Jamaa walikuwa wakishindana na wakongwe wa zamani kama Ngorika, Dar EXPRESS nk

3. SCANDINAVIA EXPRESS

Kampuni ya mabasi ya Scandinavia Express ni kampuni pekee ya kitanzania iliyowahi kutokea kwa kuwa na huduma za uhakika na za viwango vya hali ya juu kabisa kulinganisha na huduma zinazotolewa na kampuni za sasa. Kampuni hii ilijijengea jina kubwa na sifa nzuri ndani na nje ya nchi kwa huduma bora walizokuwa wakizitoa kwa abiria wake na pia kuliletea sifa taifa la Tanzania kwa kujulikana kuwa na mabasi ambayo ni quality na high class.

Scandinavia-Bus.gif

Kampuni ya Scandinavia ilianzishwa zaiidi ya miaka thelathini na tano (35) iliyopita ikiwa na mabasi machache tu aina ya LEYLAND na ilipofika mwaka 1982 kwa mara ya kwanza Scandinavia walinunua basi lao la kwanza la kisasa kutoka kampuni ya SCANIA TANZANIA COACHES aina ya SCANIA ambalo kutokana na ubora wake na uzuri wake kwa kipindi hicho waliamua kulitumia kwa safari yao mpya waliyoianzisha ya Dar es salaam hadi Iringa.


BASI LA KWANZA LA KISASA KUNUNULIWA NA SCANDINAVIA 1982

Kadiri mahitaji ya usafiri yalivyokuwa yakiongezeka ndipo michirizi ya rangi ya BLUU,KIJIVU na NYEKUNDU ikaanza kuonekana katika mabasi mengi zaidi yaliyokuwa yakisafirisha abiria karibia kila kona ya Tanzania.

Ilipofika mwaka 2001 kampuni ya Scandinavia walianzisha safari yao ya kwanza kabisa kutoka nje ya nchi kwa safari ya Dare es salaam hadi Nairobi nchini Kenya,ambapo mafanikio ya ruti hiyo yalipelekea kuzaliwa kwa ruti nyingine kati ya Nairobi hadi Mombasa na Mombasa hadi Dar es salaam. Katika mwaka wa 2002 kampuni ya Scandinavia walipanua wigo wa huduma zao kwa kuanza ruti mpya ndani ya Afrika mashariki kwa safari za Dare es salaam hadi Kampala nchini Uganda.

Ilipofika mwaka 2003 kampuni ya Scandinavia ilipanua wigo zaidi kwa kuanza kwenda katika mji mkuu wa nchi ya Zambia Lusaka.

Wakati huo wote kampuni ya Scandinavia ilikuwa chini ya mkurugenzi na mwanzilishi wake MR.MUHAMED ABDULLAH.



Kampuni ya Scandinavia ilianza kutumia mabasi ya kisasa mwaka 1982 na kuanzia hapo walikuwa wakiongeza mabasi kadili ya mahitaji ya kampuni na abiria pia na kufikia jumla ya mbasi 100 ambayo yalikuwa yakitoa huduma za usafiri ndani na nje ya nchi na mengi ya mabasi hayo yalikuwa ni ya kisasa yaliyonunuliwa kutoka kiwanda cha SCANIA na MARCOPOLO kilichopo nchini BRAZIL

4. KISWELE

1640253803784.png


Kiswele ndilo basi la kwanza Tanzania kuwa na injini nyuma.

Basi hili likitamba sana siku za nyuma na miongoni mwa njia ilizotamba ni Dar- Mbeya, Dar - Tunduma, Dar- Songea.

Mpaka leo hili basi linakumbukwa

5. SUMRI

images (11).jpeg


images (12).jpeg

Kampuni hii sasa haipo tena. Kampuni hii ilivuma sana ikihudumu njia ya Dar -Mbeya, Dar- Sumbawanga na Mbeya- Sumbawanga.

6. NGORIKA

images (13).jpeg


Kampuni hii kongwe imehudumu miaka mingi ikifanya safari zake kati ya Dar na Arusha.
 
1. TAWAQAL EXPRESS
View attachment 2054358

Pichani ni basi la kampuni ya Tawaqal. Kampuni hii ilikuwa balaa. Njia ya Dar - Mbeya, Dar- Kyela, Dar - Tunduma na Dar - Songea.

Kampuni hii ilikuwa na madereva mahiri kwelikweli. Miongoni mwao alikuwepo GIRIKI.

Jamaa alitoka Dar saa 12 asubuhi akaingia Mbeya saa 7 mchana.

2. SHABAHA EXPRESS

View attachment 2054378

Kampuni hii ilibamba sana miaka ya nyuma ikisafirisha abiria kati ya Dar na Arusha. Jamaa walikuwa wakishindana na wakongwe wa zamani kama Ngorika, Dar EXPRESS nk

3. SCANDINAVIA EXPRESS


Kampuni ya mabasi ya Scandinavia Express ni kampuni pekee ya kitanzania iliyowahi kutokea kwa kuwa na huduma za uhakika na za viwango vya hali ya juu kabisa kulinganisha na huduma zinazotolewa na kampuni za sasa. Kampuni hii ilijijengea jina kubwa na sifa nzuri ndani na nje ya nchi kwa huduma bora walizokuwa wakizitoa kwa abiria wake na pia kuliletea sifa taifa la Tanzania kwa kujulikana kuwa na mabasi ambayo ni quality na high class.
View attachment 2054407
Kampuni ya Scandinavia ilianzishwa zaiidi ya miaka thelathini na tano (35) iliyopita ikiwa na mabasi machache tu aina ya LEYLAND na ilipofika mwaka 1982 kwa mara ya kwanza Scandinavia walinunua basi lao la kwanza la kisasa kutoka kampuni ya SCANIA TANZANIA COACHES aina ya SCANIA ambalo kutokana na ubora wake na uzuri wake kwa kipindi hicho waliamua kulitumia kwa safari yao mpya waliyoianzisha ya Dar es salaam hadi Iringa.


BASI LA KWANZA LA KISASA KUNUNULIWA NA SCANDINAVIA 1982

Kadiri mahitaji ya usafiri yalivyokuwa yakiongezeka ndipo michirizi ya rangi ya BLUU,KIJIVU na NYEKUNDU ikaanza kuonekana katika mabasi mengi zaidi yaliyokuwa yakisafirisha abiria karibia kila kona ya Tanzania.
Ilipofika mwaka 2001 kampuni ya Scandinavia walianzisha safari yao ya kwanza kabisa kutoka nje ya nchi kwa safari ya Dare es salaam hadi Nairobi nchini Kenya,ambapo mafanikio ya ruti hiyo yalipelekea kuzaliwa kwa ruti nyingine kati ya Nairobi hadi Mombasa na Mombasa hadi Dar es salaam. Katika mwaka wa 2002 kampuni ya Scandinavia walipanua wigo wa huduma zao kwa kuanza ruti mpya ndani ya Afrika mashariki kwa safari za Dare es salaam hadi Kampala nchini Uganda.
Ilipofika mwaka 2003 kampuni ya Scandinavia ilipanua wigo zaidi kwa kuanza kwenda katika mji mkuu wa nchi ya Zambia Lusaka.

Wakati huo wote kampuni ya Scandinavia ilikuwa chini ya mkurugenzi na mwanzilishi wake MR.MUHAMED ABDULLAH.


Kampuni ya Scandinavia ilianza kutumia mabasi ya kisasa mwaka 1982 na kuanzia hapo walikuwa wakiongeza mabasi kadili ya mahitaji ya kampuni na abiria pia na kufikia jumla ya mbasi 100 ambayo yalikuwa yakitoa huduma za usafiri ndani na nje ya nchi na mengi ya mabasi hayo yalikuwa ni ya kisasa yaliyonunuliwa kutoka kiwanda cha SCANIA na MARCOPOLO kilichopo nchini BRAZIL

4. KISWELE

View attachment 2054432


Kiswele ndilo basi la kwanza Tanzania kuwa na injini nyuma.

Basi hili likitamba sana siku za nyuma na miongoni mwa njia ilizotamba ni Dar- Mbeya, Dar - Tunduma, Dar- Songea.

Mpaka leo hili basi linakumbukwa

5. SUMRI

View attachment 2054445

View attachment 2054448

Kampuni hii sasa haipo tena. Kampuni hii ilivuma sana ikihudumu njia ya Dar -Mbeya, Dar- Sumbawanga na Mbeya- Sumbawanga.


6. NGORIKA

View attachment 2054451

Kampuni hii kongwe imehudumu miaka mingi ikifanya safari zake kati ya Dar na Arusha.

Scandinavia gari ya kwanza kwangu kupanda ina choo ndani, tunapewa biskuti na soda.. nimetumiwa sana hela kupitia basi hili
 
Kiswele ilikuwa inatumia masaa mawili tu from Dar to Moro believe me!! ikiwa inashusha mlima kuitafuta msamvu mnaisikia sauti yake hiyooo mnajua kabisa hii ni Kiswele bjnafsi nimefanya kazi Hood Limited kuanzia mwaka 1996 mpaka 2010 mpaka ikafikia kipindi nikawa family friend wa wamiliki ikizingatia kwamba pia walikuwa wanafahamiana na baba yangu before..Nilipiga mzigo pale enzi zile Hood ni Hood hata nilipomaliza chuo sikuona umuhimu wa kuendelea na kazi nyingine kutokana na mavumba yaliyokuwa yanapatikana hapo na mimi ndio nilitoa wazo la kuwa na route ya Nairobi Arusha hapo ndio nikazidi kugongelea msumari wa kuaminiwa lakini kizuri hakidumu niliamua kufanya majukumu yangu mengine kabisa kwa hiyari baada ya kuhitaji changamoto mpya lakini maboss zangu ambao walinilea bado nipo nao karibu mpaka kesho hasa watoto zake..Hood sio kama amefirisika hapana ukweli ni kwamba kulitokea mgogoro mzee mwenyewe akiwatuhumu watoto kuwa wanafuja mali za kampuni kwa kutumia hela kwa starehe hivyo hana nia ya kuendelea na biashara hiyo ingawa bado kampuni ilikuwa top na tulikuwa kwenye process ya kuorder mabasi mapya makaliii so akaifunga taratibu kampuni mabasi kayafungia ndani na mengine anauza kwa bei ya kutupa mgogoro huu ulikuwa hasa kati ya mzee na watoto wake hasa Tiffu na Saidy ambao ni wakubwa na ndio walikuwa wakurugenzi ukiachana na yule mwingine aliyekuwa uarabuni mpaka leo Hood Hood..mzee kaamua kuwekeza kwenye biashara nyingine kama kwenye Real estates na kununua hisa kwa baadhi ya makampuni kama Azania..asante kwa uzi huu

946229_369191479852479_333001589.jpg
 
Back
Top Bottom