Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 76,107
- 160,001
- Thread starter
-
- #101
Bado ipoSahh kabisa nakumbuka nilipanda gari hii mwaka 2011 wakat nampeleka mdogo wangu seminari ya kikatoliki kuanza kidato Cha 1 STELLA MATUTINA - LIGHANO
nadhan Bado inapiga kazi hii
Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Hiyo route sio mchezoUwende lipwela chombo makete manda ludewa mbamba bay
Kwani ile bambo ya songea mbambabay imeacha routes auUSAFIRI HUU HAUVUMI LAKINI BADO WAMO
Huu ni usafiri wa kutoka Songea kuelekea Namtumbo maarufu kwa jina la 'Matimbula' ingawa kuna magari mengine ya kisasa yanayofanya safari kuelekea huko lakini gari hilo limekuwa na wapenzi wengi ingawa mwendo wake ni wa polepole kama wa kinyonga.
Huyu ni abiria aliyekuwemo kwenye basi hilo ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Abdul
Silali # Sirari, tofautisha r na l.Mwaka 2004 nilisafiri na basi la SCANDINAVIA kutoka Mwanza-Musoma-Silali-Nairobi-Namanga-Arusha-Moshi-Dar kwa wakati mmoja usiku na mchana
Kweli mkuu nimeiona Hadi miaka ya hivi karibu pale songea na Lina abiria nyomi bila kujali mabasi ya kisiasa yaliyopo barabaraniUSAFIRI HUU HAUVUMI LAKINI BADO WAMO
Huu ni usafiri wa kutoka Songea kuelekea Namtumbo maarufu kwa jina la 'Matimbula' ingawa kuna magari mengine ya kisasa yanayofanya safari kuelekea huko lakini gari hilo limekuwa na wapenzi wengi ingawa mwendo wake ni wa polepole kama wa kinyonga.
Huyu ni abiria aliyekuwemo kwenye basi hilo ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Abdul
Hii bamboo imefilisika Ina maari mawili tu yote hunzia Mbinga kwenda tunduru. Songea mbambabay imekamatwa na kampuni za wazawa kisumapai na kangaulaya na Zina magari high classKwani ile bambo ya songea mbambabay imeacha routes au
Huu uzi mzuri kweli kwa kumbukumbu. Umetukumbusha mbali mkuu, baada ya kupitia uzi kuna visa vimenivutia.
1. Kupata kiini cha kufa kwa kampuni ya Hood
2. Dereva aliyetoka Dar na kufika Mbeya saa 7, hii ni balaa.
3. Ajali iliyokula 70 dah! Bado natamani kupata mwendelezo wake, 70 kwenye bus moja ni kisanga hiki. Halafu kwanini ajali za miaka ya nyuma ziliua sana watu wengi kwa mpigo? Nakumbuka bus jingne sijui (air msae) lilipata ajali kilimanjaro likaua sana wanafunzi.
4. Simon Sirro RPC Tanga [emoji1]
5. Nami niongeze yangu nnayokumbuka ambayo sijayaona huko juu
- Air Shengena
- Kizota
- Fresh ya Shamba
- Bembea
- Royal
Tuwekee MAPANDE na FRESH YA SHAMBA iliyokua inapiga Dar Arusha1. TAWAQAL EXPRESS
View attachment 2054358
Pichani ni basi la kampuni ya Tawaqal. Kampuni hii ilikuwa balaa. Njia ya Dar - Mbeya, Dar- Kyela, Dar - Tunduma na Dar - Songea.
Kampuni hii ilikuwa na madereva mahiri kwelikweli. Miongoni mwao alikuwepo GIRIKI.
Jamaa alitoka Dar saa 12 asubuhi akaingia Mbeya saa 7 mchana.
2. SHABAHA EXPRESS
View attachment 2054378
Kampuni hii ilibamba sana miaka ya nyuma ikisafirisha abiria kati ya Dar na Arusha. Jamaa walikuwa wakishindana na wakongwe wa zamani kama Ngorika, Dar EXPRESS nk
3. SCANDINAVIA EXPRESS
Kampuni ya mabasi ya Scandinavia Express ni kampuni pekee ya kitanzania iliyowahi kutokea kwa kuwa na huduma za uhakika na za viwango vya hali ya juu kabisa kulinganisha na huduma zinazotolewa na kampuni za sasa. Kampuni hii ilijijengea jina kubwa na sifa nzuri ndani na nje ya nchi kwa huduma bora walizokuwa wakizitoa kwa abiria wake na pia kuliletea sifa taifa la Tanzania kwa kujulikana kuwa na mabasi ambayo ni quality na high class.
View attachment 2054407
Kampuni ya Scandinavia ilianzishwa zaiidi ya miaka thelathini na tano (35) iliyopita ikiwa na mabasi machache tu aina ya LEYLAND na ilipofika mwaka 1982 kwa mara ya kwanza Scandinavia walinunua basi lao la kwanza la kisasa kutoka kampuni ya SCANIA TANZANIA COACHES aina ya SCANIA ambalo kutokana na ubora wake na uzuri wake kwa kipindi hicho waliamua kulitumia kwa safari yao mpya waliyoianzisha ya Dar es salaam hadi Iringa.
BASI LA KWANZA LA KISASA KUNUNULIWA NA SCANDINAVIA 1982
Kadiri mahitaji ya usafiri yalivyokuwa yakiongezeka ndipo michirizi ya rangi ya BLUU,KIJIVU na NYEKUNDU ikaanza kuonekana katika mabasi mengi zaidi yaliyokuwa yakisafirisha abiria karibia kila kona ya Tanzania.
Ilipofika mwaka 2001 kampuni ya Scandinavia walianzisha safari yao ya kwanza kabisa kutoka nje ya nchi kwa safari ya Dare es salaam hadi Nairobi nchini Kenya,ambapo mafanikio ya ruti hiyo yalipelekea kuzaliwa kwa ruti nyingine kati ya Nairobi hadi Mombasa na Mombasa hadi Dar es salaam. Katika mwaka wa 2002 kampuni ya Scandinavia walipanua wigo wa huduma zao kwa kuanza ruti mpya ndani ya Afrika mashariki kwa safari za Dare es salaam hadi Kampala nchini Uganda.
Ilipofika mwaka 2003 kampuni ya Scandinavia ilipanua wigo zaidi kwa kuanza kwenda katika mji mkuu wa nchi ya Zambia Lusaka.
Wakati huo wote kampuni ya Scandinavia ilikuwa chini ya mkurugenzi na mwanzilishi wake MR.MUHAMED ABDULLAH.
Kampuni ya Scandinavia ilianza kutumia mabasi ya kisasa mwaka 1982 na kuanzia hapo walikuwa wakiongeza mabasi kadili ya mahitaji ya kampuni na abiria pia na kufikia jumla ya mbasi 100 ambayo yalikuwa yakitoa huduma za usafiri ndani na nje ya nchi na mengi ya mabasi hayo yalikuwa ni ya kisasa yaliyonunuliwa kutoka kiwanda cha SCANIA na MARCOPOLO kilichopo nchini BRAZIL
4. KISWELE
View attachment 2054432
Kiswele ndilo basi la kwanza Tanzania kuwa na injini nyuma.
Basi hili likitamba sana siku za nyuma na miongoni mwa njia ilizotamba ni Dar- Mbeya, Dar - Tunduma, Dar- Songea.
Mpaka leo hili basi linakumbukwa
5. SUMRI
View attachment 2054445
View attachment 2054448
Kampuni hii sasa haipo tena. Kampuni hii ilivuma sana ikihudumu njia ya Dar -Mbeya, Dar- Sumbawanga na Mbeya- Sumbawanga.
6. NGORIKA
View attachment 2054451
Kampuni hii kongwe imehudumu miaka mingi ikifanya safari zake kati ya Dar na Arusha.
Aka fresh coach laterTuwekee MAPANDE na FRESH YA SHAMBA iliyokua inapiga Dar Arusha
Mziku ule ulikua unatembea sana dar Arusha
Ni kweli kabisa mpaka sasa sijaona kampuni iliyofikia viwango vya juu kama hawa jamaa. Pale head office yao Kamata ukifika utadhani umeingia airport ndogo [emoji12][emoji12]Scandinavia gari ya kwanza kwangu kupanda ina choo ndani, tunapewa biskuti na soda.. nimetumiwa sana hela kupitia basi hili
Hii itakuwa shangazi hotel pale Moshi stend enzi hizooo...
Huyo mwenye Bus za Kiswele nikiwa Lindi wilaya ya Kilwa niliwahi kufika kijiji kinaitwa Kiswele baada ya kudadisi wenyeji kwamba kuna kampuni ya Bus zinaitwa Kiswele wakaniambia aaaah huyo ni mzaliwa wa hapa Kijijini na nyumbani kwake paleee. Kiukweli watu wanahangaika kutafuta maisha maana hicho kijiji miaka hiyo ilikuwa hata gari halifiki, mnaishia njiani mnaacha gari halafu mnatembea kwa miguu.Kiswele ilikuwa inatumia masaa mawili tu from Dar to Moro believe me!! ikiwa inashusha mlima kuitafuta msamvu mnaisikia sauti yake hiyooo mnajua kabisa hii ni Kiswele bjnafsi nimefanya kazi Hood Limited kuanzia mwaka 1996 mpaka 2010 mpaka ikafikia kipindi nikawa family friend wa wamiliki ikizingatia kwamba pia walikuwa wanafahamiana na baba yangu before..Nilipiga mzigo pale enzi zile Hood ni Hood hata nilipomaliza chuo sikuona umuhimu wa kuendelea na kazi nyingine kutokana na mavumba yaliyokuwa yanapatikana hapo na mimi ndio nilitoa wazo la kuwa na route ya Nairobi Arusha hapo ndio nikazidi kugongelea msumari wa kuaminiwa lakini kizuri hakidumu niliamua kufanya majukumu yangu mengine kabisa kwa hiyari baada ya kuhitaji changamoto mpya lakini maboss zangu ambao walinilea bado nipo nao karibu mpaka kesho hasa watoto zake..Hood sio kama amefirisika hapana ukweli ni kwamba kulitokea mgogoro mzee mwenyewe akiwatuhumu watoto kuwa wanafuja mali za kampuni kwa kutumia hela kwa starehe hivyo hana nia ya kuendelea na biashara hiyo ingawa bado kampuni ilikuwa top na tulikuwa kwenye process ya kuorder mabasi mapya makaliii so akaifunga taratibu kampuni mabasi kayafungia ndani na mengine anauza kwa bei ya kutupa mgogoro huu ulikuwa hasa kati ya mzee na watoto wake hasa Tiffu na Saidy ambao ni wakubwa na ndio walikuwa wakurugenzi ukiachana na yule mwingine aliyekuwa uarabuni mpaka leo Hood Hood..mzee kaamua kuwekeza kwenye biashara nyingine kama kwenye Real estates na kununua hisa kwa baadhi ya makampuni kama Azania..asante kwa uzi huu
View attachment 2054530
Yaani hapo kwa Sirro daah..Huu uzi mzuri kweli kwa kumbukumbu. Umetukumbusha mbali mkuu, baada ya kupitia uzi kuna visa vimenivutia.
1. Kupata kiini cha kufa kwa kampuni ya Hood
2. Dereva aliyetoka Dar na kufika Mbeya saa 7, hii ni balaa.
3. Ajali iliyokula 70 dah! Bado natamani kupata mwendelezo wake, 70 kwenye bus moja ni kisanga hiki. Halafu kwanini ajali za miaka ya nyuma ziliua sana watu wengi kwa mpigo? Nakumbuka bus jingne sijui (air msae) lilipata ajali kilimanjaro likaua sana wanafunzi.
4. Simon Sirro RPC Tanga [emoji1]
5. Nami niongeze yangu nnayokumbuka ambayo sijayaona huko juu
- Air Shengena
- Kizota
- Fresh ya Shamba
- Bembea
- Royal
Mimi simu niliyomnunulia Mzee wangu mara baada ya simu kutoka (ilikuwa Siamen ngapi sijui, ile nyeusi yenye kiantena) niliituma kwa Scandinavia kumpelekea mzee daah..Watu wa kale mlipata sana shida!!!! Kwaio pesa ilikua inatumwa kwa bus[emoji23]
Umenikumbusha ISLAM ya kwanza kwenda Arusha from Morogoro ilikuwa balaa, dereva wake aliitwa KIMARO...Ina maana ISLAM na SADIQ LINE hukuwakutaga!?